AMARIDONG
JF-Expert Member
- Jun 24, 2010
- 2,502
- 180
Kikwete kuvuliwa uenyekiti wa CCM
Wajumbe wakamiana NEC Aprili 9, Dodoma
na Mwandishi wetu
WAKATI mambo yakizidi kwenda mrama ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), mkakati unasukwa kutaka kumuengua Rais Jakaya Kikwete kwenye nafasi yake ya uenyekiti wa chama hicho taifa, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Mkakati huo unaoratibiwa na baadhi ya vigogo waandamizi wa CCM, unadaiwa kuwa na lengo la kutaka kukivua magamba chama hicho na uenyekiti wa Kikwete ni moja ya magamba yanayopaswa kuvuliwa.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa tayari baadhi ya makada wa chama hicho, wamesambaa mikoani kuwashawishi wajumbe wa Halmashauri Kuu wa CCM (NEC), kuunga mkono hoja hiyo itakapowasilishwa kwenye vikao vya juu vya chama kuanzia sasa na kukamilika mwakani kwenye mkutano mkuu wa chama.
Sababu kubwa inayotajwa na waumini wa mkakati huo ni kwamba kwa muundo wa sasa wa Rais kuwa na kofia mbili, umesababisha dhambi za chama kubebwa na serikali na zile za serikali kubebwa na chama.
Kwa mfano hivi sasa Rais Kikwete ndiye Rais na ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa, hivyo kama kuna jambo baya la serikali, linahusishwa na chama moja kwa moja na kama kuna jambo baya la chama linahusishwa na serikali.
Tumeshuhudia katika kipindi hiki kwamba ufisadi wa serikali umebebwa na chama na ule wa chama umebebwa na serikali. Dawa ya kuondoa hali hiyo ni kutenganisha kofia ya urais na uenyekiti, alisema kada mmoja wa CCM.
Kwa mujibu wa habari hizo, sababu nyingine inayosukuma hoja hiyo ni kwamba nafasi hizo haziko kikatiba bali zilitokana na utashi wa kisiasa wa Mwalimu Nyerere alipoishawishi CCM ikubali kuunganisha kofia hizo baada ya kubaini kuwa alikuwa akitofautiana kimawazo na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakati Mwalimu Nyerere akiwa Mwenyekiti wa chama.
Duru za kisiasa kutoka ndani ya CCM, zinasema ingawa muundo huo wa kutenganisha kofia uliasisiwa na Mwalimu Nyerere kwa nia njema, lakini vinara wa mkakati huo safari hii, wana nia mbaya na Rais Kikwete kwani anaweza kutimuliwa kwenye urais kama atashindwa kutekeleza Ilani ya CCM aliyoinadi mwaka 2010.
Unajua kuna watu wanaamini kabisa kuwa kama Rais Kikwete ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CCM hadi 2015, chama kitakuwa kwenye hali mbaya na CHADEMA wanaweza kuchukua nchi. Ili kukinusuru, lazima Kikwete abaki na urais na chama kiongozwe na mtu mwingine, kilisema chanzo chetu cha habari.
Athari nyingine inayotajwa na duru za siasa ni kwamba muundo huo utampunguzia nguvu Rais Kikwete kwani hatakuwa na sauti ndani ya vikao vya chama na anaweza kushughulikiwa kama mwanachama mwingine yeyote kama ataenda kinyume na Ilani ya CCM.
Hata wakati ule Nyerere alipotaka kofia hizi ziunganishwe, aliangalia mbele kwamba ikitokea chama kimepata mwenyekiti kichaa na ambaye haelewani na Rais, moto unaweza kuwaka na mfano mzuri ni Afrika Kusini ambako Thabo Mbeki alikuwa ni Rais na Mwenyekiti alikuwa Jacob Zuma. Kilichotokea, wote tunajua, alisema kada huyo ambaye pia ni mjumbe wa NEC.
Mbeki alilazimishwa kujiuzulu urais kabla ya muda wake baada ya Kamati Kuu ya chama cha ANC, kumtaka aachie ngazi kwa madai kuwa alimbambikizia kesi Mwenyekiti wa chama hicho Jacob Zuma ambaye ndiye Rais wa sasa nchini humo.
Mbeki ambaye alikuwa swahiba mkubwa wa Zuma kabla ya kuhitilafiana, alichaguliwa kuwa Rais wa Afrika Kusini mwaka 1999, akiwa Rais wa pili wa Afrika Kusini tangu utawala wa ubaguzi wa rangi ukomeshwe nchini humo. Alitarajiwa kumaliza muda wake wa urais mwaka 2009.
Mwalimu Nyerere ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wakati Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Ilipofika mwaka 1985, Mwalimu Nyerere alitaka kofia hizo ziunganishwe kwa hofu kwamba kunaweza kutokea mgongano wa uendeshaji wa chama na serikali.
Rais Benjamin Mkapa alipoingia madarakani mwaka 1995, alikabidhiwa uenyekiti na utaratibu huo uliendelea hadi sasa ambapo Rais wa CCM huwa pia Mwenyekiti wa chama hicho.
Wakati huohuo, kile kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), kilichokuwa kikisubiliwa kwa hamu na wajumbe wa chama hicho, kinatarajiwa kuitishwa Aprili 9 mjini Dodoma.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata, zilisema tayari wajumbe wamejulishwa na hivi karibuni vikao vya Sekretarieti na Kamati Kuu (CC), vitakutana kwa ajili ya kupanga ajenda.
Ingawa ajenda za NEC hazijajulikana, baadhi ya wajumbe waliliambia gazeti hili kwamba NEC hii itawaka moto kwani kuna mambo mengi yamejitokeza na hakukuwa na kikao tangu kumalizika kwa kikao cha uteuzi Agosti mwaka jana. Baadhi ya mambo yanayotarajiwa kuibuka ni pamoja na makovu ya uchaguzi kuanzia ngazi ya uteuzi, malumbano yanayoendelea ya wenyewe kwa wenyewe na tathmini ya hali ya kisiasa na sababu za kushindwa kwenye baadhi ya majimbo ya uchaguzi waliyotarajia kushinda.
Wajumbe wakamiana NEC Aprili 9, Dodoma
na Mwandishi wetu
WAKATI mambo yakizidi kwenda mrama ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), mkakati unasukwa kutaka kumuengua Rais Jakaya Kikwete kwenye nafasi yake ya uenyekiti wa chama hicho taifa, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Mkakati huo unaoratibiwa na baadhi ya vigogo waandamizi wa CCM, unadaiwa kuwa na lengo la kutaka kukivua magamba chama hicho na uenyekiti wa Kikwete ni moja ya magamba yanayopaswa kuvuliwa.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa tayari baadhi ya makada wa chama hicho, wamesambaa mikoani kuwashawishi wajumbe wa Halmashauri Kuu wa CCM (NEC), kuunga mkono hoja hiyo itakapowasilishwa kwenye vikao vya juu vya chama kuanzia sasa na kukamilika mwakani kwenye mkutano mkuu wa chama.
Sababu kubwa inayotajwa na waumini wa mkakati huo ni kwamba kwa muundo wa sasa wa Rais kuwa na kofia mbili, umesababisha dhambi za chama kubebwa na serikali na zile za serikali kubebwa na chama.
Kwa mfano hivi sasa Rais Kikwete ndiye Rais na ndiye Mwenyekiti wa CCM Taifa, hivyo kama kuna jambo baya la serikali, linahusishwa na chama moja kwa moja na kama kuna jambo baya la chama linahusishwa na serikali.
Tumeshuhudia katika kipindi hiki kwamba ufisadi wa serikali umebebwa na chama na ule wa chama umebebwa na serikali. Dawa ya kuondoa hali hiyo ni kutenganisha kofia ya urais na uenyekiti, alisema kada mmoja wa CCM.
Kwa mujibu wa habari hizo, sababu nyingine inayosukuma hoja hiyo ni kwamba nafasi hizo haziko kikatiba bali zilitokana na utashi wa kisiasa wa Mwalimu Nyerere alipoishawishi CCM ikubali kuunganisha kofia hizo baada ya kubaini kuwa alikuwa akitofautiana kimawazo na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakati Mwalimu Nyerere akiwa Mwenyekiti wa chama.
Duru za kisiasa kutoka ndani ya CCM, zinasema ingawa muundo huo wa kutenganisha kofia uliasisiwa na Mwalimu Nyerere kwa nia njema, lakini vinara wa mkakati huo safari hii, wana nia mbaya na Rais Kikwete kwani anaweza kutimuliwa kwenye urais kama atashindwa kutekeleza Ilani ya CCM aliyoinadi mwaka 2010.
Unajua kuna watu wanaamini kabisa kuwa kama Rais Kikwete ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CCM hadi 2015, chama kitakuwa kwenye hali mbaya na CHADEMA wanaweza kuchukua nchi. Ili kukinusuru, lazima Kikwete abaki na urais na chama kiongozwe na mtu mwingine, kilisema chanzo chetu cha habari.
Athari nyingine inayotajwa na duru za siasa ni kwamba muundo huo utampunguzia nguvu Rais Kikwete kwani hatakuwa na sauti ndani ya vikao vya chama na anaweza kushughulikiwa kama mwanachama mwingine yeyote kama ataenda kinyume na Ilani ya CCM.
Hata wakati ule Nyerere alipotaka kofia hizi ziunganishwe, aliangalia mbele kwamba ikitokea chama kimepata mwenyekiti kichaa na ambaye haelewani na Rais, moto unaweza kuwaka na mfano mzuri ni Afrika Kusini ambako Thabo Mbeki alikuwa ni Rais na Mwenyekiti alikuwa Jacob Zuma. Kilichotokea, wote tunajua, alisema kada huyo ambaye pia ni mjumbe wa NEC.
Mbeki alilazimishwa kujiuzulu urais kabla ya muda wake baada ya Kamati Kuu ya chama cha ANC, kumtaka aachie ngazi kwa madai kuwa alimbambikizia kesi Mwenyekiti wa chama hicho Jacob Zuma ambaye ndiye Rais wa sasa nchini humo.
Mbeki ambaye alikuwa swahiba mkubwa wa Zuma kabla ya kuhitilafiana, alichaguliwa kuwa Rais wa Afrika Kusini mwaka 1999, akiwa Rais wa pili wa Afrika Kusini tangu utawala wa ubaguzi wa rangi ukomeshwe nchini humo. Alitarajiwa kumaliza muda wake wa urais mwaka 2009.
Mwalimu Nyerere ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wakati Ali Hassan Mwinyi akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Ilipofika mwaka 1985, Mwalimu Nyerere alitaka kofia hizo ziunganishwe kwa hofu kwamba kunaweza kutokea mgongano wa uendeshaji wa chama na serikali.
Rais Benjamin Mkapa alipoingia madarakani mwaka 1995, alikabidhiwa uenyekiti na utaratibu huo uliendelea hadi sasa ambapo Rais wa CCM huwa pia Mwenyekiti wa chama hicho.
Wakati huohuo, kile kikao cha Halmashauri Kuu (NEC), kilichokuwa kikisubiliwa kwa hamu na wajumbe wa chama hicho, kinatarajiwa kuitishwa Aprili 9 mjini Dodoma.
Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata, zilisema tayari wajumbe wamejulishwa na hivi karibuni vikao vya Sekretarieti na Kamati Kuu (CC), vitakutana kwa ajili ya kupanga ajenda.
Ingawa ajenda za NEC hazijajulikana, baadhi ya wajumbe waliliambia gazeti hili kwamba NEC hii itawaka moto kwani kuna mambo mengi yamejitokeza na hakukuwa na kikao tangu kumalizika kwa kikao cha uteuzi Agosti mwaka jana. Baadhi ya mambo yanayotarajiwa kuibuka ni pamoja na makovu ya uchaguzi kuanzia ngazi ya uteuzi, malumbano yanayoendelea ya wenyewe kwa wenyewe na tathmini ya hali ya kisiasa na sababu za kushindwa kwenye baadhi ya majimbo ya uchaguzi waliyotarajia kushinda.