Kimenuka Tarime, Heche asakwa na Polisi

Kimenuka Tarime, Heche asakwa na Polisi

Mwita Maranya

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2008
Posts
10,565
Reaction score
7,988
Hali ya kisiasa wilayani Tarime inazidi kuwa tete baada ya jana mwenyekiti wa Chadema wilayani humo kuandika barua polisi kusitisha mikutano ya mwenyekiti wa BAVICHA John Heche. Taarifa za uhakika nilizonazo ni kwamba kamanda John Heche anasakwa na jeshi la polisi kanda maalum ya Tarime Rorya kwa tuhuma za kumkashifu raisi Kikwete.

Katika mkutano wake wa juzi alioufanya katika mji mdogo wa Sirari, Heche aliwaeleza wananchi kuwa Tanzania imekuwa ni nchi ombaomba wakati ina rasilimali nyingi sana za kuiwezesha kujitegemea. Akawaeleza wananchi hao kuwa raisi Kikwete ndiye anaongoza zoezi hilo la kuwa ombaomba, kwa kwenda ulaya na marekani kila mara kutembeza bakuli.

Heche alielezea masikitiko yake kwa raisi Kikwete kupishana angani na ndege zilizojaza madini yetu kupeleka ulaya na marekani huku yeye akiwa amefungashiwa vyandarua na hao wazungu wanaopora rasilimali zetu. Bado nafuatilia kujua hatma ya sakata hili na nitaendelea kuwa update kadri inavyowezekana.

UPDATES 1:
Nimezungumza na kamanda Heche muda mfupi uliopita, amenifahamisha kwamba amepigiwa simu na kaimu kamanda wa polisi kanda maalum ya Tarime Rorya ili afike kituoni kwa mahojiano.
Sasahivi ndio anaelekea kituo cha polisi Tarime mjini kwa ajili ya mahojiano hayo.

Taarifa za ndani kabisa toka polisi Tarime ni kwamba kuna shinikizo/maelekezo toka juu kwamba Heche akamatwe ama akijisalimisha azuiliwe mahabusu ya polisi hadi kesho atakapopandishwa kizimbani.

Nadhani wale mliopo Tarime mnaweza kufuatilia kwa karibu na kutujuza kinachojiri huko.

UPDATES 2:
Taarifa rasmi kutoka Tarime ni kwamba Kamanda Heche amefika kituo cha polisi Tarime kama alivyoitwa na kaimu kamanda wa Tarime Rorya lakini amegoma kuhojiwa hadi atakapokuwa na wakili wake. Kufuatia hali hiyo uongozi wa jeshi la polisi umekubaliana nae na kumpa muda hadi kesho saa tisa afike na wakili wake kwa ajili ya mahojiano.

Kwa upande mwingine Heche anaendelea na mikutano ya hadhara kjama kawaida na muda huu anaelekea eneo la Muriba kuzungumza na wananchi. Zengwe lililokuwa limewekwa na mwenyekiti wa wilaya limeshindwa na sasahivi mwenyekiti huyo anahaha huku na kule asijue hatma yake itakuwa ni nini.
 
haya sasa,aende tu akatoe maelezo,maana kutafutwa sio kufungwa
 
Kwani kamkashifu au kasema ukweli?kweli anaenaenda kuleta neti wenzake wanabeba madini.hilo jeshi la nyinyiemu police wanaendelea na kazi za kutengeneza movie zao.
 
Kwani lipi la Uongo hapo?
Nchi ambayo kila siku inaomba misaada tu wanataka iitweje?
Nchi ambayo ndege inatua na kubeba Twiga na Tembo wanataka iitweje?
Nchi ambayo Ndege inatua na kubeba madini bila kuhakikiwa Wanataka iitweje?
Rais anayeenda kuomba omba Misaada kila kukicha mnataka aitweje?
 
Tarime napaaminia hakuna mbaya itakayotokea kwani ni uwongo kuwa sisi ni ombaomba duniani? asilimia ngapi ya budget yetu inategemea bakuli? madini na michanga yote si inapelekwa ulaya? mara ngapi jk anaenda kuomba na akirudi hapa anajigamba wafadhili wametusaidia??
 
Hali ya kisiasa wilayani Tarime inazidi kuwa tete baada ya jana mwenyekiti wa Chadema wilayani humo kuandika barua polisi kusitisha mikutano ya mwenyekiti wa BAVICHA John Heche. Taarifa za uhakika nilizonazo ni kwamba kamanda John Heche anasakwa na jeshi la polisi kanda maalum ya Tarime Rorya kwa tuhuma za kumkashifu raisi Kikwete.

Katika mkutano wake wa juzi alioufanya katika mji mdogo wa Sirari, Heche aliwaeleza wananchi kuwa Tanzania imekuwa ni nchi ombaomba wakati ina rasilimali nyingi sana za kuiwezesha kujitegemea. Akawaeleza wananchi hao kuwa raisi Kikwete ndiye anaongoza zoezi hilo la kuwa ombaomba, kwa kwenda ulaya na marekani kila mara kutembeza bakuli.

Heche alielezea masikitiko yake kwa raisi Kikwete kupishana angani na ndege zilizojaza madini yetu kupeleka ulaya na marekani huku yeye akiwa amefungashiwa vyandarua na hao wazungu wanaopora rasilimali zetu. Bado nafuatilia kujua hatma ya sakata hili na nitaendelea kuwa update kadri inavyowezekana.

Kwa nini amejificha?
 
WAO WANA PESA NA DOLA, SISI TUNA PEOPLES POWER NA MUNGU. KAMWE HAWATAEZA KUZUIA M4C, NA HARAKATI ZOTE ZA KUMKOMBOA MTANZANIA KUTOKA MIKONONI MWA MKOLONI MWEUSI (chama cha mabwepande).
 
Kwani lipi la Uongo hapo?
Nchi ambayo kila siku inaomba misaada tu wanataka iitweje?
Nchi ambayo ndege inatua na kubeba Twiga na Tembo wanataka iitweje?
Nchi ambayo Ndege inatua na kubeba madini bila kuhakikiwa Wanataka iitweje?
Rais anayeenda kuomba omba Misaada kila kukicha mnataka aitweje?

Afadhali JK anaomba kwa maslahi ya Taifa , zile pesa wanazochangisha CDM wakiwa wavekwiva kwenye suti kwenye mahoteli makubwa hapa nchini kusafisha fedha haramu wanazoletewa na wazungu hao hao zinafanya nini?
 
Mkuu Mwita Maranya hilo la kuongea ukweli unaoitwa kashfa na kutafutwa na polisi ni la kawaida sana!Concern yangu ipo hapo ulipoandika kuwa mwenyekiti wa chadema wilaya Tarime aliandika barua polisi kusitisha mikutano ya Heche.
 
Last edited by a moderator:
UPDATES:
Nimezungumza na kamanda Heche muda mfupi uliopita, amenifahamisha kwamba amepigiwa simu na kaimu kamanda wa polisi kanda maalum ya Tarime Rorya ili afike kituoni kwa mahojiano.
Sasahivi ndio anaelekea kituo cha polisi Tarime mjini kwa ajili ya mahojiano hayo.

Taarifa za ndani kabisa toka polisi Tarime ni kwamba kuna shinikizo/maelekezo toka juu kwamba Heche akamatwe ama akijisalimisha azuiliwe mahabusu ya polisi hadi kesho atakapopandishwa kizimbani.

Nadhani wale mliopo Tarime mnaweza kufuatilia kwa karibu na kutujuza kinachojiri huko.
 
Suala la nchi kuwa omba omba dunia nzima inafahamu na rasilimali zetu kuchukuliwa inafahamika pia. Ila sababu za mwenyekiti wa wilaya wa Cdm kuzuia mikutano ya BAVICHA ni nini?
 
fafanua hapo mwanzoni. Mwenyekiti wilaya chadema kuandika barua polisi kusitisha mikutano ya mwenyekiti BAVICHA... hii kama haijakaa sawa.!
 
Afadhali JK anaomba kwa maslahi ya Taifa , zile pesa wanazochangisha CDM wakiwa wavekwiva kwenye suti kwenye mahoteli makubwa hapa nchini kusafisha fedha haramu wanazoletewa na wazungu hao hao zinafanya nini?
Kwa maslahi yapi uliyoyaona kwa awamu hii ya kikwete...unajua deni la taifa kwa sasa ni kiasi gani? unakumbuka wakati anaachiwa nchi hazina kulikuwa na kiasi gani? je deni likuwa kiasi gani?...vipi bei ya vyakula nikupe mfano kikwete anachukua nchi bei ya mchele ilikuwa TZS 650 sasa hivi mpaka TZS 3000, kiberiti 25 sasa hivi 100...ngoja nikomee hapo
 
Hali ya kisiasa wilayani Tarime inazidi kuwa tete baada ya jana mwenyekiti wa Chadema wilayani humo kuandika barua polisi kusitisha mikutano ya mwenyekiti wa BAVICHA John Heche. Taarifa za uhakika nilizonazo ni kwamba kamanda John Heche anasakwa na jeshi la polisi kanda maalum ya Tarime Rorya kwa tuhuma za kumkashifu raisi Kikwete.

Katika mkutano wake wa juzi alioufanya katika mji mdogo wa Sirari, Heche aliwaeleza wananchi kuwa Tanzania imekuwa ni nchi ombaomba wakati ina rasilimali nyingi sana za kuiwezesha kujitegemea. Akawaeleza wananchi hao kuwa raisi Kikwete ndiye anaongoza zoezi hilo la kuwa ombaomba, kwa kwenda ulaya na marekani kila mara kutembeza bakuli.

Heche alielezea masikitiko yake kwa raisi Kikwete kupishana angani na ndege zilizojaza madini yetu kupeleka ulaya na marekani huku yeye akiwa amefungashiwa vyandarua na hao wazungu wanaopora rasilimali zetu. Bado nafuatilia kujua hatma ya sakata hili na nitaendelea kuwa update kadri inavyowezekana.

"CHADEMA lazima tuisambaratishe ndani ya mwaka mmoja kwa njia yeyote tuiwezayo" Wasirra
 
Hali ya kisiasa wilayani Tarime inazidi kuwa tete baada ya jana mwenyekiti wa Chadema wilayani humo kuandika barua polisi kusitisha mikutano ya mwenyekiti wa BAVICHA John Heche. Taarifa za uhakika nilizonazo ni kwamba kamanda John Heche anasakwa na jeshi la polisi kanda maalum ya Tarime Rorya kwa tuhuma za kumkashifu raisi Kikwete.

Katika mkutano wake wa juzi alioufanya katika mji mdogo wa Sirari, Heche aliwaeleza wananchi kuwa Tanzania imekuwa ni nchi ombaomba wakati ina rasilimali nyingi sana za kuiwezesha kujitegemea. Akawaeleza wananchi hao kuwa raisi Kikwete ndiye anaongoza zoezi hilo la kuwa ombaomba, kwa kwenda ulaya na marekani kila mara kutembeza bakuli.

Heche alielezea masikitiko yake kwa raisi Kikwete kupishana angani na ndege zilizojaza madini yetu kupeleka ulaya na marekani huku yeye akiwa amefungashiwa vyandarua na hao wazungu wanaopora rasilimali zetu. Bado nafuatilia kujua hatma ya sakata hili na nitaendelea kuwa update kadri inavyowezekana.

"Nisipoenda kuhemea watanzania mtakufa na njaa!" - J. M. Kikwete (Tabora 2010)
 
yote haya ni kama yanajirudia na isitoshe kwa taifa kama letu lililojaa uzalimu na vimbwanga vya kila aina,ktk harakati za kusaka ukombozi misukosuko ndo mahara pake,.IF YOU DO NOT STAND FOR IT THEN PUT THE WORD FREEDOM OUT OF YOUR vocabulary,.HECHE USITISHIKE NDO MUENDELEZO HUO SIO MAPYA HAPA KWETU
 
Kwa maslahi yapi uliyoyaona kwa awamu hii ya kikwete...unajua deni la taifa kwa sasa ni kiasi gani? unakumbuka wakati anaachiwa nchi hazina kulikuwa na kiasi gani? je deni likuwa kiasi gani?...vipi bei ya vyakula nikupe mfano kikwete anachukua nchi bei ya mchele ilikuwa TZS 650 sasa hivi mpaka TZS 3000, kiberiti 25 sasa hivi 100...ngoja nikomee hapo
Crashwise acha kupoteza mda wako kumuelimisha thatha kama una mda wa kuchezea si umfundishe paka wako kusoma na kuandika?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom