Kinacho muangamiza Lowassa ni Ukimya wake!

Kinacho muangamiza Lowassa ni Ukimya wake!

Mkuu Toothpick, silence yake ndio silaha yake kubwa na ndio karata yake ya mwisho!.

Wenye akili zao, wameishaelewa!, hebu mfuatilie JK, na Kinana kama wana udhubutu wa kumtaja EL!, hao wanaotaja taja ni wajinga wajinga tuu wasio elewa who's the real one behind Richmond!, EL ni mbebaji tuu wa mizigo ya watu!.
Kimya kingi kina mshindo mkuu, subirieni 2015, kama CCM ina jeuri ya kutomteua, itakuwa ndio imemwaga ugali, naye atamwaga mboga, msioelewa ndio mtaelewa!.

Hivi mtu mwenye akili zake timamu hawezi kujiuliza, kama huyu mtu amejiuzulu kwa kashfa, anawezaje tena sio kuutaka urais, bali hata kuufikiria tuu huo urais?.

Pasco

Mkuu Pasco, Kwa kinachoendelea ndani ya watawala na utawala USISHANGAE hiyo 2015 isifike!

EL kashasalitiwa hata na RAFIKIYE!
Lowassa ajiulize hata wakiamua na wakafanikiwa kum-terminate (stricto senso), ana lipi la kuacha nyuma yake zaidi ya alikuwa fisadi, mvurugaji, msaliti, mhujumu n.k?

Man, They say, NIP THINGS IN THE BUD!
 
Japo Ukweli unauma lakini ndiyo dawa pekee ya uongo.

Lowassa ni la kuvunda,halitakuwa na ubani hapo baadaye...kwanini tunabahatisha ilihali tunajua wazi jamaa ni fisadi?

Kwani hakuna watu wengine zaidi yake ambao ni wasafi,wasio na skendo za ajabu...inakera kung'ang'ania jitu ambalo limeshaadhibiwa na lelnyewe likakubali...tubadilike!
 
mmemchukulia ben aka yahaya hatua gn baada yakutka kumlisha zitto sumu?
ben alikula BAN ndefu sana kwa kushirikiana na wahuni tu , hayo ya sumu siyajui , japokuwa kesi yao haifanani na
hii ya lowasa kabisa , huyu alilenga kufirisi nchi !
 
wana JF, kukaa kimya ni busara pia. ukianza kuropoka kujibu wambea jamii inaweza ishindwe kung'amua nani mbea. Inaeleweka wazi kwamba utendaji wake wa kazi akiwa waziri mkuu ulikuwa unamfunika presidaa kwa kiwango kukubwa. na urafiki wake na EL ulianza kudorora, kwa sababu EL haendekezi uswahiba, mzembe piga chini chapa kazi. Nakumbu sakata la richmond, wataalamu wa upelelezi yaaani TAKUKURU walipeleleza na kubariki halikuwa na shida. waliliinua hili ili kumtoa tu EL (victim of hard work). Masakata mangapi hii serikali imenyamaza, meremeta, Epa, to mention a few, mbona wameng'ang'ana na EL, maccm mengine akiwepo huyo alochukua nchi kwa pesa ya Epa usafi wake uko wapi? Epa hadi tumempoteza gavana wa benki kimtindo, mbona kimya?????
 
akijibu tu mjadala utakuwa umeisha !

Hajahusika, hakuna sehem report ya mwakyembe inamtaja kua ana hisa wala milki kwenye kampuni.. report imaonesha ali andika memo but haikumfuata kumhoji atoe maelezo kuhusu ile memo..
 
Mkuu Pasco, Kwa kinachoendelea ndani ya watawala na utawala USISHANGAE hiyo 2015 isifike!

EL kashasalitiwa hata na RAFIKIYE!
Lowassa ajiulize hata wakiamua na wakafanikiwa kum-terminate (stricto senso), ana lipi la kuacha nyuma yake zaidi ya alikuwa fisadi, mvurugaji, msaliti, mhujumu n.k?

Man, They say, NIP THINGS IN THE BUD!

NIKWELI MKUU PASCO,Wanao jaribu kumshambulia lowasa ndani ya ccm niwale tu wanao jaribu kudandia mambo wasio yajua vizuri,nawengine wanasukumwa na wanao utaka urais kupitia ccm,baya zaidi wanasahau kua wenye maamuzi wanaujua ukweli,lakini pia lowasa nimtu anae fanya mambo yake bila ya kukurupuka kwasababu anauzoefu na siasa za ccm,kundi lingine nilile linalo mhanya lowasa kwasababu ya misimamo yake linapo kuja swala la utendaji iwapo tu atafanikiwa ktk harakati hizi za urais wanahofu kubwa,
 
Jibu ni ALIHUSIKA au HAKUHUSIKA.

jibu swali mkuu, hatutaki siasa za kibongo hapa!!
Ndio maana anapaswa kufunguka
anapaswa kufunguka lini? na kivipi? na kwa nini asifunguke kipindi kile aje kufunguka leo?? kwa nini leo na sio miaka au kipindi kile cha EPA na RICHMOND???
kabla hajamalizwa.
Amalizwe kivipi embu eleza ueleweke!!!
Naomba unielewe mkuu, sio kwamba namchukia EL!! Anajitahidi na anania ya kua kiongozi wa nchi...lakini hii kashfa ya UFISADI kamwe sintamuelewa mtu katika hili!!! naimani na wewe japo utakua umelipwa ila moyoni mwako hutaweza ridhia hili!!!
AMKA MTANZANIA MWENZANGU acha kutumika!!!
 
Kila mtanzania anakumbukumbu nzuri kuhusiana na nini kilichotokea katika Bunge la Kumi(10) lililokua likiendeshwa kwa spidi na viwango.

Kujikumbushia tu kidogo, ni matokeo ya ripoti iliyotolewa na Mh. Mwakyembe katika kamati iliyoundwa na Bunge kufuatilia yaliyotokea kwa undani wake katika saga la Richmond, lililomfanya Mh. Edward Lowassa kujiuzulu nafasi ya uwaziri mkuu mwaka 2008.

Kutokana na riporti hiyo, Mh. Lowassa amekua akihusishwa na sakata hilo ambalo toka mwanzo alikataa kuhusika nalo akidai yeye si mhusika, na amechukuliwa tu kama mbuzi wa kafara, na tatizo si mkataba huo wa Richmond bali tatizo lilikua ni uwaziri mkuu.

Kutokana na kauli hizo za Mh.Lowassa watanzania tumekua na hamu ya kujua ni jambo gani analolifahamu yeye ambalo watanzania wengi hatulifahamu.

Na je kuna sababu gani ya kukaa na tuhuma ambazo hazimhusu?? Kuna ulazima gani wa yeye kuendelea kua mbuzi wa kafara kuhusiana na saga hilo??

Je haoni umuhimu wa kuweka mambo wazi hasa hasa kipindi hiki ambacho tunasikia akitaka kutuomba ridhaa ya kwenda IKULU.

Haoni kwamba mpaka sasa watanzania wote wanafahamu kwamba yeye ndiye mhusika mkuu/pekee wa Richmond.

Ukimya wake unamfanya aendelee kuonekana na hatia. Si vyema kuendelea kuficha jambo lisilo mhusu, kama hana maslahi nalo.

Muda umefika sasa atuambie kweli, la?? tutaendelea kuamini tuliyoyasikia hapo mwanzo.
 
Huyu ni mwizi, uliona wapi mwizi anaongea, mwache aongee uone kama unashauri akili au ujinga, silence inambeba sana huyu
 
Kama kwa Muhongo JK aliomba muda ajilidhishe, itakuwa kwa WAZIRI MKUU EL??? kwa tabia ya JK kujiridhisha nina imani alijiridhisha kabla ya kumpiga chini EL, leo atasema nini hadharani??? alijaribu kusema tatizo la CCM ni uongozi, makamba akambana akasema wa kata ya mto wa mbu, heheheheheh mtu mzima sio jasiri wa mambo ya umma, ni jasiri wa wizi tu
 
Fisadi anaweza kemea ufisadi?
Mula rushwa anaweza kemea rushwa?
Anae honga ili apate uongozi anaweza ongea kukemea vitendo viovu vya matumizi ya pesa kwenye uchaguzi????
Lowassa hana nguvu ya kukemea rushwa,ufisadi na matumizi ya pesa kwenye kutaka uongozi
 
Lowassa,Lowassa hadi kero
Kila kukichaLowassa, Lowassa, oooo mtu mawazo yake binafsi tu anakujana kusema ametumwa na wanainchi katikaeneo lake mfano mkoa au kanda amshauri lowassa agombee Urais.
Lowassa jamani hafai, mtu anayejitajirishakwa kutumia wadhifa wake katika utumishi wa umma hafai kuwa kiongozi kwa sababusiyo mfano wa kuigwa, yaani kuiba mali za umma siyo sifa ambayo inafaa mtumwingine aige.
Lowassa kuwa kiongozi wa ofisi ya juukutavutia wezi wenzie kuinajisi ofisi hiyo, yaani kama ukifuga fisi tegemeafisi wenzie kumtembelea fisi mwenzao hawezi kutembelewa na swala.
Jamani Lowassahafaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
Kikwete, Mangula hebu mwambieni huyo mtu kwamba hanasifa za kiti cha urais, anaweza mambo mengine na siyo urais, ni nyie mnamlealeamnamchelewesha mpeni sure za moja kwa moja na wala siyo mafumbo mafumbo
CC.

  1. Jajaya Mrisho Kikwete
  2. Jack Zoka
  3. Philip Mangula
  4. Abdrahiman Kinana
  5. Benjamin Mkapa- Uliwakemea maaskofuukasema na majoho yao haiwezekani serikali tatu kwa sababu baba wa taifaalikataza mbona Lowassa humkemei? Mnafiki wee.
  6. Ali Hassan Mwinyi
  7. Nape Nnawiye
  8. Delvis Adolf Mwamunyange
  9. Ernest Hamis Mangu
  10. JohnKomba-na unafiki wako, kama Lulu Michael kakukomba mali zote usitegemee uibukiekatika kumpigia dabe fisadi Lowassa, kufa na lywako
  11. RostamAzizi –ikulu siyo pango la walanguzi unatumia mapesa yako ya wizi ili umwekeLowasaa ikulu ili uwe ndio uchochoro wako.



 
Edo ni muhanga tu, kwani hata mwakyembe alikiri kuna mambo wameyaficha kwa maslahi ya nchi

Jk ndie mhusika mkuu shutuma zote
 
This is a hard fact!
Lowassa ana siri kubwa moyoni

Lowassa amekuwa kiongozi mkubwa katika taifa hili. Mazuri aliyoyafanya yalionekana na yataendelea kukumbukwa. Kama binadamu hawezi kukosa kasoro hapa na pale, ndio asili ya maisha na kuishi kwa binadamu yeyote.

Kilichokuja kukumbana na bwana huyu katika utendaji wake kama Waziri mkuu na sakata lililolitesa taifa la RICHMOND.
Toka wakati huo Lowassa ameonekana kama shetani, msaliti na fisadi mkubwa wa taifa hili.

Najiuliza ukweli hapa ukoje?

Nijuavyo mradi wa RICHMOND which was a MULT BILLION SHILLINGS CONTRACT, hauwezekani ukamhusu Lowassa pekee. Ni lazima cabinet yote ilihusika hatua kwa hatua hadi final conclusion yake.
Kum-single out MTU mmoja kwa jambo ambalo wengi wanapaswa kuwajibika, Its just not fair!

Kwa kauli ya Mkuu wa Nchi, hili kwa Lowassa lilikuwa ni ajali tu, (MANENO HAYA HAKUTAMKA KWA BAHATI MBAYA)

Lakini hata Lowassa mwenyewe kwa kauli yake siku ya kujiuzulu alitabanahisha kuwa anajiuzulu ili "KUKILINDA CHAMA CHAKE NA SERIKALI YAKE", Bila shaka kwa makosa haya ambayo yaneweza kukigharimu chama na serikali yake!

Leo anapigwa vita hadi ndani ya chama hicho alichokiokoa

Najiuliza siku akiamua nayeye kufunguka, Itakuwaje?

Umeandika hisia mkuu...
 
Yaani hadi raha mwezi February tayari tuna ushindi wa 67.8%
 
Back
Top Bottom