Kikwete ana siri ya makontena

Kikwete ana siri ya makontena

Waziri mkuu kumwita na kumhoji Riz1 hii sijaipenda. Hatuna vyombo vya kuchukua hatua au ni 'kupanga dili'?

Hekima saa nyingine hutakikana hata kuliko kufuata sharia, hasa ka 'vijiinji' vyetu hivi
 
Lowassa akigombea urais Hata kuku,nitampa kuku kura yangu,Hata akidhikiri utchi usiku kucha urais hatoupata
Nalog off
 
Haditihi hii inanipa imani kuwa kuja kwa Maghufuli ni matakwa ya Mola (aliyesikia shida za Watanzania). Kwa sababu aliwezaje kupita kwenye tundu ya wizi, ukorofi na kutojali huku kwa JK? Ni kama ile hadithi ya Farao aliyemlea Nabii Musa nyumbani kwake!
 
Suala sio kujiuzuru ninachotaka uelewe ni kwa nini huyu Mwakyembe alikaa na amekaa kimya hadi sasa juu ya kashfa hii ya makontena huku yamepotea yeye akiwa Waziri? Na tumemshuhudia akitokwa na povu juu ya RICHMOND na kujidai yeye aogopi chochote kwani kama kufa aliisha kufa.

Tatizo uelewa wako ni mdogo sana nahisi hata darasani mwalimu wako alikua na kazi sana,tatizo lako unaacha hoja ya msingi unakimbilia richmond,umeshaambiwa mwakyembe alishatoa taarifa kuhusu upotevu huu wa makontena na taarifa akampelekea bosi wake ambae ni raisi,sasa baada ya hapo ulitakaje ?ulitaka mwakyembe amshinikize raisi kuchukua hatua,na isitoshe baada ya taarifa yake alimishwa wizara sasa ulitaka mwakyembe aitishe waandishi wa habari aseme yale aliyo mwandikia raisi.kama hamjui namn serikali inavyo fanya kazi bora mkae kimya sio lazima kuchangia,uwezo wako mdogo wa kufikiri lakini kimbelembele kingi
 
Hapa ukileta hoja ya kuondoa kinga ya raisi hata wachangiaji hupati ila kwenye kulalama tu hatujambo.

Waheshimiwa nyie ibeni tu nchi ya wajinga hii.
 
Hapa ukileta hoja ya kuondoa kinga ya raisi hata wachangiaji hupati ila kwenye kulalama tu hatujambo.

Waheshimiwa nyie ibeni tu nchi ya wajinga hii.

Kweli mkuu kama mtindo wa kupitisha hoja bungeni utakuwa ni ule ule wa "wanaoafiki waseme ndiyo....ndiyoooooo!!!! na wasioafiki waseme siyooooo" hakuna kitu hapo.

Kuna haja ya kuondoa kinga ya rais baada ya muda wake kwisha!!!!!
 
Rais mstaafu Jakaya Kikwete imeelezwa kuwa anafahamu kilichokuwa kinaendelea katika suala la makontena bandarini na taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha alipewa taarifa na akazikalia kimya.

Imejulikana kwamba aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe alibaini upotevu wa makontena hayo, akaandika taarifa ya kina kwenda Ikulu lakini kilichomkuta hatakisahau maishani..!!.

Ripoti hiyo ilimkaanga mwenyewe Mwakyembe kwani baada tu ya JK kuipitia, akamwondoa Wizara ya Uchukuzi na kumpeleka Wizara ya Afrika Mashariki.

Taarifa za kina zinasema kuwa Rais Magufuli kabla ya kumteua Mwakyembe kwenye Wizara ya Sheria na Katiba aliyo sasa, alimwita na kumhoji kuhusu upotevu wa makontena hayo na hiyo ndio ikawa nafasi ya Mwakyembe kutoa fundo alilokuwa nalo moyoni.

Pia Mwakyembe alikutana na Waziri Mkuu Majaliwa kuhusiana na upotevu huo.

Pia Ridhiwani Kikwete anatajwa katika sakata hili na inasemekana ameshaitwa kuhojiwa na Waziri Mkuu.

Source:Gazeti la Jamhuri la leo 22/12/2015, Toleo no 221.

Hivi usipompenda kiongozi wako mstaafu kwa baadhi ya matendo yake akiwa ofisini ni dhambi? Kama ndiyo Mungu anisamehe
 
Kweli mkuu kama mtindo wa kupitisha hoja bungeni utakuwa ni ule ule wa "wanaoafiki waseme ndiyo....ndiyoooooo!!!! na wasioafiki waseme siyooooo" hakuna kitu hapo.

Kuna haja ya kuondoa kinga ya rais baada ya muda wake kwisha!!!!!
Lete tu hiyo hoja hapa uone kama utapata wachangaji wa kuboresha wazo lako au wa kuukuunga mkono.
 
Kibogo tunatakiwa kutafakari kwa kina kabla ya kuhukumu watu. Mimi nadhani ni vizuri tuwe na maswali ya kujiuliza. Hivi Waziri ameandika report na kuipeleka ngazi husika halafu kabla ya kujua nini hatima ya report yake raisi anamhamishia wizara nyingine je, hapo alitakiwa kujiuzulu kwa kuhamishwa wizara au kwa report yake? je unapokuwa waziri ukatoa report unatoa deadline kwa rais atoe majibu? Aliyemrithi Mwakyembe alitakiwa kujiuzulu na sio yeye ambaye hakuwa na mandate tena na ile wizara. Ingekuwa aliona uozo huo halafu akaufumbia macho mm nisingetoa haya maneno, lakini alipoona matatizo alitoa taarifa ya kina ( accoding to mtoa taarifa) na kumpatia mkuu wake wa kazi ili ashughulikie na wala hakuna sehemu ilipogundulika kuwa yeye ni mhusika katika sakata hilo, infact he is clean. Baadaye akapewa kazi nyingine EAC, hivi kwa kujiuzulu baada ya kuhamishiwa huko asingeonekana mwehu? hivi watanzania wangemuuliza angejibu anajiuzulu kwasababu zipi wakati kwenye wizara aliyopo hakuna tatizo? Je tusingeona kwamba yeye alikuwa na ulaji amekatiwa kule wizara ya uchukuzi? Hiyo ni tafakuri yangu ambayo watanzania wenzangu ningeomba nao wajaribu kuiangalia kwa pande zote. Tusifanye visa bali tujadiri kwa mapenzi ya nchi yetu. Itakuwa ni vibaya sana tukajadiri mada hii tukiwa na makovu ya Richmond kwenye bongo zetu.

Mungu ibariki Tanzania

Laiti waTZ wangefahamu uzalendo wa Mwakyembe kwa nchi hii, wangetamani siku moja awe Rais! Mwakembe ana usongo wa kutisha juu ya wezi wa nchi hii
 
Hata zile kesi za wahusika bandarini kuna mahali zitakosa nguvu kwani itakuja kugundulika kuwa ilikuwa ni AMRI (vimemo) kutoka mamlaka ya juu ambayo hayashikiki.. Huwezi kumwadhibu MTU aliyetekeleza amri ya rais hata kama ya kuua
Hupitwi hahaha
 
Utawala uliopita ulikuwa uozo sana na iliharibu sana nchi yetu! uraisi haukuwa taasisi bali wa KIFAMILIA kwani wote walikuwa na madaraka ya kuamua kama RAISI.

Kukosa ajira za maana ni sheedah sana, watu mnashinda jf kupiga umbea, maisha yanawagonga mnasingizia JK na familia yake, mtasubiri sana!
 
Rais mstaafu Jakaya Kikwete imeelezwa kuwa anafahamu kilichokuwa kinaendelea katika suala la makontena bandarini na taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha alipewa taarifa na akazikalia kimya.

Imejulikana kwamba aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe alibaini upotevu wa makontena hayo, akaandika taarifa ya kina kwenda Ikulu lakini kilichomkuta hatakisahau maishani..!!.

Ripoti hiyo ilimkaanga mwenyewe Mwakyembe kwani baada tu ya JK kuipitia, akamwondoa Wizara ya Uchukuzi na kumpeleka Wizara ya Afrika Mashariki.

Taarifa za kina zinasema kuwa Rais Magufuli kabla ya kumteua Mwakyembe kwenye Wizara ya Sheria na Katiba aliyo sasa, alimwita na kumhoji kuhusu upotevu wa makontena hayo na hiyo ndio ikawa nafasi ya Mwakyembe kutoa fundo alilokuwa nalo moyoni.

Pia Mwakyembe alikutana na Waziri Mkuu Majaliwa kuhusiana na upotevu huo.

Pia Ridhiwani Kikwete anatajwa katika sakata hili na inasemekana ameshaitwa kuhojiwa na Waziri Mkuu.

Source: Gazeti la Jamhuri la leo 22/12/2015, Toleo no 221.

Nasisitiza kuwa makontena si mali ya umma kama ESCROW tu.
 
Hivi gazeti la Jamhuri ni CDM!?

By the way kusema JK ndiye aliyemzuia Lowasa kuingia Ikulu ina maana kuwa JPM hakuwa mshindi halali. Angalia kauli zako.
hivi hujui kuwa Josephat Isango ni CHADEMA kindakindaki, jidanganyeni ni habari zenu zenu za kizushi, kila siku kuzusha tu bila ushahidi, but jueni kuwa hamna uwezo wa kumfanya chochote JK, mtabaki kufoka tu kwenye mitandao! huo uchungu wenu wa kushindwa uchaguzi utawakondesha tu, narudia tena u are wasting your time, fanyeni kazi kwa bidii, muda wa majungu kama huu hamtapata!
 
Tatizo uelewa wako ni mdogo sana nahisi hata darasani mwalimu wako alikua na kazi sana,tatizo lako unaacha hoja ya msingi unakimbilia richmond,umeshaambiwa mwakyembe alishatoa taarifa kuhusu upotevu huu wa makontena na taarifa akampelekea bosi wake ambae ni raisi,sasa baada ya hapo ulitakaje ?ulitaka mwakyembe amshinikize raisi kuchukua hatua,na isitoshe baada ya taarifa yake alimishwa wizara sasa ulitaka mwakyembe aitishe waandishi wa habari aseme yale aliyo mwandikia raisi.kama hamjui namn serikali inavyo fanya kazi bora mkae kimya sio lazima kuchangia,uwezo wako mdogo wa kufikiri lakini kimbelembele kingi
Wewe ndio uelewa wako mdogo labda nikupe nafasi uniambie kama huyu Mwakyembe aliishalimaliza suala LA RICHMOND pale Bungeni je kulikuwa na haja gani kulizungumzia wakati wa kampeni? Kiuhalisia suala muhimu alilotakuwa kulizungumzia ni hili la bandari na lile la madawa ya kulevya ambayo yalikuwa hayajatatuliwa lakini alikaa kimya na pia hakuwahi kuzungumza chochote kuhusu ESCROW. Kwa hiyo ndugu kama Wewe ni mchepuko wa huyo Waziri basi hafai hata kuwa mwenyekiti wa mtaa.
 
hivi hujui kuwa Josephat Isango ni CHADEMA kindakindaki, jidanganyeni ni habari zenu zenu za kizushi, kila siku kuzusha tu bila ushahidi, but jueni kuwa hamna uwezo wa kumfanya chochote JK, mtabaki kufoka tu kwenye mitandao! huo uchungu wenu wa kushindwa uchaguzi utawakondesha tu, narudia tena u are wasting your time, fanyeni kazi kwa bidii, muda wa majungu kama huu hamtapata!
Anasemwa Nyerere marehemu sembuse Kikwete anayesikia na kujibu.

Kumalizika kwa uchaguzi siyo warrant wa yeye kutosemwa, ataendelea kufuatwa na uchafu wake alioufanya akiwa madarakani hadi anakwenda kaburini.
 
nisemeni mimi muacheni magufuli afanye kazi-by JK dec 9 2015
hata mkinisema sigombei tena, kwa hiyo mnapoteza muda wenu by JK
hizi ni dalili za walioshindwa by JK
sasa mmechanganyikiwa, by JK

ujumbe murua kabisa huu.

Aiseeee.....:thumbup:
Kumekucha sasa na ndio kwanza asubuhi.... kwa hili sakata la upotevu wa makontena pamoja mapato ya serikali

Mpo sawa hazitafika popote, mchezo umeisha . Tatizo matokeo sasa sijui bila bila !au wao moja JPM bila?

Ridhiwani yumo kwenye hilo sakata, HSC, ubalozi wa heshima huko Guangzou Uchina, pia FaizaFoxy yumo humo.

Ridhiwani itakuwa ngumu sana kumpiga pini maana alitumia vema kinga ya babake kuchezea taratibu na sheria za nchi ili kupata utajiri. Ndiyo maana akina JPM na Majaliwa wataishia kumhoji tu.

Ngoja nikae hapa nisikilize siri ya makontena na wakwepa kodi

Hata zile kesi za wahusika bandarini kuna mahali zitakosa nguvu kwani itakuja kugundulika kuwa ilikuwa ni AMRI (vimemo) kutoka mamlaka ya juu ambayo hayashikiki.. Huwezi kumwadhibu MTU aliyetekeleza amri ya rais hata kama ya kuua

Waziri mkuu kumwita na kumhoji Riz1 hii sijaipenda. Hatuna vyombo vya kuchukua hatua au ni 'kupanga dili'?

Siku kikwete akijikoroga kuachia uenyekiti basi na kikwete tutamshuhudia segereaa!!!

Akamatwe aisaidie polisi

Hapo nimeamini kwa asilimia mia moja mkuu!

Rais mstaafu Jakaya Kikwete imeelezwa kuwa anafahamu kilichokuwa kinaendelea katika suala la makontena bandarini na taarifa za kiuchunguzi zinaonyesha alipewa taarifa na akazikalia kimya.

Imejulikana kwamba aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Dr Harrison Mwakyembe alibaini upotevu wa makontena hayo, akaandika taarifa ya kina kwenda Ikulu lakini kilichomkuta hatakisahau maishani..!!.

Ripoti hiyo ilimkaanga mwenyewe Mwakyembe kwani baada tu ya JK kuipitia, akamwondoa Wizara ya Uchukuzi na kumpeleka Wizara ya Afrika Mashariki.

Taarifa za kina zinasema kuwa Rais Magufuli kabla ya kumteua Mwakyembe kwenye Wizara ya Sheria na Katiba aliyo sasa, alimwita na kumhoji kuhusu upotevu wa makontena hayo na hiyo ndio ikawa nafasi ya Mwakyembe kutoa fundo alilokuwa nalo moyoni.

Pia Mwakyembe alikutana na Waziri Mkuu Majaliwa kuhusiana na upotevu huo.

Pia Ridhiwani Kikwete anatajwa katika sakata hili na inasemekana ameshaitwa kuhojiwa na Waziri Mkuu.

Source: Gazeti la Jamhuri la leo 22/12/2015, Toleo no 221.
 
Back
Top Bottom