CCM imewapuuza na Kuwadharau Watanzania

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,058
Kwa mwenye akili, ni dharau kubwa mtu akakuita akasema anataka kuusikia ushauri wako, kumbe mtu huyo alikwishafanya maamuzi yake tayari. Kwa hiyo ushauri wako kwake inakuwa ni kukupotezea muda kwa kuwa alikwishakupuuza. Lakini akaona haitoshi kukupuuza, akataka pia kukuonesha wazi namna anavyokudharau, kwa kutozingatia ushauri wako wote. Hicho ndicho kilichofanywa na CCM, Serikali yake na Bunge lake.

CCM imewafanya watanzania wote hawana maana, hawana akili, hawana haki ya kusikilizwa.

Kwanza Serikali iliwahadaa wananchi kuwa eti inataka kubadilisha sheria ya uchaguzi na ya Tume ya Uchaguzi ili kuongeza demokrasia. Nasema kuwa ni hadaa kubwa kwa sababu miswada hiyo ya sheria haikuwa imejibu malalamiko ya msingi ya wananchi.

Lakini wakaendeleza hadaa kwa kupitisa wabunge wao. Kamati ya Bunge ikawatangazia wananchi kuwa inapokea maoni kuhusiana na miswada miwili ya sheria zinazohusiana na masuala ya uchaguzi. Wananchi wengi kwa kujua umuhimu wa uchaguzi walijitokeza kwenda kutoa maoni yao.

Jambo moja ambalo liliongelewa sana na wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini, vyama vya siasa, NGOs na wananchi mmoja mmoja, ni kutaka wakurugenzi wa Wilaya na Halmashauri? ambao kimsingi ni wateule wa Rais, wasiwe wasimamizi wa uchaguzi. Wadau hawa wakashauri Tume ya uchaguzi iwe na watumishi wake kwaajili ya kusimamia uchaguzi. Jambo la pili lililoshauriwa na wadau wengi ni uchaguzi wa Serikali za mitaa kusimamiwa na Tume ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI. Na jambo la tatu lililoshauriwa na wadau wengi ni kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa maana ya tangu kuundwa kwake, wajumbe wake na utendaji wake wa kazi.

Maoni haya yote ya wananchi, yamepuuzwa, na miswada wameipitisha kama walivyoiandaa na kupanga bila ya kuzingatia maoni ya wananchi. Hii ni dharau kubwa kwa wananchi wote.

Jambo pekee walilolifanya ni kubadilisha tu jina la Tume ya Uchaguzi eti iitwe Tume Huru ya Uchaguzi. Hii ni sawa muwe na jirani jambazi. Mkawa na malalamiko huyo jambazi aondolewe mtaani penu. Halafu anayetakiwa kumwondoa, badala ya kumwondoa, akasema kwamba huyo bwana kuanzia leo asiitwe jambazi bali aitwe Raia Mwema.

Wito wangu kwa wananchi wote wenye mapenzi mema kwa Taifa letu, anayekupuuza na kukudharau, nawe umfanyie vivyo hivyo. Tuipuuze CCM, tuipuuze Serikali yake, tulipuuze Bunge lake, tuwapuuze na viongozi wao wote.

Waungwana wanasema mheshimu anayekuheshimu. Asiyekuheshimu, anayekupuuza, nawe mtende vivyo hivyo.

Na kuwaonesha kuwa tumewapuuza, tuungane kwenye maandamano yoyote yale yatakayoandaliwa na chama chochote cha siasa au taasisi nyingine yoyote kuikataa miswada hiyo, kuukataa ulaghai wa CCM na taasisi zake. Ndugu wananchi, hawa watu hawatatuheshimu hata siku moja bila ya sisi wenyewe kuwathibitishia kuwa tunastahili na tuna haki ya kuheshimiwa na kuthaminiwa.

Mabadiliko ya sheria, kutoka kwenye sheria mbovu kwenda kwenye sheria bora, kutoka kwenye katiba mbaya kwenda kwenye katiba nzuri, hatuyahitaji kwaajili ya chama fulani au taasisi fulani bali kwaajili ya nchi yetu na jamii nzima ya Watanzania wa leo na kesho.

Wanaotengeneza sheria kwaajili ya kujinufaisha wao binafsi au chama chao au familia zao, ni wahuni, na wahuni hawastahili kuheshimwa wala kusikilizwa. Mungu wetu tunaomba utujalie ujasiri wa kupigania kilicho chema kwa Taifa letu, na katika hilo tunaomba uwe nasi.

Sijawahi kushiriki maandamano ya kudai haki. Safari hii nitashiriki. Nimeamua kushiriki yale yaliyoandaliwa na CHADEMA kule Mbeya. Sitashiriki kama maandamano ya CHADEMA bali kama maandamano ya kupinga hila za watu waovu wasioraka nchibyetu iwe na mifumo mizuri ya demokrasia, utawala na sheria. Ni maandamano dhidi ya wanaoliangamiza Taifa.
 
Ndugu yangu Bams unafiki wa Wananchi ndio sababu ya matatizo haya
Wananchi ni wanafiki ndio maana kwenye maandamano hawatoki
Nchi isiyokuwa na msimamo ni sawa na uozo
Ni kweli.

Yaani tumekuwa watu wa ajabu. Tumekuwa watu wa kutarajia anayekuonea abadilike aanze kukutendea wema bila ya wewe unayeonewa kukataa kuonewa.
 
Hizo ajira za muda za uchaguzi tayari🥲
Tunapoteza pesa nyingi kwa mambo yasiyo na maana, na nyingine nyingi, kufuatana na taarifa ya CAG, zinaibiwa na viongozi wa Serikali.

Ni aheri pesa hiyo ingetumika kuajiri watumishi wa Tume ya uchaguzi, ili nchi ipate viongozi waadilifu watakaoweza kuzuia wizi unaoendelea.
 
Hizo barabara za lami, mashule, maji, bwawa la mwalimu nyerere, huduma za afya, SGR, amani na utulivu, vyuo vikuu.....ndio dharau lwa watanzania?
 
Kwa Akili ya Kawaida CCM haiwezi Kupokea ushauri wa Wapinzani

Maoni ya muswada wa Mabadiliko ya sheria za uchaguzi kimsingi yalitolewa na Wadau wa Siasa na siyo Wananchi wa Kawaida
 
Watanzania hawajielewi, hivyo wanastahili kupuuzwa. Na siyo mara ya kwanza watanzania kupuuzwa. Na wakipuuzwa huwa wanakaa kimya kama mazuzu:-

1. Magufuli a.k.a jiwe alikataza mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa. Mazuzu hayakuchukua hatua.
2. Jiwe aliminya haki za wafanyakazi kwa kuwanyima annual increment ambayo ipo kisheria (ni statutory). Na mishahara hakuongeza kabisa. Akawa anajibu kwa nyodo kwamba ni bora ajenge reli. Mazuzu yakaendelea na kazi bila kugoma.
3. Huyu bibi ameanzisha tozo wakati watanzania (mazuzu) yanalipa kodi tena isiyohimilika. Matokeo yake biashara zinakufa, kila siku assets za watu zinapigwa mnada. Lkn mazuzu hata hayaoni shida.


Kwahiyo ndugu mleta mada, hili la miswada ni dogo sana kwa mazuzu haya yanayopatikana kwenye ardhi ya Tanganyika (Danganyika).
 
Hizo barabara za lami, mashule, maji, bwawa la mwalimu nyerere, huduma za afya, SGR, amani na utulivu, vyuo vikuu.....ndio dharau lwa watanzania?
Hata mkoloni alijenga hivyo na bado tulimkataa. Itakuwa huyu mkoloni mweusi?
 
Kwa Akili ya Kawaida CCM haiwezi Kupokea ushauri wa Wapinzani

Maoni ya muswada wa Mabadiliko ya sheria za uchaguzi kimsingi yalitolewa na Wadau wa Siasa na siyo Wananchi wa Kawaida
Mnyalukolo, umerukwa na akili?

Hata ule ushauri wa KKKT na TEC, wote hao ni wanasiasa?

CCM yenyewe ni chama cha siasa, serikali na Bunge, ni mazao ya siasa. Lakini CCM inaona ushauri wa wanasiasa na vyama vya siasa, hauna maana?

Ukikatana mijafala ya kisiasa maana yake umechagua vurugu. Je, huko ndiko CCM inataka nchi iende?
 
Kwa Akili ya Kawaida CCM haiwezi Kupokea ushauri wa Wapinzani

Maoni ya muswada wa Mabadiliko ya sheria za uchaguzi kimsingi yalitolewa na Wadau wa Siasa na siyo Wananchi wa Kawaida

Kuna aliyewazuia wananchi wa kawaida kutoa maoni Yao?. Je maoni kwenye rasimu ya Warioba hawakuwa wananchi wa kawaida?
 
Watanzania hawajielewi, hivyo wanastahili kupuuzwa. Na siyo mara ya kwanza watanzania kupuuzwa. Na wakipuuzwa huwa wanakaa kimya kama mazuzu:-

1. Magufuli a.k.a jiwe alikataza mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa. Mazuzu hayakuchukua hatua.
2. Jiwe aliminya haki za wafanyakazi kwa kuwanyima annual increment ambayo ipo kisheria (ni statutory). Na mishahara hakuongeza kabisa. Akawa anajibu kwa nyodo kwamba ni bora ajenge reli. Mazuzu yakaendelea na kazi bila Kigoma.
3. Huyu bibi ameanzisha tozo wakati watanzania (mazuzu) yanalipa Kodi tena isiyohimilika. Matokeo yake biashara zinakufa, kila siku assets za watu zinapogwa mnada. Lkn mazuzu hata hayaoni Hilo.


Kwahiyo ndugu mleta mada, hili la miswada ni dogo sana kwa mazuzu haya ywnayopatikwna kwenye ardhi ya Tanganyika (Danganyika).

Kwa kweli bila Watanzania kuamka kutoka kwenye usingizi wa ujinga, CCM itaendelea kuwachezea wananchi kwa njia haramu zozote ipendavyo, kama inavyofanya sasa.
 
Hizo barabara za lami, mashule, maji, bwawa la mwalimu nyerere, huduma za afya, SGR, amani na utulivu, vyuo vikuu.....ndio dharau lwa watanzania?

Tungekuwa na Serikali inayothamini michango ya watu wake, tungeweza kujenga maradufu ya hivyo ulivyoviorodhesha.

Halafu ni uwongo kudai kuwa nchi ina amani. Nakubaliana nawe kuwa nchi ina utulivu, japo haina amani.

Kijana aliyeanzisha hair cutting saluni yake halafu hajui ni lini kutakuwa na umeme, na hivyo kukosa kipato, huwezi kusema kijana huyo ana amani. Mtu aliyejipigapiga akaanzisha restaurant yake, halafu nyama na samaki vinaozea kwenye deep freezers kwa sababu hakuna umeme, hawezi kuwa na amani.
 
Mnyalukolo, umerukwa na akili?

Hata ule ushauri wa KKKT na TEC, wote hao ni wanasiasa?

CCM yenyewe ni chama cha siasa, serikali na Bunge, ni mazao ya siasa. Lakini CCM inaona ushauri wa wanasiasa na vyama vya siasa, hauna maana?

Ukikatana mijafala ya kisiasa maana yake umechagua vurugu. Je, huko ndiko CCM inataka nchi iende?
KKKT na CCM walishirikishwa kama Wadau wa Siasa na hapo Ndio kwenye tatizo la Msingi

Usisahau mrithi wa Dr Slaa pale Karatu alikuwa Mchungaji wa KKKT
 
Kuna aliyewazuia wananchi wa kawaida kutoa maoni Yao?. Je maoni kwenye rasimu ya Warioba hawakuwa wananchi wa kawaida?
Hakuna aliyewazuia Ndio sababu hawalalamiki

Wariioba alikusanya maoni ya Katiba Mpya siyo marekebisho ya sheria za Uchaguzi
 
Kwa mwenye akili, ni dharau kubwa mtu akakuita akasema anataka kuusikia ushauri wako, kumbe mtu huyo alikwishafanya maamuzi yake tayari. Kwa hiyo ushauri wako kwake inakuwa ni kukupotezea muda kwa kuwa alikwishakupuuza. Lakini akaona haitoshi kukupuuza, akataka pia kukuonesha wazi namna anavyokudharau, kwa kutozingatia ushauri wako wote. Hicho ndicho kilichofanywa na CCM, Serikali yake na Bunge lake.

CCM imewafanya watanzania wote hawana maana, hawana akili, hawana haki ya kusikilizwa.

Kwanza Serikali iliwahadaa wananchi kuwa eti inataka kubadilisha sheria ya uchaguzi na ya Tume ya Uchaguzi ili kuongeza demokrasia. Nasema kuwa ni hadaa kubwa kwa sababu miswada hiyo ya sheria haikuwa imejibu malalamiko ya msingi ya wananchi.

Lakini wakaendeleza hadaa kwa kupitisa wabunge wao. Kamati ya Bunge ikawatangazia wananchi kuwa inapokea maoni kuhusiana na miswada miwili ya sheria zinazohusiana na masuala ya uchaguzi. Wananchi wengi kwa kujua umuhimu wa uchaguzi walijitokeza kwenda kutoa maoni yao.

Jambo moja ambalo liliongelewa sana na wadau mbalimbali, wakiwemo viongozi wa dini, vyama vya siasa, NGOs na wananchi mmoja mmoja, ni kutaka wakurugenzi wa Wilaya na Halmashauri? ambao kimsingi ni wateule wa Rais, wasiwe wasimamizi wa uchaguzi. Wadau hawa wakashauri Tume ya uchaguzi iwe na watumishi wake kwaajili ya kusimamia uchaguzi. Jambo la pili lililoshauriwa na wadau wengi ni uchaguzi wa Serikali za mitaa kusimamiwa na Tume ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI. Na jambo la tatu lililoshauriwa na wadau wengi ni kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi kwa maana ya tangu kuundwa kwake, wajumbe wake na utendaji wake wa kazi.

Maoni haya yote ya wananchi, yamepuuzwa, na miswada wameipitisha kama walivyoiandaa na kupanga bila ya kuzingatia maoni ya wananchi. Hii ni dharau kubwa kwa wananchi wote.

Jambo pekee walilolifanya ni kubadilisha tu jina la Tume ya Uchaguzi eti iitwe Tume Huru ya Uchaguzi. Hii ni sawa muwe na jirani jambazi. Mkawa na malalamiko huyo jambazi aondolewe mtaani penu. Halafu anayetakiwa kumwondoa, badala ya kumwondoa, akasema kwamba huyo bwana kuanzia leo asiitwe jambazi bali aitwe Raia Mwema.

Wito wangu kwa wananchi wote wenye mapenzi mema kwa Taifa letu, anayekupuuza na kukudharau, nawe umfanyie vivyo hivyo. Tuipuuze CCM, tuipuuze Serikali yake, tulipuuze Bunge lake, tuwapuuze na viongozi wao wote.

Waungwana wanasema mheshimu anayekuheshimu. Asiyekuheshimu, anayekupuuza, nawe mtende vivyo hivyo.

Na kuwaonesha kuwa tumewapuuza, tuungane kwenye maandamano yoyote yale yatakayoandaliwa na chama chochote cha siasa au taasisi nyingine yoyote kuikataa miswada hiyo, kuukataa ulaghai wa CCM na taasisi zake. Ndugu wananchi, hawa watu hawatatuheshimu hata siku moja bila ya sisi wenyewe kuwathibitishia kuwa tunastahili na tuna haki ya kuheshimiwa na kuthaminiwa.

Mabadiliko ya sheria, kutoka kwenye sheria mbovu kwenda kwenye sheria bora, kutoka kwenye katiba mbaya kwenda kwenye katiba nzuri, hatuyahitaji kwaajili ya chama fulani au taasisi fulani bali kwaajili ya nchi yetu na jamii nzima ya Watanzania wa leo na kesho.

Wanaotengeneza sheria kwaajili ya kujinufaisha wao binafsi au chama chao au familia zao, ni wahuni, na wahuni hawastahili kuheshimwa wala kusikilizwa. Mungu wetu tunaomba utujalie ujasiri wa kupigania kilicho chema kwa Taifa letu, na katika hilo tunaomba uwe nasi.

Sijawahi kushiriki maandamano ya kudai haki. Safari hii nitashiriki. Nimeamua kushiriki yale yaliyoandaliwa na CHADEMA kule Mbeya. Sitashiriki kama maandamano ya CHADEMA bali kama maandamano ya kupinga hila za watu waovu wasioraka nchibyetu iwe na mifumo mizuri ya demokrasia, utawala na sheria. Ni maandamano dhidi ya wanaoliangamiza Taifa.
Tungepuuzwa tu ilikuwa ni bora zaidi lakini wananchi tunafanywa wajinga. Na viongo CCM wanajua jinsi ya kutumia ujinga na njaa zetu kutimiza malengo na maslahi yao.

Umetaja Bunge, bunge lipi? Hili la akina Dr. Musukuma, Taletale na Kibajaji? You can't be serious, bunge limehamia kwenye mitandao ya kijamii na Chadema. Kiasi fulani hawa wakipiga kelele kidogo wanasikilizwa kwa mbali. Rejea tozo, sakata la bandari na mswada wa sheria ya rasilimali za nchi uliolenga kubadilishwa ili kuaccommodate mashariti tuliyopewa na Waarabu kwenye mkaba wa DPW. Bunge la wabunge walioteuliwa na kupitishwa kwa nguvu na JPM ni rubber stamp ya Rais na serikali yake, na ktk hili spika Tulia alisema wazi tangu mapema.
 
Kwa Akili ya Kawaida CCM haiwezi Kupokea ushauri wa Wapinzani

Maoni ya muswada wa Mabadiliko ya sheria za uchaguzi kimsingi yalitolewa na Wadau wa Siasa na siyo Wananchi wa Kawaida
Tatizo lenu hata maoni ya wananchi yakiwa msivyopenda mnayatupia kwenye kapu la maoni ya wapinzani, kwenu kila maoni yanayokwenda kinyume na vile mnavyopenda yanaitwa ya wapinzani, hata kama aliyetoa akiwa hana chama.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mtu kukuomba ushauri haimaanishi ataenda kufanya kama ulivyosema, unaweza mshauri na akaenda fanya opposite, ni kawaida na hutakiwi nuna
 
Tatizo lenu hata maoni ya wananchi yakiwa msivyopenda mnayatupia kwenye kapu la maoni ya wapinzani, kwenu kila maoni yanayokwenda kinyume na vile mnavyopenda yanaitwa ya wapinzani, hata kama aliyetoa akiwa hana chama.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Maoni ya Wananchi hutolewa Ndani ya Chama kupitia Idara ya Itikadi na Uenezi
 
Back
Top Bottom