Kipimo sahihi cha mapenzi ni kuvumilia mapungufu

safuher

JF-Expert Member
Feb 11, 2019
11,170
15,851
Mapenzi ukitaka kuyapima basi angalia tu kuhusu mabaya kama unaweza/anaweza kuyabeba na kuyavumilia.

Asili yetu binadamu tumeumbwa na mambo mazuri na kupenda mazuri,hivyo mtu akikupenda kwa mazuri tu huyo hajakupenda bali ndio asili yake tokea kuumbwa.

Kuna watu wanadhani mfano mwanaume kukupenda basi akusaidie fedha,,akusaidie kazi,akuhurumie,awe mpole na kadhalika.

Hivi sio vipimo sahihi vya mapenzi. Kwa sababu wapo wanaume wanaweza kuwa wanahuruma kwako laikni huruma katoka nayo kwao ndio nature yake. hivyo atakuwa na huruma hata kwa asiyekuwa wewe.

Hivyo huruma yake sio kwa sababu anakupenda wewe,bali huruma yake ni kwa sababu roho yake ndivyo ilivyo hata kabla ya kuwa na wewe.

Wapo wanaume watakuwa wapole lakini upole wake sio kwa sababu kakupenda bali kwa sababu kazaliwa ama kalelewa hivyo.

Hivyo upole wakesio kwa sababu anakupenda bali ni kwa sababu ndio alivyo hata kabla yako,usijione kwamba anafanya kitu cha pekee kwako kumbe hata kwa wengine anafanya hivyo.

Wapo wanaume wanaweza kukusaidia kazi zako za nyumbani n.k,lakini anakusaidia sio kwa sababu anakupenda bali ndo kalelewa ama kakulia hivyo.

Kwa hiyo hapo usiseme kuwa anakuoenda kwa kuona anakufanyia kazi,bali anafanya hizo kazi kwa sababu moyo wake ndo upo hivyo tokea hapo.

Sasa unaweza kukutana na mwanaume ukadhani tabia zake anazofanya anafanya kwa kukupenda kumbe anafanya kwa sababu ndio tabia zake hivyo atamfanyia kila mtu.

Kwahiyo sio sawa kusema kuwa mtu fulani anakupenda kwa kuangalia matendo yake kumbe huyo mtu bwana ndo tabia yake iko hivyo.

Kwa mtu wa aina hii ni ngumu kung'amua kwa vipi anakupenda. Ili ujue kakupenda usiangalie anakufanyia nini. Ili ujue kakupenda angalia anayavumilia vipi mapungufu yako.

Mapungufu ndio msingi wa kuyajua mapenzi.


Karibu kwa mjadala.
 
Bonnge moja la point.........unakuta mtu yuko kwenye mahusiano anachanganywa na mazur tu haangalii mabaya mwisho wa siku wakiingia kwenye ndoa ndo mziki unaanzia hapo anaanza kutiatia huruma as if watu walimchagulia mume au mke

Mm hata kabla cjakudate lazima nijue ww weakness zako ni zipi na niangalie kama nitaweza kuzivumilia au siwez kama siwez kaa mbaliiii!!!!labda tuchangamshe viungo tu
 
Bonnge moja la point.........unakuta mtu yuko kwenye mahusiano anachanganywa na mazur tu haangalii mabaya mwisho wa siku wakiingia kwenye ndoa ndo mziki unaanzia hapo anaanza kutiatia huruma as if watu walimchagulia mume au mke

Mm hata kabla cjakudate lazima nijue ww weakness zako ni zipi na niangalie kama nitaweza kuzivumilia au siwez kama siwez kaa mbaliiii!!!!labda tuchangamshe viungo tu
Sahihi kabisa mzee baba.

Manake ni kuwa kujua tabia za mpenzi wakati wa uchumba ni vigumu kwa sababu mna muda m hache wa kuwa pamoja.

Ili ujue tabia za mtu lazima uwe nae muda wmingi kama ni suala la kujua kutoka kwake
 
Mapenzi ukitaka kuyapima basi angalia tu kuhusu mabaya kama unaweza kuyabeba na kuyavumilia.

Asili yetu binadamu tumeumbwa na mambo mazuri na kupenda mazuri,hivyo mtu akikupenda kwa mazuri tu huyo hajakupenda bali ndio asili yake tokea kuumbwa. Kuna watu wanadhani mfano mwanaume kukupenda basi akusaidie fedha,,akusaidie kazi,akuhurumie,awe mpole na kadhalika.

Hivi sio vipimo sahihi vya mapenzi. Kwa sababu wapo wanaume wanaweza kuwa wanahuruma kwako laiini huruma katika nayo kwao ndio nature hivyo atakuwa na huruma hata kwa asiyekuwa wewe.

Wapo wanaume watakuwa wapole lakini upole wake sio kwa sababu kakuoenda bali kwa sababu kazaliwa ama kalelewa hivyo. Wapo wanaume wanaweza kukusaidia kazi,lakini anakusaidia sio kwa sababu anakupenda bali ndo kalelewa ama kakulia hivyo.

Sasa unaweza kukutana na mwanaume ukadhani tabia zake anazofanya anafanya kwa kukupenda kumbe anafanya kwa sababu ndio tabia zake hivyo atamfanyia kila mtu.

Kwa mtu wa aina hii ni ngumu kung'amua kwa vipi anakupenda. Ili ujue kakupenda usiangalie anakufanyia nini. Ili ujue kakupenda angalia anayavumilia vipi mapungufu yako.

Mapungufu ndio msingi wa kuyajua mapenzi.

Karibu kwa mjadala.
Umenifikilisha mkuu
 
Bonnge moja la point.........unakuta mtu yuko kwenye mahusiano anachanganywa na mazur tu haangalii mabaya mwisho wa siku wakiingia kwenye ndoa ndo mziki unaanzia hapo anaanza kutiatia huruma as if watu walimchagulia mume au mke

Mm hata kabla cjakudate lazima nijue ww weakness zako ni zipi na niangalie kama nitaweza kuzivumilia au siwez kama siwez kaa mbaliiii!!!!labda tuchangamshe viungo tu
Kuna watu wanaongea vitu sivyo sana kwenye mitandao.

Kuna mmoja anajulikana kwa jina maarufu la dokta fulani ati anasema mwanaume anaekuoenda atakuhurumia na kukuheshimu.

Hivi hajui kama kuna wanaume hizo ni tabia zao tokea utotoni hata akutane na mtu asiyemjua bado atakuwa na hizo tabia ?

Labda angefafanua kwamba kukuheshimu ni dalili ya mwanaume anayekupenda ikiwa tu mwanaume huyo asili yake hana adabu na heshima katika maisha yake yote
 
Na hayo Mapungufu ni yapi, je yanavumilika ? Kisa unapendwa na mapungufu yako yakawa unakuwa mgegedwaji/Mgegedaji nje haswa, je uvumiliwe tu kisa mtu kakupenda ?

Hata mpendaji huchagua ya kuvumilia, so be specific, “MApungufu ya kuvumiliwa ni yapi “

Msiwabebeshe wapendaji kuvumilia vit vya Ajabu
 
Na hayo Mapungufu ni yapi, je yanavumilika ? Kisa unapendwa na mapungufu yako yakawa unakuwa mgegedwaji/Mgegedaji nje haswa, je uvumiliwe tu kisa mtu kakupenda ?

Hata mpendaji huchagua ya kuvumilia, so be specific, “MApungufu ya kuvumiliwa ni yapi “

Msiwabebeshe wapendaji kuvumilia vit vya Ajabu
Ni mapungufu yote ambayo utaweza kiyavumilia hayo ndo niliyoyakusudia.

Kama kuna mapungufu huwezi kuyavumilia basi hayo mimi sijayakusudia.

Kwa sababu kuna mapungufu ambayo mimi ntayaona hayavumiliki lakini wengine wanaona yanavumilika.

Mfano kuna mwanaume namfahamu laiwahi kuchapiwa mkewe kwa kumfumania,mimi na wewe tungeona haivumiliki lakini jamaa baada ya muda akarudiana na mke wake.

Kwa hiyo siwezi kuwa specific katika hili kwa sababu hatuko katika level moja ya namna ya kuyapokea matukio ya kimaisha.

Mwingine anaona hawezi kuishi na mume bahili,wakati huo mwingine anaweza kuishi nae.

Kwa hiyo kila mapungufu ambayo utaweza kuyavumilia hayo ndio ambayo nimeyakusudia.
 
Kuna mapungufu yanayozuilika na mapungufu ambayo kiukweli hayavumiliki. Na kuna wengine wanajipa moyo kuwa wakiingia kwenye ndoa mtu ataacha kunywa pombe, au ataacha tabia ya kuwatokea vibinti vya chuo! Tunavumilia na baadaye tunakuwa watumwa. Naona nimekuzoea na pengine siwezi kuwa single, so najilazimisha kubeba madhaifu yako ambayo kwangu ni ngumu kuyabeba. As a result; chuki, kurogana, kuuana, na mateso mengi.
 
Back
Top Bottom