Kiswahili ni lugha ya watu gani?

Barubaru

JF-Expert Member
Apr 6, 2009
7,161
2,323
Kiswahili ni lugha ya watu gani?

Risala enuka hima, sikae 'kataghafali
N'na jambo 'takutuma, ubalegheshe suali
Nipate jawabu njema, yenye amani na kweli
Nauliza Kiswahili, ni lugha ya watu gani?

2
Lugha nyingi duniyani, zatamkwa mbalimbali
Na zote ulimwenguni, zina wenyewe mahali
Si Hindi Si Uzunguni, mewaumbia Jalali
Jee hichi Kiswahili, ni lugha ya watu gani ?

3
Wakamba wana kikwao, lugha yao ya asili
Na Wazungu piya nao, wana zao mbalimbali
Na Wameru wana yao, wengine ni Wasomali
Jee hichi Kiswahili, ni lugha ya watu gani ?

4
Wahindi wana Kihindi, kwa kabila mbalimbali
Na Wanandi ni Kinandi, ndizo zao akuwali
Wengine ni Wakilindi, wana yao ya asili
Jee hichi Kiswahili, ni lugha ya watu gani?

5
Kuuliza Si ujinga, musinifanye jahili
Nautafuta niuwanga, tuzinduwane akili
Ndipo shairi hatunga, kubaleghesha suali
Nielezwe Kiswahili, ni lugha ya watu gani?

6
Mara nyingi husikiya, kuwa hichi Kiswahili
Hakina mtu mmoya, ambaye ni chake kweli
Na wengine huteteya, kina wenyewe asili
Ndipo ha'mba Kiswahili, ni lugha ya watu gani?


7
Masai ana kikwao, lugha ya tangu azali
Na Mahara wana yao, wengine Mashelisheli
Na Waluo lugha zao, Si sawa na Maragoli
Jee hichi Kiswahili, ni lugha ya watu gani?
8
Na jamii wengineo, wana lugha mbalimbali
Na kujuwa ya wenzao, ni kujifunza ya pili
Lakini wana na zao, lugha za tangu asili
Jee hichi Kiswahili, ni lugha ya watu gani?
9
Sasa ambalo nataka, kwa wenye kujuwa hili
Wa Kenya na Tanganyika, na walo kulla mahali
Nipani ilo hakika, tubalegheshe ukweli
Nambiyani Kiswahili, ni lugha ya watu gani?
10
Miye mefikiri mno, kuamuwa jambo hili
Na huona lugha hino, lazima ina asili
Kwa sababu kulla neno, lina mwanzo wa usuli
Ndipo ha'mba Kiswahili, hi lugha ya watu gani?
11
Na iwapo hivi sivyo, niliyyoamuwa hili
Nionyeshani viliyyo, mubainishe ukweli
Nijuwe ambavyo ndivyo, tutowane mushkili
Kifunuke Kiswahili, ni lugha ya watu gani?
12
Na iwapo atakuja, wa kunijibu suali
Namuomba jambo moja, twambiyane kiakili
Tusionyane miuja, jambo nisilo kubali
N'anambiye Kiswahili, ni lugha ya watu gani?
 
Barubaru ndugu yangu, nimelisikia swali,
Naona una uchungu, ulioanzia mbali,
Tangu enzi za ukungu, linakusumbua hili,
Ila tuliza akili, tulione kiundani.


Wakisema Kiswahili, "HICHI" ni cha watu gani,
HICHI ni neno dhalili, tumia "HIKI" nadhani,
Ila turudie swali, haswa ni cha watu gani,
Nafikiri ni vigumu, kujua waanzilishi.


Chazungumzwa Mrima, Mombasa hata Unguja,
Pwani yote kinavuma, kwa mbwembwe na kwa lahaja,
Na bara hata Musoma, kote wanakibwabwaja,
Nafikiri ni vigumu, kujua waanzilishi.


Kina mengi makusanyo, ya maneno mbalimbali,
Wa'rabu pia Wayao, Wandengereko Wandali,
Wote wametia yao, kwa lugha kuipa hali,
Nafikiri ni vigumu, kujua waanzilishi.


Kwa leo ninanyamaza, nitakuja tena kesho,
Nitazidi kuyawaza, wote tupate fundisho,
Ila usijenyamaza, kwa hii yangu mipasho,
Endelea kuuliza, mwanzilishi wake nani?
 
Wakisema Kiswahili, "HICHI" ni cha watu gani,
HICHI ni neno dhalili, tumia "HIKI" nadhani,
Ila turudie swali, haswa ni cha watu gani,
Nafikiri ni vigumu, kujua waanzilishi.


Chazungumzwa Mrima, Mombasa hata Unguja,
Pwani yote kinavuma, kwa mbwembwe na kwa lahaja,
Na bara hata Musoma, kote wanakibwabwaja,
Nafikiri ni vigumu, kujua waanzilishi.


Kina mengi makusanyo, ya maneno mbalimbali,
Wa'rabu pia Wayao, Wandengereko Wandali,
Wote wametia yao, kwa lugha kuipa hali,
Nafikiri ni vigumu, kujua waanzilishi.


Kwa leo ninanyamaza, nitakuja tena kesho,
Nitazidi kuyawaza, wote tupate fundisho,
Ila usijenyamaza, kwa hii yangu mipasho,
Endelea kuuliza, mwanzilishi wake nani?



Daima unapotwanga, ni lazima kupepeta,
Kutenga chuya na chenga, ungo utaukamata,
Hapa ukishaboronga, mchele hataupata,
Nambiyani Kiswahili, ni lugha ya watu gani?


Ni lugha ya watu gani?, nambieni kiswahili.
Hata mimi wa omani,Kuongea ni halali.
Nasriyah wa yemeni, anatamba kila hali.
Kiarabu chetu sisi, kiswahili ni cha nani?

Kwa siri yake mtungi, aijuaye ni kata,
Na nyumba bila msingi, utapasuka ukuta,
Kila palipo na wengi, na mambo ya yatambata,
Kiarabu ni cha kwetu, kiswahili ni cha nani?


Tamati ndio akhiri, na jina langu ni hili
Hamza wa Yusufali ,Al Naamani la pili
BARUBARU mashuhuri, makazi yangu Qatari
Kiarabu lugha yetu, kiswahili ni cha nani?


Dr Hamza Yusuf Al Naamany(Barubaru)
Doha. Qatar




 
Miye mefikiri mno, kuamuwa jambo hili
Na huona lugha hino, lazima ina asili
Kwa sababu kulla neno, lina mwanzo wa usuli
Ndipo ha'mba Kiswahili, hi lugha ya watu gani?
11
Na iwapo hivi sivyo, niliyyoamuwa hili
Nionyeshani viliyyo, mubainishe ukweli
Nijuwe ambavyo ndivyo, tutowane mushkili
Kifunuke Kiswahili, ni lugha ya watu gani?
12
Na iwapo atakuja, wa kunijibu suali
Namuomba jambo moja, twambiyane kiakili
Tusionyane miuja, jambo nisilo kubali
N'anambiye Kiswahili, ni lugha ya watu gani?

Kwa kweli wewe ni mjuzi wa Lugha ya kiswahili. nakufananisha na Marhemu Shaaaban Robert.


Daima unapotwanga, ni lazima kupepeta,
Kutenga chuya na chenga, ungo utaukamata,
Hapa ukishaboronga, mchele hataupata,
Nambiyani Kiswahili, ni lugha ya watu gani?

Ni lugha ya watu gani?, nambieni kiswahili.
Hata mimi wa omani,Kuongea ni halali.
Nasriyah wa yemeni, anatamba kila hali.
Kiarabu chetu sisi, kiswahili ni cha nani?

Kwa siri yake mtungi, aijuaye ni kata,
Na nyumba bila msingi, utapasuka ukuta,
Kila palipo na wengi, na mambo ya yatambata,
Kiarabu ni cha kwetu, kiswahili ni cha nani?


Tamati ndio akhiri, na jina langu ni hili
Hamza wa Yusufali ,Al Naamani la pili
BARUBARU mashuhuri, makazi yangu Qatari
Kiarabu lugha yetu, kiswahili ni cha nani?


Dr Hamza Yusuf Al Naamany(Barubaru)
.

sasa vp tena Dr unakikana kiswahili?
 
Barubaru nami nitarudi kama Malenga na majibu ya kishairi - ila kwa sasa naomba niweke jibu hili la kiinsha:

Nukuu zifuatazo kutoka kwenye kitabu cha 'Swahili Origins' - na hasa utangulizi wake unaosema 'The Problem of Swahili Identity' - kilichotungwa na James De Vere Allen na kuchapishwa na East African Educational Publishers mwaka 1993 kinaelezea utete na utata wa wasifu wa waasisi, wamiliki na watumiaji wa Kiswahili:

"For as long as written records exist, groups of Swahilis have described themselves, not only as Mombasans (Swahili waMvita), Pateans (waPate), Kilwans (waKilwa) or whatever, but also as Arabs (waArabu), Persians (waShirazi), or something else - even, in at least one place, Portuguese (waReno) - rather than as Swahilis, and many still do so. Indeed, it is doubtful whether even today most of the people would in all contexts accept the name Swahili" (p. 1).

"Swahilis do share a language, though with considerable dialectal differences; but efforts to trace their origin and early history solely in terms of the source and development of this language are at best misleading. They also share a culture, though with great regional and some class variation. Yet ironically it is cultural differences which Swahilis themselves most often use to declare others 'not real Swahilis' (si waSwahili haswa). Traditionally the Swahilis themselves were certain that their territory extended somewhere near Kiwaiyu, in the north of Lamu...to Tunge, not far south of the Rovuma River ...and included the offshore islands along this coast and the Comoros . But in practice they often spilled over to the north, south or...west of these territories, while others interpenetrated them, so territory is of little use to define Swahili identity. This leaves us with 'shared historical experience'. On the face of it, there is no single, dramatic historical experience or series of experiences whose legacy enables Swahilis to define themselves as, for instance, the legacy of the American War of Independence permits Americans to define themselves...And yet the inability to discern any historical experience shared by all Swahilis is in large measure due to our failure to look at them as a historical people at all..." (p. 2)

"For all that Swahili identity is elusive, it is only relatively recently that Western historians have questioned their historical importance, and that some have queried their very existence. The growth of this anti-Swahili prejudice is directly connected with the rise of an 'Arab Myth' of East African coastal history. Early European visitors to East Africa had no difficulty in recognizing a large and important Swahili community with its own rich culture, quite separate from and unrelated to a second group which comprised recent immigrants from Arabia and the Gulf...The Englishman Burton was the first to make a serious attempt to alienate the Swahilis from their history. But when he first visited East Africa in the 1840s and 1850s they were still too large a community for their name to be ignored; and he himself was too honest and acute an observer to omit certain facts and traditions about them which fit ill with their later image..." (pp. 2-3)

"To most Western Scholars [in the 1800s], race (and in Africa , tribe) were paramount. It was of course, the era of the Hamitic Myth, and of countless other theories about genetic difference linked with Social Darwinism. Culture in Africa was seen as chiefly a function of race and tribe. Naturally the Swahilis, who had come to regard themselves in cultural rather than racial terms, and whose unity melted away once racial and tribal categories were superimposed upon them, were one of the first and most serious casualties of this way of thinking. They were regarded as inferior on two separate and not entirely compatible grounds: first, because they were 'cross-bred' Arab and African, a 'half-caste' or 'mongrel' race, and it was held that such races must be in some sense inferior to 'pure-bred' ones. Secondly, they were regarded as inferior in so far as the 'superior' Arab blood in their veins had been diluted by that of 'inferior' Africans..." (p. 3)

"It did indeed seem best, from the viewpoint of many [colonial] adminstrators, that the Swahilis should simply disappear. And in adminstrative terms they very nearly did. But one or two problems had to be cleared up before this could happen. First there was the question of their history. The coast was dotted with stone-built ruins, including some very impressive ones, which the Swahilis claimed had been constructed by their forefathers. Burton had begun the process of disinheriting them from this legacy, a process which now gained momentum...The next problem was what to call those residual Swahilis who, for one reason or another, could not plausibly be called 'Arabs' and could not be fitted into any African tribal group either. A solution to this was found in the label 'Shirazi'. 'Shirazi' sounded in some obscure way, 'purer' and less African than 'Swahili', with some connotations of Persian ancenstry at some period in the remote past..." (p. 4)

"To the assertion, 'There is no such person as a Swahili', there has always been a very simple retort: 'Who, in that case, developed the Swahili language ["a Bantu language [- "not a creole or pidgin or 'hybrid' in any other sense" (p. 12) -] with a proportion of Arabic loanwords" (p. 10)], and who wrote and read or sang Swahili poetry?" (p. 11)
 
Kiswahili lugha yetu, Wabara na Visiwani
Inavuma hapa kwetu, hadi huko ghaibuni
Utamu wake Kibantu, maneno yake yakini
Imekopa vya Uarabu, navyo vya Jerumani

Itaendelea...
 
Kiswahili lugha yetu, Wabara na Visiwani
Inavuma hapa kwetu, hadi huko ghaibuni
Utamu wake Kibantu, maneno yake yakini
Imekopa vya Uarabu, navyo vya Jerumani

Wabara ni watu gani,
wavisiwani ni nani,
 
Itaendelea...

Kiswahili lugha yetu, Wabara na Visiwani
Inavuma hapa kwetu, hadi huko Ghaibuni
Utamu wake Kibantu, maneno yake yakini
Imekopa vya Uarabu, navyo vya Jerumani

Uswahili ni utu, nakwambia bila matani
Kiswahili chao watu, we chakwashia nini
Enda kacheze upatu, tuachie si tughani
Lugha yetu Ubuntu, kamwe haiwi upijini

Kiswahili siyo kitu, sipojua kwa undani
Tadhani ni Kisutu, shairi la Uswahilini
Bongo ikiwa butu, tajuaje yake mizani
Vina vyenye kutu, je utaviona upenuni

Ukirioli siyo yakwetu, hii lugha amini
Zitamu lafuzi zetu, lahaja nazo makini
Tujifunze lugha yetu, na siache asilani
Wete hadi Meatu, Utanzania uwe shani
 
Kiswahili lugha yetu, Wabara na Visiwani
Inavuma hapa kwetu, hadi huko ghaibuni
Utamu wake Kibantu, maneno yake yakini
Imekopa vya Uarabu, navyo vya Jerumani

Itaendelea...

Companero mkuu, hakika umejaribu
Umetoka kijukuu, bila hata kuharibu
Ahsante kwazo nukuu, za kutoka ughaibu
Tuzidi kuutafuta, wapi ukweli ulipo.
 
campanero ujajibu swali. Unaona mwenzako ameweka bayana anauliza Kiarabu ni cha waarabu, kihindi ni cha wahindi. sasa unaposema kiswahili cha watanzania wa bara na visiwani. Vipi mombasa, lamu, pate ambako wanaongea kiswahili.

MIE SIJALIZIKA NA JIBU LAKO NAONA KAMA UMEPONDANGA PONDANGA TU
Pitia suala hapa

Daima unapotwanga, ni lazima kupepeta,
Kutenga chuya na chenga, ungo utaukamata,
Hapa ukishaboronga, mchele hataupata,
Nambiyani Kiswahili, ni lugha ya watu gani?

Ni lugha ya watu gani?, nambieni kiswahili.
Hata mimi wa omani,Kuongea ni halali.
Nasriyah wa yemeni, anatamba kila hali.
Kiarabu chetu sisi, kiswahili ni cha nani?

Kwa siri yake mtungi, aijuaye ni kata,
Na nyumba bila msingi, utapasuka ukuta,
Kila palipo na wengi, na mambo ya yatambata,
Kiarabu ni cha kwetu, kiswahili ni cha nani?


Tamati ndio akhiri, na jina langu ni hili
Hamza wa Yusufali ,Al Naamani la pili
BARUBARU mashuhuri, makazi yangu Qatari

Kiarabu lugha yetu, kiswahili ni cha nani?


Dr Hamza Yusuf Al Naamany(Barubaru)
Doha. Qatar

nakufagilia Dokta wewe ni mahiri wa lugha ya kiswahili.
 
campanero ujajibu swali. Unaona mwenzako ameweka bayana anauliza Kiarabu ni cha waarabu, kihindi ni cha wahindi. sasa unaposema kiswahili cha watanzania wa bara na visiwani. Vipi mombasa, lamu, pate ambako wanaongea kiswahili. MIE SIJALIZIKA NA JIBU LAKO NAONA KAMA UMEPONDANGA PONDANGA TU.

Mkuu swali limejibiwa. Muuliza swali karidhika. Kiswahili cha 'Waswahili'. Wapwani na Bara. Na Visiwani pia. Lamu nako Lubumbashi. Mombasa hadi Mbarara. Hata huko Ughaibuni. Wabantu na 'Swahil'. Kiswahili lugha yetu.
 
Back
Top Bottom