Kisomo Ikulu Dar es salaam

Kisomo Ikulu Dar es salaam

Huyo mpangaji wa Ikulu mbona matambiko yake yote anafanyia Bagamoyo sasa kwanini anajisi IKULU yetu kwa hicho kisomo na harusi za nduguze? Hiyo ni dalili tosha ya kiongozi asiyejari maadili ya kazi yake sawa na yule marehemu aliyegeuza ofisi za hazina kuwa msikiti wake akidhani angekuwa pale milele!!

Wanamajils,
Laiti historia ya uasisi wa African Association 1929 uasisi wa TANU
1954 na kupigania uhuru wa Tanganyika ingeliandikwa kwa usahihi
wake unaostahili leo asingelitokea mtu akakejeli "visomo."

Kwani "kisomo," ni nini?
Kisomo ni dua.

Dua nayo ni kitu gani?
Dua ni maombi kwa Allah.

Kisomo au dua katika historia ya uhuru wa Tanganyika ina nafasi ya
pekee katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mikutano yote ya TANU pale Mnazi Mmoja ilikuwa ikianza kwa dua.

Vikao vyote vya TANU pale New Street katika miaka ya mwanzo ya TANU
ilikuwa inaanza kwa dua.

Katika mikutano ya Mnazi Mmoja wakati wa kudai uhuru kabla Nyerere
hajapanda jukwaani alikuwa anatanguliwa na Sheikh Suleiman Takadir
na alisoma "Surat, Fatha," yote huku wananchi wamesimama wima na
mikono yao wamenyanyua na mwisho kwa umoja wataitikia, "Amin."

Nyerere alikuwa akienda madrasa ya Mufti Sheikh Hassan bin Amir
Mtaa wa Amani akiongozana na Abdulwahid Sykes na Dossa Aziz
kwa ajili ya hili au lile katika harakati za kupambana na Waingereza.

Hawataondoka pale ila Sheikh Hassan bin Amir atanyanyua mikono na
kuomba dua.

Hii ndiyo historia ya Tanganyika ambayo leo haitakiwi na inakejeliwa.
Kejeli na kebehi hii inakuja kwa kuwa historia hii imezikwa na viongozi
wetu hawaitaki.

Wametengeneza historia yao iliyofuta haya yote.
Yapo mengi naweza kueleza lakini na tuishie hapa.
 
Madrasa. Bahati mbaya haina grade wala syllabus maalum!

Jabulani,
Madrasa ina mtaala na ina ''grades" na inatoa vyeti.

Ungelichukua tabu kidogo tu ya kuuliza hapa majlis au hata mtaani
kwako hili ungeelezwa.

Ingekuwa tunachukua juhudi ya kufanya utafiti kidogo kabla ya
kuandika tungelinda heshima zetu.

Hivi tufanyavyo tunaonekana wajinga tusiojua kitu.
Hii haipendezi.
 
Huyo mpangaji wa Ikulu mbona matambiko yake yote anafanyia Bagamoyo sasa kwanini anajisi IKULU yetu kwa hicho kisomo na harusi za nduguze? Hiyo ni dalili tosha ya kiongozi asiyejari maadili ya kazi yake sawa na yule marehemu aliyegeuza ofisi za hazina kuwa msikiti wake akidhani angekuwa pale milele!!

Bulesi,
Usimseme mtu aliyekufa utawaudhi walio hai.

"Msikiti Hazina," umemkusudia marehemu Prof. Malima.
Hakujenga msikiti na ukitaka fanya utafiti utapata ukweli.
 
Ni kweli mahapa patakatifu ndipo panapofaa kuombea dua lakini IKULU ya leo sio mahala patakatifu tena hivyo hapafai kuombea dua kwani pamenajisiwa na kuwa PANGO la wezi tena wa mchana wanaokwenda na viroba kwenda kukwapua mapesa yetu sie maskini!!

Bulesi,
Ungekuwa unafanya utafiti lau kidogo kabla hujaandika.
Hebu soma hapa chini yaliyokuwa yakifanyika Ikulu miaka ya nyuma:

"In public Mwalimu Nyerere was a fierce defender of secularism. It is therefore quite disturbing to learn that in private he championed the sectional interests of his own church. In 1970 Nyerere invited to the State House the then Secretary General of the Tanzania Episcopal Conference, Fr. Robert Rweyemamu and the Pope's Representative to Tanzania Mgr. Giovano Cerrano. Among otherthings Nyerere told his guests that he was doing every thing in his power to strengthen Catholicism in the country. He also requested them to go and inform the Bishops that he had established a Department of Political Education in TANU (the ruling and only political party at that time), and that he had appointed a Christian Reverend to head that department, not because of his competence as a political analyst, but because of his strong faith as a Christian. His responsibility was to guide and control the political direction of the party. He also informed them that in the Party's National Executive Committee (NEC) two members were Reverends. He said he believed that was the best way of ensuring that the party got good people(van Bergen, 1981:333-336)."

Bulesi,
Haya yamo katika kitabu hicho hapo chini ambacho kilipigwa marufuku:

514jW3SCwFL._SY344_BO1,204,203,200_.jpg
 
Hakuna mtu anayebisha kuwa Nyerere hakushirikiana na waislam na yeye mwenyewe alikiri hivyo lakini hata kama alisomewa dua na wakina Sheikh Ramiya dua hizo hazikusomwa Ikulu bali huko Bagamoyo!! Ikulu ni mahala patakatifu na sio mahala pa kufanyia shrehe za harusi kama wanavyofanya siku hizi!!

Bulesi,
Wangefanya vipi visomo Government House ilhali uhuru ulikuwa bado?
 
Mkome kuchagua wapiga vidufu kuingia ikulu

Kigogo,
Unaikebehi "dufu," kwa kuwa huijui historia ya uhuru wa Tanganyika.
Nakuwekea hapa kitu kidogo utafakari tulikotoka:

"Nyerere aliporudi Lindi mwaka 1959, TANU ilikuwa ina nguvu sana na ilikuwa imekumba kila mtu. Wale watumishi wa serikali wengi wao wakiwa Wakristo, walio kuwa wakiibeza TANU mwaka 1955 kwa sababu ilikuwa ikiongozwa na Waislam wasiokuwa na elimu, ukweli ulikuwa umewadhihirikia na sasa walikuwa wakionyesha heshima kwa chama. Hawakuwa na khiyari na ilibidi waonyeshe heshima kwa sababu bwana mwenyewe, yaani serikali ya kikoloni, ilikuwa na heshima kwa TANU. Serikali ilikuwa imetambua kuwa dhamiri ya watu ya kukataa kutawaliwa haiwezi tena kupuuzwa. Nyerere alikuwa amelihutubia Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa mara mbili, mara ya pili ikiwa mwaka 1957. Ujumbe wa TANU ulikuwa wazi, watu wa Tanganyika walikuwa tayari kujitawala. Kila siku zilivyopita ndivyo TANU ilivyopata nguvu. Rashidi Salum Mpunga, dereva wa lori, aliweza kumshawishi na akafanikiwa kumuingiza TANU mmoja wa masheikh wenye kuheshimiwa sana mjini Lindi na mshairi maarufu, Sheikh Mohamed bin Yusuf Badi. Sheikh Badi alipoingia TANU kwa ajili ya heshima yake na kukubalika na watu, idadi kubwa ya Waislam walimfuata na kukata kadi za TANU. Nyerere alipokuja Lindi kujadili tatizo la kura tatu na uongozi wa Jimbo la Kusini, Sheikh Yusufu Badi alimpokea Nyerere na madras yake, wanafunzi wakimwimbia Nyerere kasda na kumpigia dufu. Kuanzia hapo sasa kila mtu alijiunga na TANU. Si Mponda wala Kanisa lilikuwa na uwezo wa kupambana na TANU kwa wakati ule. Polepole lakini na kwa uhakika, TANU ilingia ndani ya maeneo ya Kikristo huko Songea, Masasi, Tunduru na Newala, nyumbani kwa Yustino Mponda."

(Kutoka: "Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) Historia Iliyofichwa Kuhusu Harakati za Waislam Dhidi ya Ukoloni wa Waingereza Katika Tanganyika," Phoenix Publishers, Nairobi 2002).
 
Utaona mawenge tu. Mtu wa std Seven aonyeshwe syllabus ya University level, ataishia kusema Mungu ana maajabu!

Sasa labda twende kwa mifano hai.
Kwa mujibu wa imani yako PAPA ndio MSOMI na ni mwenye AKILI na Busara Kuliko nyie kondoo woote.
Na mnamuita MTAKATIFU! au sio?

Sasa tazama kitu anafanya hapa halafu unambie Mwenye elimu atafanya usanii huu?

1427212178749.jpg

Hapa anapiga busu mwasesere wa kizungu na kumpigia Goti kwa imani kuwa ni katoto ka mungu wenu.

1427212366190.jpg

Sasa hii ndio unaiita University level?
Au kuna ingine tena?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom