george ndamanya
Member
- Jul 10, 2017
- 22
- 33
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ofisi za Makao makuu ya Chadema, Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa Patrick Ole Sosopi ametoa rai kwa wananchi kuitumia siku ya maadhimisho ya Uhuru wa Tanganyika, Desemba 9, 2018 kuwatembelea wafungwa walioko katika magereza mbalimbali huku akipinga agizo la Rais John Magufuli la kufutwa kwa sherehe za Uhuru na fedha hizo kutumika kujengea Hospitali mkoani Dodoma.
Sosopi amewataka wananchi siku hiyo kutii sheria za magereza na kuwaeleza wafungwa na mahabusu wa makosa mbalimbali kwenye magereza hayo kuhusu hali ya maisha ilivyo uraiani akidai kuwa hakuna uhuru kama ilivyo kwa waliyoko magerezani
Sosopi amewataka wananchi siku hiyo kutii sheria za magereza na kuwaeleza wafungwa na mahabusu wa makosa mbalimbali kwenye magereza hayo kuhusu hali ya maisha ilivyo uraiani akidai kuwa hakuna uhuru kama ilivyo kwa waliyoko magerezani