Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Kila unapoenda vijana kwa wazee mazungumzo ni Richmond tu , kila sehemu lowasa tu , wengi wanampongeza sana kikwete kwa kazi aliyoifanya ya kumwajibisa lowasa , hawajui kwamba lowassa aliamua kujiuzuru mwenyewe kutokana na hiyo kashfa ya Richmond .
Watanzania bwana na sasa wameshasahau kuhusu EPA , BOT , IPTL , BUZWAGI na kashfa zingine kubwa ambazo ni zaidi ya hii ya Richmond na kwa hakika tume zikiundwa hapa wataondoka wengi .
Jana nilipokuwa natazama TV naona viongozi wa dini nao wanaongelea masuala ya ufisadi bila woga na kujiamini lakini tukumbuke wachungaji hawa hawa ndio wanaomwita lowasa katika matamasha yao ya kuchangia shule na miradi mengine na anachangia pesa nyingi .
Kama lowasa akiwajibishwa na kusema zile hela amepeleka wapi naamini nyingi zitakuwa zimeenda katika kuchangia haya makanisa , hizi shule za makanisa , na taasisi zingine za kikanisa je kanisa liko tayari kurudisha pesa husika ?
Wakati tunataka lowasa arudishe pesa za watanzania , tuwanyooshee vidole kuwaonya viongozi wa dini kwamba nao wanaohusika katika kupokea haya mapesa ya lowasa katika michango yake ya kanisa tunawaomba waelezee hiii michango ya lowasa wameitumia vipi au nao wajiuzuru.
Leo jioni wakati naelekea nyumbani nilipita katika kizuizi Fulani cha gari , wale jamaa wakawa wanataka mchango kwa sababu wametengeneza hiyo bara bara mara dala dala likapita yule konda akawaambia abiria zake
Eehh angalia ile ndio Richmond yao nao wanakula kiulaini .
Na usiku huu hapa nilipo nimeshituka toka usingizini , najiuliza kikwete atatushawishi vipi ili tuweze kuamini baraza lake la mawaziri litakalo tangazwa kesho , kutakuwa hakuna wafanyabiashara wanaokodisha meli mbovu na iharibikie baharini ?
Au atatuletea mawaziri ambao nao wana virichmond vyao huko pembeni ? wanakuja kuendelea na tabia zile zile za kuchota kufukuzwa , kujiuzuru au kuamua kuchoka tu ?
Ngoja tuone kila mtu na kirichmond chake
Kila unapoenda vijana kwa wazee mazungumzo ni Richmond tu , kila sehemu lowasa tu , wengi wanampongeza sana kikwete kwa kazi aliyoifanya ya kumwajibisa lowasa , hawajui kwamba lowassa aliamua kujiuzuru mwenyewe kutokana na hiyo kashfa ya Richmond .
Watanzania bwana na sasa wameshasahau kuhusu EPA , BOT , IPTL , BUZWAGI na kashfa zingine kubwa ambazo ni zaidi ya hii ya Richmond na kwa hakika tume zikiundwa hapa wataondoka wengi .
Jana nilipokuwa natazama TV naona viongozi wa dini nao wanaongelea masuala ya ufisadi bila woga na kujiamini lakini tukumbuke wachungaji hawa hawa ndio wanaomwita lowasa katika matamasha yao ya kuchangia shule na miradi mengine na anachangia pesa nyingi .
Kama lowasa akiwajibishwa na kusema zile hela amepeleka wapi naamini nyingi zitakuwa zimeenda katika kuchangia haya makanisa , hizi shule za makanisa , na taasisi zingine za kikanisa je kanisa liko tayari kurudisha pesa husika ?
Wakati tunataka lowasa arudishe pesa za watanzania , tuwanyooshee vidole kuwaonya viongozi wa dini kwamba nao wanaohusika katika kupokea haya mapesa ya lowasa katika michango yake ya kanisa tunawaomba waelezee hiii michango ya lowasa wameitumia vipi au nao wajiuzuru.
Leo jioni wakati naelekea nyumbani nilipita katika kizuizi Fulani cha gari , wale jamaa wakawa wanataka mchango kwa sababu wametengeneza hiyo bara bara mara dala dala likapita yule konda akawaambia abiria zake
Eehh angalia ile ndio Richmond yao nao wanakula kiulaini .
Na usiku huu hapa nilipo nimeshituka toka usingizini , najiuliza kikwete atatushawishi vipi ili tuweze kuamini baraza lake la mawaziri litakalo tangazwa kesho , kutakuwa hakuna wafanyabiashara wanaokodisha meli mbovu na iharibikie baharini ?
Au atatuletea mawaziri ambao nao wana virichmond vyao huko pembeni ? wanakuja kuendelea na tabia zile zile za kuchota kufukuzwa , kujiuzuru au kuamua kuchoka tu ?
Ngoja tuone kila mtu na kirichmond chake
Shy amepatia kabisa kuwa watu wanatoa credit kwa Kikwete eti "kwa kumwajibiisha Lowasa" badala ya kutoa pongezi hizo kwa Kamati ya Bunge iliyomshinikiza Lowasa kujiuzulu. Wamesahau kabisa kuwa Lowasa alijiuzulu kwa shinikizo la Kamati ya Bunge wala hakuwajibishwa na Rais.
Mkuu Kichuguu,
Ile ahadi yangu ya kumlipa Kikwete 84 cents kwa kuvunja baraza la mawaziri nimeamua kumpa Lowasa kwa kumlazimisha Kikwete avunje baraza la mawaziri!
Hii Shy inafurahisha sana, haya sasa Richmond imekuwa msamiati tena. hata mimi naandaa karichmond kangu ka kuchangisha mchango wa Sikukuu ya wapendanao.