Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Inawezekana halijui hilo. Na kama analijua basi ni genious. Ametumwa kuleta mabadiliko katika taifa hili. Kupitia yeye tutaona mengi yakifumka na mengi yakikaa sawa baadae japo 'wino' wa kutosha waweza patikana.
Bagenda nae hakukosea pale alipoandika kuwa Jakaya ni tumaini lililorejea. Matumaini yana namna nyingi ya kuwafikia walengwa. Hata Yona alitaka kumkimbia Mungu alipopewa kazi ya kwenda Ninawi lakini alifika huko via the hard way-alikaa tumboni mwa samaki kwa siku 3!
Ukimya wa Jakaya ni dalili tosha kuwa nguvu ya umma imeachiwa kufanya kazi. Mtauliza iweje achakachue matokeo ya urais ili aendelee kuwepo madarakani. Wakati fulani hata Yesu aliwahi kusema kabla ya mateso kuwa. 'Baba ikiwezekana kikombe hiki nikiepuke, ila si kwa mapenzi yangu bali yako'. Mungu ili lengo lake litimie ilimbidi mapenzi yake yatimie.
Mifano hii inafanana ila inapishana. Yesu alitaka kuyaepuka mateso lakini Jakaya hakutaka kuiachia ikulu, japo wakati unakuja atafanya hivyo. Ni lazima kupitia yeye nchi hii itakaa sawa. Patakuwa na rabsha hapa kati lakini mwisho wa siku mambo yatakaa sawa. Ndio maana tukapewa mfano wa punje ya ngano, kwamba ili ngano izae ni lazima ioze kwanza. Hata Ngugi wa Thiong'o aliwahi kuandika kuhusu A Grain of Wheat. Lakini si ngano pekee huoza ili ipate kuzaa. Ngano ni mfano wa msingi. Nafaka aina zote pamoja na mbegu huoza kwanza ndipo zikazaa zaidi.
Kwa hiyo wana wa nchi tujue kabisa kwamba jakaya ni Tumaini lililorejea, japo si lazima iwe kufumba na kufumbua ndipo tuyaone maisha bora kwa kila mtanzania. Mungu alipowatoa wana wa Israel toka utumwani Misri aliwapitisha katika jangwa penye kila aina ya shuruba na mahangaiko kwa muda wa miaka arobaini! ili kufikia nchi ya asali na maziwa-naam, nchi ya ahadi. Mungu hakushindwa kuwapaisha mara moja ili kufika Kanani bali alitaka wana wa Israel wajue kuwa yeye ndiye ALIYE! Wajue kuwa maisha si lelemama bali ni tibwili zito. Ili mwisho wa siku watu wathamini maisha pamoja na kile walicho nacho. Wamthamini na yeye (Mungu) pia.
Hata dhahabu ili iweze kuitwa dhahabu safi ni lazima ipitie kwenye moto wa nyuzi elf kadhaa ili iwe dhahabu. Tusione vyaeelea bali vimeundwa. Ndivyo wasemavyo wahenga.
Kwa hiyo ndugu watanzania tukae tukijua kabisa kuwa masiha wetu-Jakaya yupo kazini kutimiza kile alichoitiwa kutimiza-Maisha bora kwa kila mtanzania. Na haya maisha bora hayataletwa na CCM bali CCM inatumika kama chombo tu cha mchakato kuelekea hayo maisha bora. Hata Musa aliambiwa na Mungu kuwa nchi ya ahadi ni ile paleeeee lakini hutaikanyaga!
Watanzania tujiendae kuifikia nchi ya ahadi. Nchi ya asali na maziwa
Bagenda nae hakukosea pale alipoandika kuwa Jakaya ni tumaini lililorejea. Matumaini yana namna nyingi ya kuwafikia walengwa. Hata Yona alitaka kumkimbia Mungu alipopewa kazi ya kwenda Ninawi lakini alifika huko via the hard way-alikaa tumboni mwa samaki kwa siku 3!
Ukimya wa Jakaya ni dalili tosha kuwa nguvu ya umma imeachiwa kufanya kazi. Mtauliza iweje achakachue matokeo ya urais ili aendelee kuwepo madarakani. Wakati fulani hata Yesu aliwahi kusema kabla ya mateso kuwa. 'Baba ikiwezekana kikombe hiki nikiepuke, ila si kwa mapenzi yangu bali yako'. Mungu ili lengo lake litimie ilimbidi mapenzi yake yatimie.
Mifano hii inafanana ila inapishana. Yesu alitaka kuyaepuka mateso lakini Jakaya hakutaka kuiachia ikulu, japo wakati unakuja atafanya hivyo. Ni lazima kupitia yeye nchi hii itakaa sawa. Patakuwa na rabsha hapa kati lakini mwisho wa siku mambo yatakaa sawa. Ndio maana tukapewa mfano wa punje ya ngano, kwamba ili ngano izae ni lazima ioze kwanza. Hata Ngugi wa Thiong'o aliwahi kuandika kuhusu A Grain of Wheat. Lakini si ngano pekee huoza ili ipate kuzaa. Ngano ni mfano wa msingi. Nafaka aina zote pamoja na mbegu huoza kwanza ndipo zikazaa zaidi.
Kwa hiyo wana wa nchi tujue kabisa kwamba jakaya ni Tumaini lililorejea, japo si lazima iwe kufumba na kufumbua ndipo tuyaone maisha bora kwa kila mtanzania. Mungu alipowatoa wana wa Israel toka utumwani Misri aliwapitisha katika jangwa penye kila aina ya shuruba na mahangaiko kwa muda wa miaka arobaini! ili kufikia nchi ya asali na maziwa-naam, nchi ya ahadi. Mungu hakushindwa kuwapaisha mara moja ili kufika Kanani bali alitaka wana wa Israel wajue kuwa yeye ndiye ALIYE! Wajue kuwa maisha si lelemama bali ni tibwili zito. Ili mwisho wa siku watu wathamini maisha pamoja na kile walicho nacho. Wamthamini na yeye (Mungu) pia.
Hata dhahabu ili iweze kuitwa dhahabu safi ni lazima ipitie kwenye moto wa nyuzi elf kadhaa ili iwe dhahabu. Tusione vyaeelea bali vimeundwa. Ndivyo wasemavyo wahenga.
Kwa hiyo ndugu watanzania tukae tukijua kabisa kuwa masiha wetu-Jakaya yupo kazini kutimiza kile alichoitiwa kutimiza-Maisha bora kwa kila mtanzania. Na haya maisha bora hayataletwa na CCM bali CCM inatumika kama chombo tu cha mchakato kuelekea hayo maisha bora. Hata Musa aliambiwa na Mungu kuwa nchi ya ahadi ni ile paleeeee lakini hutaikanyaga!
Watanzania tujiendae kuifikia nchi ya ahadi. Nchi ya asali na maziwa