sijui kama umenielewa..... au umekataa kunielewa,Hoja imetoka kwa kukurupuka, ngoja na sisi tuoneshe mwitikio huo huo.
Uingereza wapo mataahira wa kutosha, nadhani kwa ujuvi wao wa Kiingereza wanafaa kuajiriwa kuliko wasomi wetu wanaozungumza brokeni Inglish...
Si eti eh?
Kwa mawazo haya tuna kazi kubwa kufikia maendeleo, mbona hujiulizi wao walisaidiwa na nani mpaka wamefika hapo walipo, tuna kila kitu ila tumeamua kuwa masikini, misaada haisaidii kama hatuchukui hatua,Haina haja ya kufanya research kwa mambo ambayo tunayaishi. China sio Tanzania. Wale wanajitosheleza kwa teknolojia na hawana haja ya kuomba misaada kama tufanyavyo.
Ni mtumwa ndio hujifunza lugha ya bwanaake. Sisi ni wategemezi na utegemezi wetu ndio unatugharimu. Usiniambie kuwa tuna jeuri ya kujifunza kwa lugha ya kiswahili huku entry requirements za vyuo vya ulaya tunavyokimbilia kusoma vinataka uwe na intermediate level ya Kiingereza.
Achana na kampeni za kina Makih Hassan na BAKITA yao. Hapa hapa tu ukiwa huna fluency ya kiingereza hupati kazi, leo hii mtu akutie ujinga eti kiswahili, we usijidanganye.
Am not surprised! utakuta mara nyingi wasio jua kingereza ndo wakwanza kusema hatuhitaji kingereza! utajuaje kama hukuhitaji wakati hukijui?
Ukiangalia the 'bigger picture' information na elimu tunayohitaji kuendelea ipo katika lugha ya kingereza au lugha zingine zilizoendelea zaidi kama kifaransa na kichina.
wachina na wafaransa wameweza kuendelea na lugha zao kwasababu lugha zilikuwepo toka 'industrial revolution' na zimekua kwa pamoja na utandawazi, tusisahau kwamba ni wangapi duniani wanaongea kichina na kifaransa? watu zaidi ya 1 billion wanaongea na kuandika kichina na zaidi ya 500 million wanaongea kifaransa vizuri, na 1.5 billion kingereza. swahili 30 million. ila we demand to give it equal share!
Unaweza kutrain daktari/enginneer/lawyer from scrach kwa kifaransa au kichina bila kutumia neno hata moja la kingereza je itagharimu miaka mingapi na shingi ngapi kufanya hivyo kwa kiswahili?! vitu kama matokea ya research kibao zinaandaliwa kwa kingereza, sasa ebu niambieni kama huwezi ukaelewa haya matokeo si utapoteza mda kufanya research yako? ambayo ni marudio?
Mtu anasema proudly kwamba wawekezaji wakija walazimishwe kujifunza kiswahili!!! huoni kwamba ni kupoteza mda na hela kibao, we need to get our priorities right!
Tanzania is not an island but we spend so much time and enrgy trying to make it one, acting like we dont need the rest of the word, trying to impose swahili like its the corner stone to mankind! really?!
Pole. Naona umelewa kabisa na Kiingereza na kwa bahati mbaya hata mwenyewe kinakutatiza. Ukweli ni kinyume chake; kwamba wasiokijua vema Kiingereza ndiyo wanakitetea sana na kukiabudu! Kiswahili kinaangamizwa na watu kama nyinyi na ni ukweli unaouma kwamba Kiswahili hakipigi hatua kubwa kwa kukosa msukumo wa kisiasa tu, hebu tafakari hata wabunge wetu wanavyokichakachua hadharani! Watanzania wengi wanadhani kujua Kiingereza ni kuelimika na ndiyo maana watu wasiojiamini huchapia kiingereza hata cha kuvunjavunja ili angalau waonekane wasomi. Historia itawahukumu. Binafsi sina shaka kabisa kwamba Kiswahili kinaweza kutumika kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu ili mradi kipate msukumo wa dhati wa kisiasa.Tanzania is not an island but we spend so much time and enrgy trying to make it one, acting like we dont need the rest of the word, trying to impose swahili like its the corner stone to mankind! really?!
Mkuu umesema yote niliyotaka kuyasema. Inasikitisha kuona hata baada ya kujitawala kwa karibu nusu karne wapo watanzania wanaoshobokea Kiingereza! Sijui huyu masauni yuko katika nchi gani na upeo wa uelewa wake. Waswahili tunasema ukiona chaelea ujue kimeundwa; ndivyo ilivyo kwa Kiingereza. Historia inaweka wazi kuwa Kiingereza haikuwa mojawapo ya lugha kubwa hapo awali kama ilivyo sasa duniani. Waingereza kama yalivyokuwa mataifa mengi ya ulaya yalitumia kilatini na baadae Kifaransa kilikuwa lugha rasmi ya hao wanaoabudiwa na kina masauni hadi uamuzi mgumu ulipofanywa na kuamua kutumia lugha ya 'nyumbani' kwa ajili ya kufundishia. Waingereza waliienzi lugha yao na kufanya bidii ya kuikuza hadi hapa ilipofika. Si kweli eti tutapoteza hela 'kibao' au kupata hasara ya kukimbiwa na wawekezaji tukiamua kutumia kiswahili tu, bali hao wageni kwa shida zao watafanya bidii ya kujifunza ili wapate wanachokitaka! Wachina hawazungumzi Kiingereza lakini dunia nzima sasa inahaha kujifunza lugha yao ili waweze kufanya biashara nao. Si kweli kwamba lugha itakuwa kikwazo kwa wageni watakaotaka kushiriki nasi katika nyanja za kilimo, madini, biashara n.k. ati kwa sababu tu hatuzungumzi kiingereza; mbona hata wawekezaji wengi tu tunaowapata kiiingereza si lugha yao rasmi?ndugu yangu unayo yasema huyajui, hata huko nje ya nchi uliko sijui ni wapi! mimi kwa sasa niko uholanzi, hawa jamaa ni kidachi kwa kwenda mbele, kingereza kinatumika mara chache saana katika sehem maalum zinazo husisha watu wa mataifa mengine, shule zote ni kidachi, wanashangaa kwa nini sisi tunasoma kwa lugha ya kiingereza!
nimekuwa mwalim najua namna walim wanavyo pata shida kufundisha kwa kiingereza, wanafunzi wanapata shida uelewa kwa sababu wanafikiria kwanza kwa kiswahili wanatafsiri ndo waanze kupata maana, ni kosa kubwa saana tulilotenda kuacha kiswahili kisitumike ktk mashule yetu.
Mara ngapi tumeshindwa kupata tafsiri halisi ya matatizo yetu kwa kikwazo cha lugha!
Halafu kumbuka kiswahili pamoja na kudidimizwa bado ni kati ya lugha kubwa duniani inayotumika tanzania, kenya, uganda, congo, rwanda, burundi, na nchi nyingi za afrika, tunge kithamini kingeweza kutuweka pazuri. Mataifa yote yenye nguvu sasa yanatumia lugha ya kwao!
kuthamini lugha ya kigeni ni ukoloni wa aina fulan kama tutakuwa makini kuchunguza, sisemi kwamba tuache kabisa lugha za kigeni, ni muhim kujifunza kwa sababu ya globalization ila tukumbuke siyo ligha zetu!
kunamsemo unasema "kitaka kumtawala mtu haribu, utamaduni wake" kumbuka lugha ni kiungo muhim saana katika kutunza utamaduni wa mahali, nafikiri wewe pia wa weza kuwa shuhuda kwa sasa Tz tusivyo kuwa na utamaduni wa kueleweka, uzungu si uzungu! uafrika si uafrika! watu kutaka kuishi kiingereza engereza! ndio kuliko badirisha style za watu kuongea, kuvaa, kutembea na tunathamin vyovyote wanavyo fanya wazungu kwa sababu tumedharau vya kwetu! kwa mfano utashangaa dada zetu siku hizi wanalazimisha kuvaa stockings na joto la dar lilivyo!!!!!! huku wenzetu wanavaa hivo kwa sababu ya baridi!!!!!!!!!
Ninasikitika mtu anaposisitiza tujifunze lugha za kigeni kwa gharama ya lugha yetu!
Nakipenda kiswahili lugha ya nchi yangu
Pole. Naona umelewa kabisa na Kiingereza na kwa bahati mbaya hata mwenyewe kinakutatiza. Ukweli ni kinyume chake; kwamba wasiokijua vema Kiingereza ndiyo wanakitetea sana na kukiabudu! Kiswahili kinaangamizwa na watu kama nyinyi na ni ukweli unaouma kwamba Kiswahili hakipigi hatua kubwa kwa kukosa msukumo wa kisiasa tu, hebu tafakari hata wabunge wetu wanavyokichakachua hadharani! Watanzania wengi wanadhani kujua Kiingereza ni kuelimika na ndiyo maana watu wasiojiamini huchapia kiingereza hata cha kuvunjavunja ili angalau waonekane wasomi. Historia itawahukumu. Binafsi sina shaka kabisa kwamba Kiswahili kinaweza kutumika kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu ili mradi kipate msukumo wa dhati wa kisiasa.
Hydogen achana nao nao bwana usinipotezee hewa yangu nzuri ya hydrogen bure bure tu hapa tuko watu mchanganyiko ambao ht ungekaa nao darasani wangekuwa wanapata sifuri kila siku lakini huku kwenye mitandao wanajiona wajanja wanabwabwaja tu bila reference wajitahidi tu kututengenezea search engines za kiswali pia na watafute rights za kutafsir google, yahoo, na engines zingine kwa kiswahili. Hawajui ht duni inaelekea wapi wao wamepiga about turn wanaelekea kwa mababukama ni ukoloni kwanini tusivue nguo tukatembea uchi kama babu zetu? tukaishi kwenye pango tukaachana na magari tusitumie tena sahani, sufuria wala vijiko, tusisikilize mziki wala kuangalia tv, jf ifungwe, hatutaki tena computer na internet zao, madawa kama ARV hatutaki tena, treni ya dar irudishwe ilikotoka, bandari ifungwe na meli ziondoke na makontena yao ili turudi kuwa waafrika halisi na mila zetu?!!! zote hizi ni za wazungu au kuna za waafrika kati ya hivyo nilivyotaja?!
Hydogen achana nao nao bwana usinipotezee hewa yangu nzuri ya hydrogen bure bure tu hapa tuko watu mchanganyiko ambao ht ungekaa nao darasani wangekuwa wanapata sifuri kila siku lakini huku kwenye mitandao wanajiona wajanja wanabwabwaja tu bila reference wajitahidi tu kututengenezea search engines za kiswali pia na watafute rights za kutafsir google, yahoo, na engines zingine kwa kiswahili. Hawajui ht duni inaelekea wapi wao wamepiga about turn wanaelekea kwa mababukama ni ukoloni kwanini tusivue nguo tukatembea uchi kama babu zetu? tukaishi kwenye pango tukaachana na magari tusitumie tena sahani, sufuria wala vijiko, tusisikilize mziki wala kuangalia tv, jf ifungwe, hatutaki tena computer na internet zao, madawa kama ARV hatutaki tena, treni ya dar irudishwe ilikotoka, bandari ifungwe na meli ziondoke na makontena yao ili turudi kuwa waafrika halisi na mila zetu?!!! zote hizi ni za wazungu au kuna za waafrika kati ya hivyo nilivyotaja?!
Ninaomba kuanzisha hii mada baada ya kusikia kwamba kuna mahali walimu wamefukuzwa kwa sababu ya kuongea kiswahili katika mazingira ya shule.
Niseme tu kwamba naunga mkono jambo hilo kwa asilimia mia. Sababu ni hizi hapa.
1. Tutambue kuwa kiswahili ni lugha inayozungumzwa sana Tanzania na ukitoka nje ya mipaka ya Tanzania kiswahili chako unaweka mfukoni! Lazima tujufunze lugha za kimataifa(English) ili tulahisishe mawasiliano na mataifa mengine.
2. Wageni wakija Tanzania wanapata taabu kweli, matangazo ya biashara yameandikwa kwa kiswahili, barabara nazo unakuta vibao vimeandikwa kwa kiswahil mfano PITA KUSHOTO. Sasa jamani wageni wetu ambao wengi wanakuja kwa maswala ya biashara inakuwa ngumu sana.Mgeni kuendesha gari tanzania ni ngumu sana. Mgeni kufanya biashara Tanzania ni ngumu sana!! Kuna jamaa wafanyabiashara wengi sana nawafahamu wanaprefer kwenda Kenya na Uganda kuchukua bidhaa kuliko Tanzania na sababu wanazozitoa ni ugumu wa Lugha.wanasema kwenda Tanzania ni gharama zaidi maana inabidi umtafute mkalimani ambaye utamlipa.
3. Kenya inatangaza mlima kilimanjaro kwa sababu ya Lugha wanayotumia inaeleweka duniani kote. Sisi tunatangaza mlima kilimanjaro kwa kiswahili wataelewa nini wageni?
4.Tunawasanii wazuri sana wa muziki, tamthiliya, vichekesho, ambao wangesaidia sana kuitangaza nchi yetu kimataifa na wao pia kufaidika, lakini wamebaki eti wasanii wa BONGO. (Kwa wale mliobahatika kuangalia stand up Zambia kilichorushwa na Africa magic channel mtakubaliana na mimi wale jamaa 3 walioshinda sasa hivi ni comedian wakimataifa wanazunguka nchi mabalimabali sababu ni lugha tu, maana kwa ukweli hawawezi kumfikia Joti, Masanja.
5.Tuna wachungaji wazuri sana(Pastors) lakini mahubiri yao ni kwa kiswahili. T.B Joshua anajulikana kila mahali kwa sababu mahubiri yake ni ya kiingeraza. Si kwamba Joshua unaupako kuliko wengine.
6. Mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji ni kwa sababu ya lugha tunashindwa kuilewa vizuri Wawekezaji wanapokuja ilitusionekane ni mbumbumbu wa kiingereza tunabaki kusema YES, YES YES!
7. Kwa watazamaji wenzangu wa aljazeera kuna kipindi kinaitwa 'Tea cafe (kama sijakosea)kinaongelea maswala mbalimbali yanayohusu nchi husika kipindi hicho kinapofanyika. Kipindi hicho kimefanyika,Kenya, Uganda zambia lakini Tanzania hakuna na hata katika ratiba yao Tanzania haimo simply because hakuna watu kama wanasiasa na baadhi ya watu mahalufu ambao wako tayari kujadili kwa kimombo! Sasa dunia itatuelewa vipi matatizo na mipango yetu ?
Nchi nyingi sasa hivi zinajifunza Kiingera hata china taifa kubwa wako busy kujifunza kiingereza Sisi masikini wakutupwa tunangangana na kiswahili ambacho mwisho wake ni mipakani tu! Viongozi wetu lazima pia waanalie hiyo watu waanza kufundishwa kiingereza tangu chekechea, maofisini lugha ya kiingereza isisitizwe, mikutano maofisini ifanyike kwa kiingereza. WITHOUT ENGLISH YOU ARE MARGINALIZED YOURSELF