1Timotheo 3:2
Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja,
Sasa huyo mwanamke unayetaka awe askofu ataiweza hiyo sifa ya kuwa MUME WA MKE MMOJA?
Ni kweli katika 1 Timotheo 3:2-7 imeandikwa kwamba Askofu awe “mume wa mke mmoja”
Kwenye andiko hilo, kuna mambo mawili muhimu ya kuelewa:
Kwanza, mtazamo wa wakati ule (Context ya kitamaduni)
Katika utamaduni wa Wayahudi na Warumi karne ya kwanza, wanaume ndio waliokuwa wakiongoza nyumba zao na jamii. Hivyo, Paulo aliandika kwa muktadha wa wakati ule — ndivyo jinsi jamii ile ilivyotarajia.
Paulo hakusema kwamba hiyo ni sheria ya milele isiyobadilika. Hakuandika kuwa "wanawake hawaruhusiwi kuwa maaskofu." Alikuwa anatoa mwongozo tu wa jinsi mtu aliyetaka uaskofu katika mazingira yale alivyopaswa kuwa.
Leo hii katika jamii nyingi, wanawake wanakubaliwa kushika nyazifa za juu za uongozi. Hivyo Paulo angekuwa anazungumza na jamii za leo, zinazomruhusu mwanamke kuwa kiongozi wa juu, angeweza pia kusema askofu awe mke wa mume mmoja.
Kama hujaridhika na hoja hiyo, hebu tuangalie hoja ya pili:
Katika lugha ya Kigiriki(lugha ya mwanzo iliyotumika kuandika Agano Jipya), "mume wa mke mmoja" ni tafsiri ya maneno "
aner mias gynaikos" — maana yake ni mtu asiye mzinzi, mtu mwaminifu katika ndoa yake.
Kwa tafsiri hiyo ni wazi hata mwanamke anaweza kuwa askofu mradi tu awe na mume mmoja na pia azingatie sifa zote zilizoainishwa katika andiko hilo:
"
asiye na lawama, awe mwenye kiasi, nidhamu na utaratibu; ni lazima awe mkarimu na anayeweza kufundisha; asiwe mlevi au mtu wa matata, bali awe mpole, apendaye amani; asiwe mtu wa kupenda fedha; anapaswa awe mtu awezaye kuongoza vema nyumba yake, na kuwafanya watoto wake wawe watii kwa heshima yote...Anapaswa awe mwenye sifa njema kati ya watu walio nje ya kanisa, ili asije akalaumiwa na kuanguka katika mtego wa Ibilisi."
Sifa zote hizo, mwanamke anaweza kuwa nazo.
Bado tu unapinga kuwa mwanamke hawezi kuwa Askofu? Leta hoja mpya