Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,447
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA 15
Baada ya kutayarisha chelezo wakaniweka juu yake wakanipa mikate vipande saba na gudulia la Maji, wakanishusha mle pangoni, halafu wakaliziba kwa lile jiwe wakaenda zao.
Nilipogusa chini nikajikuta nimo katika pango kubwa lililoka na harufu mbaya sana ya maiti, lilikua limejaa mifupa ya binaadamu walioteremshwa mle, nilijibwaga chini nikajilaumu, Sindbad yote haya yasingetokea kama si tamaa yako! Bora ungekufa mlimani au baharini kuliko humu pangoni! Nikiteseka kwa was was wa kufa,
Nilijilaza mle kwa muda wa saa kadhaa huku nimejaa fikra na mawazo ya kukata tamaa. Niliposhikwa na njaa nilikula kipande kidogo cha mkate nikanywa na maji kidogo, halafu nikaenda kujilaza pembeni nilipopaondoa mifupa.
Baada ya muda ile mikate na Maji yaliniishia nikawa sina la kufanya ispokua kusubiria kifo, lakini siku moja wakati nilipokua nimejinyoosha, mara niliskia lile jiwe likifunguliwa na pale pangoni palionekana kundi la waombolezi ambao walimteremsha ndani mfu mwanaume aliefuatwa na mkewe aliepiga makelele huku ameahikilia mikate saba na gudulia la maji.
Lile pango lilipozibwa nilinyanyuka taratibu kutoka pale pembeni nilipokaa, nikachukua pande la fupa la paja la mtu kutoka katika moja ya yale marundo ya mifupa, nikamrukia yule mwanamke nikamtwanga nalo kichwani na mara ile ile alianguka chini na kufa hapo hapo.
Halafu nilichukua ile mikate saba na lile gudulia lake la maji vikanifaa kwa siku kadhaa, nilipoishiwa tena lile jiwe likaiinuliwa akashushwa mfu mwanamke aliefuatwa na mumewe. Nae alikabili kifo kama maskini yule mwanamke wa kwanza.
Kwa njia hii nikaishi kwa majuma kadhaa nilimuuwa kila alieteremshwa mle na kuila mikate yake nakunywa maji yake, siku moja wakati nilipokua nimelala mahali pangu pa kila siku, niliamshwa na sauti ya mwendo iliotokea karibu nami, nikashtuka, nikanyanyuka, nikachukua fupa langu nikaelekea kule ilikotokea ile sauti.
Kwa ajili ya lile giza totoro lililotanda kote, kwa shida nikaona kijinyama kikikimbia, nikakifuata huku nikijikwaa gizani kwa ile mifupa iliyotapakaa kote mle mpaka nikafika mwisho wa lile pango ambako niliona Nuru ya mwangaza iliyoongezeka ukubwa kadri nilivyoisogelea, nilipoikaribia yule mnyama aliruka akajipenyeza mle ilimotoka ile Nuru akatoweka.
Kwa furaha nyingi isiyoweza kukisika, nikatambua kuwa nimefika penye tundu ambamo wanyama mwitu waliovutiwa na harufu ya ile mizoga ya maiti mle pangoni, waliingilia kutoka upande wa pili wa lile bonde kuja kuila, hapo bila kusita sita nilipafukua pale mahali mpaka ile tundu ikawa kubwa, nilijipenyeza huku nikitambaa kwa mikono na miguu mpaka nikatokea ufukweni upande wa pili penye mwamba mreefu uliokwenda juu.
Nilipojikuta nipo nje kuonekanako mbingu na ardhi nilipiga magoti nikamshukuru mungu kwa kuokoka kwangu, kwa ajili ya ule mwangaza wa jua na hewa safi nilioivuta, baada ya muda nikahisi vizuri, nilijaa furaha isiokua na kifani kwa kuona uzuri wa mbingu, mawingu na ardhi.
Nikawa na nguvu za kutosha baada ya muda nikarudi tena mle pangoni ambako niliichukua mikate yangu iliobakia, nikakusanya na vitu vingi vya tunu ambavyo vilizikwa mle pamoja na maiti, nikavifunga vizuri kwa nguo za wale wafu nikavibeba nje ufukweni.
Basi nikabaki pale kwa muda wa siku chache nikitizama baharini kwa upeo wa macho toka asubuhi hadi jioni,
Siku moja wakati nilipokua nimekaa chini ya jabari nikiomba mungu aniokoe, mara niliona kwa mbali tanga la chombo kilichokua kikielekea kule nilikokua, mara ileile nilinyanyuka nikachukua chuka nikaifunga vizuri kwenye fito nikaanza kuipepea juu kwa nguvu kama bendera huku nikikimbia huko na huko pale ufukweni nikipiga kelele.
Kwa bahati nzuri mabaharia wa kile chombo waliona ishara yangu wakashusha mashua wakanifuata wakaniokoa,
"Umefikaje pale kwenye ufukwe?" Akaniuliza kwa mshangao mkubwa nahodha wa ile merkebu, akiendelea, "katika safari zangu zote za kupitia sehemu hizi za upweke sijawahi kumuona mtu yoyote!"
"Bwana wangu" nikamjibu "niliokoka kutoka katika merkebu moja iliozama karibu na ule ufukwe siku nyingi zilizo pita, furushi hili ulionalo ndicho kitu cha pekee nilichoweza kukiokoa, " nilimficha ukweli isije ikawa mle merkebuni mna raia wa kisiwa kile.
Basi nikatoa lulu ya thamani kutoka mle furushini nikamkabidhi nahodha nikamwambia: "tafadhali pokea lulu hii kama shukrani zangu kwa kuyaokoa maisha yangu. Lakini yile nahodha akasema "si desturi yutu kupokea malipo kwa tendo jema, tumewaokoa wengi waliovunjikiwa na merkebu zao, tukawalisha na kuwavisha, mwisho tukawasafirisha tikawafikisha watakako huku sisi tukiwapa wao zawadi. Kwani ni mwenyezi mungu tu ndie atowae.
Nikamshukuru kwa moyo wangu wote nikamuombea kila la kheri.
Basi ile merkebu iliendelea na safari yake tukifika kisiwa hadi kisiwa. Bandari hadi bandari huku nikifurahi kuelekea kwetu, lakini kumbukumbu za maiti na wafu waliojaa mle pangoni zikawa zanijia mara kwa mara ndotoni na kunishtua.
Mwisho kwa uwezo wa mwenyez mungu tukawasili basrah Salama salmini ambako nilipumzika kwa muda mfupi halaru nilielekea Baghdad kupitia mto Tigris.
Nilifika kwetu huku nimebeba hazina iliojaa kila namna ya vitu vya tunu na bidhaa ghali.
Nilipokelewa mikono miwili na ndugu, jamaa na marafiki. Baada ya kupumzika niliuza bidhaa zangu na vile vitu vyangu vya tunu, nikatoa sadaka kwa maskini, mayatima na kwa watawa. Nikabaki nikifurahia maisha.
* * * * * * * * * * * * * * *
Na hayo waungwana ndio yalionipata katika safari yangu ya nne, kesho in sha Allah nitawasimulia yalionipata katika safari yangu ya tano.
Baada ya karamu ya jioni Sindbad Baharia alimkabidhi Hindbad Hamali reale mia za dhahabu akimiaga na kumwambia aje tena kesho.
Basi wageni wote wakaaga wakaenda zao makwao huku wakistaajabia yale yaliompata mwenyeji wao.
Itaendelea...
Baada ya kutayarisha chelezo wakaniweka juu yake wakanipa mikate vipande saba na gudulia la Maji, wakanishusha mle pangoni, halafu wakaliziba kwa lile jiwe wakaenda zao.
Nilipogusa chini nikajikuta nimo katika pango kubwa lililoka na harufu mbaya sana ya maiti, lilikua limejaa mifupa ya binaadamu walioteremshwa mle, nilijibwaga chini nikajilaumu, Sindbad yote haya yasingetokea kama si tamaa yako! Bora ungekufa mlimani au baharini kuliko humu pangoni! Nikiteseka kwa was was wa kufa,
Nilijilaza mle kwa muda wa saa kadhaa huku nimejaa fikra na mawazo ya kukata tamaa. Niliposhikwa na njaa nilikula kipande kidogo cha mkate nikanywa na maji kidogo, halafu nikaenda kujilaza pembeni nilipopaondoa mifupa.
Baada ya muda ile mikate na Maji yaliniishia nikawa sina la kufanya ispokua kusubiria kifo, lakini siku moja wakati nilipokua nimejinyoosha, mara niliskia lile jiwe likifunguliwa na pale pangoni palionekana kundi la waombolezi ambao walimteremsha ndani mfu mwanaume aliefuatwa na mkewe aliepiga makelele huku ameahikilia mikate saba na gudulia la maji.
Lile pango lilipozibwa nilinyanyuka taratibu kutoka pale pembeni nilipokaa, nikachukua pande la fupa la paja la mtu kutoka katika moja ya yale marundo ya mifupa, nikamrukia yule mwanamke nikamtwanga nalo kichwani na mara ile ile alianguka chini na kufa hapo hapo.
Halafu nilichukua ile mikate saba na lile gudulia lake la maji vikanifaa kwa siku kadhaa, nilipoishiwa tena lile jiwe likaiinuliwa akashushwa mfu mwanamke aliefuatwa na mumewe. Nae alikabili kifo kama maskini yule mwanamke wa kwanza.
Kwa njia hii nikaishi kwa majuma kadhaa nilimuuwa kila alieteremshwa mle na kuila mikate yake nakunywa maji yake, siku moja wakati nilipokua nimelala mahali pangu pa kila siku, niliamshwa na sauti ya mwendo iliotokea karibu nami, nikashtuka, nikanyanyuka, nikachukua fupa langu nikaelekea kule ilikotokea ile sauti.
Kwa ajili ya lile giza totoro lililotanda kote, kwa shida nikaona kijinyama kikikimbia, nikakifuata huku nikijikwaa gizani kwa ile mifupa iliyotapakaa kote mle mpaka nikafika mwisho wa lile pango ambako niliona Nuru ya mwangaza iliyoongezeka ukubwa kadri nilivyoisogelea, nilipoikaribia yule mnyama aliruka akajipenyeza mle ilimotoka ile Nuru akatoweka.
Kwa furaha nyingi isiyoweza kukisika, nikatambua kuwa nimefika penye tundu ambamo wanyama mwitu waliovutiwa na harufu ya ile mizoga ya maiti mle pangoni, waliingilia kutoka upande wa pili wa lile bonde kuja kuila, hapo bila kusita sita nilipafukua pale mahali mpaka ile tundu ikawa kubwa, nilijipenyeza huku nikitambaa kwa mikono na miguu mpaka nikatokea ufukweni upande wa pili penye mwamba mreefu uliokwenda juu.
Nilipojikuta nipo nje kuonekanako mbingu na ardhi nilipiga magoti nikamshukuru mungu kwa kuokoka kwangu, kwa ajili ya ule mwangaza wa jua na hewa safi nilioivuta, baada ya muda nikahisi vizuri, nilijaa furaha isiokua na kifani kwa kuona uzuri wa mbingu, mawingu na ardhi.
Nikawa na nguvu za kutosha baada ya muda nikarudi tena mle pangoni ambako niliichukua mikate yangu iliobakia, nikakusanya na vitu vingi vya tunu ambavyo vilizikwa mle pamoja na maiti, nikavifunga vizuri kwa nguo za wale wafu nikavibeba nje ufukweni.
Basi nikabaki pale kwa muda wa siku chache nikitizama baharini kwa upeo wa macho toka asubuhi hadi jioni,
Siku moja wakati nilipokua nimekaa chini ya jabari nikiomba mungu aniokoe, mara niliona kwa mbali tanga la chombo kilichokua kikielekea kule nilikokua, mara ileile nilinyanyuka nikachukua chuka nikaifunga vizuri kwenye fito nikaanza kuipepea juu kwa nguvu kama bendera huku nikikimbia huko na huko pale ufukweni nikipiga kelele.
Kwa bahati nzuri mabaharia wa kile chombo waliona ishara yangu wakashusha mashua wakanifuata wakaniokoa,
"Umefikaje pale kwenye ufukwe?" Akaniuliza kwa mshangao mkubwa nahodha wa ile merkebu, akiendelea, "katika safari zangu zote za kupitia sehemu hizi za upweke sijawahi kumuona mtu yoyote!"
"Bwana wangu" nikamjibu "niliokoka kutoka katika merkebu moja iliozama karibu na ule ufukwe siku nyingi zilizo pita, furushi hili ulionalo ndicho kitu cha pekee nilichoweza kukiokoa, " nilimficha ukweli isije ikawa mle merkebuni mna raia wa kisiwa kile.
Basi nikatoa lulu ya thamani kutoka mle furushini nikamkabidhi nahodha nikamwambia: "tafadhali pokea lulu hii kama shukrani zangu kwa kuyaokoa maisha yangu. Lakini yile nahodha akasema "si desturi yutu kupokea malipo kwa tendo jema, tumewaokoa wengi waliovunjikiwa na merkebu zao, tukawalisha na kuwavisha, mwisho tukawasafirisha tikawafikisha watakako huku sisi tukiwapa wao zawadi. Kwani ni mwenyezi mungu tu ndie atowae.
Nikamshukuru kwa moyo wangu wote nikamuombea kila la kheri.
Basi ile merkebu iliendelea na safari yake tukifika kisiwa hadi kisiwa. Bandari hadi bandari huku nikifurahi kuelekea kwetu, lakini kumbukumbu za maiti na wafu waliojaa mle pangoni zikawa zanijia mara kwa mara ndotoni na kunishtua.
Mwisho kwa uwezo wa mwenyez mungu tukawasili basrah Salama salmini ambako nilipumzika kwa muda mfupi halaru nilielekea Baghdad kupitia mto Tigris.
Nilifika kwetu huku nimebeba hazina iliojaa kila namna ya vitu vya tunu na bidhaa ghali.
Nilipokelewa mikono miwili na ndugu, jamaa na marafiki. Baada ya kupumzika niliuza bidhaa zangu na vile vitu vyangu vya tunu, nikatoa sadaka kwa maskini, mayatima na kwa watawa. Nikabaki nikifurahia maisha.
* * * * * * * * * * * * * * *
Na hayo waungwana ndio yalionipata katika safari yangu ya nne, kesho in sha Allah nitawasimulia yalionipata katika safari yangu ya tano.
Baada ya karamu ya jioni Sindbad Baharia alimkabidhi Hindbad Hamali reale mia za dhahabu akimiaga na kumwambia aje tena kesho.
Basi wageni wote wakaaga wakaenda zao makwao huku wakistaajabia yale yaliompata mwenyeji wao.
Itaendelea...