TBC1 sasa, wakiona mtu anashusha NONDO wanatoka hewani, miye nipo Mza vipi huko Dar mvua inanyesha tena? Maana siku ya Tundulisu Dodoma walisema mvua ilikatisha mambo.
Hovyo kabisa! Mitambo sijui chakavu.
Prof. Kabudi kawaambia muungano huu wa sasa uko katika hali ya fatigue (umechoka). Akaendelea kusema ni lazima tuangalie tear and wear za muungano. Baada tu ya kuzungumza maneno hayo TBC1 wakakata matangazo.
Hapana mitambo sio chakavu, ila hawataki watu wanaosema maneno ya kuwachoma kuhusu huu muungano.
Wameweka taarabu ndio wanachofikiria tunakipeenda haya nimekubali....uzuri ujinga wa mwenzio haukufanyi wewe kuwa mjinga. Kwa maneno ya mtaani kivyao vyao....
Nadhani waliona anaenda wasikokutaka!
Hahahaha naona wameweka taarabu.
Kabudi alikuwa anawachana live, amesema tusilazimishe watoto wa miaka hamsini ijayo kuishi ujinga wetu. Amesema hakuna Muungano kisheria bali kirafiki. Makombora yamezidi Tbc wakakata matangazo!!!!
Itakuwa mkuu, mambo ya kuficha ficha taarifa haya.
Mvua inanyesha balaaa.