PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 354
- 395
“NARUDI ZANGU CHADEMA”
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Jimbo la Arusha Mjini, Amani Kimati, ametangaza kujivua rasmi uanachama wa chama hicho na kuhamia CHADEMA, chama ambacho awali alikihudumia katika nyadhifa mbalimbali ikiwemo kuwa Katibu Mwenezi wa Kata ya Sombetini.
Kimati amesema amefanya uamuzi huo kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo chama cha CHAUMMA kushindwa kusimamia mabadiliko wakiwa ndani ya mchakato wa uchaguzi. Pia amekituhumu chama hicho kwa kushindwa kukemea matukio ya utekaji yanayoendelea kuripotiwa nchini.
“Tuliaminishwa Chaumma inaenda kupambana na dola hili tupate katiba mpya, tupate ‘reforms’ kwenye uchaguzi huku tukiwa ndani ya uchaguzi, lakini hatuoni movement yoyote inayofanyika ili katiba mpya ipatikane,” amesema Kimati.
Aidha, katika hatua nyingine, Kimati amesema wanachama wa chama hicho waliaminishwa kuwa Mwenyekiti wa zamani wa CHADEMA, Freeman Mbowe, angehamia ndani ya CHAUMMA na ndiye angekuwa mgombea urais wa chama hicho, lakini mpaka sasa Mbowe hajaonekana ndani ya chama hicho.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Jimbo la Arusha Mjini, Amani Kimati, ametangaza kujivua rasmi uanachama wa chama hicho na kuhamia CHADEMA, chama ambacho awali alikihudumia katika nyadhifa mbalimbali ikiwemo kuwa Katibu Mwenezi wa Kata ya Sombetini.
Kimati amesema amefanya uamuzi huo kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo chama cha CHAUMMA kushindwa kusimamia mabadiliko wakiwa ndani ya mchakato wa uchaguzi. Pia amekituhumu chama hicho kwa kushindwa kukemea matukio ya utekaji yanayoendelea kuripotiwa nchini.
“Tuliaminishwa Chaumma inaenda kupambana na dola hili tupate katiba mpya, tupate ‘reforms’ kwenye uchaguzi huku tukiwa ndani ya uchaguzi, lakini hatuoni movement yoyote inayofanyika ili katiba mpya ipatikane,” amesema Kimati.
Aidha, katika hatua nyingine, Kimati amesema wanachama wa chama hicho waliaminishwa kuwa Mwenyekiti wa zamani wa CHADEMA, Freeman Mbowe, angehamia ndani ya CHAUMMA na ndiye angekuwa mgombea urais wa chama hicho, lakini mpaka sasa Mbowe hajaonekana ndani ya chama hicho.