Kipi kifanyike kwenye kilimo?

Kipi kifanyike kwenye kilimo?

Taasisi za kifedha pia zimegoma kuwa rafiki wa mkulima, mkulima hakopesheki akikopesheka basi kwa masharti lukuki, sector za kifedha zimulike fursa zilizopo ktk kilimo ili kuwawezesha wakulima kufanya kufanya kilimo chenye tija.
Kilimo cha mkulima wa mvua kwa sasa, labda wapewe ruzuku na serikali. Hakikopesheki
 
Haya Sasa ndiyo mambo ya Kujadili! Sema Sahv watanzania asilimia kubwa akili, mawazo yao wako kwenye mambo ya udaku bongo fleva bongo movie..

Ngoja turudi kwenye uzi Sasa-
Kwanza lazima mtambue kuwa sekta ya kilimo Tanzania inachangia karibia asilimia 29 ktk uchumi wa tanzania
Kuna vikwazo vingi Ambavyo vinarudisha nyuma au kukwamisha sekta ya kilimo Tanzania, mfano uhaba wa pembejeo ambazo hazitoshelezi, mbegu nazo hazina ubora, mbolea napo kizungumkuti, madawa nayo kasheshe...., kingine Kuna changamoto ya masoko
KITU KINGINE NILICHO KIONA KAMA SERIKALI INATAKA NCHI IPIGE HATUA KUBWA KWENYE KILIMO, waje na sekta 1 au 2 Yaani sekta dume
Wahamasishe watu, wakulima kulima sana mazao 1 au 2 kwa kiasi Kikubwa Mf mahindi, mpunga na hayo mazao ndiyo yatiliwe mkwazo snaaa
Huku wengine wakilima mazao mngine kama kawaida
Hapo ndipo kutaonekana na kupata mafanikio

Ova
Kuna hoja 2 muhimu katika maelezo yako.
1. Ubora wa pembejeo.
Si kweli kwamba pembejeo hazipo, zipo nyingi sana. Tatizo lipo kwenue ubora kuwa mdogo hali inayopelekea mkulima kutojua ni zipi nzuri na zipi aachane nazo.
Nini kifanyike.
Serikali kusimamia kwa utahbiti uingizwaji na uzalishaji wa pemebejeo bora ili kupunguza utitiri wa pembejeo sokoni huku nyingi zikiwa hazifai.
2. Kutenga kanda za uzalishaji.
Endapo kutakuwa na kanda za uzalishaji (Production Zones) ambazo zitasimamiwa kiufasaha kuanzia:-
a). Elimu ya uzalishaji & udhibiti wa magonjwa na visumbufu.
b). Elimu ya uongezaji thamani ya mazao.
c). Mfumo wa masoko kuboreshwa.
d). Kuchagua mazao machache muhimu katika kanda husika na kuyasimamia kikamilifu ikiwa ni pamoja na kuimarisha masoko.

Haya yakifanyika kwa ufasaha, kero za waKulima zitapungua na tija kuongezeka.
Anywa, itoshe kusema kila eneo la uzalishaji lina changamoto tofauti na jingine na utatuzi wake pia kutofautiana.
 
Nafikiri hujawahi kulima ndio maana unasema hvyo. Mazao mengi sana hayana soko la uhakika japo hayazalishwi kwa wingi sana, Sasa yakizalishwa kwa wingi tena itakuwaje? Na ukumbuke hayazalishwi kwa wing sana coz pia wengi wenye mitaji wanakikwepa kilimo. Miaka mingi kilimo kinajiendesha chenyewe tu, kusiwepo na ruzuku watu wanalima ila mwisho masoko yanakuwa ishu. Angalia matunda na mbogamboga, mahindi, mpunga, mbaazi n.k
Katika kilimo inaweza kuwa tofauti kidogo.

Ukiwa na bidhaa kubwa ndipo inakuwa rahisi kupata soko kuliko kama utazalisha kwa kiwango kidogo.

Urahisi wa kutafuta soko la kilo 40 za Ufuta au Alizeti ukiwa kijijini ni kwamba utaishia kutegemeo wanunuzi waliokuzunguka.
Ukibadili hizo kilo kuwa tani....say tani 40, ni kiasi ambacho soko litakutafuta wewe
 
Hello JF,

Hii ni moja ya kati za threads zangu za mwisho mwisho..LOL

I am trying to cut my time spending browsing JamiiForums...

So far, i am doing great, sijapost chochote in four days..LOL.....

Anyway,

Ningependa kujua nini kinachokosekana kwenye Kilimo chetu???

Ili kiwe chenye tija kwa manufaa ya watanzania....????

Tuna depend kwenye Kilimo, yet nahisi hili ni eneo moja ambalo halijawa exploited fully...

Again, tu brainstorm wapi pana tatizo..

Thanks all..
Habari Dada !

Nipende kuchangia kuhusu kilimo chetu kimapungufu.

1. Soko la bidhaa zilizopo ni dogo - Hapa hakuna anayevutiwa kuendelea kuwekeza au kuweka juhudi kubwa.

2. Sera ya kilimo imekaa kisiasa yaani imejaa matumaini hewa - Tuna wataalamu lakini hatuwatumii tunajiongoza wenyewe kwa uzoefu, tamaa ya mafanikio au kwaajili tu wakati mwingine kujipatia chakula pasipo maana. Mfano; Huwezi kuwa mgonjwa wewe, dawa ujue wewe, kujitibu ujitibu wewe na mwisho hujui kama umepona au unaumwa.

3. Viongozi wa nchi hawana macho (vipofu katika kilimo) - Hapa nikuambie Dada yangu hawa viongozi tulionao ni vipofu nakuhakikishia kuanzia Afisa mtendaji wa Mtaa/ Kijiji mpaka Raisi wa nchi hii. Sababu kubwa ni kwamba ardhi kuu tuliyonayo na idadi ya watu tuliopo tunaishi kwa kutegemea chakula 90% maisha yetu cha ajabu wao wamekalili majukumu katika utawala na hawatazami kilimo kama jambo zuri na bora hata wao kurahisisha kutawala nchi na watu. Mfano; Pasipo chakula cha uhakika au upatikanaji wa kutosha, wananchi watafanya maovu mengi, wizi na kuuana.

4. Utandawazi hatuutumii kama nchi kujinufaisha nao hususani kimaendeleo kwenye kilimo - Vifaa na mitambo mizuri ipo cha ajabu tunatumia zana za kizamani katika uzalishaji Dada.

5. Ujinga wa kuwekeza mijini miundombinu iliyopaswa iwe mashambani au vijijini palipo kilimo - Dada nikuambie jambo la kustaajabisha hapa, Benki ya kilimo, maduka pembejeo, viwanda vya SIDO, COETECH, wataalamu wa kilimo na takwimu, na vitu vinavyofanana na hivyo vipo mijini ambapo hakuna shamba na hakuna wakulima sasa hapo nchi tutapiga hatua ipi kimaendeleo katika kilimo.

Dada yaani yapo mengi sana ila hayo ndio tatizo nionavyo mimi.
 
Kibinafsi soko linashida kubwa hapa Tz. Mkulima anapunjwa sana.

Heb imagine mkulima amelima tikiti mwisho wa siku anakuja mlanguzi ananunua kwa bei ya 1000 had 2000. Mlanguzi anaenda kuuza kuanzia 3000 had 5000.

Yani mkulima kaangaika siku 90 yani kaandaa shamba, kanunua mbegu , kapanda, kamwagilizia, kanunua madaw na hadi zikafikia kuvunwa.

Ila jamaa anayenunua kupeleka sokoni anapata faida mara mbili ya mkulima.
 
Nakubaliana na wewe lakini hebu angalia kahawa ilivyopotea na uzalishaji ulkuaga mkubwa sana, angalia mbaazi, korosho n.k kilichofanya watu wapunguze au kuacha kulima ni soko tu.
 
Nyie mnaolilia soko tafadhali mjikite kwenye mazao ya biashara pekee, chakula kikipanda bei hata hao ‘wakulima’ watashindwa kumudu na kuishia kulialia.

Endeleeni kujadili, naendelea kujifunza.
 
Ukinicheka shambani ,nakucheka sokoni.duh siku hizi haipo hivyo,Kuna changamoto kubwa kwenye masoko.unatumia nguvu nyingi ,anafaidika mwingine
 
Katika kilimo inaweza kuwa tofauti kidogo.

Ukiwa na bidhaa kubwa ndipo inakuwa rahisi kupata soko kuliko kama utazalisha kwa kiwango kidogo.

Urahisi wa kutafuta soko la kilo 40 za Ufuta au Alizeti ukiwa kijijini ni kwamba utaishia kutegemeo wanunuzi waliokuzunguka.
Ukibadili hizo kilo kuwa tani....say tani 40, ni kiasi ambacho soko litakutafuta wewe
Nyie mnaolilia soko tafadhali mjikite kwenye mazao ya biashara pekee, chakula kikipanda bei hata hao ‘wakulima’ watashindwa kumudu na kuishia kulialia.

Endeleeni kujadili, naendelea kujifunza.
Hapo kwenye woga wa njaa ndio palipochangia pia kudidimiza wakulima. Mnafunga masoko ya nje ili tu kuzuia vyakula vibaki ndani utazan tunawaza kula tu. Fungue masoko watu watalima vingi tu na tutakuwa na chakula cha kutosha
 
Kuna hoja 2 muhimu katika maelezo yako.
1. Ubora wa pembejeo.
Si kweli kwamba pembejeo hazipo, zipo nyingi sana. Tatizo lipo kwenue ubora kuwa mdogo hali inayopelekea mkulima kutojua ni zipi nzuri na zipi aachane nazo.
Nini kifanyike.
Serikali kusimamia kwa utahbiti uingizwaji na uzalishaji wa pemebejeo bora ili kupunguza utitiri wa pembejeo sokoni huku nyingi zikiwa hazifai.
2. Kutenga kanda za uzalishaji.
Endapo kutakuwa na kanda za uzalishaji (Production Zones) ambazo zitasimamiwa kiufasaha kuanzia:-
a). Elimu ya uzalishaji & udhibiti wa magonjwa na visumbufu.
b). Elimu ya uongezaji thamani ya mazao.
c). Mfumo wa masoko kuboreshwa.
d). Kuchagua mazao machache muhimu katika kanda husika na kuyasimamia kikamilifu ikiwa ni pamoja na kuimarisha masoko.

Haya yakifanyika kwa ufasaha, kero za waKulima zitapungua na tija kuongezeka.
Anywa, itoshe kusema kila eneo la uzalishaji lina changamoto tofauti na jingine na utatuzi wake pia kutofautiana.


Thanks mkuu, nimependa hio ya Kanda/production zone..ni kweli hatuwezi collectivelly kulima kwa umoja sababu mazingira tulionayo ni tofauti, 'matunda' Tanga, 'Fishery' pwani, 'Bee-keeping'; Singida na Tabora.. wote tukiwa wazalishaji katika mazingira yetu tutamove on as a nation, sijui haya ya Fishery yanafall under Kilimo?? LOL...

Katika mada hii nimeuliza specific Elimu ya Kilimo ihusu nini,naona umejibu A na B, thanks mkuu........

Hii ya kuchagua mazao machache muhimu naona imejirudia, binafsi naona, tuangalie nini kinahitajika ndio tulime na sio kwamba tulime ndio tuangalie soko linahitaji nini.....kuna mazao Demand yake haikauki kama Kahawa, sema tu hatuna FLOW nzuri ya watendaji,kutoka mkulima mpaka consumers... hapo katikati kuna watu wana interests zao.. very sad
 
Umaskini ndio sababu, tunatumia products za kutoka nje nyingi sana inapekelea kunufaisha viwanda vya nje,
Lakini ukija kwenye kile kinachozalishwa nchini kwetu, hakina thamani kwa sababu soko lake ni kumuuzia maskini mwenzako tu, na mbaya zaidi mazao ya kilimo unapochelewa kutoa ghalani ndipo ubora unazidi kupungua.
 
Umaskini ndio sababu, tunatumia products za kutoka nje nyingi sana inapekelea kunufaisha viwanda vya nje,
Lakini ukija kwenye kile kinachozalishwa nchini kwetu, hakina dhamani kwa sababu soko lake ni kumuuzia maskini mwenzako tu, na mbaya zaidi mazao ya kilimo unapochelewa kutoa ghalani ndipo ubora unazidi kupungua.
Hatufanyi processing baada ya kuvuna. "Post harvesting technologies" ziko poor sana.

Kingine tunachotakiwa kufahamu, si kweli kwamba mazao yetu hayana thamani. Sisi ndio tunayakosesha thamani kwa kikosa uelewa.

Tunazalisha mazao yenye thamani kubwa kutokana na matumizi madogo ya madawa yaani viuatilifu ukilinganisha na mataifa mengine hasa yaliyoendelea.
Ndiyo maana baadhi wameona fursa kwa kuzalisha mazao kwa njia za kibaiolojia na kuuza nje kwa mikataba.

Mfano. Kahawa Kilimanjaro wapo wanaofanya hivyo.
Mazao ya bustani huko Lushoto nk.
 
Thanks mkuu, nimependa hio ya Kanda/production zone..ni kweli hatuwezi collectivelly kulima kwa umoja sababu mazingira tulionayo ni tofauti, 'matunda' Tanga, 'Fishery' pwani, 'Bee-keeping'; Singida na Tabora.. wote tukiwa wazalishaji katika mazingira yetu tutamove on as a nation, sijui haya ya Fishery yanafall under Kilimo?? LOL...

Katika mada hii nimeuliza specific Elimu ya Kilimo ihusu nini,naona umejibu A na B, thanks mkuu........

Hii ya kuchagua mazao machache muhimu naona imejirudia, binafsi naona, tuangalie nini kinahitajika ndio tulime na sio kwamba tulime ndio tuangalie soko linahitaji nini.....kuna mazao Demand yake haikauki kama Kahawa, sema tu hatuna FLOW nzuri ya watendaji,kutoka mkulima mpaka consumers... hapo katikati kuna watu wana interests zao.. very sad

Thanks mkuu.

Kuhusu Elimu ya kilimo yapo mengi sana, cha msingi ni wakulima kuwezesha Elimu ya msingi ya uzalishaji huku lengo likiwa kupata mavuno Bora na kwa kiwango chenye tija. Kulenga kupunguza gharama za uzalishaji pamoja na njia za kuepuka madhara ya kemikali za Kilimo...zina madhara makubwa ila wengi hupuuza aidha kwa kutojua au kutoona umuhimu.
 
Uko sahihi mkuu,sisi kama wananchi hatuna muamko, inabidi tubadilishe mindset zetu kwanza...kilimo kinaonekana ni cha wachache waliofeli maisha , i guess Kilimo kiwe introduced slowly kwenye curriculum za wanafunzi..by the time wanamaliza shule wanakua na msimamo postive kuhusu kilimo.....

Question is; huko shuleni tutawafundisha nini kuhusu kilimo?? mkuu embu tiririrka..lol


Unategemea wajifunze nini wakati hata somo la agricukture(kilimo) haifundishwi siku hizi mashuleni!!
 
Kifundishwe, kisimamiwe kitaalamu na kisasa, kivipi?
-Elimu sahihi kuhusu zao husika itolewe kwa wenye nia ya kulilima.
-Wataalamu wa hilo zao, wawe karibu na wakulima, waeleze muda wa kupanda, kupalilia, kuweka dawa n.k.
-Vifaa vya kisasa vya kusafisha ardhi, upandaji, umwagiliaji, kuweka dawa, uvunaji na kuhifadhi mazao vipatikane madukani na vitumike mashambani.
-Serikali au taasisi kama Tanzania Farmers Association, tccia, viandae na kuvutia masoko ya mazao, visimamie bei rasmi zenye kuwanufaisha wakulima.
-Mabenki na taasisi za kifedha, yatoe mikopo nafuu kwa wakulima, ili wajizatiti katika vifaa vya kisasa vya kilimo na uvunaji, usafiri na wajijengee maghala ya kisasa (yenye viyoyozi au vipuliza upepo), ili waweze kusindika na kuhifadhi mazao kwa muda mrefu, wanunue na kuweka vizalisha umeme (electric generators) au vizalisha umeme kwa njia ya jua n.k.
-Taasisi kama vyama vya ushirika vishirikiane na serikali na wakulima, vipiganie maslahi ya wakulima, hasa linapokuja suala la kodi, bei za mazao, bei za pembejeo n.k.
 
Hello JF,

Hii ni moja ya kati za threads zangu za mwisho mwisho..LOL

I am trying to cut my time spending browsing JamiiForums.

So far, i am doing great, sijapost chochote in four days..LOL.

Anyway,

Ningependa kujua nini kinachokosekana kwenye Kilimo chetu?

Ili kiwe chenye tija kwa manufaa ya Watanzania?

Tuna depend kwenye Kilimo, yet nahisi hili ni eneo moja ambalo halijawa exploited fully...

Again, tu brainstorm wapi pana tatizo..

Thanks all..
Tatizo lipo kwa wakulima wenyewe, wanashindwa ku-anticipate zao gani walime wakati gani, yaani unakuta wakisikia nyanya ziko juu woooote wanaingia mkenge, mwishowe zinaoza mashambani, wakati huo huo parachichi zinaadimika na bei kupaa, hawana akili inshort
 
Tatizo la kilimo chetu hapa nchini ni kwamba kila mmoja anategemea ni jukumu la mwingine ama kikundi fulani na kwamba yeye binafsi halimgusi na ndiyo maana kuna watu wengi sana wamehitimu vyeti,astashahada,shahada, uzamili/lisensiati na wengine kwa kiwango cha Uzamivu katika kilimo na taaluma zinazoshabihiana na kilimo ila wameshindwa hata kuandaa mpango mkakati wa kututoa tulipo.
Kongole kwa dada yetu #JanethMaro ambaye ni mwanzilishi na C.O wa Sustainable Agriculture Tanzania (SAT) kwa kuamua kuonesha kwa vitendo maana ya kilimo,

 
-Tatizo kubwa ni upungufu za mbegu bora ambazo zinaweza kuwa na soko kimataifa.
-Kilimo cha kisasa hakijatiliwa mkazo,serikali iongeze ruzuku kuinua kilimo cha kisasa eg.Greenhouse farming,Irrigation farming
-fluctuation of market price on agricultural produce,discourages heavy investments.
 
Rebeca na wenzako tunapoona tatizo daima tuanatarajia wengine walitatue. Hili nalo ni tatizo la msingi. It's time we realized that we are the people we have been waiting for.

Waliotafuta fursa ya kuuza mbaazi na korosho nje walifanya vyema. Serikali iache kuingilia kwani haina ufumbuzi.

Uhuru wa mkulima kufanya atakalo na mazao yake ni muhimu. Akipenda kuuza nje ruksa. Akipenda kuuza mahindi mabichi ruksa. Akitaka kuyatengenezea kimpumu au kiamble mahindi yake ruksa. Serikali iache kuwakalia wakulima shingoni. Uhuru utaleta ubunifu na uthubutu wa kujitafutia masoko wenyewe.

Mboga mboga, matunda na maua vina soko, lakini sio la kutafutiwa na serikali. Kuna mfano mzuri wa mfanyabiashara aliyepata fursa ya kuuza nyama ya mbuzi Uarabuni. Fursa kama hizo ni nyingi. Kinachotakiwa ni elimu safi, uthubutu, na serikali kuacha wafanya biashara wafanye biashara.

Serikali iweke sera wezeshi kisha ikae pembeni.
 
Back
Top Bottom