Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,150
'Kina mama wengi Moshi wana saratani ya matiti'James Lanka, Moshi
MKOA wa Kilimanjaro umeelezwa kuwa miongoni mwa mikoa yenye kinamama wengi wenye matatizo ya saratani ya matiti na shingo ya uzazi.
Hayo yalibainika baada ya tafiti mbalimbali kufanywa na chama cha madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA) katika mkoa huo.
Taarifa hiyo, ilitolewa juzi na Mwenyekiti wa MEWATA mkoani Kilimanjaro Dk Zaitun Bokhary kwa Mkuu wa mkoa huo, Monica Mbega wakati wa ufunguzi rasmi wa ofisi ya chama hicho, uliofanyika kwenye hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi.
Alitoa mfano wa utafiti wa matatizo ya aina hiyo unaoendelea katika hospitali ya rufaa ya KCMC kwamba kati ya mwaka 2008/2009, utafiti umeonyesha kuwa kati ya wanawake 134 wenye uvimbe katika matiti, 74 kati yao walibainika kuwa na saratani ya matiti.
"Mpaka sasa wananwake wengi wa Mkoa wa Kilimanjaro hawajafanyiwa uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya kizazi, hivyo basi wanawake madaktari wa mkoa huo, wamedhamiria kujenga uwezo wa kuwafikia kinamama wengi zaidi," alifafanua Dk Bokhary.
Akizungumza katika hafla fupi ya Ufunguzi wa ofisi hiyo, Mwakilishi wa MEWATA kutoka makao makuu ya Chama hicho jijini Dar-es-Salaam, Dk Martha Mkony alisema mafanikio ya MEWATA yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na moyo wa kujitolea wa wanachama wake.
"Takwimu zinaonyesha kuwa daktari mmoja anahudumia takribani wananchi 25,000, lakini pamoja na majukumu makubwa waliyonayo, bado madaktari hawa wanawake wameamua kujitolea zaidi kuwasadia kinamama. vijana na watoto ambao ni tegemeo kubwa sana katika maendeleo ya taifa," alifafanua Dk Mkony.
Akizunguimza na Mwananchi baada ya ufunguzi huo, mmoja ya wanachama wa MEWATA mkoani hapa, Dk Wahida Shangali, alisema licha ya tawi la MEWATA Mkoa wa Kilimanjaro kundwa mwishoni mwaka jana, tayari wamefanikiwa kupima saratani ya matiti kwa kinamama 87 wa kijiji cha Uru-Shimbwe.
"Kuwa na ofisi katika hospitali ya Mawenzi, tunatarajia kupata wanachama wengi zaidi kutoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Kilimanjaro na itatuwia rahisi zaidi kuwafanyia uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya kizazi ikiwezekana kuwafikia kinamama wote wa Mkoa wa Kilimanjaro," alifafanua Dk Shangali.
Akizungumza katika ufunguzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega aliwapongeza madaktari wanawake kufungua ofisi ya katika mkoa huo.
Alitoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuiunga mkono MEWATA wa hali na mali na bosi huyo wa mkoa alichangia Sh 500,000. Mkoa wa Kilimanjaro ni mkoa wa kwanza kuwa na Tawi la MEWATA kati ya mikoa yote 26 ya Tanzania kuacha Jiji la Dar es Salaam.
MKOA wa Kilimanjaro umeelezwa kuwa miongoni mwa mikoa yenye kinamama wengi wenye matatizo ya saratani ya matiti na shingo ya uzazi.
Hayo yalibainika baada ya tafiti mbalimbali kufanywa na chama cha madaktari Wanawake Tanzania (MEWATA) katika mkoa huo.
Taarifa hiyo, ilitolewa juzi na Mwenyekiti wa MEWATA mkoani Kilimanjaro Dk Zaitun Bokhary kwa Mkuu wa mkoa huo, Monica Mbega wakati wa ufunguzi rasmi wa ofisi ya chama hicho, uliofanyika kwenye hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro ya Mawenzi.
Alitoa mfano wa utafiti wa matatizo ya aina hiyo unaoendelea katika hospitali ya rufaa ya KCMC kwamba kati ya mwaka 2008/2009, utafiti umeonyesha kuwa kati ya wanawake 134 wenye uvimbe katika matiti, 74 kati yao walibainika kuwa na saratani ya matiti.
"Mpaka sasa wananwake wengi wa Mkoa wa Kilimanjaro hawajafanyiwa uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya kizazi, hivyo basi wanawake madaktari wa mkoa huo, wamedhamiria kujenga uwezo wa kuwafikia kinamama wengi zaidi," alifafanua Dk Bokhary.
Akizungumza katika hafla fupi ya Ufunguzi wa ofisi hiyo, Mwakilishi wa MEWATA kutoka makao makuu ya Chama hicho jijini Dar-es-Salaam, Dk Martha Mkony alisema mafanikio ya MEWATA yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na moyo wa kujitolea wa wanachama wake.
"Takwimu zinaonyesha kuwa daktari mmoja anahudumia takribani wananchi 25,000, lakini pamoja na majukumu makubwa waliyonayo, bado madaktari hawa wanawake wameamua kujitolea zaidi kuwasadia kinamama. vijana na watoto ambao ni tegemeo kubwa sana katika maendeleo ya taifa," alifafanua Dk Mkony.
Akizunguimza na Mwananchi baada ya ufunguzi huo, mmoja ya wanachama wa MEWATA mkoani hapa, Dk Wahida Shangali, alisema licha ya tawi la MEWATA Mkoa wa Kilimanjaro kundwa mwishoni mwaka jana, tayari wamefanikiwa kupima saratani ya matiti kwa kinamama 87 wa kijiji cha Uru-Shimbwe.
"Kuwa na ofisi katika hospitali ya Mawenzi, tunatarajia kupata wanachama wengi zaidi kutoka katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Kilimanjaro na itatuwia rahisi zaidi kuwafanyia uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya kizazi ikiwezekana kuwafikia kinamama wote wa Mkoa wa Kilimanjaro," alifafanua Dk Shangali.
Akizungumza katika ufunguzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega aliwapongeza madaktari wanawake kufungua ofisi ya katika mkoa huo.
Alitoa wito kwa wananchi na taasisi mbalimbali kuiunga mkono MEWATA wa hali na mali na bosi huyo wa mkoa alichangia Sh 500,000. Mkoa wa Kilimanjaro ni mkoa wa kwanza kuwa na Tawi la MEWATA kati ya mikoa yote 26 ya Tanzania kuacha Jiji la Dar es Salaam.