Kila nikipiga ramli naiona Rwanda na Kagame kama dalali wa kuuza bandari zetu kwa DP World

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,426
7,213
Rwanda ni nchi ndogo ya milima na isiyo na bandari pia ina idadi kubwa ya watu kulinganisha na eneo lake. Ni tofauti na Tanzania ambayo ni nchi kubwa ardhi ya kutosha mali asili kibao na ukanda wa bahari mkubwa wenye bandari nyingi.

Rais Kagame ni mtu mwerevu sana kwenye kujenga uchumi wa nchi yake na kuwapatia maslahi tabaka la utawala huko Rwanda. Yuko tayari kutumia udhaifu wa nchi jirani kwa manufaa ya Rwanda.

Tumeona Rwanda wakivuna madini na mali asili za Congo na wala hawajali kusaidia vikundi vya kijeshi kwa kisingizio chochote mradi kuhakikisha wanadhibiti maeneo ya madini mashariki ya congo.

Nchi kama tanzania hatutakiwi kuigiza mkakati wa maendeleo wa rwanda. Hivi karibuni Rwanda wamewapa DP World kujenga bandari kavu kubwa Rwanda kwa hivyo bila shaka ni mkakati wa mjanja Kagame kuitumia DPworld kuhakikisha bandari ya Dar es Salaam inahamia Rwanda kwa bidhaa za Congo, Burundi Uganda na Sudan ya Kusini.

Mpango ni transit cargo kupelekwa Rwanda ambapo zitalipiwa kodi huko na kuongeza shughuli za kiuchumi kabla ya kusafirishwa nchini kwao Congo ya Mashariki, Uganda na Sudan ya Kusini.

Kabla ya sakata la DPW kuibuka tumeona ziara za mjanja kagame za kikazi chapchap bila shaka akimtia moyo mama asighairi mpango wa kuipa DPW bandari zetu licha jumba kutaka kumuangukia.

Tusisahau pamoja na kauli za mara kwa mara dhidi ya ubeberu kagame ni mshiriki wa karibu wa njama za kiuchumi za wamarekani dhidi ya Congo. Rwanda iko tayari kuidhuru nchi yoyote kiuchumi ili kupata makombo ya ngawira za mabeberu.

Watanzania tuchunge mali zetu asili tulizojaliwa kwa wivu vinginevyo zitatumika sio kwa manufaa ya wale mabeberu wa asili ila wajanja na mabeberu wapya wa uchumi kama rwanda na Dubai huku tukibakia masikini na kuonekana wajinga.
 
Jambo ni la kweli kabisa.Kagame ndio engineer mkuu ni bahati mbaya Huwa tunachelewa kukuona mchezo. Tukidhbiti Dar port na Mombasa port DP world hawawezi pata faida Rwanda. DP world wakishika Port za Mombasa na Dar mnufaika ni Kagame na DP world kutakuwa na misrepresentation za kutosha,Congo hata akiwa na ugomvi na Rwanda hata kua na Access ya Indian ocean bila Rwanda.
 
Nimesoma Tu kichwa cha Habari, Ramli ni utapeli uliopitwa na wakati , Kagame na mkataba uchwara wapi na wapi .

Bora ungesema hao ndugu zetu WA 254 kidogo ingeleta ukakasi
 
Utakuwa mnyarwanda mana mnapenda kumvimbisha kichwa huyo jogooo mzee
 
Akili mbovu ya mtawala wetu ndio chanzo cha kutolewa bure bandari zetu kwa mwarabu, yeye ndie kiguu na njia kila siku kwenda kwa wajomba zake Arabuni, hiyo ramli yako haina maana.
Siyo ramli ni mwendelezo wa kufanya Ana akili sanaaaaaaaa
 
Akili mbovu ya mtawala wetu ndio chanzo cha kutolewa bure bandari zetu kwa mwarabu, yeye ndie kiguu na njia kila siku kwenda kwa wajomba zake Arabuni, hiyo ramli yako haina maana.
Kuna siku Kagame alitua bongo fasta mwaka 2022 na baada ya hapo mambo ya DP world yakaja kumbuka DP world walianza project Yao Rwanda toka 2021. Kuna ukweli kuwa Kagame anaisubiri hii dili ya Dar port kwa hamu maana atanufaika nayo zaidi
 
Kuna siku Kagame alitua bongo fasta mwaka 2022 na baada ya hapo mambo ya DP world yakaja kumbuka DP world walianza project Yao Rwanda toka 2021. Kuna ukweli kuwa Kagame anaisubiri hii dili ya Dar port kwa hamu maana atanufaika nayo zaidi
Sidhani
 
Mbona hilo halihitaji ramli na liko wazi! Mizigo yote ya Congo, Malawi, Burundi kupitia Bandari ya Dar es Salaam itachukuliwa Rwanda (CIF Rwanda).
Biashara za Watanzania wenye malori zitaathirika big time! Soko la Kariakoo litabaki kwa ajili ya Bamia na Matikiti maji!
Nchi yenye Viongozi Wajinga na Wananchi wasiojitambua lazima tufanywe hivyo.
 
Nchi kama tanzania hatutakiwi kuigiza mkakati wa maendeleo wa rwanda. Hivi karibuni Rwanda wamewapa DP World kujenga bandari kavu kubwa Rwanda kwa hivyo bila shaka ni mkakati wa mjanja Kagame kuitumia DPworld kuhakikisha bandari ya Dar es Salaam inahamia Rwanda kwa bidhaa za Congo, Uganda na Sudan ya Kusini.
Naunga mkono hoja.
 
Kuna siku Kagame alitua bongo fasta mwaka 2022 na baada ya hapo mambo ya DP world yakaja kumbuka DP world walianza project Yao Rwanda toka 2021. Kuna ukweli kuwa Kagame anaisubiri hii dili ya Dar port kwa hamu maana atanufaika nayo zaidi
Kagame kuja hapa hakuna uhusiano wowote wa serikali yetu kuingia mkataba wa hovyo kama ule, au mnataka kusema Kagame aliwalewesha viongozi wetu alivyokuja mpaka wakasaini ule mkataba wa hovyo?

Siamini, tatizo letu ni akili ndogo ya Samia.
 
Hii yote ni chuki yako tu kwa Gen. Kagame, unataka kusema yeye ana control hivyo vyombo vyenu vyoote vinavyopigia debe DP? Yaani chuki zenu zinawafanya ma mbumbumbu yasiyofikiria kabisaaa. mwacheni mwamba PK achape kazi.
 
Back
Top Bottom