Kisa cha Sindbad baharia na safari saba

Kisa cha Sindbad baharia na safari saba

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,672
19148896_1147049808732418_1881421248155222657_n.jpg


SEHEMU KWANZA

Hapo kale katika enzi za Khalifa haarun al-rashid, paliishi wanaume wawili katika jiji la Baghdad. Mmoja aliitwa Sindbad baharia na wa pili aliitwa Hindbad hamali.

Hindbad mahali alikua mtu fukara alielisha mke na watoto wake kwa shida sana wakati Sindbad Baharia alikua mfanya biashara tajiri mkubwa asiejua hata wingi wa utajiri wake.

Yeye alikua mtu wa fahari aliejulikana na kuheshimiwa sana katika jiji la baghdad. Utajiri wake ulimuezesha kuwa na watumwa na vijakazi wengi katika kasri lake la fahari ambalo lilishinda hata la sultani,

Kwani kuta za kasri hilo zilinakshiwa kwa taswira nzuri nzuri za dhahabu na mawe ya tunu, na kila chumba kilinyunyiziwa kwa Maji ya marashi na kufukizwa kwa udi na ambari.

Hali kadhalika, kila chumba kilipambwa kwa maua ya nargis, waridi na yasmini yanukiayo yaliochumwa katika bustani take, katika kasri hilo siku zote vijakazi wazurizuri waliwatumikia na kuwatumbuiza wageni kwa sauti zao nzuri zilizofuatana na zana mbali mbali za muziki walizozipiga kwa ufundi mkubwa. Zana kama udi na zumari.

Huko jikoni nako siku zote kulitoka harufu nzuri ya maakuli mbalimbali yaliopikwa na yaliomtoa mtu mate kinywani.

Siku moja, wakati Hindbad mahali alipokua akiubeba kwa shida mzigo mzito uliomwelemea katika jua Kali la kiangazi lililowaka kupita kiasi, Hindbad mahali alifika kwenye kasri hilo la Sindbad Baharia ambako, kwa uchovu mwingi aliutua mzigo wake mzito ili apumue, apumzike kidogo.

Alipoutua na kufuta jasho lililomtiririka mwili mzima, Hindbad mahali alianza kupepewa na upepo mwanana uliomletea zile harufu nzuri za kunukia zilizotoka katika lile kasri huku akisikia sauti za furaha, muziki na nyimbo za kuburudisha roho.

Hapo Hindbad mahali akanyanyua macho yake juu, akatamka kwa kukata tamaa: "ah, yaa Rabby, muumba wa viumbe vyote, tofauti kubwa ilioje hii baina ya maisha yangu na maisha aishio mwenye kasri hili! Wakati Mimi nahangaika kutwa kucha kutafuta rizki kidogo ya kilisha kwa shida familia yangu, mwenye kasri hili anaishi katika maisha ya anasa na kifahari!

Nimekosa nini, yaa tabby, hata nikastahili maisha haya niishiyo?"

Baada ya kutamka maneno hayo ya kukata tamaa, Hindbad mahali akainamisha kichwa chake chini kwa huzuni. Baada ya muda mfupi, alitokea mjakazi kutoka mle ndani akamshika mkono Hindbad mahali, akamwambia:

"Bwana wangu mwenye kasri hili ameniagiza; anataka kusema nawe." Hindbad mahali kuskia maneno Yale, alisita kidogo lakini akaona hana sababu yoyote ya kutomfuata yule mjakazi; kwani kakosa nini? Hapo akanyanyuka, akanyanyua ule mzigo wake akauweka barazani palipokua na bawabu,

Akamfuata ndani yule mjakazi wa kike mpaka wailipofika katika chumba kikubwa. Humo Hindbad mahali akaona kila upande wa kile chumba kumepambwa kwa mabusati mazuri nadhifu na katikati pana chemchemi ya maji yarukayo juu na kushuka chini kutoka katika mdomo wa ndege aliesimama kwenye dimbwi la marumaru.

Chumba kizima kilijaa masheikh, madiwani na waungwana maarufu wa jiji la baghdad. Katikati yao alikaa mwenye kasri.
Hindbad mahali alipoingia aliwaamkia kwa kuwapigia magoti kwa heshima akaibusu sakafu akifikiri,
"bila shaka hiyo pepo isemwayo ni kama hii hapa nilipo mimi"
Baada ya kunyanyuka, akasimama wima kama mlingoti.

Ndipo Sindbad Baharia akamkariibisha kwa ukarimu akimwambia akae karibu take. Alipokaa, Sindbad Baharia akamuuliza jina lake.

ITAENDELEA KESHO MUNGU AKIPENDA
 
SEHEMU PILI

"Naitwa Hindbad Hamali," akajibu. "Naitwa hivyo kwa sababu kazi yangu ni kuwabebea watu mizigo yao na kuwapelekea watakako. Hiyo ndio kazi inipatiayo rizki yangu ya kila siku. Mimi ni fukara nisiejua kazi nyegine yoyote ya kuilisha familia yangu ispokua hiyo tu.
"Karibu tena!" Alitamka sindbad Baharia, akiendelea, "jua kuwa na mimi naitwa Sindbad Baharia; karibu humu kama ndugu yangu."
Sindbad Baharia baada ya kutuma mtu ampelekee Hindbad Hamali mzigo wake kule alikotaka kuupeleka, akatoa amry mgeni wake mpya aletewe maakuli ya aina aina. Aliposhiba, Sindbad Baharia alimwambia Hindbad Hamali ajihisi kama yuko kwake akiendelea: "tafadhali hebu rudia tena yale maneno ulioyasema ulipokua nje, kwani wakati ule nilikua dirishani nikikuskia."
Hindbad Hamali aliposkia maneno yale akahisi vibaya, akasema "seyyid yangu, usijali yale niliosema! Uchovu ndio ulionifanya niyatamke, kwani shida na umaskini humfanya fukara kutamka lolote."
"Aslan usifikiri nimekasirishwa na yale maneno yako," alitamka Sindbad Baharia. "Nakuhakikishia kua toka leo ujue kuwa wewe ni kama ndugu yangu. Kwa hiyo usiniogope nataka tu kuskia yale maneno yako uliyoyatamka."
Baada ya Hindbad Hamali kuyarudia tena yale maneno, mwenyeji wake akasema: ndugu yangu jua kuwa mimi naitwa Sindbbad Baharia kwa sababu ya safari nilizozifanya baharini. Kwahiyo nitakusimulia visa vilivyonipata katika safari hizo hata nikastahili kupewa jina hilo na nikaupata utajiri nilionao unaoniwezesha kuishi maisha haya ya anasa unavyoyaona katika kasri hili."
"Mimi nilifanya safari saba baharini na kila safari ilikua ni ya hatari na ya kutisha iliostahili kuandikwa kwa wino wa dhahabu."
SAFARI YAKE YA KWANZA
Jeuri, rafiki zangu, alianza Sindbad Baharia, kuwa baba yangu alikua ni mfanya biashara na mmoja wa matajiri mashuhuri wa jiji la Baghdad. Alifariki dunia wakati mimi bado ningali mtoto, akaniachia utajiri mkubwa usiokua na kifani yakiwemo mashamba na ardhi kubwa
Mara tu nilipopata umri wa utu uzima wa kuweza kumiliki ule utajiri, nilianza kuufuja kwa kula, kunywa na kuvaa majoho ghali; nikatembea na wanawake wa kila namna nikifikiri maisha yataendelea kua hivyo siku zote.
Walakin baada ya muda si mrefu, nilitambua kuwa ule utajiri aliouchuma marehemu baba, kwani jitihada kubwa umekishwa bila mimi mwenyewe kujua, kwa Mali bila daftari Hupotea bila khabari!
Hapo nilikumbuka msemo ambao marehemu baba yangu alizoea kuusema mara kwa mara: "siku ya kifo ni bora kuliko siku ya kuzaliwa; na mbwa hai ni bora kuliko simba mfu; na kifo ni bora kuliko umaskini."
Nilipoona nafilisika, niliuza mabaki ya ardhi, nyumba na vitu vyote nilivyokua navyo kwa bei ya dirham elfu tatu, nikajitayarisha na safari ya kwenda kufanya biashara katika nchi za kigeni, bila kukawia nikanunua bidhaa nikajiunga na kundi la wafanya biashara kwa safari za baharini,
Siku ya safari ilipowadia tukang'oa nanga mtoni Tirgis kwenye jiji la basrah, tukaelekea baharini, baada ya kusafiri kwa muda wa siku kadhaa kutoka kisiwa kimoja hadi kingine, na kutoka nchi moja hadi nyengine tukifanya biashara,
Siku moja tukafika kwenye kisiwa kimoja, hapo nahodha wetu akaamrisha tutie nanga, tukanyooshe miguu kisiwani. Tukashusha mbao za kwenda kufulia nguo tukachukua na vyakula vya kutosha kufanyia mandhari.
Tulipofika kisiwani tukawasha moto wakati wengine wetu wakila na kunywa wakijifurahisha, mimi na wenzangu wengine tulikwenda kukichunguza kisiwa,
Wakati tulipokua tukijishughulisha hivyo, mara nahodha wetu akitupigia kelele kutoka markebuni: "wacheni kila kitu rudini upesi muokoe maisha yenu! Hicho si kisiwa bali ni nyangumi mkubwa ambalo mchanga na udomgo umejikusanya mgongoni kwake toka miaka na miaka, ndio limeotesha miti na mimea! Sasa limehisi moto mliouwasha! Kwahio fanyeni haraka mrudi ama sivyo nyote mtaangamia!

ITAENDELEA
 
SEHEMU TATU

Tuliposikia kelele za nahodha, wengi wengi wakakimbilia markebuni wakiacha nyuma kila kitu, kuna waliowahi kufika markebuni Salama salmini; lakini kuna ambao hawakuwahi mimi nikiwa mmoja wao.
Mara kile kisiwa kikatingishika, pakazuka mawimbi makubwa kama mlima, na lile nyangumi likazama chini! Sote tusiokua na bahati tukamezwa na yale mawimbi. Nilipoibuka juu, kwa bahati nzuri mwenyezi mungu akanijaalia nikapata moja ya zile mbao za kufulia nguo, nikaling'ang'ania kama mtu ang'ang'aniavyo chochote kujisalimisha nacho wakati anapokabili kifo.
Basi kutwa nikawa napigapiga miguu kuliendesha lile bao huku nikisukumwa na mawimbi makubwa, wakati huo yule nahodha alikwasha ng'oa nanga, akatweka matanga, akatoweka na wale abiria na mabaharia waliowahi kuokoka. Ikawa sina la kufanya isipokua kuisindikiza kwa macho ile merkebu iliyokua ikitoweka kwenye upeo wa macho! Hapo nikamshukuru mungu nikingojea kifo.
Baada ya muda si mrefu giza lilitanda kote baharin. Basi usiku kucha na mchana kutwa wa siku ya pili nikawa naelea baharini nikipigwa na upepo mkali na mawimbi makubwa yakinisukuma mbele mpaka yakanifikisha kwenye kisiwa kimoja kilichokua na miamba mirefu isiyopandika.
Kwa bahati nzuri ile miamba ilikua na matawi ya miti yalioning'inia kuelekea baharini, mawimbi yaliponichukua juu nikawahi kushika tawi moja nikapanda juu nikajiokoa. Nilipojikuta kwenye nchi kavu nikawa siwezi kutembea kutokana na vidonda nilivyokua navyo miguuni vilivyo sababishwa na samaki wadogo wadogo walio nitafuna tafuna wakati nilipokua majini.
Kwa kuwa nilichoka sana nililala pale kama gogo mpaka palipo kucha. Nilipoamka miguu yangu ilikua imevimba ikiniuma hata nikashindwa kutembea, ikanibidi nitambae kwa magoti kama mtoto mchanga, basi baada ya siku chache nilipata nafuu na kwa msaada wa gongo nililolikata toka katika moja ya miti ya kile kisiwa, niliweza kujikokota nalo kukichunguza kile kisiwa. Nikamshukuru mwenyezi mungu kwa kukijaza Maji safi na matunda ya kila namna.
Siku moja wakati nilipokua nikizunguka zunguka ufukweni mbali na pale nilipo pafanya maskani yangu, nikaona kitu kilichofanana na mnyama nilipokikaribia niliona ni farasi jike aliefungwa kwenye mti.
Aliponiona, yule farasi akalia kwa sauti Kali ilionifanya nikimbie kwa woga, mara alitokea mtu mmoja alienifuata huku akinipigia kelele: "wewe ni nani na unatoka wapi? Unafanya nini hapa?" "Bwana wangu" nikasimama nikamjibu "Mimi ni msafiri nisie na bahati, niliachwa na merkebu yetu katikati na bahari kuu lakini kwa uwezo wa mungu nimeokoka na kutupwa hapa na mawimbi makubwa."
Yule bwana aliposikia maneno yangu akanishika mkono akaniongoza moja kwa moja mpaka kwenye pango lake ambako baada ya kunitaka nikae akaniletea chakula cha kutosha, niliposhiba akaniuliza juu ya masaibu yangu nilimhadithia kinagaubaga yote yalionikuta, toka awali hadi akheri.
"Lakini" na Mimi nilimuuliza baada ya kumsimulia kisa changu, "ni nini kilichokuleta na wewe hapa Kisiwani na kwa nini yule farasi jike kafungwa pale mtini?"
"Jua kuwa mimi ni mmoja wa watunza farasi wa mfalme Maharjan wa kisiwa hiki kikubwa." Akajibu. "tunawatunza farasi wake walioko sehemu mbali mbali za kisiwa, kila mwezi wakati wa mbala mwezi mpevu, tunawakusanya farasi jike wote ambao bado hawajazaa.
Tunawaleta hapa na kuwafunga karibu na ufukwe wakati sisi wenyewe tunajificha mapangoni, mara farasi dume wa baharini wanapopata harufu ya farasi jike, hutoka baharini na kuwapanda. Baadae hujaribu kuwashawishi kuelekea nao baharini, lakini hushindwa kwa sababu farasi wetu tunawafunga imara kwa kamba madhubuti.

Itaendelea...
 
SEHEMU YA NNE

Kwa milio ya hasira, farasi wa baharini huwashambulia farasi wetu kwa kuwapiga mateke kwa miguu yao ya nyuma, hapo ndipo sisi hutoka mapangoni tukawafukuza, wakatoweka tena baharini.
Baada ya muda, wale farasi wa mfalme hushika mimba na huzaa farasi wazuri sana wa thamani kubwa, leo tunafikiri itakua ni siku yetu ya mwisho. Tutakapo maliza shughuli zetu nitakuchukua mpaka kwa mfalme wetu, kwa hiyo mshukuru mola kwa kukutana nasi, usingekutana nasi ungeangamia hapa kwani si rahisi kujua mji uko pande gani wa kisiwa hiki kikubwa.
Nikamshukuru sana yule bwana nikamuombea kwa mungu amjaalie yote ya kheri, wakati tulipokua katika mazungumzo yetu, Mara kutoka nje tukaskia mlio wa kutisha! Hapo mwenyeji wangu akachomoa upnga wake alani, akatoka mbio mle pangoni huku akipiga kelele na kupiga piga upanga wake kwenye ala aliyoishika mkono wa kushoto.
Mara walitokea wachungaji farasi wengine waliokua katika mapango mengine walimojificha huku nao wameshikilia mikuki wakipiga makelele kwa nguvu zao zote, farasi wa baharini ambae alikua ameshampamda farasi jike, akatishika kwa yale makelele akakimbilia baharini akatowekea majini.
Basi baada ya kupumzika pale ufukweni kwa muda, walinzi wengine wa farasi wa mfalme wakatokea kila mmoja akimwongoza farasi jike. Baada ya kusabahiana nao mwenyeji wangu aliwasimulia yote yalionipata na wao walistaajabu sana, baadae sote tukafunga safari tukaelekea jijini kwa mfalme maharjan.
Mfalme maharjan alipoarifiwa kufika kwangu alituma mtu kuja kunichukua na kunipeleka kwake, mfalme aliposikia masaibu yalionipata alitamka "hakika umeokoka kwa qudra ya mwenyezi mungu."
Basi nikawa mmoja wa wapenzi wa mfalme maharjan, akanikabidhi wadhifa wa kuchunguza bidhaa zote zinazoingia katika bandari ya jiji lake. Na mimi nikaitekeleza kazi hiyo kwa maridhawa ya wote.

ITAENDELEA
 
SEHEMU TANO

Kwa muda ule niliokua chini ya himaya ya mfalme Maharjan, nilipendwa na wote-maskini na matajiri - wa nchi ile kwa kuwahudumia vizuri na kwa kuingia kihali na kisheria katika matatizo yao yaliofikishwa mbele ya mfalme.
Si mbali na milki ya mfalme Maharjan palikua na kisiwa kimoja kidogo ambako, usiku wa manane kulisikika milio na mipigo ya ngoma isiyo kawaida. Wasafiri na watu kutoka visiwa vya jirani waliniambia kuwa wenyeji wa kisiwa hicho walidhaniwa ni majini.
Siku moja wakati nikiwa naenda huko, katika bahari ya sehemu hiyo, nikaona samaki mkubwa ajabu mwenye kichwa kama cha bundi!
Basi ikawa kila nilipokua forodhani niliongea na mabaharia na wasafiri kutoka sehemu mbali mbali za dunia nikiwauliza kama wamewahi kusikia jiji la Baghdad, lakini kwa bahati mbaya hakuna yoyote alielijua wala kulisikia.
Ijapokua hayo talinivunja moyo lakini sikukata tamaa ya siku moja kurudi kwetu, kwani nyumbani ni nyumbani na kwao mtu ni kwao hata kama ni pangoni.
Siku moja wakati nilipokua nimesimama gatini nikiikodolea macho bahari huku nimejaa mawazo ya kukumbuka kwetu, mara kwa mbali nikaona merkebu kubwa ikielekea bandarini.
Ilipotia nanga mabaharia wakateremsha shehena na bidhaa zilizokua mle, nami nikawa nazichunguza na kuziandika kwa makini wazilipie ushuru, walipo maliza nikamuhoji nahodha kama kuna shehena nyengine yoyote ambayo haijateremshwa.
"Bwana wangu" akanijibu "merkebuni bado kumebaki robota chache tu za bidhaa ambazo ni mali ya mfanya biashara mmoja aliekufa maji baharini. Tutaziteremsha na kuziuza kesho, fedha zitakazo patikana tutawapelekea ndugu zake waishiyo Baghdad."
"Jina la mfanya biashara huyo ni nani?" Nilimuuliza. Akanijibu
"Sindbad."
Niliposkia kauli hiyo na nilipomwangalia kwa makini nilimtambua, nikampigia makelele ya furaha nikimwambia: "bwana wangu we! Hunitambui; mimi ndie Sindbad mwenyewe mwenye mali hiyo ambae mlimwacha baharini mkidhani amekufa maji pamoja na wasafiri wengine wakati lile nyangumi lilipozama baharini!
Lakini kwa kudra ya mwenyezi mungu niliokoka kwa kutupwa na mawimbi kwenye ufukwe wa kisiwa hiki ambako nimepokewa kwa ukarimu mkubwa na kuajiriwa na mfalme Maharjan kuchunguza bidhaa na shehena zinazoingia katika bandari yake."
"Ama kusema kweli," akatamka yule nahodha kwa mshangao mkubwa na kwa hasira. "Dunia haina waaminifu!
Baada tu ya kutaja mali ya mfu mara wajitokeza na kudai kuwa wewe ndie Sindbad ilhali tulimwona akifa maji mbele ya macho yetu! Unathubutuje kudai mali ya marehemu?"
"Nakusihi" nilimwambia yule nahodha, "hebu sikiliza kisa changu utakaposikia ndipo utakapojua ukweli."
Basi nikamuhadithia yote toka ile siku tulipong'oa nanga kutoka basrah mpaka ile siku tulipotia nanga kwenye kile kisiwa kilichozama, nikamkumbusha pia mambo mengi ambayo niliongea nae wakati wa safari yetu baharini.
Yule nahodha, mabaharia na wasafiri wengine waliokua mle merkebumi wakanitambua, wakanipongeza kwa kuokoka kwangu wakimshukuru mungu, "Alhamdulillah"
Basi bila kuchelewa bidhaa zangu zikateremshwa nikafurahi kuona bado ziko vile vile nilivyozifunga, nilichagua bidhaa nzuri nzuri za thamani nikampa zawadi mfalme Maharjan nikimwarifu kuwasili kwa ile merkebu niliyokuwamo awali.
Mfalme Maharjan akafurahi sana na yeye kama zawadi akanitunukia vitu vingi vya thamani kubwa.
Itaendelea.

ITAENDELEA
 
Dada Ahsante sana. Umetukumbusha mbali sisi wahenga. Enzi zetu hii ndo ilikua Jf , whatsapp, insta yetu. Alfu lela ulela. Naomba uendelee kutuburudisha.
 
Kitabu cha alfu lela ulela kwenye kitabu cha pili(vipo vitabu tisa) kilichofasiriwa na Adam Hassan kimendika vizuri sana kisa hiki.
 
SEHEMU TANO

Kwa muda ule niliokua chini ya himaya ya mfalme Maharjan, nilipendwa na wote-maskini na matajiri - wa nchi ile kwa kuwahudumia vizuri na kwa kuingia kihali na kisheria katika matatizo yao yaliofikishwa mbele ya mfalme.
Si mbali na milki ya mfalme Maharjan palikua na kisiwa kimoja kidogo ambako, usiku wa manane kulisikika milio na mipigo ya ngoma isiyo kawaida. Wasafiri na watu kutoka visiwa vya jirani waliniambia kuwa wenyeji wa kisiwa hicho walidhaniwa ni majini.
Siku moja wakati nikiwa naenda huko, katika bahari ya sehemu hiyo, nikaona samaki mkubwa ajabu mwenye kichwa kama cha bundi!
Basi ikawa kila nilipokua forodhani niliongea na mabaharia na wasafiri kutoka sehemu mbali mbali za dunia nikiwauliza kama wamewahi kusikia jiji la Baghdad, lakini kwa bahati mbaya hakuna yoyote alielijua wala kulisikia.
Ijapokua hayo talinivunja moyo lakini sikukata tamaa ya siku moja kurudi kwetu, kwani nyumbani ni nyumbani na kwao mtu ni kwao hata kama ni pangoni.
Siku moja wakati nilipokua nimesimama gatini nikiikodolea macho bahari huku nimejaa mawazo ya kukumbuka kwetu, mara kwa mbali nikaona merkebu kubwa ikielekea bandarini.
Ilipotia nanga mabaharia wakateremsha shehena na bidhaa zilizokua mle, nami nikawa nazichunguza na kuziandika kwa makini wazilipie ushuru, walipo maliza nikamuhoji nahodha kama kuna shehena nyengine yoyote ambayo haijateremshwa.
"Bwana wangu" akanijibu "merkebuni bado kumebaki robota chache tu za bidhaa ambazo ni mali ya mfanya biashara mmoja aliekufa maji baharini. Tutaziteremsha na kuziuza kesho, fedha zitakazo patikana tutawapelekea ndugu zake waishiyo Baghdad."
"Jina la mfanya biashara huyo ni nani?" Nilimuuliza. Akanijibu
"Sindbad."
Niliposkia kauli hiyo na nilipomwangalia kwa makini nilimtambua, nikampigia makelele ya furaha nikimwambia: "bwana wangu we! Hunitambui; mimi ndie Sindbad mwenyewe mwenye mali hiyo ambae mlimwacha baharini mkidhani amekufa maji pamoja na wasafiri wengine wakati lile nyangumi lilipozama baharini!
Lakini kwa kudra ya mwenyezi mungu niliokoka kwa kutupwa na mawimbi kwenye ufukwe wa kisiwa hiki ambako nimepokewa kwa ukarimu mkubwa na kuajiriwa na mfalme Maharjan kuchunguza bidhaa na shehena zinazoingia katika bandari yake."
"Ama kusema kweli," akatamka yule nahodha kwa mshangao mkubwa na kwa hasira. "Dunia haina waaminifu!
Baada tu ya kutaja mali ya mfu mara wajitokeza na kudai kuwa wewe ndie Sindbad ilhali tulimwona akifa maji mbele ya macho yetu! Unathubutuje kudai mali ya marehemu?"
"Nakusihi" nilimwambia yule nahodha, "hebu sikiliza kisa changu utakaposikia ndipo utakapojua ukweli."
Basi nikamuhadithia yote toka ile siku tulipong'oa nanga kutoka basrah mpaka ile siku tulipotia nanga kwenye kile kisiwa kilichozama, nikamkumbusha pia mambo mengi ambayo niliongea nae wakati wa safari yetu baharini.
Yule nahodha, mabaharia na wasafiri wengine waliokua mle merkebumi wakanitambua, wakanipongeza kwa kuokoka kwangu wakimshukuru mungu, "Alhamdulillah"
Basi bila kuchelewa bidhaa zangu zikateremshwa nikafurahi kuona bado ziko vile vile nilivyozifunga, nilichagua bidhaa nzuri nzuri za thamani nikampa zawadi mfalme Maharjan nikimwarifu kuwasili kwa ile merkebu niliyokuwamo awali.
Mfalme Maharjan akafurahi sana na yeye kama zawadi akanitunukia vitu vingi vya thamani kubwa.
Itaendelea.

ITAENDELEA
Dada tafadhali shusha madini mengine sehemu ya sita nakuendelea
 
Back
Top Bottom