Tetty
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 26,355
- 21,422
CCM kama taasisi haina tatizo, na vigezo vya kuanzishwa kwake ni vizuri tu, tena kuliko vigezo vya vyama kadhaa vya upinzani. Tatizo ni kwamba kuna watu ndani ya CCM ambao wanapindisha melongo mazuri ya CCM. Hili ndilo tunataka CCM ilitanbue na kutokukubali kuwa na watu wa namna hiyo.
Chachu ya maendeleo ya Tanzania ni pamoja kuwa na CCM na UKAWA vyenye nguvu. Kimoja kikiwa na nguvu sana zaidi ya kingine haitatusaidia mimi na wewe na mwananchi wa kawaida. Mara ngapi umesikia au kuona CCM wakipitisha utumbo kule Bungeni kwa kuwa tu wao ni wengi kuloko wabunge wa upinzani? Sasa hilo si nzuri kwa CCM, na haliwezi kuwa zuri kwa UKAWA kuwa na nguvu ya namna hiyo pia.
Upo pamoja na mimi sema kwa maelezo yaliyotofautiana kidogo.Sitaki ife bali ivunjike vunjike ili tupate CCM iliyobora zaidi yaani katika ubora wake na tukiwa na ukawa katika ubora wake lazima tutafika tunakoenda...
Tunahitaji viongozi watakoionea HURUMA nchi yetu,wazalendo,wakweli kwao wenyewe na kwa jamii watakayoiongoza,hatuhitaji tena mafisadi,wanaotembea na pesa kwa ajili ya kupata uongozi.
Kwa sasa ili CCM iwe na nguvu basi lazima ivunjike vipande vipande na muda wake ndiyo huu.............Hata kikombe ukipendacho kikifika muda wake kitavunjika tu.............