King'amuzi cha StarTimes: Dawa yake hii hapa

King'amuzi cha StarTimes: Dawa yake hii hapa

Mimi bado sijanunua hapa sijui hata kipi ni kipi, nasubiri GTV warudi kwa mara nyingine.
 
Heri yenu nyie mie kwenye DSTV, TBCCM haitoi sauti kabisa. kama kuna mtaalamu aje anambie nifanyaje??
 
takatata hii tupa kapuni,kwa nini ujipe stress kwa kitu cha kipuuzi.ngoma fta dish tu basi.bado sjaona umuhimu wa kulipia tv bongo wanaotuuzia hadi fta chanels.
 
kwa ukweli mi naogopa kuchomoa na kuchomeka kwa sababu huenda nikakosa hata hii migandano...! kama kuna aliyejaribu akafanikisha aje atueleze kbla wengi hatujaingia mkenge!

:smash: hahaha hiyo sentensi yako imenichekesha labda ungesema itoe irudishe na siyo chomoa chomeka. hahaha napita tu! mimi niko kwenye FTA:fish2:
 
]Katika nchi ambazo Mungu alizichagua kuwa za majaribio ya jehannum hapa duniani.. Tanzania ni mojawapo.. [/COLOR]Ukiweza kuishi hapa hata jehannum utaishi.. Startimes nawadai lakini cijui niende wapi kudai haki yangu.. Wamenikosesha vpindi vingi.. Sijui nikalalamike wapi..
MUNGU na akusaidie ungundue hitilafu ya hii kauli yako. Pamoja na matatizo mbali mbali yanayoikumba nchi yetu, huwezi ukaifananisha nchi nzuri kama hii na jehanamu (nadhani hujui unachokiongea kuhusu jehanamu).
Haya matatizo tutayamaliza kwa kuwaondoa (kwa nguvu ya umma - kwa amani madarakani ) wale wote walioyasababisha na kuusuka mpya mfumo mzima.
Hili linawezekanana kabisa!
 
MUNGU na akusaidie ungundue hitilafu ya hii kauli yako. Pamoja na matatizo mbali mbali yanayoikumba nchi yetu, huwezi ukaifananisha nchi nzuri kama hii na jehanamu (nadhani hujui unachokiongea kuhusu jehanamu).
Haya matatizo tutayamaliza kwa kuwaondoa (kwa nguvu ya umma - kwa amani madarakani ) wale wote walioyasababisha na kuusuka mpya mfumo mzima.
Hili linawezekanana kabisa!

Ha ha ha.. Mkuu tutaweza unasema haya matatizo tutayamaliza kwa kuwaondoa hao sawa.. Lakini kwa wakati huu bado niko Jehannum.. naendelea kupigwa jua.. kunyimwa mahitaji yangu ya muhimu.. kutokuwa na uhakika wa kufika kesho.. kupangiwa cha kufanya na mbaya zaidi kunyimwa uhuru wangu ambao ni haki yangu ya msingi kabisa..
 
Last edited by a moderator:
Dawa ni kwenda KISIMBUSI chako pale kwenye Ofisi zao za Mauzo Bamaga ukiwa pale kituoni kirushie kule ndani! She@##$( zaoooo
 
mkuu fikiria zaidi jinsi ya kuchakachua ,hii elfu kumi kila mwezi ni balaa
 
nyumba 180,000/= , umeme 30,000/= , maji 60,000/= , takataka 15,000/= , bili ya maziwa ya mtoto 40,000/= usafiri 90,000/= king'amuzi 18,000/=
jumla 433,000/=
bado chakula,
hapo kwenye msosi usiseme kabisaaaa.....

huu mwaka wetu mbele kwa mbele haya maisha lazima tupagawe.
 
kweli hili ndo neno shenzi zao tumechoka.
hatushabikii hapa ila ukweli hata katiba yetu startimes wameikiuka kipengele cha uhuru wa kila mtu kupata habari ,katiba haijaelekeza tuuziwe ,imesema kila mtu ana uhuru wa kupata habari kutoka popote
 
hapa nilipo nina hasira mno. nimelipia ZUKU tangu juzi
hadi leo bado hawajawasha hata sielewi niwafanye nini
nikipiga customer care ni blaa blaa tu.
 
hatushabikii hapa ila ukweli hata katiba yetu startimes wameikiuka kipengele cha uhuru wa kila mtu kupata habari ,katiba haijaelekeza tuuziwe ,imesema kila mtu ana uhuru wa kupata habari kutoka popote

Lakini hawa jamaa (Startimes) wanaweza kuturuka kwenye suala la uhuru wa kupata habari kwa mujibu wa katiba. Kwa sababu katiba hiyo haijafafanua kama ni kupata habari kwa kununua au bure..! Maan unaweza kuwa na uhuru wa kupata habari kwa kununua na pia unaweza kuwa na uhuru wa kupata habari bila kununua habari hiyo...! Rejea vyanzo vingine vya habari za serikali kama magazeti...jamani si uhuru tulionao hapo ni ama kutonunua ama kununua habari iliyomo kwenye magazeti !?

Labda kabla mchakato wa katiba mpya haujafungwa basi hili nalo katiba mpya itabidi iandaliwe kwa namna ya kulitolea ufafanuzi wa kina jambo hili.
 
hapa nilipo nina hasira mno. nimelipia ZUKU tangu juzi
hadi leo bado hawajawasha hata sielewi niwafanye nini
nikipiga customer care ni blaa blaa tu.

Inavyoelekea haya makampuni yote ukiondoa DSTV ni longolongo.. Maana yote yanalalamikiwa sana na hili ndilo tatizo pale viongozi wenye dhamana ya kuhakikisha wananchi tunapata vilivyo bora wanapokuwa na maslahi binafsi..
 
Inavyoelekea haya makampuni yote ukiondoa DSTV ni longolongo.. Maana yote yanalalamikiwa sana na hili ndilo tatizo pale viongozi wenye dhamana ya kuhakikisha wananchi tunapata vilivyo bora wanapokuwa na maslahi binafsi..
hakuna kampuni lenye afadhali yote ni utata mtupu.
 
Kuhusu kuchomoa na kuchomeka chombo kingali kinawaka siyo wazo la kiufundi otherwise unaweza kuharibu chombo.
 
Kuhusu kuchomoa na kuchomeka chombo kingali kinawaka siyo wazo la kiufundi otherwise unaweza kuharibu chombo.

Nina rafiki yangu alipata ajali hali yake ilikuwa mbaya na alifikia hali ya kutokuweza kupumua vizuri, nilishangazwa na uamuzi wa madakitari walichukuwa kifaa kimoja na kugandamiza kifuani mwake, rafiki yangu ghafula akashituka na akawa anapumua vizuri. Baadaye niliwauliza ni dawa gani waliyomwekea rafiki yangu iliyobadilisha hali ya afya yake kuimarika kwa haraka namna ile, waliniambia kile kifaa kina umeme, na kitu walichofanya ni kushitua mwili wake kwa umeme ndiyo maana afya yake iliimarika kwa kasi ya ajabu.

King'amuzi changu kilikuwa ICU nilipokumbuka utabibu aliofanyiwa rafiki yangu, niliamua kukishitua kwa shoti ya umeme na kweli kilishituka na kutoka ICU hadi sebuleni kila mtu akikifurahia hata sasa.

Nawashauri kampuni ya StarTime washitue ving'amuzi vyao kwa shoti ya umeme kabla ya kuvipeleka sokoni.
 
Nina rafiki yangu alipata ajali hali yake ilikuwa mbaya na alifikia hali ya kutokuweza kupumua vizuri, nilishangazwa na uamuzi wa madakitari walichukuwa kifaa kimoja na kugandamiza kifuani mwake, rafiki yangu ghafula akashituka na akawa anapumua vizuri. Baadaye niliwauliza ni dawa gani waliyomwekea rafiki yangu iliyobadilisha hali ya afya yake kuimarika kwa haraka namna ile, waliniambia kile kifaa kina umeme, na kitu walichofanya ni kushitua mwili wake kwa umeme ndiyo maana afya yake iliimarika kwa kasi ya ajabu.

King'amuzi changu kilikuwa ICU nilipokumbuka utabibu aliofanyiwa rafiki yangu, niliamua kukishitua kwa shoti ya umeme na kweli kilishituka na kutoka ICU hadi sebuleni kila mtu akikifurahia hata sasa.

Nawashauri kampuni ya StarTime washitue ving'amuzi vyao kwa shoti ya umeme kabla ya kuvipeleka sokoni.
safi kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom