Wadau, nina rafiki yangu mmoja tunafanya nae kazi, leo kaja na story za ajabu kuhusu ulalaji wake kitandani, yeye na mkewe. Kaja kachelewa kazini, kisa kalala saa 10 ya usiku, baada ya kuuliza sababu ndipo akashuka na mzigo wa lawama dhidi ya mkewe.
Anavyodai ni kua yeye anapenda kulala mwanzoni kabisa mwa kitanda, yaani anameza kama futi 2za mwanzo, sasa anacholalamika eti mkewe badala ya kuacha gap katikati la kama futi 2 hivi kisha akamalizia zile 2 za mwisho, ye hua anambana kabisa mpaka saa zingine anataka kudondoka. Mpaka saa zingine hua anamuuliza mkewe kama ile nafasi ya ukutani anamuwekea mtu mwingine aje kulala.
Anafika mbali zaidi pale anapodai kua anashindwa hata kupumua usiku maana akivuta au kutoa pumzi basi kunakua na obstacle ya mtu karibu hivyo anapata tabu.
Anazidi kukolezea kua hata wakati wa joto ambapo miili ikigusana inatoa jasho, bado mkewe anapenda kumbana kabisa badala ya kila mtu kulala kwa kujiachia.
Anasema saa zingine akimaliza "shughuli", anapenda apate upepo na hewa ya kutosha ili kupumzisha mwili lakini mkewe bado atamganda.
Nimeshindwa kumshauri maana sijaoa, ndio nikaileta hapa mnisaidie nimfikishie.
nimeshamwambia akamwambie rafikie akue zaidi kindoa!akiwa kweli ni mwanaume anayejitambua uanamume wake u wapi atajirekebisha!Mafundisho ya ndoa yanahitajika sana maana hayo wala sio ya kuja kusema mbele za watu wala kumhadithia mwenzio
Wengine wanalitafuta hilo kumbatio hawalioni yeye analalamika Blaki Womani, Kaunga, gfsonwin, snowhite hebu mpeni mafunzo ya nini maana ya ndoa huyu jamaa maana anaikosea ndoa maana yake
Sio mimi kaka!!Hii ishu inakuhusu,,kwanini usifunguke tu kwamba na wewe?
Kwanza unatumia jina feki, sa unaogopa nini?
Wadau, nina rafiki yangu
mmoja tunafanya nae kazi, leo kaja na story za ajabu kuhusu ulalaji wake
kitandani, yeye na mkewe. Kaja kachelewa kazini, kisa kalala saa 10 ya
usiku, baada ya kuuliza sababu ndipo akashuka na mzigo wa lawama dhidi
ya mkewe.
Anavyodai ni kua yeye anapenda kulala mwanzoni kabisa mwa kitanda, yaani
anameza kama futi 2za mwanzo, sasa anacholalamika eti mkewe badala ya
kuacha gap katikati la kama futi 2 hivi kisha akamalizia zile 2 za
mwisho, ye hua anambana kabisa mpaka saa zingine anataka kudondoka.
Mpaka saa zingine hua anamuuliza mkewe kama ile nafasi ya ukutani
anamuwekea mtu mwingine aje kulala.
Anafika mbali zaidi pale anapodai kua anashindwa hata kupumua usiku
maana akivuta au kutoa pumzi basi kunakua na obstacle ya mtu karibu
hivyo anapata tabu.
Anazidi kukolezea kua hata wakati wa joto ambapo miili ikigusana inatoa
jasho, bado mkewe anapenda kumbana kabisa badala ya kila mtu kulala kwa
kujiachia.
Anasema saa zingine akimaliza "shughuli", anapenda apate upepo na hewa
ya kutosha ili kupumzisha mwili lakini mkewe bado atamganda.
Nimeshindwa kumshauri maana sijaoa, ndio nikaileta hapa mnisaidie
nimfikishie.
Huwa anataka amwamngushie uvunguni mmewe