Kisugu, GB 64, Pasi Milioni na Mzaramo hawaikosoi Simba why? wamemzidi nguvu Ahmed Ally

ubarinolutu

JF-Expert Member
Oct 22, 2012
1,964
3,895
Hivi Simba ni Lini imewateua Hawa watu kuwa wasemaji wa Washabiki wa Simba, mana wao wamekuwa wakisifia Simba hata ikifungwa na na nguvu nyingi wameweka kuikosoa Yanga.

Tofauti na Mashabiki wengine wa Simba , wasemaji Hawa wa mashabiki wa Simba , wamesema haya ni moja ya matokeo ya Mpira hivyo wanasimba wazidi kuwa pamoja na kuisaport club.

Tunajua Hawa mashabiki ambao wamejipa uongozi wa kinyemela , Huwa wanalipiwa nauli, Guest, pamoja na posho ya kujikimu na viongozi waliopo madarakani Simba pamoja na wadhamini wa Viongozi hao. Ndio mana hata wafungwe vipi , watalaumu Kocha, na huwezi kusikia mashabiki Hawa wanne wakikosoa uongozi, tofauti na Mashabiki wengine wa Simba.

Mimi tabia ya Hawa jamaa inaleta sana, Msemqji wa Simba wakati mwingine amekuwa akikiri na kukosoa madhaifu ya Simba, ila Hawa machawa wa Mangungu huwezi kusikia wakikosoa hata kidogo, kwakuwa kula yao inategemea Mangungu kuendelea kuwepo madarakani hata kama amefeli.
 
Wote uliowaandika Hapo huwa nawaona kama vichaa

Wanajichetua Ufahamu kisa mambo ya simba na Yanga

MAJINGA YAO
 
Back
Top Bottom