Kisa cha mrembo Joyce

Memtata

JF-Expert Member
Jul 27, 2013
552
1,801
Siku moja katika pitapita zangu nikakutana na rafiki zangu walevi wakakomaa twende kijiwe kimoja cha pombe. Kilikuwa ni kigrocery kidogo lakini kimechangamka hivi, japokuwa pombe nishaacha lakini nilivutiwa sana na hili eneo. Sio kwa uchangamfu bali ni baada ya kumuona muhudumu aliyekuja kutuhudumia, kama utujuavyo wanaume rijali🤣🤣najua wale wenye matatizo yao na kujifichia kwenye uaminifu mtanikebehi hapa 🤣

Huyu dada alikua anaitwa Joyce alikuwa ni mzuri kwakweli, nnaposema mzuri si kwa macho yangu pekee hata rafiki zangu walisema “unadhani kwanini tunakuja kunywa huku kwenye hiki kigrocery mshenzi” 🤣

Mimi nilikuwa sinywi pombe, wenzangu wakiwa wanasubiri wapate starter ya kuondoa aibu ndio wamtongoze mi nikanyanyuka nae faster. Siku hiyo nikakomaa na jamaa hadi saa6 usiku ilimradi wafunge niondoke na Joyce. Hili ni jina lake halisi kabisa na nilimwambia nitaandika kisa chako akasema 'hakuna shida mi nilishavurugwa’🤣

Tumekuwa tukikutana na wanawake wazuri na wengine wazuri sana wakifanya kazi bar ama wakijiuza na maranyingi watu hujiuliza wamekosa nini hawa?! Leo kwa mara ya tatu nipo na Joyce tumejificha kwenye hoteli moja nje ya mji kabisa akigonga lager mi na maji yangu na fegi nikaanza kumuhoji kwanini yuko hapo.

Joyce akilewa ni muongeaji sana, basi akaanza kufunguka. Anasema alikuwa na mume wake mwanajeshi mwenye nafasi yake, jamaa walikutana Kibondo alipokwenda huko kikazi wakati huo Joy alikuwa kidato cha tatu lakini alikuwa mtukutu haswa bar zote za mjini wanamjua. Jamaa akampenda wakapeana namba za simu, baada ya mishe za jamaa kuisha akarudi Dar kituo chake cha kazi.

Mshkaji alivyofika Dar wakawa wanawasiliana na Joy akamwambia anataka aje kutoa mahari kwao, Joy akarahisisha mambo akamwambia wewe nitumie nauli mi nakuja hayo ya ndoa yatafata baadae.

Jamaa akatuma mpunga wa kutosha Joy akatoroka kwao… anasema alitoa taarifa kwao wasisumbuke kumtafuta yeye ameenda kuolewa, wakati huo akiwa ameshafika Kahama!

Joyce akapokelewa na jamaa kwenye gari hadi kwao. Kumbe jamaa alikuwa anaishi Chalinze lakini kituo cha kazi kilikuwa Dar. Lakini jamaa alikuwa vizuri sana, mjengo wa maana na kila kitu ndani cha maana na ndinga la kishua. Mtoto akakaribishwa mjengoni kama maza house. Waliishi yeye na jamaa, beki tatu na kijana wa kazi za nje ambaye alikuwa anahudumia kuku na usafi wa nje.

Kuna mengi Joyce kanielezea kuhusu huyu mwanaume siwezi kuandika yote lakini kifupi jamaa alimpenda sana mke wake yani sana…. Jamaa alimjali kwa kila kitu anasema hadi kumuogesha na kumfulia nguo zake hadi underwear!

Jamaa alikuwa Muislam ila Joyce alikuwa Christian (Mkatoliki). Kila jumapili alimpeleka kanisani na alimsubiri nje akiwa kwenye gari muda wote wa ibada na kisha kumrudisha nyumbani.

Ilifikia wakati mwamba akawa na mawasiliano na wazazi wa Joyce nao wakampa baraka zote. Jamaa akaanza kumpanga Joyce na kumwambia inabidi waoane na ingependeza kama Joyce angebadili dini na kuwa Muislam. Joyce alikubali na akaanza kupata mafunzo ya dini.

Tatizo la huyu jamaa alikuwa na wivu sana nadhani sababu alimpenda sana Joyce, hakutaka atoke nyumbani na kwakuwa home kulikuwa na CCTV camera ambazo zilikuwa linked na simu yake basi kila Joy akitoka jamaa anampigia na kumuuliza alikuwa wapi.

Lakini anasema hakuwahi kumpiga wala kumfokea kwa hasira bali alikuwa analalamika kwa upole na uchungu na kama Joyce angemjibu vibaya basi jamaa huishia kulia, kuacha kula na kulala mbali kitandani bila kumsemesha chochote siku hiyo. Inavyoonekana Joyce alilewa mapenzi akajiona yeye ndo yeye na jamaa hana jeuri kwake sababu anampenda sana.

Mzozo ulianza kuwa mkubwa Joyce akawa hadi anamtamkia kabisa jamaa kwamba hampendi lakini jamaa alikuwa hachoki kumbembeleza na inaonekana aliumia sana maana anasema kila wakati alikuwa hafichi hisia zake kwa Joyce na alikuwa analia sana. Fikiria mwanaume mwanajeshi mwenye kitengo chake kudondosha chozi!😢

Binafsi mimi sikushangaa hili maana Joyce anasema wakati huo alikuwa yuko moto sana hadi nikajikuta namuuliza ‘unamaana ulikuwa mzuri zaidi ya hapa!?’ akajibu ndio hapa ameharibika baada ya kuzaa na kukutana na changamoto za kimaisha. Jamani sitanii Joyce ni mzuri kuna rafiki yangu mmoja aliwahi kuniambia anataka amtongoze Joyce ili aende nae kuuza sura kwenye sherehe ya kampuni ya kufunga mwaka!😁Acheni kabisa naongea haya mjue kabisa uzuri wa Joyce si kwa jicho langu la tamaa tu 😃

Mzozo wa Joyce na jamaa yake ulikuwa zaidi hadi kufikia Joyce kumshurutisha jamaa ampe nauli arudi kwao. Unaambiwa siku hiyo jamaa alilia sana lakini Joyce hakusikia la muadhini wala mtangaza kifo akakomalia arudi kwao. Neno la mwisho la jamaa kwa Joyce “mke wangu unaondoka mimi bado nakupenda nakwambia wazi wanaokudangaya hawatokupenda kama mimi”

Haikusaidia kitu Joyce akakomaa kuondoka, jamaa akamsaidia kukusanya kila anachotaka akampeleka hadi kituoni siku ya safari mrembo Joyce akarudi kwao Kibondo. Kibondo!!! 😀

Wakati naendelea kuandika sehemu ya pili nakaribisha sumu kama sio povu
images (17).jpeg
 
huyo joyce alikuwa na age inamsumbua sana.mbona tunao wengi mpaka wanaomba nafasi ya kuwa mke mdogo
 
Sehemu ya pili

Joyce anadai alivyofika Kibondo kwa mara ya kwanza hakujutia kabisa wala hakujilaumu kwa uamuzi wake, hakumkumbuka mume wake zaidi alijihisi kumchukia kila alipomkumbuka lakini jamaa hakuacha kumpigia simu karibia kila siku.

Haya mambo yana mwisho wake, jamaa ni kama alikata tamaa akapunguza mawasiliano na Joyce. Mara ya mwisho kumpigia simu alikuwa anampa taarifa kwamba anaenda Ufaransa kikazi hivyo hatoweza kupatikana kwa muda mrefu. Jamaa akasepa…

Siku zikayoyoma Joyce akaanza kichefuchefu na kutapika, akaja kugundua ni mjamzito. Salaleeh… kumbe chuki zote zile ilikuwa ni mimba changa!! Mama yake akamfumbua akamwambia kumbe ndio maana alikuwa anamchukia sana jamaa hii ni kawaida kwa mwanamke kwa baadhi ya mimba.

Hapa Joyce ni kama alifumbuliwa macho akaanza kuwaza, hivi nimeharibu ndoa yangu? Akatamani ampigie jamaa simu lakini haikuwezekana na jamaa hakumpigia kabisa nadhani safari hiyo ilikuwa ya kikazi zaidi. Huu ndio muda ambao Joyce alianza kuteseka na maisha kumpiga alitamani arudi kwake Chalinze lakini haikuwezekana.

Sasa hivi Joyce ameshajifungua na mtoto anafanana na jamaa wala DNA haihitajiki. Jamaa alirudi Tanzania na alioa manzi ya kiarabu hadi picha Joyce alinionyesha ni mzuri pia. Unajua wakati huu Joyce alikuwa akinielezea haya huku machozi yakimlenga! Anasema kwakweli anajutia sana kwa kilichotokea 😢

Hadi kufika hapa ilikuaje? Baada ya kujifungua akapigwa na maisha haswa lakini baada ya muda akaanza kugain akawa chombo tena jamaa moja lenye nafasi yake hapo Kibondo (naomba nisitaje cheo chake maana ni cheo nyeti) likampenda likamfungulia bar kubwa na kumuhudumia kila kitu. Joyce akawa mchepuko maana jamaa alikuwa na familia yake.

Tatizo la huyu jamaa alikuwa na wivu sana na alikuwa Mandonga pia. Joyce alikuwa na tabia ya kwenda hapo bar jioni anaangalia hesabu na kurudi home. Basi akisemeshwa tu na mteja au kucheka nae basi jamaa linamfata home na kuanza kumpiga tena kipondo haswa anasema jamaa lilikuwa linapiga hadi Joyce anaumia na kukaa ndani hata wiki.

Akiongea na simu na mshkaji au akikuta sms hata ikiwa na neno ‘my' tu basi anakula kipondo, maranyingi alikuwa anamwambia “ukinizingua zaidi nakupiga risasi na hakuna wa kunifanya kitu maana mimi nna nafasi yangu serikalini” na jamaa kweli bastola alikuwa nayo.

Joyce akaona atakufa kama sio kwa ngumi basi kwa bastola mama yake akamwambia “mwanangu hapo umepatikana, utakufa”. Mbaya zaidi mwamba alikuwa hataki kusikia hata habari ya kuachana anasema hata akimuacha anamuua na huyo bwana atakayemchukua anamuua pia.

Joyce akatoroka yeye na dada yake mtoto wa mama yake mkubwa ambaye anadai alikuwa amemuajiri kwenye bar yake hapo Kibondo. Ndio wakakimbilia hapa walipo sasa, walipofika wakafikia kwa madada poa mjini bahati mbaya kwao hilo eneo kuna tajiri mmoja amelinunua akatimua wote. Katika kuhangaika wakaishia kwenye hiki kigrocery mshenzi kwasababu tu wapate sehemu ya kulaza mbavu na kula.

Joyce anasema kwa sasa anajenga kwao kwa hivi visenti anavyovipata kwa wadhamani kama sisi🤣lakini anamaisha magumu kuna wakati naenda pale namkuta amekaa na mawazo inabidi nimunulie bia na msosi anasema kuna siku huwa analala njaa bahati mbaya Joy hapendi kuomba hela na hata ukipita nae kama usipompa basi hatokuomba kabisa.

Baba wa mtoto kamwambia ampe mtoto amsomeshe shule ya maana, yeye alikuwa hataki na kuna siku alitumiwa nauli ampeleke akaila. Nimemshauri ampeleke mtoto sasaivi ana miaka miwili na nusu tena jamaa kamwambia ili mtoto wake awe salama zaidi atampeleka kwa shangazi zake na sio kwa mke wake.

Jamaa mjeda aliyekuwa mume wa Joyce kama atabahatika kusoma kisa hiki atakumbuka mbali sana, namwambia tu alifanya mazuri kwa upande wake kumnyanyua Joyce lakini demu akazingua nadhani si mimba tu iliyosababisha haya labda kuna mengi nyuma ya pazia ila ajue kabisa karma has fulfilled its duty Joyce sasa hivi anauza bar na kudanga huku kwa wachimba dhahabu 🤣

Nimemaliza, msinisumbue kuomba namba ya Joyce alipo hapa anaishi kwa wasiwasi Mandonga wa Kibondo anamsaka sana yeye kadanganya ameenda Chalinze kwa mumewe japokuwa jamaa ni kama limeshtuka baada ya kuona mtoto wa Joyce bado yupo hapo Kibondo.
images (20).jpeg
 
Ndo dada zetu hao, kazi kweli kweli , sema huyo joy ushamba ndo umemzidia. Mshauri atunze nauli asije Anza kuugua akaishia kuzikwa na counsel.
 
Kwa uandishi huo wa kulaza maneno hata mgambo huwezi kupata ikitokea wametoa nafasi
Mimi ndiye bwana ake Joyce! Sema tu umeongeza chumvi, au amekudanganya! Nilimpenda kweli; ila nilikuwa silii 😭 bhana kama ulivyosimualia hapa.

Yaani mjeda kabisa nilie kwa sababu ya mwanamke!! Hauko serious aisee.
 
Sehemu ya pili

Joyce anadai alivyofika Kibondo kwa mara ya kwanza hakujutia kabisa wala hakujilaumu kwa uamuzi wake, hakumkumbuka mume wake zaidi alijihisi kumchukia kila alipomkumbuka lakini jamaa hakuacha kumpigia simu karibia kila siku.

Haya mambo yana mwisho wake, jamaa ni kama alikata tamaa akapunguza mawasiliano na Joyce. Mara ya mwisho kumpigia simu alikuwa anampa taarifa kwamba anaenda Ufaransa kikazi hivyo hatoweza kupatikana kwa muda mrefu. Jamaa akasepa…

Siku zikayoyoma Joyce akaanza kichefuchefu na kutapika, akaja kugundua ni mjamzito. Salaleeh… kumbe chuki zote zile ilikuwa ni mimba changa!! Mama yake akamfumbua akamwambia kumbe ndio maana alikuwa anamchukia sana jamaa hii ni kawaida kwa mwanamke kwa baadhi ya mimba.

Hapa Joyce ni kama alifumbuliwa macho akaanza kuwaza, hivi nimeharibu ndoa yangu? Akatamani ampigie jamaa simu lakini haikuwezekana na jamaa hakumpigia kabisa nadhani safari hiyo ilikuwa ya kikazi zaidi. Huu ndio muda ambao Joyce alianza kuteseka na maisha kumpiga alitamani arudi kwake Chalinze lakini haikuwezekana.

Sasa hivi Joyce ameshajifungua na mtoto anafanana na jamaa wala DNA haihitajiki. Jamaa alirudi Tanzania na alioa manzi ya kiarabu hadi picha Joyce alinionyesha ni mzuri pia. Unajua wakati huu Joyce alikuwa akinielezea haya huku machozi yakimlenga! Anasema kwakweli anajutia sana kwa kilichotokea

Hadi kufika hapa ilikuaje? Baada ya kujifungua akapigwa na maisha haswa lakini baada ya muda akaanza kugain akawa chombo tena jamaa moja lenye nafasi yake hapo Kibondo (naomba nisitaje cheo chake maana ni cheo nyeti) likampenda likamfungulia bar kubwa na kumuhudumia kila kitu. Joyce akawa mchepuko maana jamaa alikuwa na familia yake.

Tatizo la huyu jamaa alikuwa na wivu sana na alikuwa Mandonga pia. Joyce alikuwa na tabia ya kwenda hapo bar jioni anaangalia hesabu na kurudi home. Basi akisemeshwa tu na mteja au kucheka nae basi jamaa linamfata home na kuanza kumpiga tena kipondo haswa anasema jamaa lilikuwa linapiga hadi Joyce anaumia na kukaa ndani hata wiki.

Akiongea na simu na mshkaji au akikuta sms hata ikiwa na neno ‘my' tu basi anakula kipondo, maranyingi alikuwa anamwambia “ukinizingua zaidi nakupiga risasi na hakuna wa kunifanya kitu maana mimi nna nafasi yangu serikalini” na jamaa kweli bastola alikuwa nayo.

Joyce akaona atakufa kama sio kwa ngumi basi kwa bastola mama yake akamwambia “mwanangu hapo umepatikana, utakufa”. Mbaya zaidi mwamba alikuwa hataki kusikia hata habari ya kuachana anasema hata akimuacha anamuua na huyo bwana atakayemchukua anamuua pia.

Joyce akatoroka yeye na dada yake mtoto wa mama yake mkubwa ambaye anadai alikuwa amemuajiri kwenye bar yake hapo Kibondo. Ndio wakakimbilia hapa walipo sasa, walipofika wakafikia kwa madada poa mjini bahati mbaya kwao hilo eneo kuna tajiri mmoja amelinunua akatimua wote. Katika kuhangaika wakaishia kwenye hiki kigrocery mshenzi kwasababu tu wapate sehemu ya kulaza mbavu na kula.

Joyce anasema kwa sasa anajenga kwao kwa hivi visenti anavyovipata kwa wadhamani kama sisilakini anamaisha magumu kuna wakati naenda pale namkuta amekaa na mawazo inabidi nimunulie bia na msosi anasema kuna siku huwa analala njaa bahati mbaya Joy hapendi kuomba hela na hata ukipita nae kama usipompa basi hatokuomba kabisa.

Baba wa mtoto kamwambia ampe mtoto amsomeshe shule ya maana, yeye alikuwa hataki na kuna siku alitumiwa nauli ampeleke akaila. Nimemshauri ampeleke mtoto sasaivi ana miaka miwili na nusu tena jamaa kamwambia ili mtoto wake awe salama zaidi atampeleka kwa shangazi zake na sio kwa mke wake.

Jamaa mjeda aliyekuwa mume wa Joyce kama atabahatika kusoma kisa hiki atakumbuka mbali sana, namwambia tu alifanya mazuri kwa upande wake kumnyanyua Joyce lakini demu akazingua nadhani si mimba tu iliyosababisha haya labda kuna mengi nyuma ya pazia ila ajue kabisa karma has fulfilled its duty Joyce sasa hivi anauza bar na kudanga huku kwa wachimba dhahabu

Nimemaliza, msinisumbue kuomba namba ya Joyce alipo hapa anaishi kwa wasiwasi Mandonga wa Kibondo anamsaka sana yeye kadanganya ameenda Chalinze kwa mumewe japokuwa jamaa ni kama limeshtuka baada ya kuona mtoto wa Joyce bado yupo hapo Kibondo.
View attachment 2451031


Ila we jamaa
 
Back
Top Bottom