kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,224
- 1,686
KWA UFUPI
"Anatakiwa ajiamini katika kutekeleza majukumu yake, pia asiogope kushindwa kwani ni sehemu ya mapambano katika maisha. Hivyo, hatakiwi kuwa na hofu katika kutekeleza majukumu yake".
Baba yangu alinipa zawadi ambayo mtu yeyote angeweza kuitoa kwa mtoto wake. Alikuwa akiniamini. Kila baba ana nafasi maalumu katika maisha ya binti yake. Kama shujaa katika macho yake, baba ana jukumu kubwa la kumwonyesha binti yake jinsi mwanamume wa kweli anavyompa nguvu ya kuukabili ulimwengu kwa kujiamini, huku akiwa na nguvu zote. Pamoja na yote, anatakiwa amwonyeshe binti yake kuwa baba ni mwanamume wa kwanza katika maisha ya mtoto wa kike.
Yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo kila baba anapaswa kumfundisha binti yake ili kumthibitishia kuwa yeye ni baba bora dunuani.
Yeye ni wa kipekee
Kimsingi kila mtu ni wa kipekee. Ni kwamba, baba anatakiwa kumsaidia binti yake kujitambua na kujua nafasi yake katika maisha. Pia anatakiwa kuelewa kuwa yeye ni ndiye pekee na hakuna kama yeye duniani. Baba mzuri ni yule anayemheshimu na kumkubali binti yake.
Kitendo hiki kitamsaidia kumfanya awe na furaha siku zote. Zaidi ya hayo kama mzazi, unatakiwa kumfundisha mtoto upendo. Hii itamsaidia kuwa na maadili mema na kuwa na mtazamo chanya wa maisha.
Anastahili mazuri katika maisha yake
Nafikiri kila baba anafahamu kuwa binti yake anastahili kila kilicho kizuri katika ulimwengu huu. Ni jukumu la baba kuhakikisha binti yake anaelewa kuwa anastahili heshima, upendo na shukrani.
Ikiwa unahitaji binti yako afurahie maisha, basi mfundishe kuwa anatakiwa kuangalia yeye anataka nini na siyo watu wengine wanamfikiriaje.
Anaweza kufanya moja kati ya mambo muhimu ambayo baba anapaswa kumfundisha binti yake. Kwamba, ana nguvu za kutosha kumudu na kuyakabili mambo na mitihani mbalimbali ya kimaisha.
Anatakiwa ajiamini katika kutekeleza majukumu yake, pia asiogope kushindwa kwani ni sehemu ya mapambano katika maisha. Hivyo, hatakiwi kuwa na hofu katika kutekeleza majukumu yake.
Katika jamii zetu, uwepo wa mfumo dume kwa kiasi fulani umetokomezwa, hivyo baba anatakiwa kumlea binti yake akihakikisha kuwa anakuwa shupavu na mwenye uthubutu.
Awe huru kueleza mawazo yake
Najua mara nyingi huwa ni vigumu kuukabili woga, pia kuwa na uhuru wa kuongea kile unachofikiria kwako ni sawa. Nilipokuwa mdogo, wakati mwingine nilikuwa najisikia vibaya kuuliza maswali.
Baadaye nilihofia kuumiza na kumvunja moyo mtu mwingine kutokana na kile ninachokiwaza juu yake. Wasichana wengi huwa na aibu katika kufanya mambo. Hivyo kama baba unatakiwa kumfundisha binti yako asione tabu kutoa maoni yake juu ya mtazamo wake.
Awe na nidhamu
Nidhamu pia ni jambo la msingi kabisa katika makuzi ya mtoto. Hivyo ni jukumu lako kama baba kuhakikisha binti yako anakuwa na nidhamu ya kutosha kwani huo ndiyo mwongozo madhubuti wa maisha yake ya baadaye.
Ajisimamie
Kuna imani kuwa mtoto wa kike hawezi kufanya kitu kikakamilika bila mkono wa mwanamume. Hili hutokea kutokana na kulegalega kwa kazi ya baba katika kutoa mwongozo wa malezi mema kwa mwanawe. Baba ni mtu nambari moja, anayejua jinsi ya kuilinda familia yake katika njia sahihi. Sasa kwa kuwa kila mtu anatakiwa kujua kujisimamia mwenyewe, baba ana nafasi kubwa ya kumfundisha binti yake jinsi ya kujilinda na kujisimamia.
Maisha yamejaa migogoro na mara nyingi unyonge wa wanawake huwasababishia kuoenewa na kunyimwa haki zao. Hivyo, baba akifanya vizuri kazi yake katika hili ni wazi kuwa hali hii itatoweka.
Awe anaridhika
Hili pia ni muhimu. Binti yako anatakiwa kuelewa kuwa jasho lake lina thamani kubwa katika maisha yake. Anatakiwa kujifunza pia kuwa utegemezi hauna nafasi katika maisha yake. Baba siku zote ni msaada wa familia, lakini kama mwanamke hatakiwi kumchukulia kama mashine ya kutolea pesa.
Unatakiwa kufundisha binti yako kujitegemea. Hatakiwi amtegemee. mwanaume kwa kila kitu.
Chanzo: Mwananchi
"Anatakiwa ajiamini katika kutekeleza majukumu yake, pia asiogope kushindwa kwani ni sehemu ya mapambano katika maisha. Hivyo, hatakiwi kuwa na hofu katika kutekeleza majukumu yake".
Baba yangu alinipa zawadi ambayo mtu yeyote angeweza kuitoa kwa mtoto wake. Alikuwa akiniamini. Kila baba ana nafasi maalumu katika maisha ya binti yake. Kama shujaa katika macho yake, baba ana jukumu kubwa la kumwonyesha binti yake jinsi mwanamume wa kweli anavyompa nguvu ya kuukabili ulimwengu kwa kujiamini, huku akiwa na nguvu zote. Pamoja na yote, anatakiwa amwonyeshe binti yake kuwa baba ni mwanamume wa kwanza katika maisha ya mtoto wa kike.
Yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo kila baba anapaswa kumfundisha binti yake ili kumthibitishia kuwa yeye ni baba bora dunuani.
Yeye ni wa kipekee
Kimsingi kila mtu ni wa kipekee. Ni kwamba, baba anatakiwa kumsaidia binti yake kujitambua na kujua nafasi yake katika maisha. Pia anatakiwa kuelewa kuwa yeye ni ndiye pekee na hakuna kama yeye duniani. Baba mzuri ni yule anayemheshimu na kumkubali binti yake.
Kitendo hiki kitamsaidia kumfanya awe na furaha siku zote. Zaidi ya hayo kama mzazi, unatakiwa kumfundisha mtoto upendo. Hii itamsaidia kuwa na maadili mema na kuwa na mtazamo chanya wa maisha.
Anastahili mazuri katika maisha yake
Nafikiri kila baba anafahamu kuwa binti yake anastahili kila kilicho kizuri katika ulimwengu huu. Ni jukumu la baba kuhakikisha binti yake anaelewa kuwa anastahili heshima, upendo na shukrani.
Ikiwa unahitaji binti yako afurahie maisha, basi mfundishe kuwa anatakiwa kuangalia yeye anataka nini na siyo watu wengine wanamfikiriaje.
Anaweza kufanya moja kati ya mambo muhimu ambayo baba anapaswa kumfundisha binti yake. Kwamba, ana nguvu za kutosha kumudu na kuyakabili mambo na mitihani mbalimbali ya kimaisha.
Anatakiwa ajiamini katika kutekeleza majukumu yake, pia asiogope kushindwa kwani ni sehemu ya mapambano katika maisha. Hivyo, hatakiwi kuwa na hofu katika kutekeleza majukumu yake.
Katika jamii zetu, uwepo wa mfumo dume kwa kiasi fulani umetokomezwa, hivyo baba anatakiwa kumlea binti yake akihakikisha kuwa anakuwa shupavu na mwenye uthubutu.
Awe huru kueleza mawazo yake
Najua mara nyingi huwa ni vigumu kuukabili woga, pia kuwa na uhuru wa kuongea kile unachofikiria kwako ni sawa. Nilipokuwa mdogo, wakati mwingine nilikuwa najisikia vibaya kuuliza maswali.
Baadaye nilihofia kuumiza na kumvunja moyo mtu mwingine kutokana na kile ninachokiwaza juu yake. Wasichana wengi huwa na aibu katika kufanya mambo. Hivyo kama baba unatakiwa kumfundisha binti yako asione tabu kutoa maoni yake juu ya mtazamo wake.
Awe na nidhamu
Nidhamu pia ni jambo la msingi kabisa katika makuzi ya mtoto. Hivyo ni jukumu lako kama baba kuhakikisha binti yako anakuwa na nidhamu ya kutosha kwani huo ndiyo mwongozo madhubuti wa maisha yake ya baadaye.
Ajisimamie
Kuna imani kuwa mtoto wa kike hawezi kufanya kitu kikakamilika bila mkono wa mwanamume. Hili hutokea kutokana na kulegalega kwa kazi ya baba katika kutoa mwongozo wa malezi mema kwa mwanawe. Baba ni mtu nambari moja, anayejua jinsi ya kuilinda familia yake katika njia sahihi. Sasa kwa kuwa kila mtu anatakiwa kujua kujisimamia mwenyewe, baba ana nafasi kubwa ya kumfundisha binti yake jinsi ya kujilinda na kujisimamia.
Maisha yamejaa migogoro na mara nyingi unyonge wa wanawake huwasababishia kuoenewa na kunyimwa haki zao. Hivyo, baba akifanya vizuri kazi yake katika hili ni wazi kuwa hali hii itatoweka.
Awe anaridhika
Hili pia ni muhimu. Binti yako anatakiwa kuelewa kuwa jasho lake lina thamani kubwa katika maisha yake. Anatakiwa kujifunza pia kuwa utegemezi hauna nafasi katika maisha yake. Baba siku zote ni msaada wa familia, lakini kama mwanamke hatakiwi kumchukulia kama mashine ya kutolea pesa.
Unatakiwa kufundisha binti yako kujitegemea. Hatakiwi amtegemee. mwanaume kwa kila kitu.
Chanzo: Mwananchi