Kikwete azidiwa jukwaani, akimbizwa mapumziko

kwakweli he needs to rest, akae ikulu apumzike afanye kazi from there, hizi shughuli zingine atume wawakilishi. Tena na campaign inakuja around the corner he really needs to pace himself.
 
Kwenye gazeti la raia mwema la wiki hii nimependa sana kisehemu hiki cha makala kuhusu "ugumu wa kumshauri Kikwete". Mwenye akili na aelewe
Baada ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kustaafu urais na kubakia kuwa mwenyekiti wa chama, nilipata bahati ya kutumwa naye na wenzangu wawili, kwenda kumjulia hali rafiki yake mmoja aliyekuwa anaumwa, lakini wakati huo akiendelea kuongoza chombo muhimu cha dola katika taifa moja la Afrika.

Tulipofika, tulikuta ugomvi ambao hata mkuu wa nchi ile alikuwa amejaribu kusuluhisha bila mafanikio.

Ugomvi ulihusu nafasi ya waganga wa kienyeji katika kumshauri mkubwa yule juu ya afya yake. Mara mbili alipelekwa hospitalini Ulaya na Marekani, na
madaktari walishauri afanyiwe upasuaji lakini kila alipoandaliwa kwa ajili hiyo, alibadili mawazo dakika za mwisho na madaktari waliheshimu uamuzi wake.

Kisa cha kubadili kilikuwa ni ushauri wa waganga wa kienyeji kuwa wazungu wanataka kumuua kupitia upasuaji huo. Mkubwa yule aliendelea kudhoofu kwa kuchelewa kufanyiwa upasuaji kwa sababu tu waganga wa kienyeji wametoa ushauri na ukaheshimika.

Hatimaye waganga hao walihamia nyumbani kwa mkubwa yule, wakapewa gari lao maalumu katika misafara ya mkubwa yule. Washauri na wasaidizi wakapuuzwa na hata ushauri wa marafiki kama Mwalimu Nyerere haukufua dafu.

Nalisema hili kusisitiza jambo moja muhimu kuwa, viongozi wengi wa Kiafrika wanajiweka katika mazingira%
 
kwakweli he needs to rest, akae ikulu apumzike afanye kazi from there, hizi shughuli zingine atume wawakilishi. Tena na campaign inakuja around the corner he really needs to pace himself.

Hawezi kupumzika kwa kuwa 2005 maswahiba wake (EL na RA) walifanya kazi ya kuratibu kampeni. Sasa hivi wako pembeni na hajui wanafikiria nini, wanaweza kuwa wanapanga namna ya kuhujumu kampeni za JK. Kuanzia sasa na kuendelea JK ataanza kuchanja mbuga mikoani ili kuweka mazingira ya uchaguzi wa 2010.

Mwaka 2005 wanamtandao walikuwa wamesambaa nchi nzima, sasa hivi JK hajui amtumie nani na amwamini nani. Maana wenye mtandao ndo wamekuwa "adui" zake, na hawezi kuwatumia tena, labda aanzishe mtandao wake mpya ama awatumie CCM ambao nao wamejaa wana mtandao watupu.

Lowassa tayari ameishautangazia umma wa watanzania kwamba yeye ndiyo alikuwa Mwenyekiti wa Kampeni za JK mwaka 2005. In a way inaweza kuwa ni kumkumbusha JK kwamba asije akajisahau kwa kuwa hao mafisadi ndiyo waliomsaidia kufika hapo na may be wanaweza kufanya chochote kumvurugia kampeni zake.
 
Kikwete anaumwa, tena seriously.Watu hawataki kusema tu.

Hii incident wala ile ya 2005 si habari za uchovu wa safari
 
Kwani anaumwa nini mzee?

Si ngoma kama wengi wanavyoweza kufikiri, lakini hao watu wa Raia Mwema hapo juu wanajua, maana katika hadithi yao wamemwandika Kikwete ila kwa kificho, kwa sababu Kikwete ndiye anayekataa upasuaji na anayependa kuendekeza mambo ya waganga wa kienyeji.

Uzuri au ubaya ni kwamba wenye kuujua ugonjwa hawasemi, wenye kusema hawaujui.
 
JK kama sikosei anatafuta SYMPATH kutoka kwa wananchi haswaaaa wanawake... nakumbuka baada ya kuanguka pale Jangwani... Alijizolea kura nyingi kutoka KWAOOO!!!
 
Kuna habari kwamba rais ameonekana kuwa dhaifu na kushidwa kumalizia hotuba yake huko Mwanza ktk uzinduzi wa kanisa..au wapenda walikemea mapepo kwa rais nini?
 
Jamani kama mlivyosoma ukweli halisi ndio huu...wapendwa walikuwa wanakemea mapepo gafla mh RAIS akaanza kuweweseka na kushindwa kuendelea na hotuba....tunaitaji maombi kwa rahisi wetu...
 
Aisee hawakumwambia kwamba vi amulet vya Bwagamoyo havitakiwi wakati wapendwa wanakemea? Naona vilizidiwa megawatts.
 
Aisee hawakumwambia kwamba vi amulet vya Bwagamoyo havitakiwi wakati wapendwa wanakemea? Naona vilizidiwa megawatts.

inaonekana rahisi alikuwa anatumia ANALOG

wakati wapendwa walishaanza kutumia DIGITAL


Kazi kweli kweli;....hawa wapendwa wanaitajika sana;inabidi tujue maombi waliotumia ;unajua kuna mambo maombi mengine ukitaja majina husika wanakwenda na maji...mfano halisi majina ya majini yanayovunja ndoa...yaani haya ukiwasha moto kukemea kwa kuyataja na majina weeeeeeeeee akukaliki...sasa mhhh sijui

afadhali RAIS aliwahi kuchapa lapa
 
Akuna cha ugonjwa waulizeni waliokuwepo...wapendwa walikuwa wanakemea mapepo sasa hawakujua rais nae ndio anaanza kuhutubia...rais akiwa anaendelea jamaa huku wanaongeza moto..//loh!!!!!!rais akaona iswe tabu ikabidi kala chapa huyoo....sio wa kwanza ,rais kamuzu banda aliwahi kudondka pale chuo kikuu wakati vijana wako nje wanakemea na kusali....
 
Akuna cha ugonjwa waulizeni waliokuwepo...wapendwa walikuwa wanakemea mapepo sasa hawakujua rais nae ndio anaanza kuhutubia...rais akiwa anaendelea jamaa huku wanaongeza moto..//loh!!!!!!rais akaona iswe tabu ikabidi kala chapa huyoo....sio wa kwanza ,rais kamuzu banda aliwahi kudondka pale chuo kikuu wakati vijana wako nje wanakemea na kusali....

kwa hiyo ana mapepo?
 
Kikwete anaumwa, tena seriously.Watu hawataki kusema tu.

Hii incident wala ile ya 2005 si habari za uchovu wa safari

Ni kweli muungwana ni mgonjwa anasumbuliwa na ninadhani ni tatizo la NERVE katika sehemu za medula oblangata(nerve compression) kwa lugha ya kitaalam, na kwa taarifa nilizonazo baada ya kuanguka pale jangwani wakati anamalizia kampeni zake za Urais 2005 alipata kutibiwa na Daktari mmoja huko ufaransa na alishauri afanyiwe upasuaji lakini muungwana hakukubaliana na hilo. Baadae akapata Daktari mmarekani nadhani wa Boston ambaye anamtibu mara zote kwa kumpatia dawa, na huyu Daktari kamshauri aachane na kazi za siasa baada ya 2010 kwani ndizo zinampatia stress na tatizo alilonalo halihitaji stress, lakini madaraka matamu hataki kufuata masharti ya Dr.

Huyu Dr wa marekani ndo yule alimleta akampeleka mbuga za wanyama na baadae alitoa misaada pale MOI. Tatizo hili la kupoteza fahamu na ku collapse limekuwa likimtokea mara kwa mara hata akiwa IKULU tu, nakumbuka ile ziara ya mkoani Mbeya aliopopolewa mawe alipata kuanguka pia katika moja ya shughuli zake za ndani ikulu ndogo ya huko.

Mimi nawashauri wasaidizi wa Rais wawaambie watanzania ukweli, waache kutupamba kwa maneno kuwa anafanya kazi nyingi ndo maana ananguka, wawaeleze watanzania tatizo la msingi la afya ya Rais wao. Hizi safari za Marekani kila kukicha ni danganya toto, kinachompeleka huko ni matibabu tu.
 
!?

Akuna cha ugonjwa waulizeni waliokuwepo...wapendwa walikuwa wanakemea mapepo sasa hawakujua rais nae ndio anaanza kuhutubia...rais akiwa anaendelea jamaa huku wanaongeza moto..//loh!!!!!!rais akaona iswe tabu ikabidi kala chapa huyoo....sio wa kwanza ,rais kamuzu banda aliwahi kudondka pale chuo kikuu wakati vijana wako nje wanakemea na kusali....



Si ngoma kama wengi wanavyoweza kufikiri, lakini hao watu wa Raia Mwema hapo juu wanajua, maana katika hadithi yao wamemwandika Kikwete ila kwa kificho, kwa sababu Kikwete ndiye anayekataa upasuaji na anayependa kuendekeza mambo ya waganga wa kienyeji.

Uzuri au ubaya ni kwamba wenye kuujua ugonjwa hawasemi, wenye kusema hawaujui.




JK kama sikosei anatafuta SYMPATH kutoka kwa wananchi haswaaaa wanawake... nakumbuka baada ya kuanguka pale Jangwani... Alijizolea kura nyingi kutoka KWAOOO!!!
..................................
:confused:
 
Hapo tuko pamoja nilikuwa navuta pumzi sehemu ya kuanzia...mhhhhh kazi kweli kweli....hii itakuwa fundisho kwa wale viongozi wa siasa wanaotumia uchawi kuingia madarakani na wanaokimbilia kujishebedua ....wanamaombi msiache kupiga sala lazima mapepo yakimbizwe hata wkija na usalama wa taifa ....
 
kasharudi dar..

True... Ameonekana mida ya saa tatu usiku msafara wake unatokea Bagamoyo kurudi mjini....

...ukweli ni kuwa afya mgogoro...kwa hiyo ni lazima awasikilize madaktari wake ..kama kweli ana nia ya dhati ya kuwatumikia watanzania vipindi viwili....ana tatizo la ku collapse linalojirudia....

...katika hali ya kawaida na umri alionao wa wastani anao uwezo wa kuhimili mikiki mikiki ya sasa... kama si vinginevyo.... kama ni kuzimia angekuwa anazimia Nyerere kila siku kwani alikuwa na ratiba ngumu kuliko ya muungwana ukizingatia miundombinu ya wakati ule na comfrortability level ya magari waliyokuwa wakitumia the best for off-road was landrover 109....au foker kama ni ndege ...you how noise it is, na hata safari za nje enzi zile zilichukua muda zaidi.....sembuse sasa ambapo ukisafiri business VIP class ....ni almost unasafiri kwenye kitanda...kinachokunjika kuwa kiti....level ya fatigue imepungua sana!!!
 
Back
Top Bottom