Kikwete unatuachaje baada ya utawala wako 2015

Kikwete unatuachaje baada ya utawala wako 2015

kensh

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2012
Posts
527
Reaction score
113
Uliingia kwa falsafa nzuri sana iliyotujaza matumaini. ARI Mpya,Nguvu Mpya na KASI Mpya. Ukanikosha sana pale ulipotuletea mabilioni ya KIKWETE. Ingawa sikujua yamefikia ofisi gani na nani ameyapeleka wapi na kufanya nini ! Ila niliamini ipo siku utatuma mabilioni mengine na yatanifikia.

Tukaamini kuwa mambo yatakua murua,swadaktaa au shwaaariii !

Taratibu tukaanza kuona kiza kinainyemelea falsafa yako.Yakaibuka mambo ya ajabu,RICHMOND,BUZWAGI,MEREMETA na funga mwaka 2014 ESCROW. Tukajua ungechukia na kuwatimua haraka waliopiga dili,ila ukaanza kuuzunguka na hata kujaribu kuukumbatia MBUYU !

Tulishuhudia watu wakianza kujadili na kujigamba kwa UDINI . Wengine wakawamwagia wenzao tindikali na hata kuwauwa kwa risasi na mabomu eti kwasababu sio watu wa DINI yao,hivyo hawafai kuishi !

Watu walienda katika nyumba za ibada wakiwa na hofu kubwa, nyumba za ibada zilichomwa na hakuna aliyekamatwa!?

Sasa kumezuka panya road,mbwa mwitu na wametunyima raha na wakataka hata kuyumbisha jeshi la polisi.Polisi walijikanganya kwa kauli zao walipojaribu kujibu kama kweli kuna panyaroad au la !

Mbaya zaidi, unakaribia kuondoka ofisini ukiwa unaacha tatizo la Polisi kuvamiwa na kuuwawa na hata kunyang'anywa silaha.Hatujui silaha hizo zipo kwa nani,zinafanya nini na kwanini?

Hayo yoote tisa,kumi ni hili sakata la UGAIDI. Vyombo vya usalama vinasema kuwa wale waliolianzisha timbwili kule tanga eti ni wahuni na si magaidi! wanamliwaza nani ? au wanakuliwaza JK ?

Hivi wahuni wanaweza kumuua mwanajeshi na wasikamatwe?! Hivi inawezekana muhuni akafungwa pingu na kumtoroka askari mwenye mafunzo thabiti? Kuna ubaya gani UKWELI ukisemwa ili watu wamtafute nyoka aliyemo chumbani mwao badala ya kutoa lugha zinazofanya tatizo lionekane ni dogo?

Kuna nchi zilipuuza matukio kama haya,zikasema kama sisi tunavyosema leo.Zikadai ni wahuni tu. Leo kule Nigeria kundi lililoonekana ni la kihuni miaka ya 2000,limegeuka kuwa BOKOHARAMU na sasa ni shiidah !

JK usipuuze mambo haya, vinginevyo utatuacha na vitu kama ISIS, BOKOHARAMU,AL SHA BAAB nk

Fanya hima utuache shwari kama ulivyotukuta,hatutaki UDINI ambao umekua ndiyo sababu ambayo vikundi vya MAGAIDI vinaitumia kuanzisha na kuhamasisha vurugu.

JK UNATUACHAJE ?
 
all things are planned, just to implement & to fullfil their hiden agenda.

4ever u won't know whatever the case, but u sh'd go ahead to speculate unspeculative issues. May be one day u'll be disclosed.
 
Hata kama tusingekuwa na rais na kubaki hivyohivyo, Tanzania tungekuwa mbali sana
 
unawaaamini MAGAMBA!! hakuna jipya!!! alivyoingia ndivyo alivyotuacha.
 
Ni ujinga na upuuzi mkubwa kudhani kuwa ugaidi utaondolewa na JK pekee.
 
Hata kama tusingekuwa na rais na kubaki hivyohivyo, Tanzania tungekuwa mbali sana
Huko mbali sana ni wapi ilhali kutwa unashinda kwenye keyboard huku ukinywa gongo na viroba?
 
Tatizo kubwa la Rais wetu amezungukwa na wasaka matonge, yaani yeye mwenyewe hana hamu kabisa anaomba hata leo aondoke magogoni.
 
Kiongozi wetu amezidiwa na mambo mazito,pengine hakuyategemea kama yangemkuta,na sasa ni kama hana mbinu za kuyakabili ila kuyaacha yajimalize yenyewe
 
Tumekuwa bila uongozi kwa miaka 10. We are on the way to remove this.
 
Napenda kuchukua fursa hii adimu kumuuaga rais wangu kipenzi Kikwete ambaye ifikapo october mda wake kuongoza kikatiba utakua ukingoni.

Tutakukumbuka kwa mema mengi na pia tutakukumbuka kwa changamoto ulizozipata katika utawala wako,hakika changamoto zilikua ni nyingi kwa kuzitaja chache rushwa,migomo,ajali na mengi,na mimi nitumie usemi maarufu kuwa SISI WATANZANIA UNATUACHAJE?

Wapo wachache walio nufaika na utawala wako lkn je umma wa watz tukukumbuke kwa lipi?

Mwisho nikutakie maisha mema baada ya kustaafu,nina imani historia itakuhukumu.

Nawasilisha
 
Hivi wewe ndorobo unajua tofauti ya changamoto na matatizo? Unaanzaje kuita matatizo changamoto au ndio lugha ya kufarijiana after failure
 
Sasa hakuna ubishi tena kwamba rais wetu ataondoka madarakani mwishoni mwa mwaka huu, licha ya tetesi kwamba angejiongezea muda ili akamilishe mchakato wa katiba mpya aliouanzisha, tumeshindwa kujua ni kwa nini rais wetu alishindwa kusimama wima haswa mwishoni mwishoni kama alivyokua ameanza mwanzo kwa uteuzi makini wa wajumbe wa kukusanya maoni.Eneo hili la katiba mpya ndilo lilionekana kumpa alama nyingi mh kikwete kama angefaulu kuwapatia watanzania katiba mpya waliyokuwa wanaingoja kwa hamu kubwa, lkn kwa bahati mbaya au nzuri rais wetu alishindwa kusimamia mchakato huu vizuri licha matamko yake mazuri aliyokua ameyatoa tangu mwanzo, mf rais alituambia wana ccm tujiandae kisaikolojia juu ya jambo hili kwa sababu watanzania wanaweza kuamua tofauti, sasa wakati huu rais wangu anapokwenda kuhitimisha ngwe yake watanzania tutamkumbuka kwa lipi kubwa kama rais wa nchi.
 
-Kajenga Daraja la Kigamboni........
-Mabasi yaendayo kwa Kasi
-Na Kuwapasha wanafunzi wanaopata Mimba kwamba ni Kiherehere chao........ LOL
 
Deni la taifa kufikia trilioni 35...
Shs ya Tanzania kufikia US Dollar 2280...
Rais aliyepata kusafiri zaidi toka nchi ipate uhuru...
Tembo kupungua kwa zaidi ya nusu ya idadi yake...
 
Atakumbukwa kwa kung'oa watu kucha kwa praise bila ganzi pamoja na meno,pia kutoboa watu macho!
 
Atakumbukwa kwa kuzurura karibu dunia nzima.

Atakumbukwa kwa kupenda kucheka cheka hata kwenye mambo yasiyochekesha.

Atakumbukwa kwa kusema hajui kwa nini Tanzania ni maskini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom