Kitendo cha Wabunge Kuzomea sio Ishara njema

Kitendo cha Wabunge Kuzomea sio Ishara njema

Nilishikwa na bumbuwazi niliposikia hii kauli!! Wengi wa viongozi wa CCM hawajitambui na hawajui nini cha kufanya!!

Kwa mtu anaejielewa huwezi sema unafanya vitu kwa surprise!! Hii serikali inaishi kwa matukio sioni dira yoyote!!
Jaji Sinde Warioba aliwahi kulisema hilo, "suprise" aliyosema Jennister ndio "matukio" kama ambavyo Jaji Warioba alisema kuonesha vile nchi inavyoendeshwa na serikali. Angalia serikali ya mkoa wa Dar es salaam ilivyo kituko. Hakuna kazi zaidi ya kusubiri "suprise".

Jaji Warioba: Nchi imepoteza mwelekeo, inaendeshwa na matukio
 
Mkuu kuna kitu kimekupita kidogo. Na nadhani sio oeke yako Bali wengi tuu.
Wageni waliokuwa wamekaa pale juu wana impact kubwa na mabadiliko uliyoona leo bungeni kwa wabunge wa ccm.
Mpwa Elli, moyo ni kitu cha ajabu sana. Hujawahi kuona umpendaye hata kama ni kwa siri tabasamu linaweza kukuumbua?
Ukweli ni kuwa wabunge wengi wa ccm wanamoenda sana Lowassa kuliko Magufuli ila wanalinda tumbo tuu.
Kwenye masuala ya nchi magufuli hajawahi kuwa wala hana urafiki na mtu..hiyo ndio tofauti yake na lowasa na wengine wengi..magu is a unique man..kweli ukawa mmebanwa leo mnafikia kuwasifia opportunists wa ccm wanaomtaka lowasa..tena mnasema kabisa ati wanalinda matumbo yao..so lowassa angepita wangekula sana ee??hahah..go magufuli go
 
Kwenye masuala ya nchi magufuli hajawahi kuwa wala hana urafiki na mtu..hiyo ndio tofauti yake na lowasa na wengine wengi..magu is a unique man..kweli ukawa mmebanwa leo mnafikia kuwasifia opportunists wa ccm wanaomtaka lowasa..tena mnasema kabisa ati wanalinda matumbo yao..so lowassa angepita wangekula sana ee??hahah..go magufuli go

Kwenye masuala ya nchi hana urafiki na mtu? Wewe ni mtu wa Msumbiji nini? Anzia kwenye sakata la nyumba, njoo kwenye utoaji wa zabuni za barabara za ndani utajua nini unachokisema tofauti na ukweli. Tatizo ukisoma gazeti la Uhuru una kuja na conclution zako.
Kula ni jambo la lazima kama unakula vilivyo halali, sasa hivi watu hata malipo yao stahiki watu hawapati unadhani ni sawa hiyo?
 
Kwenye masuala ya nchi hana urafiki na mtu? Wewe ni mtu wa Msumbiji nini? Anzia kwenye sakata la nyumba, njoo kwenye utoaji wa zabuni za barabara za ndani utajua nini unachokisema tofauti na ukweli. Tatizo ukisoma gazeti la Uhuru una kuja na conclution zako.
Kula ni jambo la lazima kama unakula vilivyo halali, sasa hivi watu hata malipo yao stahiki watu hawapati unadhani ni sawa hiyo?
We endelea kufukua makaburi ukidhani utaikuta sura ya bibi yako..magufuli aliyekuwa chini ya utawala ni tofauti na magufuli anayetawala..alipoingia ikulu mlisema TV magogoni rimoti msoga..sasa kila santuri mnayojaribu kuicheza haimalizi siku imechuja..zikiisha zote nadhani mtachukua majembe mkalime..maana hakutakuwa na namna tena
 
Wanajua maisha ya wapiga kura wao yalivyo magumu wakijitoa ufahamu itakula kwao 2020
 
RAHA YA KUWA NA MBUNGE WA CCM KTK JIMBO
LAKO HII HAPA "Mheshimiwa Spika, kabla
sijaingia kuchangia bajeti hii, nataka niseme
kuwa naona upinzani wamefikia pabaya
sana, wanaikashifu serikali sikivu ya CCM.
Chama kimefanya mengi sana, maendeleo makubwa tumepata, shule za msingi,
sekondari na vyuo viko vingi sana tofauti na
zamani, barabara za lami, umeme nchi nzima
mpaka vijijini, lakini wapinzani wanakebehi.
Naipongeza sana serikali ya Chama Cha
Mapinduzi. Mheshimiwa Spika, bila kupoteza muda sasa niingie kwenye jimbo langu,
naomba nielezee kwa kifupi matatizo ya
jimbo langu. Kule hatuna shule za sekondari
katika kata sita, maji ni ndoto, tunategemea
mvua za msimu. Shule zilizopo hazina ubora
wala walimu wa kutosha. Rais alikuja sasa ni miaka sita katuahidi umeme lakini mpaka
leo hakuna lolote. Barabara ni mbovu
hazipitiki. Nauliza ni lini serikali hii (ya CCM)
ITATUSIKIA NA KUTULETEA MAENDELEO?"(Wab
unge Makofi) kwa! Kwa! Kwa!. Naombeni
sana tena sana jimbo langu liangaliwe kwa jicho la Huruma. Baada ya kusema hayo
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa
100%
 
Ukimsikiliza tu anacho ongeaga na subject matter you can tell she is very simple.
 
Kama mmesikiliza na kusoma magazeti ya leo mtaelewa kuwa wabunge wa ccm sasa wamebadilika.......naona sasa watu wanataka kupitia madirishani kwani gari ni bovu na limeshaanza kuacha njia
 
Leo wakati Mama Jenista Mhagama (Sijui hata Wizara yake) akijibu hoja za Mheshimiwa Mbowe kwa mbwembwe alijikuta akizomewa na Wabunge wote hasa wa CCM baada ya kusema Serikali inafanya mambo kwa "surprise" kama surprise ya kuwasomesha bure watoto wote hadi kidato cha NNE!!

Kwangu Mimi hii sio ishara njema kwa wana CCM, tulizoea kuwaona wakiwa pamoja hata kwenye mambo ya "vichekesho" lakini Leo hii eti wanamzomea Mama Jenista.

Hii sio kawaida something is wrong somewhere, huenda ushauri wa Mheshimiwa Lema wa Jana umeanza kuwaingia. All the best!!



Unaweza kuwahadaa baadhi ya watu wakati wowote lakini huwezi kuwapumbaza na kuwahadaa watu wote wakati
wote!!! Wahenga walisema
mwanzo wa ngoma ni lele!!
 
Kuna mtu mmoja nimemwambia, Lowasa bado ana nguvu sana ndani ya CCM, kuliko wananvyodhani. Hii ndiyo hofu kubwa sana ndani ya chama tawala. Mabya zaidi hawawezi kufanya chochote, maana matokeo yake hakuna nayeyajua...speculations tu.

Ati, surprise!!! Ngoja tuone hayo masaprizee
 
Back
Top Bottom