Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,153
Wadau, nina rafiki yangu mmoja tunafanya nae kazi, leo kaja na story za ajabu kuhusu ulalaji wake kitandani, yeye na mkewe. Kaja kachelewa kazini, kisa kalala saa 10 ya usiku, baada ya kuuliza sababu ndipo akashuka na mzigo wa lawama dhidi ya mkewe.
Anavyodai ni kua yeye anapenda kulala mwanzoni kabisa mwa kitanda, yaani anameza kama futi 2za mwanzo, sasa anacholalamika eti mkewe badala ya kuacha gap katikati la kama futi 2 hivi kisha akamalizia zile 2 za mwisho, ye hua anambana kabisa mpaka saa zingine anataka kudondoka. Mpaka saa zingine hua anamuuliza mkewe kama ile nafasi ya ukutani anamuwekea mtu mwingine aje kulala.
Anafika mbali zaidi pale anapodai kua anashindwa hata kupumua usiku maana akivuta au kutoa pumzi basi kunakua na obstacle ya mtu karibu hivyo anapata tabu.
Anazidi kukolezea kua hata wakati wa joto ambapo miili ikigusana inatoa jasho, bado mkewe anapenda kumbana kabisa badala ya kila mtu kulala kwa kujiachia.
Anasema saa zingine akimaliza "shughuli", anapenda apate upepo na hewa ya kutosha ili kupumzisha mwili lakini mkewe bado atamganda.
Nimeshindwa kumshauri maana sijaoa, ndio nikaileta hapa mnisaidie nimfikishie.
Anavyodai ni kua yeye anapenda kulala mwanzoni kabisa mwa kitanda, yaani anameza kama futi 2za mwanzo, sasa anacholalamika eti mkewe badala ya kuacha gap katikati la kama futi 2 hivi kisha akamalizia zile 2 za mwisho, ye hua anambana kabisa mpaka saa zingine anataka kudondoka. Mpaka saa zingine hua anamuuliza mkewe kama ile nafasi ya ukutani anamuwekea mtu mwingine aje kulala.
Anafika mbali zaidi pale anapodai kua anashindwa hata kupumua usiku maana akivuta au kutoa pumzi basi kunakua na obstacle ya mtu karibu hivyo anapata tabu.
Anazidi kukolezea kua hata wakati wa joto ambapo miili ikigusana inatoa jasho, bado mkewe anapenda kumbana kabisa badala ya kila mtu kulala kwa kujiachia.
Anasema saa zingine akimaliza "shughuli", anapenda apate upepo na hewa ya kutosha ili kupumzisha mwili lakini mkewe bado atamganda.
Nimeshindwa kumshauri maana sijaoa, ndio nikaileta hapa mnisaidie nimfikishie.