Kinachotokea Iringa, Tafsiri Yangu...

Kinachotokea Iringa, Tafsiri Yangu...

Tatizo kubwa la mtoa maoni wetu ni udhaifu wa fikra na kwa hakika unakwaza kwa kiasi kikubwa matamanio yake ya kutaka kutambulika kama mtu mweledi ,mahiri,mtu anayepaswa kusikilizwa!Asichoelekea kuelewa,nasi tusingependa kuacha kukumbusha kila mara,ni kuwa,kuweza kujivika wajibu wa kuelimisha umma mpana,sharti la awali kabisa ni mhusika kufanya jitihada za makusudi kujielimisha kiasi cha kutosha.Vinginevyo,ukinzani dhidi ya 'tafsiri' zake utaendelea kwa kuwa mapambano hayajafikia tamati.
 
Maggid tangu ulipoanza kuitetea serikali na maccm kwa kifo cha Mwangosi nilishtuka, likaja suala la Ludovic na Lwakatare ndo nikajua hufai, sasa hapa napo unatafuta kuwaonyesha maccm na serikali yao kuwa wamachinga hawana haraka na maisha eti wasubirie hadi maamuzi ya ngazi za juu yatakapoamua
 
Kwani wewe si gamba? Huwezi andika kilicho jiri kwa usahihi. Lazima ujue wamchinga wananyongo ya siku nyingi. Walihamishiwa sehemu isiyo na biashara wala huduma. Ni haki yao wafanye bishara zao kwenye watu hadi hapo watakapopewa sehemu muafaka.
 
Ningekuona mpenda haki kweli kama ungeonyesha kuwa haki na utulivu katika kutatua tatizo vinatakiwa vitoke pande zote mbili za tatizo. Je Halmashauri ilitumia busara gani kulitatua jambo hilo?
Je Msigwa kwa kukosea kisiasa (nakubali kama kweli alihamasisha machinga waendelee kufanya biashara), hicho ni kigezo cha Halamashauri kuamrisha Polisi kuwadhuru wananchi?????????? Wao Halmashauri hawahitajiki kutumia busara?? Wao wamepewa idhini ya 100 kwa mia kutumia mabavu????
Naomba jibu Mjengwa.
 
Maisha ni magumu sana....vijana wanaamua kujiajiri kwa kuuza bidhaa tofauti tofauti kwa kufuata kanuni za uchumi (4p's or 7p's of marketing mix) mojawapo ni people (customer) ili waweze kuuza bidhaa zao na wajikwamue kichumi....tumeona mifano jinsi ya wamachinga wa karume walivyogoma kuhamia machinga complex kwa kigezo hiki. Msigwa akichangia bajeti ya wizara ya viwanda na Biashara alimsihi waziri kwa dhati awaonee wamachinga wa Iringa huruma, ili wafanye biashara eneo la Mashine tatu huku akimsihi kuwa serikali iache kuwaona wamachinga hao kama kero, ilihali na wao ni watanzania ambao wameacha kufanya shughuli ziso halali na kufanya zilo halali. Hii inaonesha tu (kwa nadharia) kuwa Mchungaji amefanya mambo mengi kutatua tatizo hili bila mafanikio. Shida ya viongozi wetu ambao wengi maisha yao ni mazuri ni kushindwa kuwakumbuka vijana wengi walio masikini......na shida kama hii ikitokea usidhani kuwa wana hofu ya amani katika mioyo yao bali wana hofu ya kupoteza mali zao......kwa kuwa ni walafi waso na utu hata kidogo. Majid fikiria kwa pande zote kaka.
Kweli mkuu,huwezi zungumza biashara kama hakuna customers,products,tatizo hawa ndugu zetu wanaiba(mafisadi),wapo kwenye viyoyozi,uhakika wa kula na kusaza upo,kwao maisha ni marahisi,amani,dunia kwao ni bora kuliko Mbingu na wangekuwa hawafi wanyonge wangelia na kusaga meno,ukidai haki yako watakwambia umevunja sheria,always they want to be there by anymeans.,resources ni kwa wote na sio watu maalumu..ukiwasubiri watapanda juu zaidi the only solution nikuwafuata hukohuko juu..
 
Majjid amenena jambo la kweli kabisa. Tatizo la Msigwa (ambaye nina shaka na uchungaji wake), ni kwamba anataka kujipatia umaarufu kwa nguvu kubwa kwa staili ya Lema. Wahenga walisema ukimwiga tembo kunya, utapasuka msamba!

Msigwa anapaswa kutumia weledi na busara. Hata kama Chadema wataongoza nchi hii, lazima wafuate taratibu za mazungumzo na kuheshimu sheria. Kumbuka, kuondolewa kwa machinga hapo walipo ni kutokana na kuonekana kunaweza kutokea maafa ya ajali na kupoteza vijana/watu wengi. Sioni kosa la Manispaa kuchukua hadhari mapema kabla ya kufikwa na maafa.

Siasa nyepesi na kutafuta umaarufu haraka haraka ni mambo yasiyoweza kuisaidia tanzania. Siasa za kina Gandhi na kina Martin Luther King Jr, hata kina Mwalimu Nyerere za kutumia nguvu za hoja bila vurugu, zina tija kubwa sana. Msigwa anapaswa kujitafakari na kurejea maandiko ambayo anataka tuamini kuwa ameyasoma kiasi cha kustahili kuitwa Mchungaji.

Naunga mkono hoja ya Majjid.

Uandishi wako Jackton na huu wa mwenzako Maggid unanipeleka nyuma zaidi na kutafakari kuwa je matukio ya Ulimboka, Kibanda, Muaji ya Nyororo, Morogoro, etc wakati huo mliandika nini hasa? kadri siku zinavyokwenda nazidi kuwa na wasiwasi wa huyu Mr Maggid kwani zamani hakuwa hivi, kuhusu wewe ni zamani nilishakutoa na makala zako za kumsafisha shoga yako Lowassa
 
Hakikisha Maggid naye anakuwa shaidi wa hii kesi inaonekana anaelewa sana kilichotokea hajapima kwamba watanzania huwa wanaogopa kusema ukweli kwa waandishi wa habari hasa inapotokea ukweli unaihusu serikali
 
Tujiulize swali dogo sana, hao wanaitwa machinga kama serikali ingewaandalia mazingira mazuri ya kufanyia kazi huyo mh. Msigwa angewambia nini mpaka wamwelewe kupambana na police? Chanzo hapa ni serikali kutotoa huduma stahili kwa wananchi na kuwaona wanaowambia wananchi ukweli kama wachochezi. Kwa hali ilivyo bila busara, uwajibikaja na uadilifu, tutashuhudia mengi.
 
Majjid amenena jambo la kweli kabisa. Tatizo la Msigwa (ambaye nina shaka na uchungaji wake), ni kwamba anataka kujipatia umaarufu kwa nguvu kubwa kwa staili ya Lema. Wahenga walisema ukimwiga tembo kunya, utapasuka msamba!

Msigwa anapaswa kutumia weledi na busara. Hata kama Chadema wataongoza nchi hii, lazima wafuate taratibu za mazungumzo na kuheshimu sheria. Kumbuka, kuondolewa kwa machinga hapo walipo ni kutokana na kuonekana kunaweza kutokea maafa ya ajali na kupoteza vijana/watu wengi. Sioni kosa la Manispaa kuchukua hadhari mapema kabla ya kufikwa na maafa.

Siasa nyepesi na kutafuta umaarufu haraka haraka ni mambo yasiyoweza kuisaidia tanzania. Siasa za kina Gandhi na kina Martin Luther King Jr, hata kina Mwalimu Nyerere za kutumia nguvu za hoja bila vurugu, zina tija kubwa sana. Msigwa anapaswa kujitafakari na kurejea maandiko ambayo anataka tuamini kuwa ameyasoma kiasi cha kustahili kuitwa Mchungaji.

Naunga mkono hoja ya Majjid.

Kimsingi nakubali kuwa Msigwa anatakiwa kutmia weledi na busara, Swali, Halmashauri inatakiwa kutumia nini??????
Ukiweza kujibu kwa usahihi na pia kwa busara utashangaa kupata mwanga ndani ya ubongo.
 
Naona huyu Maggid ana bifu binafsi na msigwa kwanini hukuwalaumu polisi ambao wameenda kupiga mabomu wakatumia busara kutatua tatizo hilo, acheni kusaliti taaluma zenu kwa sababu ya njaa zenu wewe na mwenzako Manyerere.
 
Tatizo Msingwa anaiga tabia ya Lema, lakini inabidi ajue kuwa hulka ya mnyalukolo ni tofauti kabisa na hulka ya chalii.

Hizi zote ni harakati za Msigwa kujaribu kujisafisha jina lake baada ya kujidhalilisha kwa hotuba mbovu aliyotoa. Kama hotuba kashatoa, maji yameshamwagika, ajitahidi tu next time atoe hotuba yenye mashiko.

Maggid, poleni sana hapo. tafadhli jitahidi kumtafuta Msigwa muongee, afanye siasa za kujenga nchi. Naona katuma vijana wake waje kusema kashikwa na polisi kumbe yuko kwenye Harambee!!!

Kiongozi!

Heshima kwako!

Hivi siasa za kujenga nchi zikoje Kiongozi? Ni hizi za wakubwa wa serikali ya MAGAMBA kuvunja sheria za nchi ikiwemo ufisadi na hatimaye hukumu zao ni kupandishwa vyeo au? Ningeunga hoja yako mkono kama ungeniambia kwamba Mzee wa Vijisenti baada ya kubainika na tuhuma za Rada na Mikataba ya Madini ni za kweli, basi ange chukuliwa hatua stahiki. badala yake ndio hivyo MAGAMBA wamemkweza zaidi ya tunavyo ona.

Hivi ubovu wa hotuba ya Mh. Mch. Msigwa upo wapi? Kwamba kwa MAGAMBA Tanganyika ya leo mtu akiusema ukweli basi, mtu huyo ametoa kauli mbovu? Ndivyo mnavyo taka kuiaminisha dunia kwamba ukweli sio stahiki ya waTanganyika!!??

Nani asiye juwa kwamba "MSHIKWA NA NGOZI NDIYE MUIBA NG'OMBE". Mbona wabunge wako hawakuta udhibitisho wa tuhuma za Katibu wako, badala yake mapovu na mishipa iliwatoka kwa kumtetea mshutumiwa?

Je, sheria ya nyara za serikali inasema nini juu ya jambo kama hili la kukamatwa kwa Nyara za serikali? Kwamba hata chombo kilicho husika kubeba nyara za serikali ni lazima kitaifishwe. Je, ile kampuni na meli za Katibu wako si zime sajiliwa hapa Tanzania? Mbona zinaendelea kupiga mzigo bila tatizo lolote!?

Ndio maana tunasema kwa serikali hii iliyo kauka kama Kambale, inabidi inapo hitajika kutumia nguvu ili kuapta haki stahiki ya waTanganyika. Maana viongozi tulio nao hawana tena utashi wa kuwa tumikia waTanganyika. Ni utawala ulio paraganyika.

Hakuna cha kuiga tabia za Mh. Lema. Ifike mahala viongozi watambue kwamba kwa sasa waTanganyika tunazijua haki zetu na wajibu wa serikali kwa waTanganyika ni nini.
 
Majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu Nijibu ni lini Huyu Yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa Mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la Yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug CHADEMA,violence and crime of political gain are filling our nation,and Satan is using Mchungaji msigwa to torn apart this innocent Nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani Mungu anazibariki kazi hizi za Ibilisi.

Mungu lete utulivu watu Wako tumalize kazi,Yesu urudi kulichukua kanisa lako,Amen

Usitafute laana bure imeandikwa' touch not my anointed ' unapo ongea siasa toa hoja ya Msigwa kama Msigwa ofisi yake ya kichungaji iweke pembeni yeye ndio anajua agano lake na Mungu. Ushauri wa bure, ongea kuhusiana na Msigwa na siasa zake sio uchungaji alionao na siasa; yeye mwenyewe anajua hilo ndo maana watu wa Iringa hawakumchagua kwa uchungaji wake .Ndg usije jipatia makubwa ukamtafuta na usimpate.
 
Maggid tunakushukuru kwa kutia neno ambalo limebebwa na uliyoyaona kwa macho yako na kutafakari kwa hekima na busara zako kama ulivyobainisha hapa.

Huyu Mh. Msigwa hata ukimuona bungeni, ni mtu ambaye ana hulka ya fuata upepo. Kila mara Mbunge wa upinzani akianza kurumbana au kuzomea, huwa hapitwi, lazima tu na yeye ataungana naye.

Kwa sasa ameanza kufuata nyendo za Mh. Lema wakati huo huo akijibainisha ni mchungaji aliyeusomea uchungaji wa dini ambayo MSINGI wake ni MAPENDO. Hata Kardinali Pengo alisema maneno haya wakati wa Mazishi ya wahanga wa bomu Arusha, "Mimi nawaambia "Tujifunze kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo: 'Tusidiriki kulipia uovu kwa uovu, lakini tutende mema ili kushinda uovu'.". Hii ni sentensi fupi, lakini imebeba UJUMBE MZITO kwa watu waliobarikiwa hekima na busara. Mh. Msigwa amuamua kutenda the other way around.

Kama ni uovu, kuna msusuru wa wanasiasa waliofanyiwa ouvu hapa duniani, lakini kwao NGUVU ZA HOJA NA MAPENDO ndizo ziliushinda huo uovu.

Polisi nao lazima wabebe lawama katika hili kwa kutokutumia busara katika utendaji wao. Kwani haya mabomu lazima yafanye kazi zake tu?. Inakuwa kama polisi siku hizi, wanafanya majaribio ya vifaa vyao vya dola kwa wananchi hata kwa mambo ambayo yanahitaji kumalizwa kwa maongezi (Peaceful).

Nani kwa sasa anaye athirika?. Watu wanapigwa mabomu, yeye yuko kwenye HARAMBEE na chupa ya maji ya kunywa juu ya meza.

Hizi ndizo siasa zetu zisizokuwa na sheria.
 
Uandishi wako Jackton na huu wa mwenzako Maggid unanipeleka nyuma zaidi na kutafakari kuwa je matukio ya Ulimboka, Kibanda, Muaji ya Nyororo, Morogoro, etc wakati huo mliandika nini hasa? kadri siku zinavyokwenda nazidi kuwa na wasiwasi wa huyu Mr Maggid kwani zamani hakuwa hivi, kuhusu wewe ni zamani nilishakutoa na makala zako za kumsafisha shoga yako Lowassa


Haya ndiyo matatizo ya kutaka kusikia kile unachokipenda. Nchii hii bila kutumia busara, itaingia kwenye machafuko. Kutafuta umaarufu kwa njia za mkato kama hizi za kina Msigwa, si mambo ya fahari. Lowassa hasafishwi, isipokuwa ukweli ndiyo unaomsafisha. Swali aliloumwuliza Mwenyekiti wa CCM pale Dodoma ndani ya NEC, la kwamba kipi kakukijua kwenye Richmond, mbona halijajibiwa? Alipotaka Richmond ifutwe, Mwenyekiti akakataa kwa kigezo cha kuheshimu maoni ya makatibu wakuu, nini kilifuata? Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Tunapohoji makosa ya Lowassa na wengine, lazima ninyi mlioshupaa mje na vilelezo na ushahidi wa kuturidhisha. Haiwezekani mtu mmoja aibuke leo aseme wewe mleta mada ni shoga, halafu sote tuamini hivyo! Haiwezekani.
 
serikali sikivu in:A S-fire1:gewapa hao vijana RUZUKU iliwakifunga hizo biashara zao waweze kujikimu badala yakutumia mabomu waliowahi kusema walisema WAO WANAJIFUNZA KUUA NA SISI TUNAJIFUNZA KUFA shauri yenu
 
Hii tafsiri yako ni rojorojo sana Msigwa. Haina mantiki hata kidogo. Huna uelewa wa tatizo ndiyo maana unamshabulia Msigwa bila tafakari ya undani wa tatizo.
Mimi kwa mtazamo wangu naweza kusema kuwa yote haya yanatokana na serikali ilyozowea kuwaburuza wananchi wake ambayo haijajielimisha kufanya kazi kwa weledi na busara za KIDEMOKRASIA. Uongozi sehemu nyingi nchini bado ni wa ki-Amri Amri, Ubabe ubabe na Ubambikiaji bambikiaji. Hiyo siyo DEMOKRASIA. Na zaidi ni kutokuelimika kiutawala na kiuongozi. Kama huwezi kuwaongoza watu huwezi kuwatala.
Ndiyo maana unawasikia wanasiasa wengi wa CCM wanalalamikia upinzani kuwa wanataka nchi isitawalike. Yaani wanataka kutawala bila kuongoza? Balaa gani hii!
 
nimesoma kwa makini cjaona point ya maana unatetea wajinga wenzako ccm hakuna dhambi kubwa duniani kama mwoga harakati mwanzo mwisho mpaka kieleweke
 
Tatizo Msingwa anaiga tabia ya Lema, lakini inabidi ajue kuwa hulka ya mnyalukolo ni tofauti kabisa na hulka ya chalii.

Hizi zote ni harakati za Msigwa kujaribu kujisafisha jina lake baada ya kujidhalilisha kwa hotuba mbovu aliyotoa. Kama hotuba kashatoa, maji yameshamwagika, ajitahidi tu next time atoe hotuba yenye mashiko.

Maggid, poleni sana hapo. tafadhli jitahidi kumtafuta Msigwa muongee, afanye siasa za kujenga nchi. Naona katuma vijana wake waje kusema kashikwa na polisi kumbe yuko kwenye Harambee!!!

Ha ha Msigwa yuko kwenye listi ya wabunge wa chama chako unaowachukia sana kwa sababu hawakukopeshi,Maggid ni mshirika wako kwenye kesi ya Ludovick na Denis Msacky
kwa CCM wamachinga hawana maana manake wanataka wote wawe wameandikisha makampuni brela,maggid yeye anaongea na wahindi,waarabu na wazungu wanaotaka machinga waondolewe katikati ya mji ili wakose soko
 
Majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu Nijibu ni lini Huyu Yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa Mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la Yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug CHADEMA,violence and crime of political gain are filling our nation,and Satan is using Mchungaji msigwa to torn apart this innocent Nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani Mungu anazibariki kazi hizi za Ibilisi.

Mungu lete utulivu watu Wako tumalize kazi,Yesu urudi kulichukua kanisa lako,Amen
Mimi sifikiri Msigwa alikuwa akifanya kazi ya kichungaji pale stendi na wala sidhani alikwenda bungeni kufanya kazi hiyo; halafu labda nikushauri tu ndugu yangu kwamba ulimi ni kwa ajili ya kubariki na sio kulaani
 
Back
Top Bottom