Boran Jakutay
Senior Member
- Apr 8, 2023
- 110
- 255
Mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka mitatu na nusu (3.5) Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro, inadaiwa amelawitiwa na binamu yake aitwaye Underson Alex (19) maarufu kwa jina Nngwe, wakati wakiwa wanachunga ng’ombe eneo la karibu na nyumbani kwao wilayani humo.
Shangazi wa mtoto huyo akizungumza na GADI TV akiwa nyumbani huko, amesema majira ya jioni siku moja kabla ya kujua tatizo hilo, mtoto huyo alirudi nyumbani akiwa amegeuza suruali yake ndani nje, na siku iliyofuata alianza kueleza anasikia maumivu sehemu ya makalio huku akionyesha kwa ishara na kusema “Nngwe amenichapa na kitu chake huku”.
Aidha, Inaelezwa wazee wa pande zote mbili (Mtuhumiwa na Mhanga) mpaka sasa wamekaa vikao viwili vyakutaka kumaliza jambo hilo kifamilia, kwa kauli mtoto atatibiwa kwa kupewa mafuta ya Ng’ombe, huku mtuhumiwa akiwa mafichoni.
Hata hivyo, Mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Jairy Khanga amekiri mtoto huyo amepokelewa na kufanyiwa vipimo, na kusema majibu ni siri ya mgonjwa na Daktari, hivyo hayupo tayari kuongea chochote.
Chanzo: GADI TV
Shangazi wa mtoto huyo akizungumza na GADI TV akiwa nyumbani huko, amesema majira ya jioni siku moja kabla ya kujua tatizo hilo, mtoto huyo alirudi nyumbani akiwa amegeuza suruali yake ndani nje, na siku iliyofuata alianza kueleza anasikia maumivu sehemu ya makalio huku akionyesha kwa ishara na kusema “Nngwe amenichapa na kitu chake huku”.
Aidha, Inaelezwa wazee wa pande zote mbili (Mtuhumiwa na Mhanga) mpaka sasa wamekaa vikao viwili vyakutaka kumaliza jambo hilo kifamilia, kwa kauli mtoto atatibiwa kwa kupewa mafuta ya Ng’ombe, huku mtuhumiwa akiwa mafichoni.
Hata hivyo, Mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Jairy Khanga amekiri mtoto huyo amepokelewa na kufanyiwa vipimo, na kusema majibu ni siri ya mgonjwa na Daktari, hivyo hayupo tayari kuongea chochote.
Chanzo: GADI TV