Komeo
JF-Expert Member
- May 3, 2011
- 2,498
- 1,171
Samahani wadau, najua suala hili lilishawahi jadiliwa sana humu jamvini, lakini naomba tena kuuliza ili wanaolifahamu vizuri watujuze nasi. Jana usiku taarifa za habari za itv na tbc zilimuonyesha JK akisaini kitabu cha wageni kule VETA Ntwara (sijakosea, ndivyo inavyotamkwa), akiwa amekalia kiti kinachofanana kabisa na kile anachotumia siku zote akiwa Ikulu. Je, ni kile kile ila kilisafirishwa tu kwa kazi hiyo, au vipo vingi hata VETA wanavyo?