Ukubwa wa Upinzani ndio uliomfanya Kinana apite kila mtaa ,hivi kuna kumbukumbu zozote kwa mkuu wa CCM kufanya ziara kubwa ya kutumia hela za chama kiasi anavyozitafuna Kinana ,usifikiri yeye na Nape wanazunguka bure ? Kuna ulaji hapo wenzao wanakula BMK wao wanatafuna vijijini ,akushindae kea tonge mshinde kwa kutowea ,upo ?
Weka kando hayo ya ulaji ni yao ! Kinana anachokifanya ni kuwalewesha wananchi kwa mtindo uleule wa kiccm kuwadanganya wananchi kwa ahadi ,unafikiri wananchi hawalielewi hilo ? tumewasikia wananchi wakimlalamikia Kinana malalamiko lukuki ,anachokifanya Kinana kama umeangalia ni kuwa mkali sana kwa watekelezaji wa serikalini na huwabebesha mzigo wenziwe ,mambo ambay walikuwa walaumiane ndani ya baraza lao la ya CCM ,Kinana anawatwisha wenziwe kuwa ndio sababu ya kucheleweshwa miradi na maendeleo mbalimbali huko vijijini. Anashindwa kuwaeleza kuwa Chama chake hakifuatilii mambo hayo ila unapokaribia uchaguzi.
Anachokifanya kinana ni kurahisisha wizi wa kura na ubadilishaji wa matokeo ya uchaguzi ,itakubidi uwe mwelewa sana hapo ili upaone.
Hivi ni kweli kinana anakula kwa mama ntilie ,hivi ni kweli kinana anaendesha baiskeli ,hivi ni kweli kinana analima ,Kinana kwa kuyafanya yote hayo ni kujivisha ngozi ya kondoo ili aonekane na yeye ni katika hao.
Wananchi hawataki kiongozi wao ashike jembe wala apande baiskeli mbele ya macho yao ,ninachokiona ni kwa wananchi hao kukilalamikia Serikali ya CCM kuwa imewatupa vibaya sana na suluhisho ni kuwa haiwajali ,sasa Kinana amekuja kuwambia nini wakati huu unapokaribia uchaguzi,hilo ndilo wanalokwenda kulisikia kwa Kinana na sikumuona akilima au kupanda baiskeli ,au hufuatilii mikutano yake ni malalamiko tu kutoka kwa wananchi ,hakuna sehemu ambayo wananchi wanaishukuru serikali kupitia Kinana ,hakuna !
Jawabu analolitoa Kinana ni kuwajibu ,nitalifuatilia ,nani mwenyekiti wa Kijiji nani mbunge ,nani mkuu wa mkoa ,nitataka kujua kabla sijaondoka hapa ,yuko wapi mwite na viambatanisho kibao vya ubabaishaji ,akiondoka anawaachia mzigo watawala wa maeneo ,anakuwa ameshajenga chuki ,kwa kweli anawavuruga na kujenga makundi.