Kitabu Cha Abdulwahid Sykes Kimewasili

Kitabu Cha Abdulwahid Sykes Kimewasili

Mzee,

Wewe wazee wako hawakuwa na Jina la Ukoo.

Maana naona unaitwa Mohamed Said, majina ya Kiarabu.

Jamii yako haikuwahi kuwepo kabla ya ujio wa Mwarabu??

Maana tunajua Wazarami, Wanayakyusa, Wadengereko, Wamatumbi walikuwa na majina yao.
Mpwimbe,
Hili la majina ya wazee wangu na Uarabu yana uhusiano gani na mjadala huu?

Naweza kukupa majina ya vizazi saba nyuma hadi kwa wazee kutoka Manyema, Congo.
 
Mpwimbe,
Hili la majina ya wazee wangu na Uarabu yana uhusiano gani na mjadala huu?

Naweza kukupa majina ya vizazi saba nyuma hadi kwa wazee kutoka Manyema, Congo.
Kumbe kwenu Kigoma?

🤣🤣🤣🤣

Watu wa Kigoma ni changamoto sana
 
Kumbe kwenu Kigoma?

🤣🤣🤣🤣

Watu wa Kigoma ni changamoto sana
Mpwimbe,
Hapana mimi ni Mmanyema lakini nimezaliwa Dar es Salaam na wala sijapata kufika Kigoma.
 
Hapa jamvini kumekuwa na mjadala mkali kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza kitabu kitapatika lini baada ya kuwa "out of print" kwa muda mrefu.

Nina furaha kuwafahamisha kitabu cha Abdulwahid Sykes kimewasili nchini na kwa sasa kinapatika Ibn Hazm Media Center Msikiti wa Manyema.

Mipango inafanyika In Shaa Allah kukitawanya kwenye maduka yao mengine Msikiti wa Mtoro, Mtambani na Kichangani.

View attachment 3623969
Unawapambia waislamu ili ionekane kuwa wana mchango mkubwa sana katika upatikanaji wa uhuru..
Hapo unaleta udini mkuu..
 
Kwanza kwanini kiunauzwa msikitini?
Kashang...
Nimejibu hili swali mara nyingi kuwa kitabu hakiuzwi misikitini kitabu kipo katika maduka ya Ibn Hazm Media Center na halikadhalika Mkuki na Nyota, Samora Avenue.

Cathedral Bookshop ni duka la vitabu la Wakatoliki ndiyo tuseme vitabu vinauzwa makanisani?
 
Kwa Mzee Mohammed jambo likifanywa na Mwislamu ni la Mwisalamu ila likifanywa na wa imani nyingine ni la Watanganyika wote.

Kwanini wakina Mzee Sykes tusiwatambue kama wapigania Uhuru na waasisi wa hili Taifa badala ya kuwabrand kama watu wa dini? Kuna ubaya gani Sheikh wangu?
 
Unawapambia waislamu ili ionekane kuwa wana mchango mkubwa sana katika upatikanaji wa uhuru..
Hapo unaleta udini mkuu..
Kashang...
Bahati mbaya kwa mwenye kudhani ipo faida katika kufuta mchango wa Waislamu katika kupigania uhuru.
 
Dallas,
Hapo kuna vitabu kuanzia shule ya msingi, sekondari hadi Chuo Kikuu.

Kitabu cha Chuo Kikuu ni hiyo Dictionary of African Biography (DAB) wamechapa Oxford University Press New York na kitabu cha Abdul Sykes kimechapwa na Minerva Press, London na Uamuzi wa Busara Abantu Publishers, Nairobi.

Vilivyobaki ni vya shule za msingi na sekondari.

Lakini ninacho kingine biography ya Sal Davis (Shariff Salum Abdallah) hiki kipo Amazon:

View attachment 3624061
Chuo gan au coz gani gani chuoni wanatumia icho kitabu cha abdul skys cjui?
 
Kinauzwa misikitini; means, walengwa wanunuzi ni Waislamu.
 
Kinauzwa misikitini; means, walengwa wanunuzi ni Waislamu.
Blue...
Kitabu hiki kina miaka 28.
Kimetoka kwa Kiingereza mara ya kwanza 1998.

Unakiuza msikiti gani ulio na wasomaji wa Kiingereza?

Tafsiri ikafanywa mwaka wa 2002 na kitabu kikachapwa
na Phoenix Publishers, Nairobi.

Kuanzia hapa kitabu hiki kikaanza kupata umaarufu na ndiyo
leo tunatazama mbele toleo la tano.

Kitabu hakiuzwi misikitini lakini ikiwa mnapenda iwe hivyo mbona
mimi nashukuru kwa kuwa mmekipa kitabu ''publicity'' kubwa na
ya bure.

Lakini nadhani unajua kuwa pale Kanisa la Mtakatifu Joseph kuna
Cathedral Bookshop.

Kitabu cha Padri Sivalon kikiuzwa Cathedral Bookshop.
Je vitabu vinauzwa kanisani na kanisa?
 
Hapa jamvini kumekuwa na mjadala mkali kuhusu historia ya uhuru wa Tanganyika.

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza kitabu kitapatika lini baada ya kuwa "out of print" kwa muda mrefu.

Nina furaha kuwafahamisha kitabu cha Abdulwahid Sykes kimewasili nchini na kwa sasa kinapatika Ibn Hazm Media Center Msikiti wa Manyema.

Mipango inafanyika In Shaa Allah kukitawanya kwenye maduka yao mengine Msikiti wa Mtoro, Mtambani na Kichangani.

View attachment 3623969
Kwanini kinauzwa misikitini tu ,badala ya maduka ya vitabu vya wazi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom