Kipi kikomo cha kusalimia shikamoo?

Kipi kikomo cha kusalimia shikamoo?

Samahani

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
237
Reaction score
355
Habari za majukumu wana jamvi...

Natamani mnipanue fikra kidogo juu ya hii heshima tuliyoizoea ya kusalimiana "SHKAMOO". Kwa jamii yetu Tanzania, matumizi ya salamu hii ni ishara mojawapo ya utii na heshma kwa aliyekuzidi umri. Lakini natamani kujua, MTU ANAPOFIKIA UMRI GANI ANAPASWA KUACHA KUITUMIA?? Nimejaribu kufutilia kwa sisi watu wazima, kuna wakati hatuitumii tena na badala yake tunatumia aina nyingine ya salamu za kujuliana hali... Naomba kuelewa, ni upi wakati sahihi wa kuacha kuwasalimia waliotuzidi "SHIKAMOO?"
 
Mkuu salamu haina muda wa kuachwa kutumika hata uwe na miaka 80 kuna watu bado ukikutana nao utatii na kuwasalimia... Sema hii SHIKAMOO imesimama kiutumwa utumwa tofauti na kusema Assalamu-alaykum, hii haibagui mtoto, wala mkubwa wote tutasalimiana hivyo hata uwe na mvi mwili mzima!
 
Kama ni mwislamu salimia asalaam aleykum, kwa mkristo bwana asifiwe, kwa ndugu salimia kilugha, ukikutana na wajivuni salimia kidhungu inatosha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Naunga hoja mkono.

Binafsi huwa naona mzigo sana kusalimia mtu ''Shikamoo", natumia salamu za kidini, habari yako, habari za saa hizi, habari za asubuhi, habari za mchana, habari za jioni, mambo nk. kulingana na aina ya mtu.

Kuna wengine wanamind sana wasiposalimiwa ''Shikamoo", kuna mmoja alinimid akaniuliza kwa nini hunisalimii ''Shikamoo" nikamwambia nimezoea kusalimia hivyo(nilimsalimia habari za asubuhi), akaniambia ''mimi sio mdogo(yaani yeye)" nikamwambia ''sawa" na nikamshukuru kwa kunikumbusha japo moyoni nilikereheka. Kwa sasa kila nikikutana naye namsalimia hivyo anavyopenda.

Japo salamu inaonesha heshima miongoni mwa jamii, ni vyema kusalimia kulingana na hali/hadhi ya mtu, wengine hawapendi kusalimiwa Shikamoo na wengine wanapenda.
 
Tuliowengi shikamooo kutoa au kupokea n taab sanaaaa...hiii salam kwanza ya kitumwa mataifa mengine wanaozungumza lugha tofaut hakuna iki kitu.
 
Mimi nashangaaga kwakweli unakuta mtu mzima kabisa unamsalimia shkamoo yeye haipokei shkamoo yako badala yake anakuambia za sahizi au mambo...nakasirika
Au mwingine anakuwahi kukusalimia utasikia"habari za saahizi "hata Kama wewe ndiyo ulipaswa umuanze, yote hiyo kukwepa shkamoo halafu ni mtu mzima kabisaa mfyuuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo ukifika miaka 24 humsalimii tena baba ako wala mama yako???? Mamaeee hivii Jf imekuwaje siku hizi mbona kuna watu wana akili fupi sanaa...??? At lst useme 60 huko ushakuwa babuu... Yani hata 50 bado utasalimia wenye 80... Ila dar wakubwa hawapendi shikamoo so usipoteze muda wako kusalimia watu Mabarabarani hukoo... Mkoani ndo kuna habari za shikamoo sanaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nini asili ya hii salamu? nini maana ya neno "Shikamoo?" tukipata hayo majibu nadhani ndio tutapata conclusion ya kuitumia hii salamu au tusiitumie,haijalishi huyu ni mkubwa au mdogo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom