Kilichotokea Hanang, kikitokea Mwanza itakuwaje?

Jbst

JF-Expert Member
Nov 29, 2020
1,925
3,951
Nimejaribu kufikiria tu huko Hanang kwa yaliyotokea sasa hebu tujiulize ile milima ya Mwanza na yale mawe makubwa itakuwaje? Tuombe Mungu isitokee kabisa huko mwanza.

Kuna mawe ni makubwa kuliko hata nyumba ya gorofa moja yapo milimani huko yananing'inia tu, haya yakiporomoka mpka huku tambarare hakuna kifaa chochote cha kuyasogeza pembeni kwasababu ni makubwa sana.

Au labda milima ya mwanza haina majanga ya asili?

Nimejaribu kuwaza tu ila kuna hatari sana huko
 
Kwamba tumuombe Mungu huko kwingine hawaombia Mungu?

Hapa hapa Daslam tu kakitokea katetemeko kadogo sijui itakuwaje. maeneo kama tandale, buguruni n.k watu wanaishi kwenye nyumba mbovu sana juu yananing'ia matofali.
 
Nimejaribu kufikiria tu huko hanang kwa yaliyotokea sasa hebu tujiulize ile milima ya mwanza na yale mawe makubwa itakuwaje? Tuombe Mungu isitokee kabisa huko mwanza...
Mungu angekuwepo, kungekuwa hakuna haja ya kumuomba kitu.

Kwa upendo wake mkuu, angekupa unachohitaji kabla hata hujajua unakihitaji.

Ukiona kuna haja ya kumuomba Mungu tu, ujue huo ni uthibitisho Mungu hayupo, pambana na hali yako mwenyewe.
 
Mwanza sehemu nyingi hazina tope, milimani kuna mawe na tambarare kuna mchanga, kwahiyo mimi sio engineer ila naona possibility ya landslide ya kisa mvua ni minimum ila risk ni mafuruko maana drainage ya maeneo ya milimani kama Mabatini na Igogo haipo sawa hivyo kuna sehemu ziko na uwezekano wa kukumbwa na mafuriko kwa wale walioko maeneo ya chini na majanga mengine kama matetemeko ambayo haijalishi upo baharini au tambarare kuna mawee au topee unachapwa tu.
 
Kwamba tumuombe Mungu huko kwingine hawaombia Mungu?

Hapa hapa Daslam tu kakitokea katetemeko kadogo sijui itakuwaje. maeneo kama tandale, buguruni n.k watu wanaishi kwenye nyumba mbovu sana juu yananing'ia matofali.
Nimeongelea mwanza na ww ungeweza andika uzi wako ukaongelea tandale
 
Mwanza sehemu nyingi hazina tope, milimani kuna mawe na tambarare kuna mchanga, kwahiyo mimi sio engineer ila naona possibility ya landslide ya kisa mvua ni minimum ila risk ni mafuruko maana drainage ya maeneo ya milimani kama Mabatini na Igogo haipo sawa hivyo kuna sehemu ziko na uwezekano wa kukumbwa na mafuriko kwa wale walioko maeneo ya chini na majanga mengine kama matetemeko ambayo haijalishi upo baharini au tambarare kuna mawee au topee unachapwa tu.
Yale mawe yakiporomoka iatakuwaje ndo nilichozungumzia mimi sio tope
 
Kila mahali we ni kumponda Mungu tuu, hujaona hoja kuu ya mleta mada.
Mkuu,

Ukichofanya hapa ni logical fallacy. Kilatini inaitwa "ad hominem ". Yani, umeshindwa kujibu hoja ya mtu, unaiacha hoja, unamshambulia mtu.

Mara nyingi hii hufanywa na mtu asiye na hoja ya kujibu hoja, anakimbilia kumkashifu mtoa hoja, bila ya kuigusa hoja.

Hoja ya imani ya Mungu ni mtambuka.

Mimi sikuileta hoja hii, mtoa mada kaitaja. Na kaitaja kwa sababu huko kwetu ipo katikati ya kila kitu. Haikwepeki.

Mimi sikuanzisha habari za Mungu katika thread ambayo haijamtaja Mungu. Nimeangazia tu habari ya Mungu ambayo ilishaletwa na mtoa mada.

Yani badala ya kuangalia Geological Survey Mwanza kuna uwezekano wa kuwa na tetemeko la ardhi kubwa kiasi gani, kila baada ya miaka gani, na likitokea, yale mawe yatadondoka vipi, na yakidondoka tutajikinga vipi, tunasema tumuombe Mungu ambaye hayupo atuepushe na majanga!

Sasa mbona humshambulii mtoa mada kwamba nyie mbona kila kitu mnamuweka Mungu, unanishambulia mimi kwa kusema habari za Mungu ni upuuzi tu?

Huoni kwamba una selective and convenient outrage, kwa mtu ambaye yuko against worldview yako tu?

Mtu anaweza kuona hili hapa jiwe nikijenga hapa ni hatari sana, lakini akaamua kujenga bila hata kupata ushauri wa wataalamu, kwa kuamini tu "Mungu atanilinda".

Ndivyo majanga nengi yanavyotokea hivyo, kutojali usalama katika vyombo vya usafiri, katika kujenga, katika mambo mengi sana.

Sasa, katika utamaduni kama huu wa kuishi kwa kudra za Mungu, kulitazama hili suala la uwepo wa Mungu ni muhimu sana.

Kwa sababu, kama kweli huyo Mungu hayupo, na watu hawataki kujua hilo, ni muhimu angalau wajue kuwa huyo Mungu hayupo na wanapochujua risk ya kujenga ovyo, kuna siku linaweza kutokea janga, wakaumia au kufa, wasije kufikiri kumuomba Mungu kutawasaidia.

Tubishane kwenye facts. Mungu yupo au hayupo?

Kama unaweza kuthibitisha yupo, halafu mimi nasema uongo, hapo unaweza kuwa na point ya kunishambulia.

Lakini, wewe hujaweza kukanusha kile ninachokisema, unakuja kunifanyia censorship? Unanifunga mdomo nisitoe maoni yangu kwa uhuru? Hapa JF ambapo tunasema "We Dare to Talk Openly"?

Pinga hoja kwa hoja, usitake kunyamazisha watu wasitoe maoni yao.
 
Tatizo wananchi pia uelewa mdogo sana ndio maana wanasiasa wanawafanya mtaji wanasubiria janga litokee waende na chopa wakapige picha yaani hapo ukiwaambia waondoke wataanza kuilaumu serikali.
 
Kwa Mwanza ni ngumu kutokea. Kuna aina mbili za milima yenye mawe ya Kwanza mawe yapo juu na ya pili mawe yamejikita aridhini mpaka juu.
Mara nyingi sehemu ambapo mawe yalianguka na kuuwa watu chanzo chake ni kuyachimba na kutoa udongo unao yashikilia. Possible ya mawe kudondoka maybe kuwa na tetemeko kwa magnitude kubwa, ila kwa swala la mvua haiwezekani mawe kudondoka.
 
Kwa Mwanza ni ngumu kutokea. Kuna aina mbili za milima yenye mawe ya Kwanza mawe yapo juu na ya pili mawe yamejikita aridhini mpaka juu.
Mara nyingi sehemu ambapo mawe yalianguka na kuuwa watu chanzo chake ni kuyachimba na kutoa udongo unao yashikilia. Possible ya mawe kudondoka maybe kuwa na tetemeko kwa magnitude kubwa, ila kwa swala la mvua haiwezekani mawe kudondoka.
Haya ni maoni yako au utafiti wa Kisayansi?
 
Haya ni maoni yako au utafiti wa Kisayansi?
Ni maoni yangu pia Mimi ni mkazi wa huko. Kuhusu kudondoka na kuanguka kwa mawe imetokea kwa mitaa jirani kabisa mfano mabatini, Sinai na ustawi . Pote huko sababu zilikuwa hivyo. Pia nature ya milima ya mwanza ndivyo ilivyo mfano kitangiri, isamiro huko mawe kidokidogo na yapo juu juu ila bwiru, mahina, mkorani, mkuyuni, nyegezi , mabatini ya nyerere A na B ,pamoja na bugarika na sehemu za karibu huko ni hatari mawe kuyachimba maana utajizika
 
Mkuu,

Ukichofanya hapa ni logical fallacy. Kilatini inaitwa "ad hominem ". Yani, umeshindwa kujibu hoja ya mtu, unaiacha hoja, unamshambulia mtu.

Mara nyingi hii hufanywa na mtu asiye na hoja ya kujibu hoja, anakimbilia kumkashifu mtoa hoja, bila ya kuigusa hoja.

Hoja ya imani ya Mungu ni mtambuka.

Mimi sikuileta hoja hii, mtoa mada kaitaja. Na kaitaja kwa sababu huko kwetu ipo katikati ya kila kitu. Haikwepeki.

Mimi sikuanzisha habari za Mungu katika thread ambayo haijamtaja Mungu. Nimeangazia tu habari ya Mungu ambayo ilishaletwa na mtoa mada.

Yani badala ya kuangalia Geological Survey Mwanza kuna uwezekano wa kuwa na tetemeko la ardhi kubwa kiasi gani, kila baada ya miaka gani, na likitokea, yale mawe yatadondoka vipi, na yakidondoka tutajikinga vipi, tunasema tumuombe Mungu ambaye hayupo atuepushe na majanga!

Sasa mbona humshambulii mtoa mada kwamba nyie mbona kila kitu mnamuweka Mungu, unanishambulia mimi kwa kusema habari za Mungu ni upuuzi tu?

Huoni kwamba una selective and convenient outrage, kwa mtu ambaye yuko against worldview yako tu?

Mtu anaweza kuona hili hapa jiwe nikijenga hapa ni hatari sana, lakini akaamua kujenga bila hata kupata ushauri wa wataalamu, kwa kuamini tu "Mungu atanilinda".

Ndivyo majanga nengi yanavyotokea hivyo, kutojali usalama katika vyombo vya usafiri, katika kujenga, katika mambo mengi sana.

Sasa, katika utamaduni kama huu wa kuishi kwa kudra za Mungu, kulitazama hili suala la uwepo wa Mungu ni muhimu sana.

Kwa sababu, kama kweli huyo Mungu hayupo, na watu hawataki kujua hilo, ni muhimu angalau wajue kuwa huyo Mungu hayupo na wanapochujua risk ya kujenga ovyo, kuna siku linaweza kutokea janga, wakaumia au kufa, wasije kufikiri kumuomba Mungu kutawasaidia.

Tubishane kwenye facts. Mungu yupo au hayupo?

Kama unaweza kuthibitisha yupo, halafu mimi nasema uongo, hapo unaweza kuwa na point ya kunishambulia.

Lakini, wewe hujaweza kukanusha kile ninachokisema, unakuja kunifanyia censorship? Unanifunga mdomo nisitoe maoni yangu kwa uhuru? Hapa JF ambapo tunasema "We Dare to Talk Openly"?

Pinga hoja kwa hoja, usitake kunyamazisha watu wasitoe maoni yao.
Aseee we jamaa Kiranga kweli Kiranga, kwa maelezo uliyonipa sina nguvu ya kukubishia wala kukukubalia.
Maana nikibisha sijui nitakuwa nabisha nini vivyo hivyo nikikubali.
Anyway huko USA kuna ramani gani nijichange niibuke maana degree yangu hadi sahivi sijaipa maana inayostahili.
 
Aseee we jamaa Kiranga kweli Kiranga, kwa maelezo uliyonipa sina nguvu ya kukubishia wala kukukubalia.
Maana nikibisha sijui nitakuwa nabisha nini vivyo hivyo nikikubali.
Anyway huko USA kuna ramani gani nijichange niibuke maana degree yangu hadi sahivi sijaipa maana inayostahili.
Mkuu,

Strategy ya kumuomba Mungu huikubali?

Maana umenishambulia sana kwa kumponda Mungu.

Ngoja nikurudishe kwa Mungu ufurahi sasa.
 
Mkuu,

Strategy ya kumuomba Mungu huikubali?

Maana umenishambulia sana kwa kumponda Mungu.

Ngoja nikurudishe kwa Mungu ufurahi sasa.
Mimi namuamini Mungu.
Wewe unaamini nini?

Vipo hapo USA elimu zetu za kibongo bongo zinasoko?
 
Back
Top Bottom