Kitendo cha kuongeza muda ndicho kitakachowaunganisha Watanzania kupinga bila kujali itikadi zao

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Watanzania hatujawa na desturi ya kuwa na sauti moja katika kudai haki zetu, kila mtu hudai kivyake, wasanii hudai haki zao kivyao, madaktari hudai haki zao kivyao nk. huku kada zingine zikisema madai hayo hayawahusu kwa sababu sisi sio wasanii sisi sio madakitari.

Pamoja na kuwa Watanzania ni waoga wa kudai haki kwa pamoja lakini kuna wakati kutokana na mazingira na misukumo ya kijamii, kimaisha hulazimika kuungana na kujenga sauti moja.

Mwanzoni mwa miaka ya 90 tulishuhudia wimbi kubwa la wananchi kutoka kwa kada mbalimbali wana sheria, wanasiasa na wananchi wa kawaida bila kujali itikadi zao wakiungana kutaka mabadiliko ya utawala, vuguvugu ambalo lilizaa mfumo wa vyama vingi.

Kikundi cha Wazanzibari KAMAHURU kilichokuwa kinapigania demokrasia kiliungana na Civic Movement lililokuwa kundi la kupigania haki za binadamu Tanzania Bara na kuunda Chama cha Wananchi CUF. Chama cha NCCR - Mageuzi kilitokana na Wajumbe wa Kamati iliyoundwa kwa ajili ya mageuzi ya Katiba, National Committee for Constitution Reform - NCCR.

Kitendo cha wanasiasa wachache kutaka kubadili katiba ili kuongeza muda kwa maslahi ya wachache bila ridhaa ya wananchi walio wengi kinakwenda kuzalisha vuguvugu jingine ambalo litawafanya wananchi kuungana kupinga mabadiliko hayo. Ikumbukwe kuwa sio wana CCM wote wanaotaka mabadiliko hayo.

Kitawafanya wakulima, wanasiasa, wafanyabiashara, machinga, walimu, wahadhiri, madereva, wana sheria nk wote kuungana pamoja na wanaharakati kupinga mabadiliko hayo, tutaanza kushuhudia kamati mbalimbali kama zile za National Committee for Constitution Reform - NCCR zikiazishwa na huo ndio utakuwa mwanzo wa harakari za mabadiliko chanya kama yaliyofanywa miaka ya 90.
 
Katiba sio msahafu, tunaweza kubadilisha kwa maslahi mapana ya vizazi vya sasa na vijavyo. Watu wazima wenye upeo mpana wa kufikiri tunaona jinsi kile kikundi cha walafi, wezi na wafujaji wa raslimali za taifa wakisaidiwa na mabeberu kinavyojipanga kurudi baada ya Uongozi wa JPM kupita! Tumejipanga kuwaumiza, tunamuongezea rais mihula mingine! Sisi sio wa kwanza kufanya hivyo duniani.
 
Hawa wanaopiga mboyoyo wanamaslahi binafs na huyu bwana kayafa, alafu wanampa kichwa eti anapendwa npo mkoa flan nmefurahi sana wananch wanajieelewaaa munoo unaulizwaa nan ulimpigia kura ndoo kakope hukoo.
 
Katiba sio msahafu, tunaweza kubadilisha kwa maslahi mapana ya vizazi vya sasa na vijavyo. Watu wazima wenye upeo mpana wa kufikiri tunaona jinsi kile kikundi cha walafi, wezi na wafujaji wa raslimali za taifa wakisaidiwa na mabeberu kinavyojipanga kurudi baada ya Uongozi wa JPM kupita! Tumejipanga kuwaumiza, tunamuongezea rais mihula mingine! Sisi sio wa kwanza kufanya hivyo duniani.
Basi rudisheni fao la kujitoa halafu mengine mfanye mnavyotaka hata kama ni kumfanya awe rais wa milele ni sawa tu.
 
Kwa mujibu wa mtumishi wa Mungu Polepole ulimwengu unaelekea kwenye kipindi cha miaka 7 ya dhiki kuu.

Sidhani kama kuna kiongozi atapenda kipindi hicho kimkute akiwa madarakani!
 
Hivi bado unatuamini watanzania? Mkuu unadhani Watanzania wanaweza kufanya lolote? Tena watanzania bara. Kuweka matumaini kwenye hilo ni kutafuta kuja kuwa disappointed kabisa.
 
Kama ambavyo masanduku ya kura 2020 yalijaa kura za DR. John Joseph Pombe Magufuli ndvyo itakuwa tukiungana kuondoa ukomo wa mihula ya urais....tumechoka na "mzaoea ya AWAMU MOJA KUJENGA NA KISHA AWAMU NYINGINE KUBOMOA"

Shime watanzania wenye mapenzi mema tushirikiane kufunga na kuomba ili Mungu akampe nguvu JPM aongoze bila ukomo....hadi makuwadi wa akina Robert Amsterdam na wenzake wakate tamaa na kujitafutia njia halali za kulisha familia zao! SASA HIVI WAPO Hibernation!


download.jpg
 
Hivi bado unatuamini watanzania? Mkuu unadhani Watanzania wanaweza kufanya lolote? Tena watanzania bara. Kuweka matumaini kwenye hilo ni kutafuta kuja kuwa disappointed kabisa.
Wameishasahau jinsi Rais wa chama cha madereva wa malori alivyokuwa akilia mbele ya kamera za waandishi wa habari huku akisisitiza maandamano, kesho yake alisikika akisema......" mgomo ni wa madereva sio wa viongozi wa chama (kesi ya kuujumu uchumi ni mbaya asikwambie mtu!)
 
Back
Top Bottom