Kinachotokea Iringa, Tafsiri Yangu...

Kinachotokea Iringa, Tafsiri Yangu...

Majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu Nijibu ni lini Huyu Yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa Mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la Yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug CHADEMA,violence and crime of political gain are filling our nation,and Satan is using Mchungaji msigwa to torn apart this innocent Nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani Mungu anazibariki kazi hizi za Ibilisi.

Mungu lete utulivu watu Wako tumalize kazi,Yesu urudi kulichukua kanisa lako,Amen
Mbona huyo Yesu alipindua meza za wafanyabishara na kuzitupa bidhaa zao ama wewe hulijui hilo? wacha chuki binafsi wewe!
 
Maggid Mjengwa a corrupted mind!

hivi Msigwa ana cheo au mamlaka gani ya kutoa order au kuwalazimisha wamachinga kufanya vurugu? ieleweke kwamba wamachinga wana interest na eneo lile kwa ajiri ya kipato wala msigwa hahusiki kimaslahi!

katika kila mkutano wa hadhara anaoufanya msigwa pale Iringa lazima watu wamkumbushie ni lini watarudishwa mashine tatu!
 
Watawala wanajua kabisa kuwa wamachinga wanatafuta ridhiki yao ya kihalali, sasa kama Manispaa ya Iringa ilikuwa inataka kuwaondoa kwanini wasishirikishe washika dau wote wa mji? chama cha wamachinga, wafanyabiashara, madiwani, wabunge na mkurugenzi wangekaa chini pamoja na kujadiliana. Tanzania ya leo sio ya kujichimbia kifichoni halafu unatoka na amri za kijinga bila kupima athari zake kijamii, kiuchumi na kisiasa. Wachimbaji wadogo wadogo wengi tu wanavunja sharia kwa kuchimba bila leseni, magamba wamekaa kimya kani adhari zake kisiasa ni kubwa mno...Msigwa anatetea wananchi wake, Majid wewe ni sehemu ya matatizo acha lawama...tofauti ya kimawazo na mtazamo ndo zinazo leta maendeleo sio NDIYO MWALIMU au zama za ZIDUMU FIKRA ZA MWALIMU
 
Siku zote wamekuwa wakifanyia biashara hayo maeneo! Serikali ilikuwa wapi?
 
Kwanza wewe mjengwa ni mtuhumiwa wa utekaji sidhani kuna kitu ambacho ninaweza kuchukua kutoka kwako zaidi ya kutaka leniency kutoka master CCM ili deal zako ziende. uzalendo wako mjengwa ni wa kuangalia kwa darubini zaidi ya mtu unayetaka kufika usikokujua.

Rejea tukio la Mwangosi alipouwawa kikatili na CCM police haraka haraka ukachangisha hela kwa ajili ya mjane na watoto wa shujaa mwangosi, baada ya michango hiyo kuisha umeingia mitini wala hujui tena huyu mama anaendeleaje hatusikii ukisema kitu. kama wewe ni mtu wa watu kama unavyotaka ujulikane basi ningekuona shujaa sana kama hizo hela ungezichanga kwa ajili ya kuweka lawyer ili mama mwangosi apate haki mahakamani kuligana na ukatili aliofanyiwa na CCM police.
Kuhusu machinga wa Iringa ni vijana Watanzania wanaotaka kupata riziki zao mitaani sasa katka suala ni pahala gani wafanyabiashara wafanye biashara wapi ni suala mipango miji na ustawi wa mji. lakini kama bendera za wakereketwa wa chama fulani wakipeperusha bendela fulani wanahaki ya kufanya chochote kile hata kama ni kupakia meno ya tembo katika vyombo usafiri na kusema baadaye kuwa hawana uhusiano wowote na mauaji ya tembo. very low unasema hizo siasa reja reja. kwa kauli yako hiyo umemfanya nyerere angeuke huko kaburini.
 
s
Majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu Nijibu ni lini Huyu Yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa Mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la Yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug CHADEMA,violence and crime of political gain are filling our nation,and Satan is using Mchungaji msigwa to torn apart this innocent Nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani Mungu anazibariki kazi hizi za Ibilisi.

Mungu lete utulivu watu Wako tumalize kazi,Yesu urudi kulichukua kanisa lako,Amen
Acha upuuzi wako wa kulinajisi jina la aliye Mkuu wa yote na vyote ili kuwafurahisha wadhalimu wanaokulipa elfu saba saba kwa kila response kwa threads za kuutetea udhalimu wao (CCM).
Ghasia za namna hii si za kwanza kutokea nchini na huko zilikotokea hakukuwa na wabunge wa CHADEMA waliohamasisha. Kwa nini Mch. abebeshwe lawama namatusi mazito yanayoikejeli pia jumuia iliyompa uchungaji - hadi umuite shetani? Una akili kweli wewe?
Kwa nini polisi waliokuwa wakitupa ovyo mabomu kwa maelekezo ya makada wa CCM wasilaumiwe?
Ni lini uongozi wa manispaa uliwaita kuketi nao mezani machinga na kujadili nao jinsi ya kufanya shughuli zao bila ya bughudha? Ni lini manispaa ilipowatengea eneo ama kuwajengea jengo la kufanyia shughuli zao kisha hawa machinga wakakataa?
Inashangaza sana kuona jinsi CCM inavyojidhihirisha kwamba haina hata chembe ya uaminifu! Ni katika uchaguzi uliopita tu mwenyekiti wenu alikuwa akipita huku na huko akiahidi ajira kwa vijana na kuboresha maisha ya vijana ambao baada ya uchaguzi wamesahaulika mithili ya makobazi ya kuingilia msalani!
Dar kulitokea ghasia kama hizo, hakuwepo Msigwa kule; Mwanza, Songea, Shinyanga na kwingineko ambako halmashayri zinaongozwa na CCM.
Mimi naamini yanayotokea sasa ni matokeo ya cheap politics za CCM ambapo waliwapa vijana matumaini zaidi ya uwezo wao wakijua fika wanawadanganya. Huu ndiyo mshindo nyuma. Katika hili shetani si Msigwa bali ni wale walioziakisi ghasia na kuzitekeleza - CCM na Polisi na iko siku watajibu wakibubujikwa na mchozi. Aibu kwao!
 
Heshima kwako Kiongozi!

Kwanza naamini tangu siku ile ulipoitwa kuhojiwa kuhusu suala la Ugaidi na Ludovick umesha kuwa muoga na serikali hii. Vile vile ninaona hoja zako katika mabandiko mbali mbali zimekuwa za ki- muegemeo kwenye serikali.

Kiongozi! Nina hofu huenda ndio zile mbio za kuminywa uhuru wa habari zimekutembelea kwa kunyooshewa kidole, au?!

Kiongozi!

Hivi kweli inaingia akilini kusema kwamba Mh. Mch Msigwa awashauri machinga kutii amri ya kuto kufanya shughuli zao huku akijikita kwenye mazungumzo ya namna ya kuondokana na ufanyaji shughuli zao kwenye eneo la Mashine Tatu? Unataka kuniambia kwamba suala hili ni la jana au leo asubuhi? Mbona lina muda mrefu na hakuna suluhu yoyote iliyo patikana kupitia serikali kama si Halmashauri ya Iringa?

Kipi kinge stahili kuanza kati ya kutafuta eneo jipya la kufanyia shughuli za wamachinga kabla au kuwaondoa kwanza? Na wakiondoka kwanza kabla ya kujua hatima yao, je, kipato chao cha kila siku walicho kuwa wanakitegemea watakipatia wapi. Je, tegemezi wao ikiwa ni pamija na watoto wanao hitaji kugharimiwa shuleni watakuwa kwenye hali gani?
Ukizingatia kwamba hata hiyo serikali inayo wafukuza hao wamachinga,tayari ilisha wasusa watoto wetu huko mashuleni kwa kuambulia viwango vya Division 0.

Kwa serikali hii ambayo wakubwa wakivunja sheria wanaongezewa kama sio kupandishwa vyeo, ifike mahali kila tunacho dai, tukidai kwa nguvu maana wanyonge wanaonekana kukosa haki, huku wakubwa wakivunja sheria na kutunukiwa nishani na kuzidi kusifiwa.

Ukweli ndio utarudisha heshima ya nchi hii ambayo tayari imesha potea kwenye macho ya dunia ya leo.

KIONGOZI!

TUFIKE MAHALI KWA UMOJA WETU TUKIRI KWAMBA SERIKALI YETU IMEFIKIA KIWANGO CHA KUTO KUWAJALI WANANCHI WAKE. VIONGOZI WENYE MAAMUZI KATIKA NCHI HII WANAJALI MASLAHI YAO TU!!!!!

Pole kama nimekukwaza Kiongozi!

Dahii komeni imenifanya niumie moyoni!
Ukweli mtupu,na Mungu atusaidie
 
Ndugu yetu Maggid kwanza tunashukuru kwa kuwa bado uko huru baada ya kukiepuka kile kikombe!
hebu ni jibu haya maswali
1. ulitambuaje na kuhakiki kuwa miliyo uliyokuwa ukiisikia ilikuwa ni ya "mabomu ya machozi" ilhali ulikuwa hujafika kwenye eneo la tukio?? Au ulihudhurishwa kwanye mafunzo maalumu? na nani? ili iweje?
2. Umeonesha concern kubwa sana kwa muuza nyama na wenye daladala na kutoa dukuduku lako kuwa watakosa faida za bihashara zao. Hujaona haja kabisa ya umuhimu wa Machingas nao kufanya bihashara zao ilikujikimu na maisha, ukizingatia kwamba bihashara zao imebeba vijana wengi ambao wasipojengewa mazingira mazuri ya kufanya shughuli zao nahisi hata huo usalama unaohuzungumzia hautakwepo, na hata hiyo jogging yako ya alfajiri haitakuwa salama. kwako wewe mmchinga asipofanya bihashara ni sahihi kabisa, ila mwenye bucha hahaa!!!??

Upuuzi huu utawagharimu sana. lazima serikali na wewe pia mkumbuke kuwa hata "Mbwa Mwoga akichoka kuonewa anang'ata" tena vibaya sana! Nafikiri wewe kama kioo cha jamii wapaswa kufanya uchambuzi wa haja ili kubalance stori! sishangai tena manake baadhi ya waandishi wetu wa habari siyo tena "kioo cha jamii" bali wamegeuka kuwa "Choo cha Jamii"!!!



...Kunako saa tatu asubuhi nilipokuwa nyumbani nikisoma magazeti, ndipo niliposikia mlio wa kwanza wa bomu la machozi. Idadi yake ikaanza kuongezeka.
...Nilichokiona ni vurugu kati ya Wamachinga na Jeshi la Polisi.
..Niliziona Daladala zikitoka Kituo cha Miyomboni bila hata abiria..,

..Nimeongea na mwuza nyama ya bucha aliyeniambia kuwa mgomo wa Daladala wa hivi karibuni ulimfanya apate hasara kubwa kwenye biashara yake ya nyama kwa vile wateja wake wengi wanatoka nje ya mji. Na anachokiona leo ni hasara nyingine kwa vile hakutakuwa na biashara nzuri...



 
  • Thanks
Reactions: Izz
Maggid, nadhani ingekuwa vyema kama ungeclarify kosa la mbunge Msigwa ni nini haswa? Kupingana kimawazo sio kosa ni demokrasia. Pia nashindwa kuelewa kwa nini unamlaumu Msigwa wakati polisi ndio waliokuwa wakirusha mabomu? Je ni sahihi kwa polisi kutumia unnecessary force? Nadhani article yako hiko biase!

Majjid,ubarikiwe,hakika chadema shetani anawatumia kuliangamiza taifa,wewe unayejiita mchungaji hebu Nijibu ni lini Huyu Yesu unedai kumtumikia alikua akihamasisha umma kupinga utawala na kuleta machafuko,wewe ni ajenti wa kuzimu,unatimiza unabii mkuu wa Mungu wa siku za mwisho,wewe ni mtumishi wa dunia hii sio wa ulimwengu ujao,acha kutumia jina la Yesu kwa tumbo lako,shetani amewakamata mmeamua kuliangamiza taifa letu,na sisi hatutawaacha ,the current state of our dear nation is fast filling up its cup of iniquity throug CHADEMA,violence and crime of political gain are filling our nation,and Satan is using Mchungaji msigwa to torn apart this innocent Nation.

The youth who walk the streets are surrounded with handbills and noice of crime and sin,their mind are educated to misbehave and crime,hatred and sin against the government,ole wenu chadema mnaodhani Mungu anazibariki kazi hizi za Ibilisi.

Mungu lete utulivu watu Wako tumalize kazi,Yesu urudi kulichukua kanisa lako,Amen
mpumbafuuuuuuuu
 
Ndugu zangu,

Leo saa mbili na nusu asubuhi nilifika Jengo la NSSF nikitokea kufanya jogging yangu ya asubuhi. Nilifika hapo kuwahi kununua magazeti.

Hali ilikuwa shwari kama ilivyo kawaida ya Iringa Jumapili asubuhi. Kunako saa tatu asubuhi nilipokuwa nyumbani nikisoma magazeti, ndipo niliposikia mlio wa kwanza wa bomu la machozi. Idadi yake ikaanza kuongezeka.

Nikiwa na kamera yangu nikajisogeza hadi katikati ya mji kufahamu zaidi kinachotokea. Nilichokiona ni vurugu kati ya Wamachinga na Jeshi la Polisi.

Tatizo?

Ni dogo sana, lakini linakuzwa kwa vile siasa imepelekwa mbele badala ya kutanguliza hekima na busara. Kwa kufuatilia suala la Wamachinga kufanya biashara eneo la barabarani pale Mashine tatu naamini kabisa, kuwa Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa angeweza kuepusha hali inayoendelea sasa kwa kuwasihi Wamachinga watii kwanza amri ya Manispaa, na yeye, kama Mbunge wao, kujiingiza kwenye mazungumzo ya dhati na wenzake kwenye Halamshauri ya Manispaa ya Iringa katika kutafuta ufumbuzi wa suala hili. Na hiyo ndio siasa. Siasa ina maana ya majidiliano endelevu badala ya kuhamasisha matumizi ya nguvu au vurugu pale milango ya majadiliano ingali wazi.

Kinachotokea Iringa kwa sasa ni doa kubwa kwa mji wetu wenye sifa ya muda mrefu ya utulivu. Kina athari kubwa kiuchumi pia. Pale Iringa mjini nilichokiona leo ni kama mji ulio katika mapigano ya kivita. Watu ni wachache na wenye hofu.

Biashara nyingi zimesimama. Niliziona Daladala zikitoka Kituo cha Miyomboni bila hata abiria, watoke wapi? Wakati kwa sasa walio nje ya mji wameambiwa na jamaa zao walio katikati ya mji kuwa wasijaribu kufika mjini, kwamba hali imechafuka.

Nimeongea na mwuza nyama ya bucha aliyeniambia kuwa mgomo wa Daladala wa hivi karibuni ulimfanya apate hasara kubwa kwenye biashara yake ya nyama kwa vile wateja wake wengi wanatoka nje ya mji. Na anachokiona leo ni hasara nyingine kwa vile hakutakuwa na biashara nzuri. Je, ni wafanyabiashara wangapi watakaoathirika na hali hii ya leo?

Na kwa kuwa mkweli, kisiasa kinachotokea Iringa kwa sasa kinaweza kuwa na athari hasi kwa Mchungaji Msigwa badala ya kumjenga kisiasa, kwani, wengi niliozungumza nao katikati ya mji wanamwona Mchungaji Msigwa kuwa ni mtu ambaye angeweza kuiepusha hali hii kama asingeyatumia majukwaa ya siasa kuwahamasisha Wamachinga kuendelea kufanya biashara, na hivyo, kutokutii amri ya Manispaa.

Mchungaji Msigwa ni rafiki yangu, muda mfupi uliopita nimempigia simu. Imeita bila majibu. Mmoja wa watu wake wa karibu ameniambia yuko kwenye Harambee pale Tumaini University.

Kama Mchungaji Msigwa angejibu simu yangu, basi, ningemwambia haya ninayoyaandika hapa.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio







Busara na akili ni zilezile za ajabu ajabu mtiririko wa kijani, kwa nini hao wahusika upande wa pili (polisi na municipal nk) nao wasitumie busara hiyohiyo? Acha hizo kuangalia upande mmoja, kama watawala wangekuwa makini haya yote yasingekuwa yanatokea.
 
Haya ndiyo matatizo ya kutaka kusikia kile unachokipenda. Nchii hii bila kutumia busara, itaingia kwenye machafuko. Kutafuta umaarufu kwa njia za mkato kama hizi za kina Msigwa, si mambo ya fahari. Lowassa hasafishwi, isipokuwa ukweli ndiyo unaomsafisha. Swali aliloumwuliza Mwenyekiti wa CCM pale Dodoma ndani ya NEC, la kwamba kipi kakukijua kwenye Richmond, mbona halijajibiwa? Alipotaka Richmond ifutwe, Mwenyekiti akakataa kwa kigezo cha kuheshimu maoni ya makatibu wakuu, nini kilifuata? Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni. Tunapohoji makosa ya Lowassa na wengine, lazima ninyi mlioshupaa mje na vilelezo na ushahidi wa kuturidhisha. Haiwezekani mtu mmoja aibuke leo aseme wewe mleta mada ni shoga, halafu sote tuamini hivyo! Haiwezekani.

Unajitia aibu. Mwanaume mzima huna utashi unatumikia tumbo tu! Hivi na wewe katika orodha ya waandishi nawe upo? Tunajua bado mnavuta kasi tu mwanze kazi ya kulamba miguu ya Lowassa kwenye kipeperushi alichowakabidhi cha Jamuhuri. Get back to your senses man Lowassa anasafishika kwenu nyie mlio kwenye payroll lake. Ganga njaa tu Mura ila akili yako tunajua inafikiri kwenye mabano ya white hair. Poor you
 
Ndugu zangu,

Leo saa mbili na nusu asubuhi nilifika Jengo la NSSF nikitokea kufanya jogging yangu ya asubuhi. Nilifika hapo kuwahi kununua magazeti.

Hali ilikuwa shwari kama ilivyo kawaida ya Iringa Jumapili asubuhi. Kunako saa tatu asubuhi nilipokuwa nyumbani nikisoma magazeti, ndipo niliposikia mlio wa kwanza wa bomu la machozi. Idadi yake ikaanza kuongezeka.

Nikiwa na kamera yangu nikajisogeza hadi katikati ya mji kufahamu zaidi kinachotokea. Nilichokiona ni vurugu kati ya Wamachinga na Jeshi la Polisi.

Tatizo?

Ni dogo sana, lakini linakuzwa kwa vile siasa imepelekwa mbele badala ya kutanguliza hekima na busara. Kwa kufuatilia suala la Wamachinga kufanya biashara eneo la barabarani pale Mashine tatu naamini kabisa, kuwa Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa angeweza kuepusha hali inayoendelea sasa kwa kuwasihi Wamachinga watii kwanza amri ya Manispaa, na yeye, kama Mbunge wao, kujiingiza kwenye mazungumzo ya dhati na wenzake kwenye Halamshauri ya Manispaa ya Iringa katika kutafuta ufumbuzi wa suala hili. Na hiyo ndio siasa. Siasa ina maana ya majidiliano endelevu badala ya kuhamasisha matumizi ya nguvu au vurugu pale milango ya majadiliano ingali wazi.

Kinachotokea Iringa kwa sasa ni doa kubwa kwa mji wetu wenye sifa ya muda mrefu ya utulivu. Kina athari kubwa kiuchumi pia. Pale Iringa mjini nilichokiona leo ni kama mji ulio katika mapigano ya kivita. Watu ni wachache na wenye hofu.

Biashara nyingi zimesimama. Niliziona Daladala zikitoka Kituo cha Miyomboni bila hata abiria, watoke wapi? Wakati kwa sasa walio nje ya mji wameambiwa na jamaa zao walio katikati ya mji kuwa wasijaribu kufika mjini, kwamba hali imechafuka.

Nimeongea na mwuza nyama ya bucha aliyeniambia kuwa mgomo wa Daladala wa hivi karibuni ulimfanya apate hasara kubwa kwenye biashara yake ya nyama kwa vile wateja wake wengi wanatoka nje ya mji. Na anachokiona leo ni hasara nyingine kwa vile hakutakuwa na biashara nzuri. Je, ni wafanyabiashara wangapi watakaoathirika na hali hii ya leo?

Na kwa kuwa mkweli, kisiasa kinachotokea Iringa kwa sasa kinaweza kuwa na athari hasi kwa Mchungaji Msigwa badala ya kumjenga kisiasa, kwani, wengi niliozungumza nao katikati ya mji wanamwona Mchungaji Msigwa kuwa ni mtu ambaye angeweza kuiepusha hali hii kama asingeyatumia majukwaa ya siasa kuwahamasisha Wamachinga kuendelea kufanya biashara, na hivyo, kutokutii amri ya Manispaa.

Mchungaji Msigwa ni rafiki yangu, muda mfupi uliopita nimempigia simu. Imeita bila majibu. Mmoja wa watu wake wa karibu ameniambia yuko kwenye Harambee pale Tumaini University.

Kama Mchungaji Msigwa angejibu simu yangu, basi, ningemwambia haya ninayoyaandika hapa.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio






tatizo watanzania wengi hawajazoea kudai haki zao kwa nguvu, kisa ni kisingizio cha amani na utulivu! Tatizo la sasa la tanzania na si iringa tu, watanzania hawakuzoea kutafuta haki zao, bali wamezoea kuwaachia viongozi wawaburuze! Itachukua muda kuzoea hali hii!
 
Msigwa anafuata upepo? You don't make sense! Kwa fikra zako, mtu akitoa mwavuli Songea leo kwa kuwa kuna mvua inanyesha Songea, halaf wiki tatu baadaye Mtu akitoa Mwavuli Dar es Salaam kwa kuwa kuna mvua kama ile ya Songea basi anafuata upepo. You don't make sense at all.

Kwa nini tiba ya tatizo la mahala fulani linalofanana na tatizo la mahala pengine iwe iwe tofauti? Why should you waste time discovering tyres wakati tayari matairi yashagunduliwa Sehemu nyingine? Kuogopa kuonekana unafuata upepo, au?

Mimi sijasema Msigwa hajafuata upepo. Ninachotaka kukuambia hapa ni kwamba dhana ya kufuata upepo wala hata si kosa. What if hicho kilichofanyika mahala pengine ni sahihi.





Maggid tunakushukuru kwa kutia neno ambalo limebebwa na uliyoyaona kwa macho yako na kutafakari kwa hekima na busara zako kama ulivyobainisha hapa.

Huyu Mh. Msigwa hata ukimuona bungeni, ni mtu ambaye ana hulka ya fuata upepo. Kila mara Mbunge wa upinzani akianza kurumbana au kuzomea, huwa hapitwi, lazima tu na yeye ataungana naye.

Kwa sasa ameanza kufuata nyendo za Mh. Lema wakati huo huo akijibainisha ni mchungaji aliyeusomea uchungaji wa dini ambayo MSINGI wake ni MAPENDO. Hata Kardinali Pengo alisema maneno haya wakati wa Mazishi ya wahanga wa bomu Arusha, "Mimi nawaambia "Tujifunze kutoka kwa Bwana wetu Yesu Kristo: 'Tusidiriki kulipia uovu kwa uovu, lakini tutende mema ili kushinda uovu'.". Hii ni sentensi fupi, lakini imebeba UJUMBE MZITO kwa watu waliobarikiwa hekima na busara. Mh. Msigwa amuamua kutenda the other way around.

Kama ni uovu, kuna msusuru wa wanasiasa waliofanyiwa ouvu hapa duniani, lakini kwao NGUVU ZA HOJA NA MAPENDO ndizo ziliushinda huo uovu.

Polisi nao lazima wabebe lawama katika hili kwa kutokutumia busara katika utendaji wao. Kwani haya mabomu lazima yafanye kazi zake tu?. Inakuwa kama polisi siku hizi, wanafanya majaribio ya vifaa vyao vya dola kwa wananchi hata kwa mambo ambayo yanahitaji kumalizwa kwa maongezi (Peaceful).

Nani kwa sasa anaye athirika?. Watu wanapigwa mabomu, yeye yuko kwenye HARAMBEE na chupa ya maji ya kunywa juu ya meza.

Hizi ndizo siasa zetu zisizokuwa na sheria.
 
Mjengwa ni ccm na sitashangaa kuona siku moja anajaza fomu kugombea ubunge IRINGA MJINI na ndio maana ana jenga hoja kumlaumu msigwa ingawa haoneshi amejihusisha kwenye vurugu za leo.je, hiyo saa tatu wakati vurugu zinaanza alikuwepo hapo mashine tatu?
 
Tatizo Msingwa anaiga tabia ya Lema, lakini inabidi ajue kuwa hulka ya mnyalukolo ni tofauti kabisa na hulka ya chalii.

Hizi zote ni harakati za Msigwa kujaribu kujisafisha jina lake baada ya kujidhalilisha kwa hotuba mbovu aliyotoa. Kama hotuba kashatoa, maji yameshamwagika, ajitahidi tu next time atoe hotuba yenye mashiko.

Maggid, poleni sana hapo. tafadhli jitahidi kumtafuta Msigwa muongee, afanye siasa za kujenga nchi. Naona katuma vijana wake waje kusema kashikwa na polisi kumbe yuko kwenye Harambee!!!

Ze marco lini mtaacha unafiki na kua wazalendo kwa kvlipenda hili taifa na kuacha kujali maslahi binafsi.
 
When tolerance reach a climax,is where a war starts.Mwanablogu ni umenena vyema.lakini vizuri ungejipa muda kujua kama huko nyuma kuliwahi kuwepo juhudi zozote za kukaa mezani kumaliza suala hili.Tatizo hili halijaanza leo.
 
Ndugu zangu,

Leo saa mbili na nusu asubuhi nilifika Jengo la NSSF nikitokea kufanya jogging yangu ya asubuhi. Nilifika hapo kuwahi kununua magazeti.

Hali ilikuwa shwari kama ilivyo kawaida ya Iringa Jumapili asubuhi. Kunako saa tatu asubuhi nilipokuwa nyumbani nikisoma magazeti, ndipo niliposikia mlio wa kwanza wa bomu la machozi. Idadi yake ikaanza kuongezeka.

Nikiwa na kamera yangu nikajisogeza hadi katikati ya mji kufahamu zaidi kinachotokea. Nilichokiona ni vurugu kati ya Wamachinga na Jeshi la Polisi.

Tatizo?

Ni dogo sana, lakini linakuzwa kwa vile siasa imepelekwa mbele badala ya kutanguliza hekima na busara. Kwa kufuatilia suala la Wamachinga kufanya biashara eneo la barabarani pale Mashine tatu naamini kabisa, kuwa Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa angeweza kuepusha hali inayoendelea sasa kwa kuwasihi Wamachinga watii kwanza amri ya Manispaa, na yeye, kama Mbunge wao, kujiingiza kwenye mazungumzo ya dhati na wenzake kwenye Halamshauri ya Manispaa ya Iringa katika kutafuta ufumbuzi wa suala hili. Na hiyo ndio siasa. Siasa ina maana ya majidiliano endelevu badala ya kuhamasisha matumizi ya nguvu au vurugu pale milango ya majadiliano ingali wazi.

Kinachotokea Iringa kwa sasa ni doa kubwa kwa mji wetu wenye sifa ya muda mrefu ya utulivu. Kina athari kubwa kiuchumi pia. Pale Iringa mjini nilichokiona leo ni kama mji ulio katika mapigano ya kivita. Watu ni wachache na wenye hofu.

Biashara nyingi zimesimama. Niliziona Daladala zikitoka Kituo cha Miyomboni bila hata abiria, watoke wapi? Wakati kwa sasa walio nje ya mji wameambiwa na jamaa zao walio katikati ya mji kuwa wasijaribu kufika mjini, kwamba hali imechafuka.

Nimeongea na mwuza nyama ya bucha aliyeniambia kuwa mgomo wa Daladala wa hivi karibuni ulimfanya apate hasara kubwa kwenye biashara yake ya nyama kwa vile wateja wake wengi wanatoka nje ya mji. Na anachokiona leo ni hasara nyingine kwa vile hakutakuwa na biashara nzuri. Je, ni wafanyabiashara wangapi watakaoathirika na hali hii ya leo?

Na kwa kuwa mkweli, kisiasa kinachotokea Iringa kwa sasa kinaweza kuwa na athari hasi kwa Mchungaji Msigwa badala ya kumjenga kisiasa, kwani, wengi niliozungumza nao katikati ya mji wanamwona Mchungaji Msigwa kuwa ni mtu ambaye angeweza kuiepusha hali hii kama asingeyatumia majukwaa ya siasa kuwahamasisha Wamachinga kuendelea kufanya biashara, na hivyo, kutokutii amri ya Manispaa.

Mchungaji Msigwa ni rafiki yangu, muda mfupi uliopita nimempigia simu. Imeita bila majibu. Mmoja wa watu wake wa karibu ameniambia yuko kwenye Harambee pale Tumaini University.

Kama Mchungaji Msigwa angejibu simu yangu, basi, ningemwambia haya ninayoyaandika hapa.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio

Bw. Maggid, Hongera kwa kutoa nasaha labda zinazojenga kifikra, ila nina mashaka nawe kuona kuwa eti leo baada ya mashambulizi ya mabovu kwa wananchi kuanza wewe kama mwandishi wa habari, mwananchi wa Iringa tena mwenye uwezo wa kuongea na Mbunge muda wowowte (nimenukuu) ukawa unafikiria kumshauri jambo, jamani umshauri nini dakika zile za mabomu?? Tizama ndg. yangu; kama umepata maoni ya wanaCCM wa Iringa juu ya tukio la leo ndio unaweza ukasema kuwa status ya MP Msigwa itashuka graph ila kama maoni yalitolewa ni ya wana-Iringa tena watanzania wazalendo na wapenda maendeleo nitaamini kuwa ume-cook taarifa hii........No Evidence no Right to speak.
 
Ndugu zangu,

Leo saa mbili na nusu asubuhi nilifika Jengo la NSSF nikitokea kufanya jogging yangu ya asubuhi. Nilifika hapo kuwahi kununua magazeti.

Hali ilikuwa shwari kama ilivyo kawaida ya Iringa Jumapili asubuhi. Kunako saa tatu asubuhi nilipokuwa nyumbani nikisoma magazeti, ndipo niliposikia mlio wa kwanza wa bomu la machozi. Idadi yake ikaanza kuongezeka.

Nikiwa na kamera yangu nikajisogeza hadi katikati ya mji kufahamu zaidi kinachotokea. Nilichokiona ni vurugu kati ya Wamachinga na Jeshi la Polisi.

Tatizo?

Ni dogo sana, lakini linakuzwa kwa vile siasa imepelekwa mbele badala ya kutanguliza hekima na busara. Kwa kufuatilia suala la Wamachinga kufanya biashara eneo la barabarani pale Mashine tatu naamini kabisa, kuwa Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Msigwa angeweza kuepusha hali inayoendelea sasa kwa kuwasihi Wamachinga watii kwanza amri ya Manispaa, na yeye, kama Mbunge wao, kujiingiza kwenye mazungumzo ya dhati na wenzake kwenye Halamshauri ya Manispaa ya Iringa katika kutafuta ufumbuzi wa suala hili. Na hiyo ndio siasa. Siasa ina maana ya majidiliano endelevu badala ya kuhamasisha matumizi ya nguvu au vurugu pale milango ya majadiliano ingali wazi.

Kinachotokea Iringa kwa sasa ni doa kubwa kwa mji wetu wenye sifa ya muda mrefu ya utulivu. Kina athari kubwa kiuchumi pia. Pale Iringa mjini nilichokiona leo ni kama mji ulio katika mapigano ya kivita. Watu ni wachache na wenye hofu.

Biashara nyingi zimesimama. Niliziona Daladala zikitoka Kituo cha Miyomboni bila hata abiria, watoke wapi? Wakati kwa sasa walio nje ya mji wameambiwa na jamaa zao walio katikati ya mji kuwa wasijaribu kufika mjini, kwamba hali imechafuka.

Nimeongea na mwuza nyama ya bucha aliyeniambia kuwa mgomo wa Daladala wa hivi karibuni ulimfanya apate hasara kubwa kwenye biashara yake ya nyama kwa vile wateja wake wengi wanatoka nje ya mji. Na anachokiona leo ni hasara nyingine kwa vile hakutakuwa na biashara nzuri. Je, ni wafanyabiashara wangapi watakaoathirika na hali hii ya leo?

Na kwa kuwa mkweli, kisiasa kinachotokea Iringa kwa sasa kinaweza kuwa na athari hasi kwa Mchungaji Msigwa badala ya kumjenga kisiasa, kwani, wengi niliozungumza nao katikati ya mji wanamwona Mchungaji Msigwa kuwa ni mtu ambaye angeweza kuiepusha hali hii kama asingeyatumia majukwaa ya siasa kuwahamasisha Wamachinga kuendelea kufanya biashara, na hivyo, kutokutii amri ya Manispaa.

Mchungaji Msigwa ni rafiki yangu, muda mfupi uliopita nimempigia simu. Imeita bila majibu. Mmoja wa watu wake wa karibu ameniambia yuko kwenye Harambee pale Tumaini University.

Kama Mchungaji Msigwa angejibu simu yangu, basi, ningemwambia haya ninayoyaandika hapa.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0754 678 252
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio
Na mimi naungana na hoja za watu wanaotofautiana na tafsiri yako isiyo sahihi. Tafasiri yako ni one way traffic (ni ya kuegemea upande mmoja) bila ya kuangalia upande wa pili. Upande wa pili ambao haujauangalia ni juu ya maamuzi ya zima moto yanayofanywa na viongozi wetu wawe wa halmashauri, serikali kuu au vyombo vyetu vya dola. Kwanza kabisa ni good practice kuwashirikisha wadau katika kupanga juu ya mambo yanayowagusa- kwa swala hil halmashauri ilipaswa iwashirikishe wamachinga katika kuwaondoa siyo kutoa amri, amri inayowaona kana kwamba wamachinga ni watoto au ni wajinga wasio na uwezo wa kufikiri au kutoa michango ya mawazo. Km wahusika wangefanya hivyo basi wangeweza kuwaondolea wamachinga wasiwasi wa namna ya kufanya biashara yao au namna watakavyohamia eneo jingine lililotengwa kwa ajili yao, na pia wangepeana muda wa kuhama na kusainishiana. Polisi nao kukutana nao wakaongea ili wananchi wasio na hatia wasisumbuliwe, na hapo wangebandika matangazo kuwa iwapo watakaidi basi wataingilia. Saa nyingine siyo lazima polisi watumie mabomu kila wakati, wanaweza kufika eneo husika na kuwasihi wamachinga waondoke na wali-act tu pale watakaposhambuliwa na si pia kwa kuumiza watu. Nina uhakika kwamba polisi wamepitia mafunzo ya kudhibiti uhalifu pasipo kudhuru au kuumiza raia- hivi huwa hawaoni majeshi ya polisi ya nje ya nchi yanavyodhibiti uhalifu bila mabomu au kuua? Mchungaji msigwa anahaki ya kusimamia maoni na mawazo ya wapiga kura wake yawe sahihi au siyo sahihi kwa mitizamo yetu, lakini yeye kama mwakilishi wa wananchi anayohaki ya kusimamia maslahi ya wapiga kura wake hadi kanuni, taratibu na sheria za kuwaondoa wanachinga zinapozingatiwa na wahusika. Kumbuka serikali yetu ina sera mbaya sana dhidi ya wamachinga achilia mbali maamuzi ya zima moto yasiyopewa nafasi ya kufikiria. Hebu tuangalie wapiga debe wa Dar kipindi walitimuliwa na kuamriwa warudi makwao wakalime? Km serikali yetu ingekuwa na fikra nzuri ingewachukua hao wapiga debe na kuwapeleka katika vyuo vyake vya veta wakasomee ticketing au customer care ili waje waweze kuwahudumia wateja vizuri zaidi au wajipatie ujuzi hata wa kuajiriwa kwa mikataba, lakini serikali iliwatimua tu pasipo kujua wataenda wapi? Matokeo yake wengi wa wapiga debe waliishia kuishi pale jangwani na kigogo na kuwapiga roba (robbery) akina dada wenye vi mikoba au wajasiriamali wanajihimu asubuhi sana kuja kariakoo au mjini kuchukua biashara zao. Kwa hiyo basi ukiangalia tafasiri yako Mjengwa is so short of critical and impartial analysis.
 
ukombozi dhidi ya dhalimu lzm uendelee kujikomba ni kosa kubwa sana! Hao waliokuwa wanatupa mabomu ni roboti? Si watu, wao na viongozi wao hawakujua kwamba wanahatarisha amani? Kwa nini hawakuwaita viongozi wa hao wamachinga na kukaa nao kikao na kuyamaliza kuliko kutumia nguvu. Maggid usiwe mwoga wamachinga hawakuleta fujo pale polisiccm walipopiga mabomu ndipo amani ikatoweka
 
Back
Top Bottom