Kinacho endelea sasa TBC live "KONGAMANO"

Kinacho endelea sasa TBC live "KONGAMANO"

Kwa nini hawajachanganya watoa mada? wangeingiza tundu lissu hapo atoe maelezo
 
Hivi tbc bado mnaona mnayohaki ya kutuchagulia habari na kuamua kutukatia matangazo??? Dawa yenu iko jikoni. Sasa sisi tunafuatilia maelezo ya kina kuhusu muungano kutoka kwa wataalam nyie mnatukatia!
Watu hawawezi kuelewa unachokisema... Hujatoa maelezo ni ni kimetokea... Hebu eleza ili watu waelewe nani alikuwa anaongea na anaongelea nini walipokata matangazo.
 
Tena wakati Prof. Kabudi alikuwa alishusha nondo halisia...!
Then wakaweka, taarabu

Tena zilikuwa ni nondo za usoni, maana Prof. Kabudi alikuwa anaongea kwa ujasiri usio wa kawaida mbele ya Makamu Rais wa JMT kwamba muungano tulionao umechoka na tusilazimishe vizazi vijavyo vikaishi kwa ujinga wetu. Aisee, ilikuwa ni balaa. TBC1 kama kawaida yao walivyoona nondo za usoni zinazidi wakakata matangazo. Aibu kubwa kwa TBC!
 
imekua ni jambo la kawaida sasa hii tbc kuwakatia watu matangazo kila anaesema ukwel kuhusu muungano au anaetetea serikali 3,leo tena kwenye mdahalo unarushwa live na tbc hapa znz,tbc wamefanya tena upuuz wao wa kumtoa hewan prf kabudi pale alipoanza kuelezea changamoto ya muungano ya 1984 na alipogusia sababu ya mzee jumbe kufukuzwa ccm,ndipo cha kushangaza wakakata ghafla matangazo baada ya kumaliza kuongea prof kabudi ndo wakarudisha wameniharibia pasaka yangu
 
Tbc ilikuwa inaonyesha matangazo ya moja kwa moja ya mhadhara uliokuwa unahutubiwa profesa Kabudi,nimekuta anazungumzia kuhusu kutohukumu historia kwa hali ya sasa,na Taifa linaendelea leo ukisema kuhusu Karume watu watashtuka lakini siyo mwaka 2064.inavyoeleke jamaa wanaoamini serikali 2 hawana uvumilivu wa hoja kinzani.wanajenga hoja za hila,kukata matangazo kuzuia mikutano ya wenye hoja kinzani ni vizuri tungejenga utamaduni wa kusikiliza na hoja za upande wa pili kama alivyopata kusema Thomas Jefferson "na tuusikilize upande wa pili kwa uwazi kabisa"
ikiwa tunataka katiba mpya ni lazima tupambane kwa hoja na sio hila.ni lazima tuwasikilize hata ambao hatukabaliani nao.lazima mawazo elfu moja yagongane ili maua mia moja yachanue.
 
anataka 'kumrukana' Mwalimu kama alivyofanya Mh. Tundu Lissu!
Hawa wau wengi wetu upeo wa kuwaelewa kwa sasa ni mdogo sana lakini pale tutakapokuwa tumeanza kulia na kusaga meno ndipo tutaujua umuhimu wao.
 
Back
Top Bottom