Kila kitambulisho cha Taifa kimegharimu tsh 89,800

Kila kitambulisho cha Taifa kimegharimu tsh 89,800

Hesabu ni shida bongo pamoja na kwamba kila mtu ana calculator mfukoni siku hizi!!
 
NIDA walipewa shilingi bilioni 179.6 kwa ajili ya kutengeneza vitambulisho vya taifa.Vitambulisho walivyotegeneza na kugawia wananchi ni milioni mbili.Ukigawa pesa walizopewa na vitambulisho walivyotengeneza utapata jawabu kuwa kila kitambulisho kimoja kimegharimu shilingi milioni 89.8.

Nchi hii ina wezi.Ndio maana Maghufuli kweli ana hasira nao.
Accountability was sent on paid leave and corruption appointed in darkness where counts of votes were by show of hands only
 
Hii ni trillion moja.

Ebu cheki mdogo mdogo tueleweshane!
10 ni kumi
100 ni mia moja.
1,000 ni elfu moja.
10, 000 ni elfu kumi.
100, 000 ni laki moja.
1,000,000 ni milioni moja.
10,000,000 ni milioni kumi.
100,000,000 ni milioni mia.
1,000,000,000 ni BILIONI moja au milioni elfu moja.
10, 000,000,000 ni bilioni kumi.
100,000,000,000 ni bilioni mia moja.
1,000,000,000,000 ni bilioni elfu moja au TRILIONI MOJA.

......

.......Mkuu salute
 
NIDA walipewa shilingi bilioni 179.6 kwa ajili ya kutengeneza vitambulisho vya taifa.Vitambulisho walivyotegeneza na kugawia wananchi ni milioni mbili.Ukigawa pesa walizopewa na vitambulisho walivyotengeneza utapata jawabu kuwa kila kitambulisho kimoja kimegharimu shilingi milioni 89.8.

Nchi hii ina wezi.Ndio maana Maghufuli kweli ana hasira nao.
Duuuuuuh
Halafu kuna mtu anaibuka anasema waliosapoti ukawa wanaonewa hahahahhahhah
 
niulize wadau hivi katika hayo mapesa gharama za wakandarasi ni ngapi? na gharama za majengo labda ni ngapi? ? tukitoa hizo kwanza tunaweza pata sasa gharama ya kitambulisho. labda kama hela zote walizopewa Ilikuwa kwa ajili ya kutoa vitambulisho tu. we need have an analytical review on this issue. otherwise tunaweza kujitumbukiza kwenye ushabiki usiokuwa na faida kwetu wananchi. tuelezwe mahesabu kiundani tuelewe.
 
Bilioni moja ni milioni milioni moja.Ngoja nikuandikie kabisa bilioni moja ina sifuri 12.Kwa tarakimu inaandikwa hivi

1,000,000,000,000
Nafikiri bilion ina sifuri 9 na sio 12.
Huandikwa hivi...
1,000,000,000
Bilion moja ina milion elfu moja.
Bado unaendelea kubisha?
 
Kama kitambulisho cha taifa kina thamani ya milioni 89 basi Yehodaya miye nauza cha kwangu. Kwani siwezi kufa njaa ilihali Nina lulu ndani. Nitafute ukiwa na hata 50m nikupe na nitakutafutia vingine vingi tu.
 
Huyo mzee wa push up nae kama dawa ya mswaki tu...hana sumu maneno mengi tu na tambo zenye vitisho
 
Inaonekana wewe ulisoma ile Historia ya binadamu wa kwanza alikuwa sokwe ya darasa la sita, kipindi cha Hisabati ulikuwa ukijificha nyuma ya choo ch shule. Hesabu rahisi hivi inakushinda?
 
Watanzania wenzangu leo nimesoma kwenye magaezeti ya leo kuwa vitambulisho vya taifa kila kimoja kimeigharimu serikali 85,000/=.

Hii ni baada ya zaidi ya bilioni 170 kutumika kwa mikoa ya Dar na Pwani pekee ambapo vitambulisho milioni 2 vimetolewa.

Kwa kifupi ukichukua bilioni 170 ukagawa kwa vitambulisho milioni 2 utapata gharama ya kila kitambulisho 85,000/= kwa hiyo ili kupata vitambulisho vya raia wote inahitajika trilioni 3.8 sawa na gharama ya ujenzi wa reli mpya standard gauge.

Naona kunahitaji kuweka adhabu ya kunyongwa kwa mafisadi na wahujumu uchumi kama hawa.
 
Namwonea huruma miss tanzania,wanavyomdandia tu,kuja kushtuka kazalishwa watoto 8
 
Aaah!!!!! Kudadadaki!!!! hawa jama wamepiga mpunga wa maana aseeee!!! kumbe JPM yuko sahihi kuwatumbua
 
hatuna vitambulusho tangu tumepeleka barua zza serikali za mtaa hata picha bado kupigwa


mbona vya kura ni fasta tu?
 
Aaah!!!!! Kudadadaki!!!! hawa jama wamepiga mpunga wa maana aseeee!!! kumbe JPM yuko sahihi kuwatumbua
Kugawa 179B kwa idadi ya vitambulisho vilivo gawiwa ni makosa makubwa maana ndani ya hizo pesa kuna capital investment kama majengo (yaliyo jengwa kama data center na data recovery), ofisi karibu kila wilaya, magari, vifaa vya kusajilia, ambavyo gharama zake ni one time investment... unapo sema vitambulisho 2m vilivo gawiwa kuna vitambulisho vingi tu havijagawiwa.... kuna mengi ya NIDA hayafahamiki na nashindwa kuelewa kwa nini NIDA wasiweke ukweli wao pia.... kama wanaogopa kujibu sababu ya insurbodination maana sio vizuri kujibishana na Mh. Raisi basi waandishi wa habari ( investigative journalists ) ndo kazi yao......
 
Back
Top Bottom