AFRIKAMOJA
Member
- Aug 11, 2022
- 30
- 37
Ujiji, Kigoma
01 Septemba, 2022
Umoja na mshikamano wa watanzania na Taifa kwa ujumla ni masuala yaliyopewa kipaumbele kabla na baada ya uhuru kupitia vyama vya TANU na Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya viongozi na waasisi wake hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.
Mara kadhaa siasa zenye mwelekeo wa kuwagawa watanzania zimeonekana kukemewa wazi wazi na viongozi wa Chama tawala CCM, wanataaluma wazalendo na waumini wote wa umoja.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Ndg Abdulrahman Omari Kinana akiongea katika kikao cha ndani cha kupokea taarifa za kazi za chama na serikali amesema CCM kimekuwa chama bora na kinachoungwa mkono na watanzania walio wengi kwa sababu nyingi ikiwemo kupinga ubaguzi wa aina zote na kuwaunganisha watanzania.
"CCM kupitia sera zake imejitambulisha kuwa chama kinachojali utu, usawa wa binadamu na umoja kwa maana ya kuunganisha watu pamoja na kupiga vita ubaguzi. Sasa nawashauri viongozi wenzangu, katika uchaguzi unaoendelea kote nchini wakateni viongozi wanaotumia udini, ukabila au ukanda kama sifa ya kupata uongozi maana hao hawafai kuongoza chama chetu. Tuwapime na kuwapa watu uongozi kwa kuzingatia uwezo, sifa na uadilifu wao na sio kwa misingi ya ubaguzi wa aina yoyote." Alisema Kinana
Kinana alilazimika kusema hayo baada ya kupewa taarifa ya kamati ya siasa ya Halmashauri kuu ya mkoa wa Kigoma iliyowasilishwa na Katibu wa CCM mkoa huo Ndg. Mobutu Malima iliyoeleza kumeanza kuibuka hisia za ukabila, udini na ukanda kutafuta uongozi katika uchaguzi unaoendelea ndani ya CCM mkoani humo.
Aidha Kinana amewataka wanachama na viongozi wa CCM Mkoani Kigoma kujua wanao wajibu wa msingi wa kusema na kutangaza mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi unaofanywa na serikali ya CCM Awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ili wananchi wajue nini serikali yao inafanya.
Kinana yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kuimarisha chama, kukagua utekelezaji wa ilani na kusikiliza kero za wananchi akiwa ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka.
01 Septemba, 2022
Umoja na mshikamano wa watanzania na Taifa kwa ujumla ni masuala yaliyopewa kipaumbele kabla na baada ya uhuru kupitia vyama vya TANU na Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya viongozi na waasisi wake hayati Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.
Mara kadhaa siasa zenye mwelekeo wa kuwagawa watanzania zimeonekana kukemewa wazi wazi na viongozi wa Chama tawala CCM, wanataaluma wazalendo na waumini wote wa umoja.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Ndg Abdulrahman Omari Kinana akiongea katika kikao cha ndani cha kupokea taarifa za kazi za chama na serikali amesema CCM kimekuwa chama bora na kinachoungwa mkono na watanzania walio wengi kwa sababu nyingi ikiwemo kupinga ubaguzi wa aina zote na kuwaunganisha watanzania.
"CCM kupitia sera zake imejitambulisha kuwa chama kinachojali utu, usawa wa binadamu na umoja kwa maana ya kuunganisha watu pamoja na kupiga vita ubaguzi. Sasa nawashauri viongozi wenzangu, katika uchaguzi unaoendelea kote nchini wakateni viongozi wanaotumia udini, ukabila au ukanda kama sifa ya kupata uongozi maana hao hawafai kuongoza chama chetu. Tuwapime na kuwapa watu uongozi kwa kuzingatia uwezo, sifa na uadilifu wao na sio kwa misingi ya ubaguzi wa aina yoyote." Alisema Kinana
Kinana alilazimika kusema hayo baada ya kupewa taarifa ya kamati ya siasa ya Halmashauri kuu ya mkoa wa Kigoma iliyowasilishwa na Katibu wa CCM mkoa huo Ndg. Mobutu Malima iliyoeleza kumeanza kuibuka hisia za ukabila, udini na ukanda kutafuta uongozi katika uchaguzi unaoendelea ndani ya CCM mkoani humo.
Aidha Kinana amewataka wanachama na viongozi wa CCM Mkoani Kigoma kujua wanao wajibu wa msingi wa kusema na kutangaza mafanikio ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi unaofanywa na serikali ya CCM Awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ili wananchi wajue nini serikali yao inafanya.
Kinana yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kuimarisha chama, kukagua utekelezaji wa ilani na kusikiliza kero za wananchi akiwa ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi Ndg Shaka Hamdu Shaka.