Kingunge: Hatutokubali Lowassa akatwe jina

Kingunge: Hatutokubali Lowassa akatwe jina

olwasa pesa inaongoza akili sijui ni mtu wa karne ya ngapi,
 
Siku ya Jumamosi Edward Lowassa alikuwa mkoani Dar kusaka wadhamini wa CCM katika mbio zake za kutaka kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka huu, hapa chini ni baadhi ya ahadi alizozitoa Lowassa mwenyewe mbele ya wanaCCM.

1/Atamaliza tatizo la Miundo mbinu yote ya Dar(Barabara, mifereji, mitaro, mtandao wa maji safi na taka, madampo nk) ndani ya miezi sita tu, toka siku anatangazwa kuwa rais.

2/Atajenga nyumba milioni moja kila mwaka jijini Dar ili
Kuboresha makazi ya wakazi wa Dar.

3/Atajenga urafiki wa karibu na matajiri na maskini.

Source:Gazeti Mwananchi la Jana.
Abunuwasi au Mfalme Juha!?
 
Siku ya Jumamosi Edward Lowassa alikuwa mkoani Dar kusaka wadhamini wa CCM katika mbio zake za kutaka kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka huu, hapa chini ni baadhi ya ahadi alizozitoa Lowassa mwenyewe mbele ya wanaCCM.

1/Atamaliza tatizo la Miundo mbinu yote ya Dar(Barabara, mifereji, mitaro, mtandao wa maji safi na taka, madampo nk) ndani ya miezi sita tu, toka siku anatangazwa kuwa rais.

2/Atajenga nyumba milioni moja kila mwaka jijini Dar ili
Kuboresha makazi ya wakazi wa Dar.

3/Atajenga urafiki wa karibu na matajiri na maskini.

Source:Gazeti Mwananchi la Jana.

Madabida lzma amtayarishie umat wa watu anajua ukawa wakiingia kesi yakeya kendesh kwanda cha kutngeneza ARV fake itafufuka
 
Nawaheshimu sana wazee, maana wazazi wangu wamepitia hatua hiyo, na mie najua nitapitia, Mungu akibariki. Hata hivyo ni ukweli usiofichika kwamba ule msemo "kuna watu wanazeeka vibaya" unakuwa kweli sana ninapochunguza kauli za Kingunge kuhusu uteuzi wa CCM wa mgombea uraisi.

Nimeshindwa kabisa kumwelewa mzee huyu, na ninachoweza kusema ni kwamba pengine Kingunge anazeeka vibaya.

Wengi tunajua Kingunge, licha ya kuwa kiongozi wa CCM, ni kiongozi wa "kitaifa", na katika hili amejijengea heshima kubwa kwa muda mrefu. Ninachoshindwa kuelewa ni kwa nini huyu mzee ameamua kuiweka heshima yake rehani kwa kuwa msemaji wa kambi ya Lowassa?

Mie nilitarajia Kingunge angekuwa muwakilishi na mshauri wa wagombea wote wa CCM, badala ya kujikita katika kambi moja tu ya Lowassa, ukizingatia historia yake Kingunge katika uongozi wa CCM na kitaifa. Hivi amewaza nini huyu mzee na kuamua kuwa sambamba na Lowassa?

Na mbaya zaidi, kwa namna moja au nyingine ameamua kuendeleza ule mkakati wa kuishinikiza na kuitishia nyau CCM ili kumteua Lowassa kama mgombea wao wa uraisi. Amefikia kudiriki kuonyesha kwamba CCM wasipomteua Lowassa basi CCM itafia awamu ya nne! Hivi Kingunge haelewi kwamba lolote analolisema sasa, ushauri au maonyo yeyote anayoyatoa hadi sasa kuhusu CCM watu wote wenye akili wanaona kabisa yanalenga kumsaidia mgombea wake aliyeamua kwa sababu anazozifahamu yeye, kupalilia njia ya kuelekea hiyo inayosemwa safari ya matumaini?

Lowassa amemuahidi nini Kingunge hadi mzee wa watu aamue kujishusha hadhi kisiasa kwa kiasi hiki?

Watu wote wenye akili wangeona labda Kingunge anaongea jambo la maana ikiwa angesema haya anayosema dhidi ya CCM bila kuwa amejiweka kambi ya mgombea mmojawapo wa CCM, Lowassa. Kinyume cha hapo ni kwamba Kingunge anadhani viongozi wa CCM wana upeo mdogo sana wa kufikiri na kutambua anachofanya, kwamba anatumiwa na Lowassa kuishinikiza CCM. Sidhani kama mbinu hii itamsaidia Lowassa au Kingunge mwenyewe.

Anachofanya Kingunge ni usaliti wa kiwango cha juu kwa CCM, na CCM inapaswa kutambua hilo. Kingunge anataka kuleta mgawanyiko mkubwa ndani ya CCM ili tu amnufaishe Lowassa. Ameamua kwamba liwe na liwalo, the end justifies the means. Kama JK bado hajamuita Kingunge na kumweka sawa bila kumuonea aibu, basi ningeshauri JK afanye hivyo haraka sana, kabla huyu mzee hajawaharibia CCM hata zaidi.

Ushauri wangu kwa Kingunge ni kwamba baada ya haya yote uliyofanya, makosa makubwa sana ya kisiasa, nenda kijijini ukakae kimya huko na kuwa mjamaa halisi, kama ambavyo siku zote ulijionyesha kwa Nyerere, kwamba wewe ni zaidi ya mjamaa.
 
Ha ha ha! Mkuu Mchambuzi, acha fujo. Tunahitaji CCM na UKAWA vilivyo na nguvu, sasa hawa kina Kingunge wanapopotoka tunahitaji kuwaeleza ukweli, hata kama sisi ni watoto sana kwao.

Tunahitaji CCM iliyovipande vipande.Kansa iliyonayo hatutaki tena kuendelea kuitibu,maana madaktari wamesema kuipasua tu ndiko kutaifanya CCM iendelee kuishi bila hivyo itakufa,bora ibaki ikijikongoja kuliko ife kabisa.Wazee wanasema ADUI mwombee UHAI ili azidi kuishi aone Mungu anavyokubariki ..........................
 
Kingunge ameanzakujidhihirisha kuwa siyo mtu msafi pamoja na kwamba ana jifanya kuwa ni mfuasi wa itikadi za Nyerere.

Kitendo cha kumuunga mkono Lowassa mtu ambaye moja kwa moja ni mtuhumiwa wa ufisadi ni ishara mbaya kwake kuwa siyo mtu muadilifu hata kidogo.

Siyo kwamba ana muunga mkono Lowassa kwa kuwa ni mtu anae faa kuwa kiongozi bali ana muunga mkono Lowassa,kwa kuwa Lowassa ni fisadi na Kingunge ni fisadi na hakuna anae weza kuchukua maamuzi magumu ya kumulinda fisadi mwenzake isipokuwa ni Lowassa peke yake.
 
Yaani tunahangaika na mzee huyu kweli tuko serious, yaani kingunge aongee jambo ulitilie maanani na kutaka tulijadili hapa kha!ama kweli tuna muda wa masikhara!Yule mzee ukimwangalia anapoongea, ukimsilikiza anachoongea unajua kabisa hayuko sawa!Sitaki kumvunjia heshima kwamba "kawa chizi" hapana, ila ndhani uzee umepunguza upeo wake wa kupambua mambo na kujikuta anarudi utotoni kabisa na ushabiki wa kitoto kama watoto wengine!
 
Tunahitaji CCM iliyovipande vipande.Kansa iliyonayo hatutaki tena kuendelea kuitibu,maana madaktari wamesema kuipasua tu ndiko kutaifanya CCM iendelee kuishi bila hivyo itakufa,bora ibaki ikijikongoja kuliko ife kabisa.Wazee wanasema ADUI mwombee UHAI ili azidi kuishi aone Mungu anavyokubariki ..........................

CCM kama taasisi haina tatizo, na vigezo vya kuanzishwa kwake ni vizuri tu, tena kuliko vigezo vya vyama kadhaa vya upinzani. Tatizo ni kwamba kuna watu ndani ya CCM ambao wanapindisha melongo mazuri ya CCM. Hili ndilo tunataka CCM ilitanbue na kutokukubali kuwa na watu wa namna hiyo.

Chachu ya maendeleo ya Tanzania ni pamoja kuwa na CCM na UKAWA vyenye nguvu. Kimoja kikiwa na nguvu sana zaidi ya kingine haitatusaidia mimi na wewe na mwananchi wa kawaida. Mara ngapi umesikia au kuona CCM wakipitisha utumbo kule Bungeni kwa kuwa tu wao ni wengi kuloko wabunge wa upinzani? Sasa hilo si nzuri kwa CCM, na haliwezi kuwa zuri kwa UKAWA kuwa na nguvu ya namna hiyo pia.
 
Yaani tunahangaika na mzee huyu kweli tuko serious, yaani kingunge aongee jambo ulitilie maanani na kutaka tulijadili hapa kha!ama kweli tuna muda wa masikhara!Yule mzee ukimwangalia anapoongea, ukimsilikiza anachoongea unajua kabisa hayuko sawa!Sitaki kumvunjia heshima kwamba "kawa chizi" hapana, ila ndhani uzee umepunguza upeo wake wa kupambua mambo na kujikuta anarudi utotoni kabisa na ushabiki wa kitoto kama watoto wengine!

Mkuu, labda kwa kuwa wewe umemwona unaweza ukasema hivyo. Lakini kumbuka wengine wengi wanaishia tu kusoma magazetini yale anayoongea, na mbaya zaidi, wengine wanashawishika na kuona yale anayosema kama yan ukweli fulani.

Unajua mwanzoni wengi walimwona Hitler kuwa mpuuzi tu mmoja ambaye alipayuka sana kwenye kuongea. Taratibu akaanza kukuna masikio ya waliomsikiliza, na mwisho wake ikawa ni majuto.
 
Huyu mzee hatuach kabisaa ametuacha pabaya, mashirika mengi yamekufa yye akiwa kiongozi, yeye kama mshauri alishauri nini mpaka akatuacha huku
11393114_1854602138098255_8163957453014648361_n.jpg


1619162_1854602801431522_3157569483259582179_n.jpg
 
Back
Top Bottom