Kikwete asimulia alivyoiba wali JKT!

Kikwete asimulia alivyoiba wali JKT!

Niliwahi fundishwa na wazazi wangu nikiwa mdogo;

"Ukiwa mwaminifu kwa madogo utakuwa mwaminifu kwa makubwa pia"

Mi naona Mh. rais anajisahau sana wakati mwingine, huwezi kuonge vitu kama hivi kwenye hadhara. Halafu kweli anakinyongo na mwalimu yaani hataki hata kumpa 'credit' yoyote kwenye kuanzisha JKT wala jinsi alivyotaifisha shule ili wote wasome.
 
Tunasubiri simulizi yake jinsi alivyoiba uchaguzi wa kumpata mgombea wa CCM 2005 na alivyoiba uchaguzi 2010.
 
Inaonesha jinsi alivyo kamanda wa siasa,maana wale makamanda wdenzake huwa wanenda kuzamia jikoni na kuiba bila kuonekana wala kusikika...yeye kshikwa ni ishara tosha kila assigment zake huwa hazifanyi kwa uwezo wake woote!si ajabu hata nchi imemshinda ilhali anauzoefu tosha kabisa wa kuendesha serikali na kujua mfumo woote wa uendeshaji...bla bla tu!!
 
Jeshini wizi sio kosa ni sehemu ya mafunzo(mbinu za medani) mfano huna bunduki na unamuona adui yako ana bunduki wazo lako kubwa ni ama umyang'anye kwa nguvu ikiwezekana umvunje shingo na kumuulia mbali au uibe bunduki kwa manufaa ya makamanda wenzio. Au mpo frontline na chakula kimewaishia lakin jirani kuna raia wana chakula so kupona kwenu mtakwenda kusweep chakula kwa faida ya makamanda,
Somo la pili ni UONGO. ukitekwa kama ulizoea kusema ukweli utataja uwezo wa kikosi chenu mpo wangapi aina ya silaha mlizo nazo. Tatu Ukatili n sehemu ya mafunzo ndio maana soja anaua ananyonga bila huruma. HILO NDILO GESHI.
safi kikwete kunikumbusha nilivyokwiba sukari jikoni

Kwa hali hiyo siyo sehemu nzuri vijana wetu kupita kule. Mkiangalia vizuri hawa wezi kwenye system wamepitia kule ndo maaana wanaiba kwa ujasiri mkub wa mno, kumbe JKT

Ahsante JK T kwa kutuonesha uliko pata ujasiri wa unyang'anyi
 
safi sana, imefikia wakati kwa vijana wote sasa kujiunga na jeshi letu la kujenga taifa ili kupata msasa wa uzalendo, usharo na umagharibi umezidi
 
kuiba ubwabwa jkt lazima ujue mbinu za medani na kuruta aliyeiva hawezi kukamatwa.
 
“Akaniambia piga magoti, huku nimeshikilia mestini zangu za wali. Akaniambia hivi! Brother maana alikuwa anapenda sana kuita brother , wewe ni form six (kidato cha sita) umekuja kuchukua mafunzo.

Kwa wazoefu wa jeshi tunafahamu lugha inayotumika ni 'afande'; 'kuruta' ama 'service man/woman'; hiyo ya 'brother' ni dhahiri kuwa amechapia na story yenyewe haina tofauti na mipasho aliyoizoea siku zote.
 
Kumbe udokozi hukuanza ulipopewa urais ni toka ukiwa jeshini, ila naona sasa hivi umezidisha tena unajificha nyuma ya riz moko, acha tabia hiyo brother km wahenga wanavyosema "za mwizi ni..."
 
Hebu wana Jf tuache unafiki!
Nani miongoni mwetu hakupitia hayo utotoni?
 
Kumbe wizi kaanza zamani... Ndiyo maana wezi wa EPA waliorudisha hela ni siri yake hadi leo
 
Huyu jamaa anapenda sana huruma,baada ya kuja kupelekwa hague atasimulia jinsi alivowaibia na kuwaua watanzania
 
Hivi baada ya kukamatwa na kupiga magoti,alivyoachiwa aliachwa aende na ubwabwa wake au aliurudisha?
Ubwabwa aliondoka nao na ndio maana hiyo spirit aliifanya alipokamata watu wa EPA
 
Back
Top Bottom