Kinacho muangamiza Lowassa ni Ukimya wake!

Kinacho muangamiza Lowassa ni Ukimya wake!

Mkuu Toothpick, silence yake ndio silaha yake kubwa na ndio karata yake ya mwisho!.

Wenye akili zao, wameishaelewa!, hebu mfuatilie JK, na Kinana kama wana udhubutu wa kumtaja EL!, hao wanaotaja taja ni wajinga wajinga tuu wasio elewa who's the real one behind Richmond!, EL ni mbebaji tuu wa mizigo ya watu!.
Kimya kingi kina mshindo mkuu, subirieni 2015, kama CCM ina jeuri ya kutomteua, itakuwa ndio imemwaga ugali, naye atamwaga mboga, msioelewa ndio mtaelewa!.

Hivi mtu mwenye akili zake timamu hawezi kujiuliza, kama huyu mtu amejiuzulu kwa kashfa, anawezaje tena sio kuutaka urais, bali hata kuufikiria tuu huo urais?.

Pasco

Silaha yake ya Mwisho ni kukaa kimya. Ile kanuni ya "keep them in suspense of terror"

Lakini sasa anaonekana opportunist tu

Ataulizwa mbona hakusema siku zote ?Ataonekana anajitetea tu
 
Fisadi anaweza kemea ufisadi?
Mula rushwa anaweza kemea rushwa?
Anae honga ili apate uongozi anaweza ongea kukemea vitendo viovu vya matumizi ya pesa kwenye uchaguzi????
Lowassa hana nguvu ya kukemea rushwa,ufisadi na matumizi ya pesa kwenye kutaka uongozi

Ni kweli kabisa mkuu
 
Silaha yake ya Mwisho ni kukaa kimya. Ile kanuni ya "keep them in suspense of terror"

Lakini sasa anaonekana opportunist tu

Ataulizwa mbona hakusema siku zote ?Ataonekana anajitetea tu

Hilo lisikupe shida watanzania wote wanafahamu ukweli kuwa mbuzi wa kafara kafufuka
 
Lowassa ni kama ule mti wa mbuyu uliokatwa Tabora (W) Uyui halafu ukasimama ghafla wenyewe.
 
jibu swali mkuu, hatutaki siasa za kibongo hapa!!

anapaswa kufunguka lini? na kivipi? na kwa nini asifunguke kipindi kile aje kufunguka leo?? kwa nini leo na sio miaka au kipindi kile cha EPA na RICHMOND???

Amalizwe kivipi embu eleza ueleweke!!!
Naomba unielewe mkuu, sio kwamba namchukia EL!! Anajitahidi na anania ya kua kiongozi wa nchi...lakini hii kashfa ya UFISADI kamwe sintamuelewa mtu katika hili!!! naimani na wewe japo utakua umelipwa ila moyoni mwako hutaweza ridhia hili!!!
AMKA MTANZANIA MWENZANGU acha kutumika!!!


Acha ujinga wewe pimbi. Ni wewe ndio uwe mwelewa. Una lazima ufisadi wa Richmond kwa Lowasa na mbona huwaongelei kina escrow ya 1.6bilion but unamngangania tu Lowasa. Shame on you. Sakata la escrow halina tofauti na Richmond. Mbona Lowasa awajibishwe na si Picha? Kuna nini kama sio chuki zenu Maembe. Ujumbe wangu kwa ko ni kwamba MUNGU ni wa haki siku zote. Endeleeni kumchafua Lowassa ili muweze kulipa kodi ya nyumba. La msingi ni kwamba watanzania sio wajinga tena.
 
Aongee ili iweje,ajibizane na inzi na hawa mbu akina Nape na Makonda?THE MIGHTY LION WOULD LOSE HIS REPUTATION ONCE HE TOOK THE DECISION TO FIGHT THE MICE CROSSING HIS PATH!
 
Silaha yake ya Mwisho ni kukaa kimya. Ile kanuni ya "keep them in suspense of terror"

Lakini sasa anaonekana opportunist tu

Ataulizwa mbona hakusema siku zote ?Ataonekana anajitetea tu
Mkuu Ben, kuna things you can't afford to loose or let it go!, kuliko aseme, wataamua au bora ateuliwe yeye!, (as a reward kwa silence yake), au anyamazishwe jumla!.

Yaani leo Watanzania waambiwe the 'real richmond' ambaye ndiye huyo huyo 'dowans', na ndiye huyu huyu 'simbion!' na usikute anaweza pia kutoa siri za yule mwenye zile 50% ya PAP anayeitwa Simba!, kweli patakalika hapo?!, hapo si ni itakuwa kuifungulia malango yote ya ikulu na Chadema kufanya just a walk over!. Mtu ukiisha jijua na mwizi, na kuna mtu alikuona siku ulipoiba, ama utakuwa tayari kulipia any cost kwa silence yake, au kumyamazisha jumla!. Hili la pili ndilo ninalolihofia!. Hilo la posibility ya kutoteuliwa wala sina shaka nalo!.

Jamaa wa jikoni, anatumia style ya kumtuma kila mtu kugombea, ili wagombea wawe wengi, wakichinjiwa baharini, kiwe ni kilio cha wengi, hivyo ni kama harusi!, nimenong'onezwa kuna mtoto wa jina jema ambaye naye ameshauriwa achukue tuu fomu ili kumuenzi baba yake!, tena subirieni, hao wengi waliojitangaza wengi ni wasindikizaji tuu!, Januari na Mwigulu ni serious kwa kuitumia JK style ya 1995, they are not for 2015 bali wanajiweka tayari for 2025!, na kwa maoni yangu, that will be the time ripe kuwakabidhi the opposition, kina Ben huo sasa ndio utakuwa muda wenu!.

Pasco

Pasco
 
This is a hard fact!
Lowassa ana siri kubwa moyoni

Lowassa amekuwa kiongozi mkubwa katika taifa hili. Mazuri aliyoyafanya yalionekana na yataendelea kukumbukwa. Kama binadamu hawezi kukosa kasoro hapa na pale, ndio asili ya maisha na kuishi kwa binadamu yeyote.

Kilichokuja kukumbana na bwana huyu katika utendaji wake kama Waziri mkuu na sakata lililolitesa taifa la RICHMOND.
Toka wakati huo Lowassa ameonekana kama shetani, msaliti na fisadi mkubwa wa taifa hili.

Najiuliza ukweli hapa ukoje?

Nijuavyo mradi wa RICHMOND which was a MULT BILLION SHILLINGS CONTRACT, hauwezekani ukamhusu Lowassa pekee. Ni lazima cabinet yote ilihusika hatua kwa hatua hadi final conclusion yake.
Kum-single out MTU mmoja kwa jambo ambalo wengi wanapaswa kuwajibika, Its just not fair!

Kwa kauli ya Mkuu wa Nchi, hili kwa Lowassa lilikuwa ni ajali tu, (MANENO HAYA HAKUTAMKA KWA BAHATI MBAYA)

Lakini hata Lowassa mwenyewe kwa kauli yake siku ya kujiuzulu alitabanahisha kuwa anajiuzulu ili "KUKILINDA CHAMA CHAKE NA SERIKALI YAKE", Bila shaka kwa makosa haya ambayo yaneweza kukigharimu chama na serikali yake!

Leo anapigwa vita hadi ndani ya chama hicho alichokiokoa

Najiuliza siku akiamua nayeye kufunguka, Itakuwaje?

Kwani na yeye hajui kuwa yaliyompata Ulimboka yanaweza kumpata yeyote...
 
Mh. Ndugu Edward Lowassa Mpigania haki za wanyonge na Adui wa wazembe aendelee kukaa kimya maana maadui zake wanataka aongee watumie Fursa hiyo kum Victimize kama walivofanya kwa Vijana kama Hussein Bashe. Historia ya Utendaji uliotukuka kwa Kiwango cha juu wa Lowassa ndio utamjibia Mipasho yote inayoelekezwa kwake. Silaha ya Ushindi ya Ndugu Lowassa ipo kwa Mh. Mwenyekiti wetu wa Chama ambaye anajua na anakubali utendaji wa ndugu Lowassa na hata kumteua kuwa PM hakukutokana na urafiki nbali uwezo na kipaji chake kama alivowahi kunukuliwa mh. Rais December 2005 mara baada ya kumchagua.

Haki gani za wanyonge kapigania??
 
Kiukweli huyu jamaa ana akili ya ziada, mwanzoni mimi pia nilidhani angekurupuka kupambana na adui zake ktk media lakin baadae nikagundua ukimya wake umedhihirisha hekma yake na kuwafanya maadui zake waonekane mburula. Just imagine mtu hajatangaza nia lakini anaandamwa yeye wanaachwa waliojitangaza je siku akisema hana mpango wa kugombea watasema nini hawa waropokaji.
 
Japo Ukweli unauma lakini ndiyo dawa pekee ya uongo.

Lowassa ni la kuvunda,halitakuwa na ubani hapo baadaye...kwanini tunabahatisha ilihali tunajua wazi jamaa ni fisadi?

Kwani hakuna watu wengine zaidi yake ambao ni wasafi,wasio na skendo za ajabu...inakera kung'ang'ania jitu ambalo limeshaadhibiwa na lelnyewe likakubali...tubadilike!

jinga mwenywe njoo na MTU wako unayefikiri ni msafi tumchambue Kama karanga
 
Binafsi napenda kiongozi asiye muongeaji hovyo hovyo.
 
Back
Top Bottom