Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kwa tabia yake ya kutostushwa na jambo lolote hata liwe baya kiasi gani, Kikwete ameonyesha ni bonge la Amiri Jeshi Mkuu. Kwa kutumia nguvu nyingi kuhalalisha mishahara "kiduchu" kwa wafanyakazi wa Tz amethibitisha kwamba yeye ni Chaguo la Mungu
Uwezo wake wa kuzima hoja ya Kadhi kwa kumtupia Lawama Augustine Mrema na Juma Ngasongwa ameonyesha yeye ni mtu mwenye uwezo wa hali ya Juu wa mazingaombwe.
Kwa kusema kwake kwamba watoto wa tanzania wataanza kutumia Kompyuta kusomea wakati hata madawati na madarasa ya kutosha hakuna, amethibitisha yeye hawezekaniki.
Magari yake anayosafiria yanapozimika zimika na kutoka matairi yeye anaona ni mipango ya Mungu. Kwa KWELI Kikwete ni bonge la Rais ambaye hajapata kutokea Tanzania na hatapata kutokea katika nchi yetu!!
Uwezo wake wa kuzima hoja ya Kadhi kwa kumtupia Lawama Augustine Mrema na Juma Ngasongwa ameonyesha yeye ni mtu mwenye uwezo wa hali ya Juu wa mazingaombwe.
Kwa kusema kwake kwamba watoto wa tanzania wataanza kutumia Kompyuta kusomea wakati hata madawati na madarasa ya kutosha hakuna, amethibitisha yeye hawezekaniki.
Magari yake anayosafiria yanapozimika zimika na kutoka matairi yeye anaona ni mipango ya Mungu. Kwa KWELI Kikwete ni bonge la Rais ambaye hajapata kutokea Tanzania na hatapata kutokea katika nchi yetu!!