Kinachonikera katika filamu za Jacob Stephen (JB)

Kinachonikera katika filamu za Jacob Stephen (JB)

Hahahaa! usiogope! unaweza ukakuta unachat na JB mwenyewe ama ray K... sasa si kingenuka humu mamii?

em ngoja kwanza nivute upepo, mambo ya camera rolling, action, mara pause, sijui long shot na madudu mengine tuyaache kwanza hapa hapa nyuma ya pazia! lol..

Mie nakusubiria pm.........lol
 
Haya ya budget ndogo ndio yana zaa movie mbovu na ndio mwanzo wa kufanya kila kitu wewe mwenye!

Halafu wengi wanafanya movie za budget ndogo halafu wanataka matokeo makubwa.

tatizo sio bajeti tatizo weledi ,characterization,ubunifu,good script ,good story,ideal story,flow of incidence
 
Mkuu kidamva Bongo movie wanatakiwa wawashukuru sana wamiliki wa mabus wanawapa shavu la nguvu sana mara nyingi sana ninaposafiri na mabus ndio napata fursa ya kuangalia movie za bongo ambazo kwa kiasi kikubwa zimepwaya sana na zimeegemea kuiga movie za kiNaigeria.

Kuna siku nilikuwa nasafiri na Lim Safari kutoka Dar - Arusha wakatuwekea movie ya Vicent Kigosi kilichonivutia katika movie yake ni makosa mengi ambayo hata mimi nisiyekuwa na ujuzi wa kutengeneza filamu niliuona dhahiri.Kwanza ni utumiaji wa mbaya wa sauti mtu anapaiza sauti mahali ambapo hapastahili,Vicent anakwenda kwa wakwe watarajiwa anafanya mambo ya uchizi uliopitiliza (hauna tafauti na ukichaa wa kuokota makopo barabarani) wahusika hawajapangiliwa vizuri umri na nk.Kifupi makosa yalikuwa mengi mno kiasi unashangaa hawa watengeneza filamu wamekaa kwenye fani kwa muda mrefu hakuna walichojifunza ?.Pili zoezi la kutengeneza filamu lazima lihusishe watu wengi lakini utakuta mhusika mkuu ndio mwongozaji,huyu huyu ndio mtungaji wa filamu kila kitu anaamua yeye nadhani hapo ndio makosa yanapojitokeza.Tatu wacheza filamu wa Tanzania wanapenda kuiga sana filamu za Nigeria ambazo wakati mwingine hazina utamaduni unaofanana na Tanzania.Nne wadau wengi wa filamu za Bongo hawana elimu ya fani husika na wakati mwingine hawana hata elimu ya kawaida mfano certificate,diploma au degree ya fani yoyote.


Mimi sio mpenzi sana wa kuangalia filamu, ila mara chache tu huwa naangalia hasa kwenye mabasi ninaposafiri.

Kitu kinachonikera kwenye hizi Bongo movie hasa za JB ni kutumia wahusika wale wale na theme ile ile mwisho ana bore sasa.

Mfano ni huyu Shamsa Ford, huwezi kuangalia picha ya JB usimkute, tena kwenye filamu hiyo lazima ataishia kuolewa na JB.

Ni kweli Shamsa ni mzuri, lakini kwani yuko pee yake kwenye filamu?

Halafu kwa nini theme iwe mapenzi tu?

Nachoka kabisa
 
Mkuu kidamva Bongo movie wanatakiwa wawashukuru sana wamiliki wa mabus wanawapa shavu la nguvu sana mara nyingi sana ninaposafiri na mabus ndio napata fursa ya kuangalia movie za bongo ambazo kwa kiasi kikubwa zimepwaya sana na zimeegemea kuiga movie za kiNaigeria.

Kuna siku nilikuwa nasafiri na Lim Safari kutoka Dar - Arusha wakatuwekea movie ya Vicent Kigosi kilichonivutia katika movie yake ni makosa mengi ambayo hata mimi nisiyekuwa na ujuzi wa kutengeneza filamu niliuona dhahiri.Kwanza ni utumiaji wa mbaya wa sauti mtu anapaiza sauti mahali ambapo hapastahili,Vicent anakwenda kwa wakwe watarajiwa anafanya mambo ya uchizi uliopitiliza (hauna tafauti na ukichaa wa kuokota makopo barabarani) wahusika hawajapangiliwa vizuri umri na nk.Kifupi makosa yalikuwa mengi mno kiasi unashangaa hawa watengeneza filamu wamekaa kwenye fani kwa muda mrefu hakuna walichojifunza ?.Pili zoezi la kutengeneza filamu lazima lihusishe watu wengi lakini utakuta mhusika mkuu ndio mwongozaji,huyu huyu ndio mtungaji wa filamu kila kitu anaamua yeye nadhani hapo ndio makosa yanapojitokeza.Tatu wacheza filamu wa Tanzania wanapenda kuiga sana filamu za Nigeria ambazo wakati mwingine hazina utamaduni unaofanana na Tanzania.Nne wadau wengi wa filamu za Bongo hawana elimu ya fani husika na wakati mwingine hawana hata elimu ya kawaida mfano certificate,diploma au degree ya fani yoyote.

wewe km mimi naangalia niwapo safarini tu
yaani km rey ndo anaharibu kweli
mi kwa kweli naonekanaga s mzalendo ila for sure wanaboa
 
Wewe tuliaaaa JB ni next level...
Halafu taja movie 5 alizoact na huyu shamsa....

1.Shikamoo mzee
2.Birthday gift
3.Zawadi yangu. 4.Loading.........................................................................................................................................................................................................
 
Back
Top Bottom