Kinachotokea Iringa, Tafsiri Yangu...

Kinachotokea Iringa, Tafsiri Yangu...

maggid na Manyerere Jackton kwa ukaribu wenu na Ludovick na kujua mambo yake ya ndani, kumshawishi kufanya uasi CHADEMA; ninyi ni devil's snitch!
 
Last edited by a moderator:
Maggid, update us jinsi mh. Msigwa alivyo toka hukuepo kuchukua picha? Update hapa jf blog yako naona uvivu kufungua.
 
Heshima yako Maggid!!

Bwana Maggid mimi nakutambua na kukufahamu kupitia maandiko yako na kwa maana hiyo nakuheshimu kwa sababu hiyo.

Kidogo siku hizi, tangu ukamatwe na kuhojiwa kuhusiana na video ya Lwakatare, na mimi nakuona uandishi wako umebadilika,na umekaa Ki-TBC TBC,uanaitetea serikali hata isipostahili kutetewa!

Kwanza nilisoma makala yako moja katika gazeti la Raia-mwema ukimtetea na kumsafisha katibu mkuu wa CCM Bwana Kinana anayehusishwa na kashfa ya ujangili wa Tembo wetu kwa kutumia historia yake, sasa umekuja hapa JF na hili la Msigwa vs Vurugu za wamachinga hapo Iringa vs Serikakali

Kwanza nijuavyo mimi ni kuwa, wewe kitaaluma ni mwandishi wa habari. Na nilifikiri kuwa badala ya kuja na habari yeye matazamo wa upande mmoja tena wa juu juu tu wa kuitengeneza picha ya hatia ya moja kwa moja ya mbunge wako Msigwa.......ungekuja na taarifa inayochambua tukio lenyewe kwa kina na hadhi ya taaluma yako na wewe mwenyewe

Mfano ungetueleza hivi sakata hili lilianza lini? Kulikuwa na sehemu mbadala hawa wamachinga waliloandaliwa na serikali? Je walikataa na wao kulazimisha tu kuwepo hapo? Kwa nini walikataa(iwapo walikataa) na msimamo wa mbunge wao ulikuwa upi?

Kila mtu anafahamu kuwa Baraza la madiwani la manispaa ya Iringa linaundwa kwa kiasi kikubwa na idadi kubwa ya madiwani wa CCM. Wote tunafahamu kuwa Msigwa ni Mbunge kwa tiketi ya CHADEMA. Wote tunafahamu kuwa hawa jamaa wa CCM hapo Iringa wanaweza kufanya lolote ili mradi tu liwe katika namna ya Msigwa kulaumiwa kama ulivyofanya wewe katika thread yako. Pia wote tunafahamu kuwa miongoni mwa wabunge wa upinzani hasa CHADEMA ambao ni mwiba kwa CCM na serikali yake Rev. Msigwa ni miongoni mwao......ukiwa hivi wewe ni adui wa serikali na CCM pia !!

Mwisho nijuavyo mimi, mbunge Rev. Msigwa hawezi kuwa mwendawazimu wa kuwahamasisha tu hao wamachinga kuendelea na shughuli zao katika maeneo hayo. Lazima kuna sababu na ni wazi kabisa kuwa ni za kisiasa kati ya CCM na CHADEMA.....victim Msigwa!!....Na hawa jamaa wanafanya hivyo katika maeneo yote ambayo yana wabunge wa upinzani....kutengeneza matukio ya upuuzi na yanayozaa maafa badae au wabunge wa maeneo husika kuishia kuwa na kesi!!

Hata mimi ningekuwa katika nafasi ya Msigwa kama Mbunge mwalilishi wao na watu wangu wanaondolewa katika maeneo waliyoyatumia miaka na miaka kwa biashara zao pasipo kuwapatia maeneo mbadala na yanayofaa kwa kazi zao na pia kuwapa muda wa kutosha kuhamia huko, ningepinga na kuungana nao kupinga kwa nguvu zote!!!

Mimi ningependa kusikia Msigwa mwenyewe anasemaje kuhusu hili. Na pia manispaa inasemaje. Mwisho, baada ya hao kusema na sisi wengine ndiyo tuanze kutoa judgement zetu!!
 
Mkuu mbona unajenga hoja kwa hisia?. Unajenga hoja kwa kujiaminisha kama unaifahamu dini yangu na viongozi wangu wa dini.

Kwako mtu yoyote anagusia imani ya dini ya Msigwa katika hali hasi, bali huyo ni yuko against dini ya msigwa. Hizi ni hoja mfu kama siyo za kitoto.

Kwa kukusaidia, mimi ni practising Roman Catholic na hata secondary nimesomea seminary baada ya kuwa mtumikiaji wa artare nikiwa primary school. Kwa hiyo Kardinali Pengo ni kiongozi wangu na ndiyo maana nikatumia maneno yake katika kuweka ujumbe.

Badilisha mtazamo wako na ufahamu siyo wote wanaoponda maamuzi ya Msigwa wanafanya hivyo kwa msukumo wa dini yake. Tatizo kwa sasa nchini la Watanzania wachache kama wewe, fikra zenu kisiasa zimejaa msukumo wa kidini hata kwa mambo ambayo ni PURE POLITICS.

Badilikeni.

Huwezi kukwepa lawama.. Suala la iringa ni mgogoro wa wamachinga.. UCHUNGAJI wa msigwa umeingiaje?... Hizo ndizo nasema ni hoja dhaifu.. Ungemjadili kama mbunge sawa.. Hivi wale wamachinga wameriakti kwa vitu alivyowafundisha kanisani?.. Kusoma kwako seminari kulitakiwa kukufungua ili uweze kujadili hoja objectively.
 
Mkuu mbona unajenga hoja kwa hisia?. Unajenga hoja kwa kujiaminisha kama unaifahamu dini yangu na viongozi wangu wa dini.

Kwako mtu yoyote anagusia imani ya dini ya Msigwa katika hali hasi, bali huyo ni yuko against dini ya msigwa. Hizi ni hoja mfu kama siyo za kitoto.

quote_icon.png
By Ng'wamapalala ni mchungaji aliyeusomea uchungaji wa dini ambayo MSINGI wake ni MAPENDO. Mh. Msigwa amuamua kutenda the other way around. Hizi ndizo siasa zetu zisizokuwa na sheria.
Kukiri kuwa umechemka ni uungwana... IRINGA msigwa hakufanya kosa la kidini.

 
Kwa muda mrefu mi nishaacha kusoma andiko lolote la huyu Mjengwa. Ukishakua jounalist lazima uepuke biasness. Unaposema tafakuli yako unamaanisha kua profession unaiweka kando? Nilisoma comment zake kwa issue ya kinana na pembe saga... ulimlaumu Msigwa before even going through ushahidi aliokua msigwa analalia. poor u!
 
Article hii ya Maggid imeniumiza sana kwani ni wazi ilikuwa na lengo la kumchafua mbunge Msigwa. Mbaya zaidi, mwandishi ameandika mambo mengi ya kumlaumu Mbunge bila ya kusikiliza hadithi kutoka kwa upande wa mchungaji. Ni lazima waandishi wa habari watambue ya kuwa maandishi yao yana uzito na wakati mwingine yanaweza kuharibu sifa za watu na hata kuathiri matokeo ya kesi.

Huyo ndie maggid. Tumbo kwanza, uzalendo badae
 
Last edited by a moderator:
Wewe unafanya biashara ya habari na kuna jinsi unanufaika na mfumo wa serikali iliyopo madarakani njaa ndio inakusumbua tena njaa yako ni ya kiwango cha lami.
 
Umetazama upande mmoja....na ndio tatazo la waandishi habari wa siku hizi...on sided story doent feed society
 
Huyu jamaa anafanya watu waache kusoma RAIA MWEMA kwa ajili ya makala zake.
Anapenda kutetea waovu kwa maslahi yake tu.
 
Mke wa mzungu sijui unajisikiaje?
cc. maggid
 
Last edited by a moderator:

Na kwa kuwa mkweli, kisiasa kinachotokea Iringa kwa sasa kinaweza kuwa na athari hasi kwa Mchungaji Msigwa badala ya kumjenga kisiasa, kwani, wengi niliozungumza nao katikati ya mji wanamwona Mchungaji Msigwa kuwa ni mtu ambaye angeweza kuiepusha hali hii kama asingeyatumia majukwaa ya siasa kuwahamasisha Wamachinga kuendelea kufanya biashara, na hivyo, kutokutii amri ya Manispaa.

Kwa siasa za uonevu zilivyo hivi sasa mkuu maggid nakuhakikishia ina athari chanya kwa Mchungaji Msigwa, watu wamechoka kuonewa watu wanataka mabadiliko juhudi zinazo fanyika nikuchelewesha mabadiliko Iringa, miaka 50 ya uhuru watu wana ishi hawana uhakika wa kupata huduma safi za afya, elimu bora, barabara zinazo pitika siku 365, maji safi sasa anapotokea mtetezi wao lazima wananchi wamuunge mkono kwa kupaza sauti dhidi ya dhuluma zinazo fanywa juu yao. Hata Samwel Machel, Nelson Mandera wakati wanapigania ukombozi wa watu wapo watu waliwabeza kama hivi leo.
msgw1_0e1cc.jpg

Wananchi wangekuwa wamechukizwa na tukio la Wamachinga mbunge wao wasinge mfanyia hivi na kuonekana shujaa mbele wananchi walala hoi. Leo hii mchungaji Msigwa ni shujaa mbele ya walalahoi.
 
Last edited by a moderator:
Ngoja wenyewe waje wasiopenda kuambiwa ukweli na wasiopenda kuoneka wamekosea. Mnyanyii wakikutukana wewe kaa kimya.

wanaopenda kuambiwa ni kina nani? kama hampindishi maneno basi ningesema its just the opposite of what you people mean. cdm hawapendi uongo, ukisema uongo lazima watapinga kwa nguvu zote. ila ccm wanapenda sana kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa, kupindisha lugha na kusema uongo. na yote hiyo ni kwa sababu wanaona wamefika, hawafikirii tena kitu kingine zaidi ya kutaka ku-maintain position na status.
sisi ambao bado tuna safari ndefu ni lazima tuseme ukweli na kwa hilo watusamehe tu wapenzi wa ccm. kwenye uongo daima progress haipatikani, tafuta reference yoyote unipatie, ya maendeleo yaliyopatikana kwa kusema uongo.
bara la afrika angalieni mfano halisi wa nchi ya rwanda, they are doing good kwa kuwa kagame haishi kwa uongo, the man is realistic kiasi hicho nathubutu kusema.
 
A good journalist is fair and should relie on objectivity rather than subjectivity otherwise it is a political propaganda!
 
Majid;
nina uhakika Msingwa atakuwa alifanya kila liwezekano kuongea na manispaa kuhusu watu hawa wanaopata riziki kila jpili kupitia biashara ndogo ndogo katika mtaa huu; nadhani alivyoona hapati ushirikiano wowote toka halmashauri pamoja na viongozi wa mkoa, hakukata tamaa hata akafikia hatua ya kuisihi serikali juu ya kutafuta suruhu ya kudumu la kundi hili la watu maskini kabisa; msigwa akalipeleka jambo hili bungeni wakati akichangia mjadala wa wizara ya mambo ya ndani; kwa kuonya kuwa lazima serikali itafute suruhu ya kudumu sababu wamachinga ni vijana wetu na wanahitaji kuishi ndani ya nchi yao, so ni vizuri kutafuta suruhisho la kudumu kwa kuwashirikisha wadau wote.

Nafikiri busara haikuwepo juu ya wale walioamua kuwashambulia kwa mabomu watu maskini kabisa bila kuwasikiliza na kufikia mwafaka. Watawala wamekuwa wakiwathamini watu hawa wakati wa uchaguzi tu, na mifano ni mingi hata ile ya mtwara pia ni hai kwamba serikali mpaka sasa haina mpango wa kuwasikiliza watu hao kwa madai kwamba hawawezi kusitisha mipango ya serikali.

Hongera Msigwa kutetea maslahi ya watu maskini kabisa wa nchi hii; kama serikali ya mkoa ingekuwa sikivu basi ingeweza kutatua tatizo hili kwa busara zaidi badala ya kutumia mabomu ambapo kulikuwa hakuna haja ya kufanya hivyo.

Magid huna machungu ya vijana na kima mama wanaotafuta mlo wa siku sababu wewe una uhakika wa kuishi na hata unaenda jogging kupunguza mafuta mwilini asubuhi, wenzako haya maisha ni jogging tosha ndugu yangu.
 
Nilikuwa navutiwa sana na Makala za Maggid lakini kwasasa huwa napoma kijujuu ili nione upuuzi gani ameandika navyofahamu mm mtu ambaye background yake ni Iringa hasa lazima atakuwa mwanamapinduzi hata akiwa ndani ya CCM ila kama ni wakuja lazima awe kama Maggid
 
majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu nijibu ni lini huyu yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug chadema,violence and crime of political gain are filling our nation,and satan is using mchungaji msigwa to torn apart this innocent nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani mungu anazibariki kazi hizi za ibilisi.

Mungu lete utulivu watu wako tumalize kazi,yesu urudi kulichukua kanisa lako,amen

hivi wewe unamjua mungu wa ibrahimu, isaka na yakobo au nibmungu yupi unayemsema hapo? Acha kutetea uovu ni dhambi kubwa!!
Halafu acha kuhukumu watu,mungu ndio mtoa hukumu, kipimo hicho hicho utapimiwa na wewe.

Nani anaeliangamiza taifa kama si ccm? Maandiko matakatifu ktk biblia yanasema " haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote.."
hakuna haki ktk nchi hii na haswa kwa wasionacho matokeo yake taifa limeingiwa na aibu, tunachekwa mpaka tunachorwa vikatuni ni watu wa nchi zingine (rejea katuni ya tanzania parliament), ni aibu hiyo! Sababu hamna haki.

Tunachotakiwa ni kumsihi mungu ktk chaguzi zijazo atupe viongozi wenye hofu yake, watakaosimamia haki ndipo taifa kama taifa litakapoinuka na kushamiri, sio kuleta ushabiki wa kipuuzi wa kisiasa kama wako, tena utubu
 
Hizi zinaitwa Ngano za Maggid, kuna thread nyingine ya jana anasema alipigiwa simu na Msigwa. akili kichwani mwenu.
 
Ni bahati mbaya sana viongozi wakuu wa polisi wanafikiria mabavu ni suluhisho la kila kitu kumbe siyo kweli; maeneo mengine vurugu zinaanza mara tu baada ya polisi kuanza kurusha mabomu. Ni wakati sasa wa polisi kujifunza mikakati mingine ya kulinda amani badala ya hali ilivyo sasa. Moto hauzimwi kwa moto huzimwa kwa maji.
 
Majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu Nijibu ni lini Huyu Yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa Mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la Yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug CHADEMA,violence and crime of political gain are filling our nation,and Satan is using Mchungaji msigwa to torn apart this innocent Nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani Mungu anazibariki kazi hizi za Ibilisi.

Mungu lete utulivu watu Wako tumalize kazi,Yesu urudi kulichukua kanisa lako,Amen

Yesu mwenyewe alipokuta watu wanafanya biashara hekaluni, hasira zilimpanda akaanza kuvimwaga na kusababisha vurugu tena kubwa. Sasa iweje mchungaji Msigwa??
 
Back
Top Bottom