Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
KISA KILICHONITOA MACHOZI WAKATI NIPO MTWARA.
Kwa wale wakazi wa Mtwara,mtakuwa mnaijua vizuri ile barabara itokayo pale Ligula Hospitali inashuka chini kuelekea kwa Jionee, Cocobeach,TTC mpaka kiyangu, hii ni barabara kubwa na ina nzuri kwani ina kiwangi kizuri cha lami. Ukifika pale kwa jionee kuna junction, ile barabara inayoelekea CHUNO, na hapa ndipo kisa hiki kimelalia.
Hii barabara ilikuwa ipo kwenye service, labda inawezekana ukweli kwamba kipindi hiki cha uchaguzi mara nyingi barabara za huku mtwara nyingi zinafanyiwa marekebisho. Sasa Muhandisi wa hii barabara(Contractor) ni kijana flani wa makamu(miaka 35-40) simfamu kwa jina ila tu nikimwona mwona na wafanyakazi wengine wa barabara hii wakijishughulisha kuweka lami hii barabara.
Hivi majuzi huyu bwana, alitokea kumpenda(sidhani kama ni kumpenda au ni hulka ya mwili) mdada flani(jina nalihifadhi) ambae amepanga nyumba flani inatazama na hii barabara. ifahamike kwamba huyu dada alikaa zaidi ya miaka miwili hospitali na ni mwasirika wa VVU, na still anaendelea kutumia ARV kusogeza siku mbele, na hapo mtaani watu wote kama sio wengi wanamfamu vizuri tu huyu dada. Ikumbukwe kipindi cha nyuma miaka ya 2000 huyu dada kutokana na uzuri wake alikuwa 'matawi ya juu' sana!
Huyu Contractor bila kujua hilo(ni mkazi wa Dar) akaja siku hiyo pale kwake akamtongoza wakakubaliana, akalala nae.
Siku ya pili huyu bwana akaja tena, akanunua soda, akaket mduleni akaanza kunywa. Bahati nzuri mama mwenye nyumba siku hiyo alikuwepo pale na huu 'mchongo' alikuwa keshaupata. Basi yule mama nae akaenda kukaa na yule baba pale mduleni, na 'akamchana live' kwamba ulyefanya nae ngono jana ni muathirika ana UKIMWI......
Yule baba alivunja ile soda aliyekuwa anakunywa palepale, akaanza kulia na kutoa michozi huku akisema kwa uchungu kwamba alikuwa hakujua hilo, mbaya zaidi alisema kwamba kabla ya kukutana nae alienda duka la jirani kununua Condomz, lakini yule dada alikataa katakata kutumia kondom nna jamaa akaziweka kando....kikubwa zaidi wakati analia akisikika akisema kwamba ana mke na watoto, na hajui atamwambia nini mke wake akirudi huko Dar.
Baada ya siku mbili kupita tangu ule mkasa niliona magari ya mchanga yakija na kuanza kusomba zile changarawe ambazo ilibidi zitumike kwenye ile barabara na mpaka sasa hivi hii barabara ina changarawe zenye vumbi na ule uji wa lami haujawekwa bado, nilijaribu kuwauliza wale jamaa wakiopaikiza changanrawe kulikoni walisema yule contractor kaenda Dar es salaam..sasa sikujua kwamba mkataba kaukatisha au ilikuaw vp wameiacha hii barabara na vumbi lake...Imenisikitisha sana hii taarifa.
source:http://erwinsizinga.blogspot.com/
Kwa wale wakazi wa Mtwara,mtakuwa mnaijua vizuri ile barabara itokayo pale Ligula Hospitali inashuka chini kuelekea kwa Jionee, Cocobeach,TTC mpaka kiyangu, hii ni barabara kubwa na ina nzuri kwani ina kiwangi kizuri cha lami. Ukifika pale kwa jionee kuna junction, ile barabara inayoelekea CHUNO, na hapa ndipo kisa hiki kimelalia.
Hii barabara ilikuwa ipo kwenye service, labda inawezekana ukweli kwamba kipindi hiki cha uchaguzi mara nyingi barabara za huku mtwara nyingi zinafanyiwa marekebisho. Sasa Muhandisi wa hii barabara(Contractor) ni kijana flani wa makamu(miaka 35-40) simfamu kwa jina ila tu nikimwona mwona na wafanyakazi wengine wa barabara hii wakijishughulisha kuweka lami hii barabara.
Hivi majuzi huyu bwana, alitokea kumpenda(sidhani kama ni kumpenda au ni hulka ya mwili) mdada flani(jina nalihifadhi) ambae amepanga nyumba flani inatazama na hii barabara. ifahamike kwamba huyu dada alikaa zaidi ya miaka miwili hospitali na ni mwasirika wa VVU, na still anaendelea kutumia ARV kusogeza siku mbele, na hapo mtaani watu wote kama sio wengi wanamfamu vizuri tu huyu dada. Ikumbukwe kipindi cha nyuma miaka ya 2000 huyu dada kutokana na uzuri wake alikuwa 'matawi ya juu' sana!
Huyu Contractor bila kujua hilo(ni mkazi wa Dar) akaja siku hiyo pale kwake akamtongoza wakakubaliana, akalala nae.
Siku ya pili huyu bwana akaja tena, akanunua soda, akaket mduleni akaanza kunywa. Bahati nzuri mama mwenye nyumba siku hiyo alikuwepo pale na huu 'mchongo' alikuwa keshaupata. Basi yule mama nae akaenda kukaa na yule baba pale mduleni, na 'akamchana live' kwamba ulyefanya nae ngono jana ni muathirika ana UKIMWI......
Yule baba alivunja ile soda aliyekuwa anakunywa palepale, akaanza kulia na kutoa michozi huku akisema kwa uchungu kwamba alikuwa hakujua hilo, mbaya zaidi alisema kwamba kabla ya kukutana nae alienda duka la jirani kununua Condomz, lakini yule dada alikataa katakata kutumia kondom nna jamaa akaziweka kando....kikubwa zaidi wakati analia akisikika akisema kwamba ana mke na watoto, na hajui atamwambia nini mke wake akirudi huko Dar.
Baada ya siku mbili kupita tangu ule mkasa niliona magari ya mchanga yakija na kuanza kusomba zile changarawe ambazo ilibidi zitumike kwenye ile barabara na mpaka sasa hivi hii barabara ina changarawe zenye vumbi na ule uji wa lami haujawekwa bado, nilijaribu kuwauliza wale jamaa wakiopaikiza changanrawe kulikoni walisema yule contractor kaenda Dar es salaam..sasa sikujua kwamba mkataba kaukatisha au ilikuaw vp wameiacha hii barabara na vumbi lake...Imenisikitisha sana hii taarifa.
source:http://erwinsizinga.blogspot.com/