Kikwete sio wewe uliowaleta real madrid

Kikwete sio wewe uliowaleta real madrid

Jaslaws

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2011
Posts
6,016
Reaction score
5,301
Wakuu nadhani nyote mnakumbuka kua kwenye kampeni za uraisi Kikwete aliahidi kuwaleta real madrid, ni kweli veteran wa real madrid wamekuja, ila kinachonishangaza ni rais Kikwete kujivisha hizi sifa kua yeye ndo kawaleta, huu ni uongo wa mchana, real madrid wameletwa na mwarabu mwenye supermarket za tsn na wazo lilikuja baada ya jamaa kukutana na Luis Figo Dubai wala wazo halikutokana na ahadi za raisi.

Ombi: Kikwete na vyombo vya habari acheni kupotosha watu.
 
Ngoja mazuzu waje hapa kukupinga! Wenzetu huwa wana-promote utalii kwa kutumia timu halisi wakati wa pre-season, ila sisi tunafanyiwa uzuzu usio na maelezo! Kikwete, you are the worst that could ever happen to our beloved country.
 
Mleta mada nae aachekupotosha.hyo tajiri wake wa kuuza pipi hawezi kuleta r.madrid.mkono wa mkulo ni mkubwa hapa.
 
kikwete ana jezi yake kapewa huko barnebeu kwikwikwi....
 
hapa tbc1 naona kina maginga full kumpamba mr dhaifu.
 
Alafu hii Nchi acha Kabisa...., hata kama angekuwa yeye ndio amewaomba waje.., swali la kujiuliza hizo gharama atakuwa amezitoa mfukoni mwake ? Nadhani hio ya mfanyabiashara ina-make sense kidogo sababu kama atatumia akili na kuongea na TFF kuhusu mapato na kupata wadhamini wa maana basi anaweza akapunguza gharama alizotumia..

Alafu lazima tutambue kwamba hawa sio Real Madrid.., wengine hata hawakumaliza kucheza mpira wao hapo Real Madrid.., Mimi ningekuwa Nina Stake Real Madrid ningewashitaki hawa watu kwa kuchafua jina letu..., Hii iitwe wale waliowahi kuchezea Real Madrid
 
Mh Kikwete ndiyo mkuu wa kaya hivi kwenu hakuna baba jamani,huo ni utaratibu,unafikiri angegoma mkuu wa kaya wangekuja hpa.
 
Mleta mada nae aachekupotosha.hyo tajiri wake wa kuuza pipi hawezi kuleta r.madrid.mkono wa mkulo ni mkubwa hapa.
Sijapotosha mkuu kilicho mfanya kikwete kua involved ni clouds fm,baada ya huyo mwarabu kuona ishu inaitaji promo kubwa hivyo alikubaliana na ruge mtahaba wagawane costs na faida 50/50 sipotoshi...
 
chuki zikizidi sana huwa ujinga!!!

Sinachuki na kikwete hata kidogo,we ndo utaonekana mjinga kukataa mambo usiyojua,nenda tff ama mtafute mtu yoyote wa tff akuelezee ishu imeendaje.mi sio mjinga na wala sina chuki na raisi.
 
Mh Kikwete ndiyo mkuu wa kaya hivi kwenu hakuna baba jamani,huo ni utaratibu,unafikiri angegoma mkuu wa kaya wangekuja hpa.

Ndo unavyojindaganya?nchi ina sheria na taratibu zake na wala sio nchi ya ki dikiteta ..
 
Wakuu nadhani nyote mnakumbuka kua kwenye kampeni za uraisi kikwete aliahidi kuwaleta real madrid,ni kweli veteran wa real madrid wamekuja,ila kinachonishangaza ni rais kikwete kujivisha hizi sifa kua yeye ndo kawaleta,huu ni uongo wa mchana,realmadrid wameletwa na mwarabu mwenye supermarket za tsn na wazo lilikuja baada ya jamaa kukutana na luis figo dubai wala wazo halikutokana na ahadi za raisi,
Ombi..kikwete na vyombo vya habari acheni kupotosha watu.

Huyo tajiri wa ma-supermarket wala si mwarabu,ni mswahili wa Tanga
 
Back
Top Bottom